Wimbo wa Sulemani
7 “Miguu yako inapendeza sana katika viatu vyako,
Ee binti mwenye cheo!
Mikunjo ya mapaja yako ni kama mapambo,
Kazi ya mikono ya fundi.
2 Kitofu chako ni bakuli la muviringo.
Lisikose hata kidogo divai yenye kuchanganywa.
Tumbo lako ni rundo la ngano,
Lenye kuzungukwa na maua ya mayungiyungi.
3 Maziwa yako mbili ni kama paa wadogo wawili,
Mapacha wa paa.+
4 Shingo yako+ ni kama munara wa pembe ya tembo.+
Pua yako ni kama munara wa Lebanoni,
Wenye unaelekea Damasko.
5 Kichwa chako kinakuvalisha taji kama Karmeli,+
Na mashungi ya nywele zako*+ ni kama manyoya ya kondoo ya rangi ya zambarau.+
Mufalme amevutiwa* na nywele zako zenye kulembelea.
6 Wewe ni mwenye sura na umbo ya muzuri sana, na unapendeza sana,
Ee kijana mwanamuke mupendwa, unapita vitu vyote vyenye kupendeza!
8 Nilisema: ‘Nitapanda juu ya muti wa mutende
Ili nishike vitawi vyake vya matunda.’
Maziwa yako yakuwe kama vishada vya mizabibu,
Pumuzi yako ikuwe na harufu ya muzuri kama matunda ya matofaa,
9 Na kinywa chako* kama divai ya muzuri sana.”
“Acha itiririke polepole kwa ajili ya mupenzi wangu,
Itiririke kwa vyepesi juu ya midomo ya wale wenye kulala usingizi.
10 Mimi ni wa mupenzi wangu,+
Naye ananitamani.
12 Tuamuke asubui sana na kuenda kwenye mashamba ya mizabibu
Ili tuone kama muzabibu umechipuka,*
Kama maua yamefunguka,+
Kama miti ya mikomamanga imetoa maua.+
Kule nitakuonyesha upendo wangu.+
13 Matunda ya dudai+ yanatoa harufu yake ya muzuri,
Kwenye milango yetu kuko kila namna ya matunda ya muzuri sana.+
Ya mupya na ya zamani vilevile,
Ee mupenzi wangu, nimekuwekea.