Yobu
23 Yobu akajibu:
2 “Hata leo nitatoa malalamiko yangu kwa kichwa-nguvu;*+
Nguvu zangu zimeisha juu ya kulia kwa sababu ya maumivu.
3 Ingekuwa muzuri kama ningejua mahali kwenye ningemupata Mungu!+
Ningeenda mahali pake kwenye anakaa.+
4 Ningepeleka kesi yangu ya hukumu mbele yake
Na kujaza kinywa changu mawazo ya kujitetea;
5 Ningejua namna angenijibu
Na ningefikiria mambo yenye angeniambia.
6 Je, angeshindana na mimi kwa nguvu zake nyingi?
Hapana, hakika angenisikia.+
7 Pale mutu munyoofu angenyoosha mambo pamoja naye,
Na Muamuzi wangu angetangaza kuwa sina kosa milele.
8 Lakini nikienda upande wa mashariki, haiko kule;
Na nikirudia, simupate.
9 Wakati anafanya kazi upande wa kushoto, siwezi kumuangalia;
Kisha anageukia upande wa kuume, lakini tu simuone.
10 Lakini anajua njia yenye nimefuata.+
Akiisha kunijaribu, nitatoka nikiwa safi kama vile zahabu.+
11 Miguu yangu imefuata karibu-karibu alama za miguu yake;
Nimefuata njia yake bila kugeukia upande mwingine.+
12 Sijaacha amri ya midomo yake.
Nimeweka maneno yake kama hazina+ kuliko hata mambo yenye niliombwa kufanya.*
13 Wakati amekusudia kufanya jambo fulani, ni nani anaweza kumupinga?+
Wakati anataka* kufanya jambo fulani, yeye analifanya.+
14 Kwa maana atatenda mambo yote yenye amekusudia kunitendea,
Na ametayarisha mambo mengi kama hayo.
15 Ndiyo maana nimekuwa na wasiwasi kwa sababu yake;
Wakati ninawaza juu yake, woga wangu unaongezeka.
16 Mungu amenifanya nikuwe na moyo wa woga,
Na Mweza-Yote ameniogopesha.
17 Lakini bado sijanyamazishwa na giza
Ao na giza nzito lenye limefunika uso wangu.