Yoshua
13 Basi Yoshua alikuwa amezeeka na alikuwa ameishi miaka mingi.+ Kwa hiyo Yehova akamuambia: “Umezeeka na umeishi miaka mingi; lakini kungali sehemu kubwa ya inchi yenye haijakamatwa. 2 Hii ndiyo inchi yenye imebakia:+ maeneo yote ya Wafilisti na ya Wageshuri+ 3 (kuanzia mukono wa Muto Nile wenye* kuwa upande wa mashariki wa* Misri kufikia kwenye mupaka wa Ekroni upande wa kaskazini, wenye ulionwa kuwa sehemu ya eneo la Wakanaani)+ pamoja na eneo la mabwana tano (5) wa Wafilisti+—Wagaza, Waashdodi,+ Waashkeloni,+ Wagati,+ na Waekroni;+ eneo la Waavimu+ 4 upande wa kusini; inchi yote ya Wakanaani; Meara ya Wasidoni,+ kufikia Afeki, kwenye mupaka wa Waamori; 5 inchi ya Wagebali+ na inchi yote ya Lebanoni kuelekea mashariki, kuanzia Baal-gadi chini ya Mulima Hermoni mupaka Lebo-hamati;*+ 6 wakaaji wote wa eneo lenye milima kuanzia Lebanoni+ mupaka Misrefot-maimu;+ na Wasidoni+ wote. Nitawafukuza* mbele ya Waisraeli.+ Utagawia inchi hiyo Israeli kuwa uriti, kama vile nimekuamuru.+ 7 Sasa gawanya inchi hii kuwa uriti kwa makabila kenda (9) na nusu ya kabila la Manase.”+
8 Na hiyo nusu ingine ya kabila, na watu wa kabila la Rubeni na Gadi walikamata uriti wao wenye Musa aliwapatia upande wa mashariki wa Yordani, kama vile Musa mutumishi wa Yehova alikuwa amewapatia:+ 9 kuanzia Aroeri,+ wenye kuwa pembeni ya Bonde la Arnoni,*+ na muji wenye kuwa katikati ya bonde hilo, na eneo lote tambarare la juu la Medeba mupaka Diboni; 10 na miji yote ya Mufalme Sihoni wa Waamori, mwenye alitawala Heshboni, kufikia kwenye mupaka wa Waamoni;+ 11 pia Gileadi na eneo la Wageshuri na Wamaakati+ na Mulima wote wa Hermoni na Bashani+ mupaka Saleka;+ 12 ufalme wote wa Ogu kule Bashani, mwenye alitawala Ashtaroti na Edrei. (Alikuwa mumoja wa Warefaimu wenye walibakia.)+ Musa aliwashinda na kuwafukuza.*+ 13 Lakini Waisraeli hawakufukuza*+ Wageshuri na Wamaakati, kwa maana Wageshuri na Wamaakati wanaendelea kuishi katikati ya Israeli mupaka leo.
14 Ni kabila la Walawi tu ndilo hakupatia uriti.+ Uriti wao ulikuwa matoleo yenye yalitolewa kwa Yehova Mungu wa Israeli kwa njia ya moto,+ kama vile aliwaahidi.+
15 Kisha Musa akapatia kabila la Rubeni uriti kulingana na familia zao, 16 na eneo lao lilianzia Aroeri, pembeni ya Bonde la Arnoni,* na muji wenye kuwa katikati ya bonde hilo, na eneo lote tambarare la juu la Medeba; 17 Heshboni na miji yake yote+ katika eneo tambarare la juu, Diboni, Bamot-baali, Bet-baal-meoni,+ 18 Yahazi,+ Kedemoti,+ Mefaati,+ 19 Kiriataimu, Sibma,+ na Seret-shahari kwenye mulima wenye kuwa katika bonde,* 20 Bet-peori, miteremuko ya Pisga,+ Bet-yeshimoti,+ 21 miji yote ya eneo tambarare la juu, na eneo lote la Mufalme Sihoni wa Waamori, mwenye alitawala Heshboni.+ Musa alimushinda+ na wakubwa wa Midiani, ni kusema, Evi, Rekemu, Suri, Huru, na Reba,+ watawala wadogo* wa Mufalme Sihoni wenye walikaa katika inchi. 22 Waisraeli waliua kwa upanga Balaamu+ mwana wa Beori, ule muaguzi,+ pamoja na watu wenye walibakia. 23 Na mupaka wa kabila la Rubeni ulikuwa Yordani; na eneo hilo lilikuwa uriti wa kabila la Rubeni kulingana na familia zao, pamoja na miji na makao yake.
24 Pia, Musa akapatia kabila la Gadi uriti, kulingana na familia zao, 25 na eneo lao lilikuwa Yazeri+ na miji yote ya Gileadi na nusu ya inchi ya Waamoni+ mupaka Aroeri, mbele ya Raba;+ 26 na kutoka Heshboni+ mupaka Ramat-mispe na Betonimu, na kutoka Mahanaimu+ kufikia kwenye mupaka wa Debiri; 27 na katika bonde,* Bet-haramu, Bet-nimra,+ Sukoti,+ na Safoni, eneo lenye lilibakia la Mufalme Sihoni wa Heshboni,+ na Yordani ilikuwa mupaka wenye kuanzia upande wa chini wa Bahari ya Kinereti,*+ upande wa mashariki wa Yordani. 28 Huo ndio ulikuwa uriti wa kabila la Gadi kulingana na familia zao, pamoja na miji na makao yake.
29 Tena, Musa akapatia nusu ya kabila la Manase uriti, ukakuwa uriti wa nusu ya kabila la Manase kulingana na familia zao.+ 30 Na eneo lao lilianzia Mahanaimu+ na eneo lote la Bashani, eneo lote la Mufalme Ogu wa Bashani, na vijiji vyote vya mahema vya Yairi+ kule Bashani, miji makumi sita (60). 31 Na nusu ya eneo la Gileadi, na Ashtaroti na Edrei,+ miji ya Mufalme Ogu kule Bashani, ilipewa wana wa Makiri+ mwana wa Manase, nusu ya wana wa Makiri kulingana na familia zao.
32 Hizo ndizo sehemu zenye Musa aliwapatia kuwa uriti katika maeneo tambarare ya jangwa la Moabu ngambo ingine ya Yordani, upande wa mashariki wa Yeriko.+
33 Lakini Musa hakupatia kabila la Walawi uriti.+ Yehova Mungu wa Israeli ndiye uriti wao, kama vile aliwaahidi.+