Zaburi
Kwa kiongozi. Muziki wa Daudi.
20 Yehova akujibu katika siku ya taabu.
Jina la Mungu wa Yakobo likulinde.+
3 Akumbuke matoleo yako yote ya zawadi;
Akubali kwa wema* toleo lako la kuteketezwa. (Sela)
5 Tutapiga vigelegele vya shangwe kwa sababu ya matendo yako ya wokovu;+
Tutainua bendera zetu katika jina la Mungu wetu.+
Yehova atimize maombi yako yote.
6 Sasa ninajua kwamba Yehova anamuokoa mutiwa-mafuta wake.+
7 Watu fulani wanategemea magari na wengine farasi,+
Lakini sisi tunaitia jina la Yehova Mungu wetu.+
8 Wameporomoka na kuanguka,
Lakini sisi tumesimama na kurudishwa wima.+
9 Ee Yehova, okoa mufalme!+
Atatujibu siku yenye tutaomba musaada.+