Yoshua
20 Kisha Yehova akamuambia Yoshua: 2 “Ambia Waisraeli, ‘Mujichagulie miji ya makimbilio+ kama vile niliwaambia kupitia Musa, 3 ili muuaji mwenye ataua mutu* bila kukusudia ao bila kutazamia* akimbilie kule. Itakuwa makimbilio yenu ili kumuepuka mulipiza-kisasi cha damu.+ 4 Anapaswa kukimbilia kwenye muji mumoja kati ya miji hiyo+ na kusimama kwenye muingilio wa mulango mukubwa wa muji+ na kueleza kesi yake katika masikio ya wazee wa muji huo. Kisha wanapaswa kumupokea katika muji huo na kumupatia mahali pa kuishi na ataishi pamoja nao. 5 Kama mulipiza-kisasi cha damu anamufuatilia, wazee hawapaswe kutia muuaji huyo katika mikono yake, kwa maana alimuua mwenzake bila kutazamia* na hakukuwa anamuchukia.+ 6 Anapaswa kukaa ndani ya muji huo mupaka jambo lenye alifanya lisikilizwe mbele ya mukusanyiko,+ na atabakia kule mupaka wakati kuhani mukubwa+ mwenye kuwa katika madaraka wakati huo atakufa. Kisha muuaji huyo anaweza kurudia katika muji kwenye alitoka, na anaweza kuingia katika muji wake na nyumba yake.’”+
7 Basi wakafanya miji hii kuwa mitakatifu:* Kedeshi+ kule Galilaya katika eneo la milima la Naftali, Shekemu+ katika eneo la milima la Efraimu, na Kiriat-arba,+ ni kusema, Hebroni, katika eneo lenye milima la Yuda. 8 Na katika eneo la Yordani, upande wa mashariki wa Yeriko, wakachagua muji wa Beseri+ katika jangwa kwenye eneo tambarare la juu katika eneo la kabila la Rubeni, Ramoti+ kule Gileadi katika eneo la kabila la Gadi, na Golani+ kule Bashani katika eneo la kabila la Manase.+
9 Hiyo ndiyo miji yenye ilichaguliwa kwa ajili ya Waisraeli wote na wakaaji wageni wenye waliishi kati yao, ili mutu yeyote mwenye ataua mutu* bila kukusudia akimbilie kule+ na ili asiuawe katika mukono wa mulipiza-kisasi cha damu kabla ya kuhukumiwa mbele ya mukusanyiko.+