Yobu
9 Yobu akajibu:
2 “Kwa kweli ninajua kwamba ni vile.
Lakini namna gani mwanadamu mwenye anaweza kufa anaweza kuwa na haki katika kesi ya hukumu pamoja na Mungu?+
3 Kama mutu anataka kubishana Naye,*+
Mutu huyo hawezi kujibu ulizo moja kati ya maulizo Yake elfu moja (1 000).
4 Yeye ni mwenye hekima katika moyo na mwenye nguvu nyingi sana.*+
Ni nani anaweza kumupinga na akose kuumia?+
5 Anahamisha* milima bila mutu kujua;
Anaipindua katika kasirani yake.
6 Anatikisa dunia itoke mahali pake,
Na hivyo nguzo zake zinatetemeka.+
7 Anaamuru jua lisitoe mwangaza
Na anazuia mwangaza wa nyota;+
8 Anatandika mbingu yeye peke yake,+
Na anakanyanga juu ya mawimbi makubwa ya bahari.+
9 Alifanya kundi la nyota la Ashi,* Kesili,* na Kima,*+
Na makundi ya nyota ya anga la kusini;*
10 Anafanya mambo makubwa na yenye hayawezi kuchunguzwa,+
Mambo ya ajabu yenye hayawezi kuhesabiwa.+
11 Anapita pembeni yangu, lakini siwezi kumuona;
Anapita karibu na mimi, lakini simutambue.
12 Wakati anakamata kitu kwa nguvu, ni nani anaweza kushindana naye?
Ni nani anaweza kumuuliza, ‘Unafanya nini?’+
14 Namna gani basi wakati ninamujibu
Ninapaswa kuchagua kwa uangalifu maneno yangu ili kubishana naye!
15 Hata kama ningekuwa na haki, singemujibu.+
Ningemulilia tu muamuzi* wangu anionyeshe rehema.
16 Nikimuita, atanijibu?
Siamini kama atasikiliza sauti yangu,
17 Kwa maana ananiponda kwa zoruba
Na anaongeza vidonda vyangu bila sababu.+
18 Haniache nipumue;
Anaendelea kunijaza mambo machungu.
19 Kama ni nguvu, ni yeye mwenye kuwa na nguvu.+
Kama ni haki, anasema: ‘Ni nani anaweza kunishitaki?’
20 Kama ningekuwa na haki, kinywa changu mwenyewe kingenihukumu;
Hata kama ninaendelea kuwa muaminifu-mushikamanifu,* atasema niko na hatia.*
21 Hata kama ninaendelea kuwa muaminifu-mushikamanifu,* sijiamini mimi mwenyewe;*
Ninakataa* maisha yangu.
22 Yote ni sawa. Ndiyo sababu ninasema,
‘Anaharibu wenye hawana kosa* na pia waovu.’
23 Kama mafuriko yanatokeza kifo cha kushitukia,
Atachekelea hali ya kupoteza tumaini ya watu wenye hawana kosa.
Kama haiko yeye, ni nani basi?
25 Siku zangu zinakimbia mbio kuliko mukimbiaji;+
Zinakimbia bila kuona mema.
27 Kama ninasema, ‘Nitasahau malalamiko yangu,
Nitabadilisha sura yangu na kufurahi,’
28 Ningeendelea kuogopa kwa sababu ya maumivu yangu yote,+
Na ninajua ungenipata na kosa.
29 Ningeonwa kuwa na hatia.*
Basi sababu gani nijisumbue bure?+
30 Nikinawa na teluji* yenye kuyeyuka,
Na kusafisha mikono yangu na sabuni,*+
31 Basi, ungenitupa ndani ya shimo,
Na hata nguo zangu zingenichukia.
32 Kwa maana yeye haiko mwanadamu kama mimi ili niweze kumujibu,
Ili tuende naye kwenye tribinali.+