Yobu
8 Kisha Bildadi+ Mushua+ akajibu:
2 “Utaendelea kusema hivi mupaka wakati gani?+
Maneno ya kinywa chako ni kama tu upepo wenye nguvu!
3 Je, Mungu atapotosha haki,
Ao Mweza-Yote atapotosha uadilifu?*
4 Kama wana wako wamemutendea zambi,
Anawaacha wapewe azabu kwa sababu ya uasi wao;*
5 Lakini kama tu unamutafuta Mungu+
Na kumulilia Mweza-Yote ili akuonyeshe wema,
6 Na kama kwa kweli ungekuwa safi na munyoofu,+
Angekukazia uangalifu*
Na kukurudisha mahali pako penye kustahili.
7 Na hata kama mwanzo wako ulikuwa mudogo,
Wakati wako wenye kuja ungekuwa mukubwa.+
8 Tafazali, uliza kizazi chenye kilitangulia,
Na ukazie uangalifu mambo yenye baba zao walijionea.+
9 Kwa maana tulizaliwa jana tu, na hatujue kitu,
Kwa sababu siku zetu katika dunia ziko kama kivuli.
10 Je, hawatakufundisha
Na kukuambia mambo yenye wanajua?*
11 Je, mumea wa mafunjo* utakuwa murefu mahali kwenye hakuna tingitingi?
Je, matete yatakuwa ya murefu bila maji?
12 Wakati majani yake yangali yanafungana, mbele hayajakatwa,
Yatakauka mbele ya mumea mwingine wowote.
13 Huo ndio mwisho wa* wale wote wenye kumusahau Mungu,
Kwa maana tumaini la mwenye hamuogope Mungu* litapotea,
14 Mwenye tegemeo lake ni la bure
Na mwenye tegemeo lake liko zaifu kama vile utando wa* buibui.
15 Ataegemea nyumba yake, lakini haitaendelea kusimama;
Atajaribu kuishikilia, lakini haitadumu.
16 Yeye ni mumea wenye majimaji katika mwangaza wa jua,
Na matawi yake yanaenea katika bustani.+
17 Mizizi yake inasukana-sukana katika rundo la majiwe;
Anatafuta nyumba kati ya majiwe.*
18 Lakini wakati atangolewa* mahali pake,
Mahali pale patamukana na kusema, ‘Sijakuonaka hata siku moja.’+
20 Kwa kweli Mungu hatakataa watu wenye kuendelea kuwa waaminifu-washikamanifu;*
Wala hataunga* mukono watu waovu,
21 Kwa maana atajaza tena kinywa chako kicheko
Na midomo yako sauti za furaha.
22 Wenye kukuchukia watafunikwa na haya,
Na hema ya watu waovu haitakuwa tena.”