Yobu
17 “Roho yangu imevunjika, siku zangu zimezimishwa;
Kaburi linaningojea.+
2 Watu wenye kufanya zihaka wananizunguka,+
Na macho yangu yanalazimika kutazama* mwenendo wao wa uasi.
3 Tafazali, kubali kitu chenye ninakuwekesha, na ukiweke.
Ni nani mwingine atanishika mukono na kutoa ahadi kwa ajili yangu?+
4 Kwa sababu umeficha utambuzi mbali na moyo wao;+
Ndiyo maana hauwainue.
5 Anaweza kuamua kufurahia vitu vyake pamoja na marafiki wake,
Lakini wakati uleule macho ya watoto wake yako zaifu.
6 Amenifanya kuwa kitu cha kuzarauliwa* kati ya vikundi vya watu,+
Na hivyo nimekuwa mutu wa kutemewa mate kwenye uso.+
7 Macho yangu yanafifia kwa sababu ya uchungu,+
Na viungo vyote vya mwili wangu viko kama kivuli.
8 Watu wanyoofu wanashangaa kwa sababu ya jambo hilo,
Na mutu mwenye hana kosa anasumbuka kwa sababu ya mutu mwenye hamuogope Mungu.*
10 Lakini, ninyi wote munaweza kuja na kusema tena mawazo yenu,
Kwa maana sikuona mutu mwenye hekima kati yenu.+
12 Wanaendelea kugeuza usiku kuwa muchana,
Wanasema, ‘Mwangaza unapaswa kuwa karibu kwa sababu kuko giza.’
14 Nitaambia shimo* kwa sauti kubwa,+ ‘Wewe ni baba yangu!’
Na funza,* ‘Wewe ni mama yangu na dada yangu!’
15 Basi, tumaini langu liko wapi?+
Ni nani anaweza kuona tumaini langu?