Yobu
26 Yobu akajibu:
2 “Mumesaidia mutu mwenye hana nguvu kabisa!
Mumeokoa mukono wenye hauna nguvu kabisa!+
3 Kwa kweli mumemupatia mutu mwenye hana hekima mashauri ya muzuri sana!+
Na mumefunua kwa wingi hekima yenu yenye kutenda!*
4 Munajaribu kusema na nani,
Na ni nani aliwaongoza kusema mambo kama hayo?*
5 Wale wenye hawana uwezo katika kifo wanatetemeka;
Wako chini hata kuliko maji na viumbe vyenye kukaa ndani yake.
7 Anatandika anga la kaskazini* mahali kwenye hakuna kitu,*+
Ananinginiza dunia mahali kwenye hakuna kitu;
8 Anafunga maji katika mawingu yake,+
Ili mawingu yasipasuke kwa sababu ya uzito wa maji;
9 Anafunika kiti chake cha ufalme kisionekane,
11 Nguzo za mbingu zinatikisika;
Na zinashangaa sana kwa sababu ya kukemea kwake.
12 Anavuruga bahari kwa nguvu zake,+
Na kwa uelewaji wake anavunja vipande-vipande munyama mukubwa wa bahari.*+
13 Kwa pumuzi yake* anasafisha anga;
Mukono wake unatoboa nyoka mwenye kuenda mbio kwa kutereza.
14 Angalia! Hizo ni sehemu za pembeni-pembeni tu za njia zake;+
Ni sauti ya chini-chini tu ndiyo tumesikia juu yake!
Basi ni nani anaweza kuelewa mungurumo wake wenye nguvu?”+