Ezekieli
39 “Na wewe, mwana wa binadamu, toa unabii juu ya Gogu,+ na umuambie, ‘Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema hivi: “Nitapigana na wewe, Gogu, mukubwa wa wakubwa wa Mesheki na Tubali.+ 2 Nitakugeuza na kukuongoza na kukufanya ukuje kutoka sehemu za mbali zaidi za kaskazini+ na kukuingiza kwenye milima ya Israeli. 3 Nitapiga upinde wako utoke kwenye mukono wako wa kushoto na kufanya mishale yako ianguke kutoka kwenye mukono wako wa kuume. 4 Utaanguka kwenye milima ya Israeli,+ wewe na wanajeshi wako wote na vikundi vya watu vitakuwa pamoja na wewe. Nitakufanya kuwa chakula cha kila namna ya ndege wenye kuwinda na wanyama wa pori.”’+
5 “‘Utaanguka katika eneo lenye kuwa wazi la mashamba,+ kwa maana mimi mwenyewe nimesema,’ ni vile Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema.
6 “‘Na nitatuma moto juu ya Magogu na juu ya wale wenye kukaa katika visiwa kwa usalama,+ nao watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova. 7 Nitafanya jina langu takatifu lijulikane kati ya watu wangu Israeli, na sitaruhusu jina langu takatifu lichafuliwe tena; na mataifa yatalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova,+ Mutakatifu katika Israeli.’+
8 “‘Ndiyo, jambo hilo linakuja, na litafanywa,’ ni vile Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema. ‘Hii ndiyo siku yenye nimesema kuihusu. 9 Wakaaji wa miji ya Israeli watatoka inje na kuwasha mioto kwa silaha—ngao za kidogo* na ngao za mukubwa, pinde na mishale, magongo ya vita* na mikuki. Nao watazitumia kuwasha mioto+ kwa miaka saba (7). 10 Hawatahitaji kutafuta kuni katika eneo la mashamba wala kukusanya kuni katika mapori kwa sababu watatumia silaha kuwasha mioto.’
“‘Watachukua vitu kutoka kwa wale wenye walikuwa wanachukua vitu vyao na watanyanganya vitu vya wale wenye walikuwa wanawanyanganya vitu vyao,’ ni vile Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema.
11 “‘Siku hiyo, nitamupatia Gogu+ kaburi katika Israeli, katika bonde la wale wenye kusafiri upande wa mashariki wa bahari, na kaburi hilo litafunga njia ya wale wenye kupita kule. Ni pale watamuzika Gogu na vikundi vyake vyote vya watu, nao wataliita Bonde la Hamon-Gogu.*+ 12 Nyumba ya Israeli itatumia miezi saba (7) kuwazika ili kutakasa inchi.+ 13 Watu wote wa inchi watafanya kazi ya kuwazika, na hilo litawaletea sifa siku yenye nitajitukuza,’+ ni vile Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema.
14 “‘Watu watapewa kazi ya kupita katika inchi kwa kuendelea na kuzika miili yenye ilibakia juu ya uso wa dunia, ili kutakasa dunia. Wataendelea kutafuta kwa miezi saba (7). 15 Wakati wale wenye kupita katika inchi wataona mufupa wa mwanadamu, watatia alama pembeni ya mufupa huo. Kisha wale wenye walipewa kazi ya kuzika watauzika katika Bonde la Hamon-Gogu.+ 16 Na kule, kutakuwa pia muji wenye kuitwa Hamona.* Nao watatakasa inchi.’+
17 “Sasa wewe, mwana wa binadamu, Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema hivi: ‘Ambia ndege wa kila namna na wanyama wote wa pori, “Mukusanyike pamoja na mukuje. Mukusanyike pande zote kuzunguka zabihu yangu yenye ninawatayarishia, zabihu kubwa kwenye milima ya Israeli.+ Mutakula nyama na kunywa damu.+ 18 Mutakula nyama ya wenye nguvu na kunywa damu ya wakubwa wa dunia—kondoo-dume, na wana-kondoo, mbuzi, na ngombe-dume—wanyama wote wenye kunenepa wa Bashani. 19 Mutakula mafuta mupaka mushibe na kunywa damu mupaka mulewe kutokana na zabihu yenye ninawatayarishia.”’
20 “‘Kwenye meza yangu, mutashiba farasi na waendesha-magari, watu wenye nguvu na kila namna ya wapiganaji-vita,’+ ni vile Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema.
21 “‘Nitaonyesha utukufu wangu kati ya mataifa, na mataifa yote yataona hukumu yenye nimeleta na nguvu zenye* nimeonyesha kati yao.+ 22 Kuanzia siku hiyo, nyumba ya Israeli watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova Mungu wao. 23 Na mataifa yatalazimika kujua kwamba nyumba ya Israeli walienda katika uhamisho kwa sababu ya kosa lao wenyewe, kwa sababu hawakukuwa waaminifu kwangu.+ Kwa hiyo niliwaficha uso wangu+ na kuwatia katika mukono wa maadui wao,+ na wote wakaanguka kwa upanga. 24 Niliwatendea kulingana na uchafu wao na makosa yao, na niliwaficha uso wangu.’
25 “Kwa hiyo, Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema hivi: ‘Nitarudisha watu wa Yakobo wenye walikamatwa mateka+ na kuonyesha rehema nyumba yote ya Israeli;+ na nitatetea kwa bidii* jina langu takatifu.+ 26 Wakati watakuwa wamepatishwa haya kwa sababu ya ukosefu wao wote wa uaminifu kunielekea,+ watakaa kwa usalama katika inchi yao, bila mutu wa kuwaogopesha.+ 27 Wakati nitawarudisha kutoka katika vikundi vya watu na kuwakusanya kutoka katika inchi za maadui wao,+ mimi pia nitajitakasa kati yao mbele ya macho ya mataifa mengi.’+
28 “‘Watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova Mungu wao wakati nitawatuma katika uhamisho kati ya mataifa na kisha niwarudishe kwenye inchi yao, bila kuacha nyuma mutu yeyote kati yao.+ 29 Sitawaficha tena uso wangu,+ kwa maana nitamwanga roho yangu juu ya nyumba ya Israeli,’+ ni vile Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema.”