Yobu
16 Yobu akajibu:
2 “Nimesikia mambo mengi kama hayo zamani.
Ninyi wote ni wafariji wenye kusumbua!+
3 Je, maneno yenye hayana maana yatakuwa na mwisho?
Ni nini inawachochea kujibu hivi?
4 Mimi pia ningeweza kusema kama ninyi.
Kama mungekuwa katika hali yangu,*
Ningesema maneno yenye kusadikisha ili kuwashambulia
Na ningetikisa kichwa changu juu yenu.+
5 Lakini, kuliko kufanya vile, ningewatia nguvu kwa maneno ya kinywa changu,
Na faraja ya midomo yangu ingewatuliza.+
6 Hata nikisema, maumivu yangu hayatulie,+
Na nikiacha kusema, maumivu yangu yanapunguka kwa kadiri gani?
8 Pia unanikamata, na huo umekuwa ushahidi,
Na hivyo kukonda kwangu kunaonekana na kunatoa ushahidi mbele ya uso wangu.
9 Kasirani yake imenipasua vipande-vipande, na ananiwekea kinyongo.+
Ananisagia meno yake.
Adui yangu ananitoboa na macho yake.+
10 Wamefungua kinywa chao wazi juu yangu,+
Na wamepiga machafu yangu kwa zarau;
Wanakusanyika kwa wingi ili kunishambulia.+
11 Mungu ananiweka katika mikono ya vijana wadogo wanaume,
Na ananitupa kwa nguvu katika mikono ya waovu.+
12 Nilikuwa nimekaa bila wasiwasi, lakini akanivunja-vunja;+
Alinikamata nyuma ya shingo na kuniponda-ponda;
Kisha akanifanya kuwa shabaha yake.
13 Wapiga-mishale wake wananizunguka;+
Anatoboa figo zangu+ na hasikie huruma;
Anamwanga nyongo* yangu juu ya udongo.
14 Ananitoboa matundu-matundu;
Ananishambulia kama mupiganaji-vita.
16 Uso wangu ni mwekundu kwa sababu ya kulia,+
Na kuko kivuli kizito* juu ya kope za macho yangu,
17 Hata kama mikono yangu haijafanya jeuri yoyote
Na sala yangu iko safi.
18 Ee dunia, usifunike damu yangu!+
Na acha kilio changu kisikuwe na mahali pa kupumuzikia!
19 Hata sasa, shahidi wangu iko* mbinguni;
Mwenye anaweza kunitetea iko katika nafasi za juu.
21 Acha mutu akuwe muamuzi kati ya mwanadamu na Mungu,
Kama vile mutu anaweza kufanya kati ya mwanadamu na mwenzake.+