Kumbukumbu la Torati
13 “Kama nabii ao mutu mwenye kutabiri kupitia ndoto anatokea katikati yako na kukupatia alama ao jambo la ajabu, 2 na alama ao jambo hilo la ajabu lenye alikuambia linatimia wakati anasema, ‘Tufuate miungu mingine,’ miungu yenye haukujua, ‘na tuitumikie,’ 3 haupaswe kusikiliza maneno ya nabii huyo ao mwota-ndoto huyo,+ kwa sababu Yehova Mungu wenu anawajaribu+ ili ajue kama munamupenda Yehova Mungu wenu kwa moyo wenu wote na kwa nafsi* yenu yote.+ 4 Munapaswa kumufuata Yehova Mungu wenu, munapaswa kumuogopa yeye, munapaswa kushika amri zake, munapaswa kusikiliza sauti yake; yeye ndiye munapaswa kutumikia, na munapaswa kushikamana naye kabisa.+ 5 Lakini nabii huyo ao mwota-ndoto huyo anapaswa kuuawa,+ kwa sababu alichochea uasi juu ya Yehova Mungu wenu—mwenye aliwatosha katika inchi ya Misri na kukukomboa katika nyumba ya utumwa—ili kukutosha katika njia yenye Yehova Mungu wako amekuamuru utembee ndani yake. Na unapaswa kuondoa jambo la mubaya katikati yako.+
6 “Kama ndugu yako, mutoto mwanaume wa mama yako, ao mutoto wako mwanaume ao mutoto wako mwanamuke ao bibi yako mwenye unapenda ao rafiki yako wa karibu sana* anajaribu kukushawishi kwa uficho, na kusema, ‘Tuende na tutumikie miungu mingine,’+ miungu yenye wewe wala mababu zako hawakujua, 7 kati ya miungu ya vikundi vya watu vyenye kuwazunguka pande zote, ikuwe karibu na ninyi ao mbali na ninyi, kuanzia mwisho mumoja wa inchi mupaka mwisho mwingine wa inchi, 8 haupaswe kukubali ushawishi wake wala kumusikiliza,+ wala usimusikitikie wala kumusikilia huruma wala kumulinda; 9 lakini, unapaswa kumuua kabisa.+ Mukono wako unapaswa kuwa wa kwanza kuja juu yake ili kumuua, kisha mukono wa watu wote utafuata.+ 10 Na unapaswa kumupiga majiwe mupaka akufe,+ kwa sababu alitafuta kukugeuza umuache Yehova Mungu wako, mwenye alikutosha katika inchi ya Misri, katika nyumba ya utumwa. 11 Halafu Israeli wote watasikia na kuogopa, na hawatafanya tena jambo lolote la mubaya kama hilo kati yako.+
12 “Kama unasikia ikisemwa katika mumoja kati ya miji yako yenye Yehova Mungu wako anakupatia ili ukae ndani yake, 13 ‘Watu wenye hawana mafaa yoyote wametokea kati yako ili kupotosha wakaaji wa muji wao, na kusema, “Tuende na tutumikie miungu mingine,” miungu yenye haukujua,’ 14 unapaswa kupeleleza jambo hilo, kufanya uchunguzi na kuuliza habari kwa uangalifu;+ na kama inahakikishwa kwamba ni kweli jambo hilo lenye kuchukiza limefanywa kati yako, 15 unapaswa kabisa kupiga na kuua wakaaji wa muji huo kwa upanga.+ Haribu muji huo na kila kitu chenye kuwa ndani yake, pamoja na mifugo yake kwa upanga.+ 16 Kisha utakusanya vitu vyote vya muji huo katikati ya kiwanja cha watu wote cha muji huo na kuteketeza kwa moto muji huo, na vitu vya muji huo vitakuwa toleo nzima kwa ajili ya Yehova Mungu wako. Na muji huo utakuwa rundo la mabomoko milele. Haupaswe kujengwa tena. 17 Mukono wako haupaswe kukamata kitu chochote chenye kilitiwa pembeni ili kuharibiwa,*+ kusudi Yehova aache kasirani yake yenye kuwaka na akuonyeshe rehema na huruma na kukufanya uongezeke, kama vile ameapia mababu zako.+ 18 Kwa maana unapaswa kumutii* Yehova Mungu wako kwa kushika amri zake zote zenye ninakuamuru leo, na hivyo kufanya mambo yenye kuwa sawa mbele ya macho ya Yehova Mungu wako.+