Yobu
25 Bildadi+ Mushua akajibu:
2 “Utawala na uwezo wenye kuogopesha ni vyake;
Anaweka amani mbinguni.*
3 Je, majeshi yake yanaweza kuhesabiwa?
Ni nani mwenye haangaziwe na mwangaza wake?
4 Basi namna gani mwanadamu mwenye anaweza kufa anaweza kuwa mwenye haki mbele ya Mungu,+
Ao namna gani mutu mwenye alizaliwa na mwanamuke anaweza kuwa bila kosa?*+
5 Hata mwezi haungae
Na nyota haziko safi mbele ya macho yake,
6 Namna gani basi mwanadamu mwenye anaweza kufa, ambaye ni funza,*
Na mwana wa binadamu, ambaye ni munyoo!”