Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • Ezekieli 37
  • Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

Habari Zenye Kuwa Katika Ezekieli

      • Maono ya bonde la mifupa yenye kukauka (1-14)

      • Vipande mbili vya muti vitaunganishwa pamoja (15-28)

        • Taifa moja chini ya mufalme mumoja (22)

        • Agano la milele la amani (26)

Ezekieli 37:1

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Ufu 21:10

Ezekieli 37:2

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Eze 37:11

Ezekieli 37:3

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Kum 32:39; 1 Sa. 2:6

Ezekieli 37:5

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Mwa 2:7; Eze 37:14

Ezekieli 37:9

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “pumuzi; roho.”

Ezekieli 37:10

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “roho.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Ufu 11:11

Ezekieli 37:11

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Eze 36:10
  • +Isa 49:14

Ezekieli 37:12

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Isa 66:14
  • +Eze 11:17; Amo 9:14

Ezekieli 37:13

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Zab 126:2

Ezekieli 37:14

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Isa 32:14, 15; Eze 36:27

Ezekieli 37:16

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “wenye kuwa washiriki wake.”

  • *

    Ao “wenye kuwa washiriki wake.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +2Nya 15:9; 30:11
  • +1 Fal. 11:31; 12:20

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Munara wa Mulinzi (Gazeti la Funzo),

    7/2016, uku. 31-32

Ezekieli 37:17

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Isa 11:13; Yer 3:18

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Munara wa Mulinzi (Gazeti la Funzo),

    7/2016, uku. 31-32

Ezekieli 37:18

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “wana wa watu wako.”

Ezekieli 37:19

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Yer 50:4; Zek 10:6

Ezekieli 37:21

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Kum 30:3; Isa 11:12; Yer 16:14, 15; Amo 9:14

Ezekieli 37:22

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Yer 3:18; Ho 1:11
  • +Mwa 49:10; Zab 2:6; Isa 9:6; Yer 23:5; Lu 1:32
  • +Eze 37:19; Zek 10:6

Ezekieli 37:23

Maelezo ya Chini

  • *

    Pengine neno la Kiebrania lenye linatumiwa hapa linahusiana na maneno “mavi ya wanyama” na linatumiwa ili kuonyesha zarau.

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Isa 2:18; Eze 11:18; Ho 14:8; Zek 13:2
  • +Yer 31:33; Eze 36:28

Ezekieli 37:24

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Yer 23:5; 30:9; Ho 3:5; Lu 1:32
  • +Yoh 10:16; 1 Pe. 5:4
  • +Kum 30:8-10; Yer 32:39; Eze 36:27

Ezekieli 37:25

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “wana.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Yer 30:3
  • +Yoe 3:20
  • +Isa 60:21; Amo 9:15
  • +Eze 34:24; Lu 1:32

Ezekieli 37:26

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Eze 34:25
  • +Yer 30:19; Zek 8:5

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Munara wa Mulinzi,

    15/3/2010, uku. 27-28

Ezekieli 37:27

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “Makao; Nyumba.”

  • *

    Ao “juu yao.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Law. 26:12; Eze 11:19, 20; 43:7; Ho 2:23; Ufu 21:3

Ezekieli 37:28

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Eze 36:23

Maandiko ingine

Eze. 37:1Ufu 21:10
Eze. 37:2Eze 37:11
Eze. 37:3Kum 32:39; 1 Sa. 2:6
Eze. 37:5Mwa 2:7; Eze 37:14
Eze. 37:10Ufu 11:11
Eze. 37:11Eze 36:10
Eze. 37:11Isa 49:14
Eze. 37:12Isa 66:14
Eze. 37:12Eze 11:17; Amo 9:14
Eze. 37:13Zab 126:2
Eze. 37:14Isa 32:14, 15; Eze 36:27
Eze. 37:162Nya 15:9; 30:11
Eze. 37:161 Fal. 11:31; 12:20
Eze. 37:17Isa 11:13; Yer 3:18
Eze. 37:19Yer 50:4; Zek 10:6
Eze. 37:21Kum 30:3; Isa 11:12; Yer 16:14, 15; Amo 9:14
Eze. 37:22Yer 3:18; Ho 1:11
Eze. 37:22Mwa 49:10; Zab 2:6; Isa 9:6; Yer 23:5; Lu 1:32
Eze. 37:22Eze 37:19; Zek 10:6
Eze. 37:23Isa 2:18; Eze 11:18; Ho 14:8; Zek 13:2
Eze. 37:23Yer 31:33; Eze 36:28
Eze. 37:24Yer 23:5; 30:9; Ho 3:5; Lu 1:32
Eze. 37:24Yoh 10:16; 1 Pe. 5:4
Eze. 37:24Kum 30:8-10; Yer 32:39; Eze 36:27
Eze. 37:25Yer 30:3
Eze. 37:25Yoe 3:20
Eze. 37:25Isa 60:21; Amo 9:15
Eze. 37:25Eze 34:24; Lu 1:32
Eze. 37:26Eze 34:25
Eze. 37:26Yer 30:19; Zek 8:5
Eze. 37:27Law. 26:12; Eze 11:19, 20; 43:7; Ho 2:23; Ufu 21:3
Eze. 37:28Eze 36:23
  • Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
  • 22
  • 23
  • 24
  • 25
  • 26
  • 27
  • 28
Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
Ezekieli 37:1-28

Ezekieli

37 Mukono wa Yehova ulikuwa juu yangu, na Yehova akanibeba kupitia roho yake na kuniweka chini katikati ya bonde tambarare,+ na bonde hilo lilikuwa limejaa mifupa. 2 Akanipitisha kuizunguka pande zote, na nikaona kwamba kulikuwa mifupa mingi sana katika bonde tambarare, na ilikuwa yenye kukauka sana.+ 3 Akaniuliza: “Mwana wa binadamu, je, mifupa hii inaweza kuishi?” Nikajibu: “Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova, wewe ndiye unajua.”+ 4 Kwa hiyo akaniambia: “Toa unabii kuhusu mifupa hii, na uiambie, ‘Enyi mifupa yenye kukauka, musikie neno la Yehova:

5 “‘Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anaambia hivi mifupa hii: “Nitafanya pumuzi iingie ndani yenu, na mutaishi tena.+ 6 Nitatia mishipa na nyama juu yenu, na nitawafunika kwa ngozi na kutia pumuzi ndani yenu, na ninyi mutaishi; na ninyi mutalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.”’”

7 Kisha nikatoa unabii kama vile nilikuwa nimeamuriwa. Wakati tu nilitoa unabii, sauti ikasikika, sauti ya kugongana-gongana, na mifupa ikaanza kukaribiana, mufupa kwa mufupa. 8 Kisha nikaona mishipa na nyama zikikuja juu ya mifupa hiyo, na ngozi ikaifunika. Lakini bado hapakukuwa pumuzi ndani ya mifupa hiyo.

9 Kisha akaniambia: “Tolea upepo unabii. Toa unabii, mwana wa binadamu, na uambie upepo, ‘Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema hivi: “Ingia kutoka kwenye zile pepo ine (4), Ee upepo,* na upulize juu ya watu hawa wenye waliuawa, ili waishi tena.”’”

10 Kwa hiyo nikatoa unabii kama vile aliniamuru, na pumuzi* ikaingia ndani yao, nao wakaanza kuishi na kusimama kwa miguu yao,+ walikuwa jeshi kubwa sana.

11 Kisha akaniambia: “Mwana wa binadamu, mifupa hii ni nyumba muzima ya Israeli.+ Wanasema, ‘Mifupa yetu imekauka, na tumaini letu limepotea.+ Tumeondolewa kabisa.’ 12 Kwa hiyo toa unabii na uwaambie, ‘Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema hivi: “Nitafungua makaburi yenu+ na kuwainua kutoka katika makaburi yenu, watu wangu, na kuwaleta katika inchi ya Israeli.+ 13 Na ninyi mutalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova wakati nitafungua makaburi yenu na kuwainua kutoka katika makaburi yenu, Enyi watu wangu.”’+ 14 ‘Nitatia roho yangu ndani yenu, na ninyi mutaishi,+ na nitawafanya mukae katika inchi yenu; na ninyi mutalazimika kujua kwamba mimi mwenyewe, Yehova, nimesema na nimefanya jambo hilo,’ ni vile Yehova anasema.”

15 Neno la Yehova likakuja tena kwangu, na kusema: 16 “Na wewe, mwana wa binadamu, kamata kipande cha muti na uandike juu yake, ‘Kwa ajili ya Yuda na kwa ajili ya watu wa Israeli wenye kuwa pamoja naye.’*+ Kisha ukamate kipande kingine cha muti na kuandika juu yake, ‘Kwa ajili ya Yosefu, kipande cha muti cha Efraimu, na nyumba yote ya Israeli wenye kuwa pamoja naye.’*+ 17 Kisha uvifanye vikaribiane ili vikuwe kipande kimoja tu cha muti katika mukono wako.+ 18 Wakati watu wako* watakuambia, ‘Je, hautatuambia mambo haya yanamaanisha nini?’ 19 uwaambie, ‘Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema hivi: “Nitakamata kipande cha muti cha Yosefu, chenye kuwa katika mukono wa Efraimu, na makabila ya Israeli yenye kuwa pamoja naye, na nitayaunganisha kwenye kipande cha muti cha Yuda; na nitavifanya kuwa kipande kimoja cha muti,+ na vitakuwa kipande kimoja cha muti katika mukono wangu.”’ 20 Vipande vya muti vyenye utaandika juu yake vinapaswa kuwa katika mukono wako ili wavione.

21 “Kisha uwaambie, ‘Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema hivi: “Nitatosha Waisraeli katika mataifa kwenye wameenda, na nitawakusanya pamoja kutoka kila upande na kuwaleta katika inchi yao.+ 22 Nitawafanya kuwa taifa moja katika inchi hiyo,+ kwenye milima ya Israeli, na mufalme mumoja atawatawala wote,+ nao hawatakuwa tena mataifa mbili; wala hawatagawanyika tena kuwa falme mbili.+ 23 Hawatajichafua tena kupitia sanamu zao zenye kuchukiza* na kupitia matendo yao yenye kuchukiza na kupitia makosa yao yote.+ Nitawaokoa kutokana na ukosefu wao wote wa uaminifu wenye kupitia huo wamefanya zambi, na nitawasafisha. Watakuwa watu wangu, na mimi mwenyewe nitakuwa Mungu wao.+

24 “‘“Mutumishi wangu Daudi atakuwa mufalme wao,+ na wote watakuwa na muchungaji mumoja.+ Watatembea katika maamuzi yangu ya hukumu na watashika sheria zangu kwa uangalifu.+ 25 Wataishi katika inchi yenye nilimupatia mutumishi wangu, Yakobo, kwenye mababu zenu waliishi,+ na watakaa kule milele,+ wao na watoto* wao na watoto wa watoto wao;+ na mutumishi wangu Daudi atakuwa mukubwa wao milele.+

26 “‘“Na nitafanya agano la amani pamoja nao;+ litakuwa agano la milele pamoja nao. Nitawafanya imara na kuwafanya wakuwe wengi+ na nitatia patakatifu pangu kati yao milele. 27 Hema* yangu itakuwa pamoja nao,* na mimi nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu.+ 28 Na mataifa yatalazimika kujua kwamba mimi, Yehova, ninatakasa Israeli wakati patakatifu pangu patakuwa katikati yao milele.”’”+

Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili (Congo)
  • Tumia Wengine
  • Préférences
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Kanuni za Matumizi
  • Kanuni za Kutunza Siri
  • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
  • JW.ORG
  • Ingia
Tumia Wengine