Yobu
24 “Sababu gani Mweza-Yote haweke wakati?+
Sababu gani wale wenye kumujua hawaone siku yake?*
2 Watu wanasogeza alama za mipaka;+
Wanaiba makundi kwa ajili ya malisho yao.
3 Wanafukuzia mbali punda wa watoto wenye hawana baba
Na wananyanganya ngombe-dume wa mujane kusudi akuwe kitu chenye kinawekeshwa kwa ajili ya mukopo.+
4 Wanasukuma maskini waondoke katika barabara;
Watu wazaifu wa dunia wanalazimika kujificha mbali nao.+
5 Maskini wanatafuta chakula kama punda wa pori+ katika jangwa;
Wanatafutia watoto wao chakula katika jangwa.
6 Wanalazimika kuvuna katika mashamba ya wengine*
Na kuokota masalio katika shamba la mizabibu la waovu.
7 Wanalala usiku wakiwa uchi, bila nguo;+
Hawana kitu cha kujifunika wakati wa baridi.
8 Wanalowanishwa na mvua ya milima;
Wanashikamana sana na miamba kwa sababu ya kukosa mahali pa kujificha.
9 Mutoto mwenye hana baba anaondolewa kwa nguvu kwenye maziwa ya mama yake;+
Na nguo za maskini zinakamatwa ili zikuwe kitu chenye kinawekeshwa kwa ajili ya mukopo,+
10 Wanawalazimisha kutembea uchi, bila nguo,
Na wakiwa na njaa, wakati wanabeba mafungu ya nafaka.
11 Wanafanya kazi ya jasho kati ya kuta za matuta wakati wa joto;*
Wanakanyanga vikamulio vya divai, lakini wanabakia na kiu.+
12 Wenye kuwa karibu kufa wanaendelea kulia kwa maumivu katika muji;
Wenye waliumizwa sana wanalilia* musaada,+
Lakini Mungu haone kama hilo ni kosa.*
14 Muuaji anaamuka asubui sana;
Anaua watu wenye hawana uwezo na maskini,+
Na wakati wa usiku anafanya kazi ya kuiba.
Na anafunika uso wake.
16 Wanavunja* nyumba wakati wa giza;
Muchana wanajifungia ndani.
Hawajue mwangaza ni nini.+
17 Kwa maana wanaona asubui kuwa sawa na giza nzito;
Wanajua vitu vyenye kuogopesha vya giza nzito.
18 Lakini wanabebwa kwa vyepesi na maji.*
Sehemu yao ya inchi italaaniwa.+
Hawatarudia kwenye mashamba yao ya mizabibu.
19 Kama vile ukame na joto vinakausha teluji* yenye kuyeyuka,
20 Mama yake atamusahau;* na funza* atafanya karamu juu yake.
Hatakumbukwa tena.+
Na ukosefu wa haki utavunjwa kama vile muti.
21 Anatesa mwanamuke tasa,
Na anamutendea mubaya mujane.
22 Mungu* atatumia nguvu zake ili kuharibu wenye nguvu;
Hata wakisimama, hawana uhakika wa kuishi.
24 Wanatukuzwa kwa wakati mufupi, kisha hawako tena.+
Wanashushwa chini+ na kukusanywa kama watu wengine;
Wanakatwa kama vichwa vya nafaka.
25 Sasa ni nani anaweza kuonyesha kama mimi niko muongo
Ao kupinga maneno yangu?”