Isaya
27 Siku hiyo Yehova, akiwa na upanga wake mukali na mukubwa na wenye nguvu,+
Atamuelekezea uangalifu Leviatani,* ule nyoka mwenye kuenda mbio kwa kutereza,
Leviatani, ule nyoka mwenye kujiviringa-viringa,
Na ataua munyama mukubwa mwenye kuwa katika bahari.
2 Siku hiyo mumuimbie ule mwanamuke:*
“Shamba la mizabibu la divai yenye kutoa pofu!+
Kila wakati ninamumwangilia maji.+
Ninamulinda usiku na muchana,
Ili mutu yeyote asimuumize.+
4 Hakuna kasirani kali ndani yangu.+
Ni nani atapambana na mimi katika vita kwa kutumia miti midogo-midogo ya miiba na magugu?
Nitavikanyanga-kanyanga na kuvichoma moto vyote pamoja.
5 Kama haiko vile, acha ashike kwa nguvu ngome yangu,
Afanye amani pamoja na mimi;
Amani aifanye pamoja na mimi.”
6 Katika siku zenye kuja Yakobo atatia mizizi,
Israeli atatoa maua na kuchipuka,+
Na watajaza mazao katika inchi.+
7 Je, lazima apigwe kwa pigo la ule mwenye kumupiga?
Ao, je, lazima auawe kwa mauaji kama ya watu wake wenye waliuawa?
8 Utashindana naye kwa mulio wa kushitua wakati utakuwa unamufukuza.
Atamufukuza kwa mulipuko wake mukali katika siku ya upepo wa mashariki.+
9 Basi kwa njia hii kosa la Yakobo litafunikwa,+
Na mazao kamili wakati zambi yake itaondolewa yatakuwa haya:
Atafanya majiwe yote ya mazabahu
Yakuwe kama majiwe ya chokaa yenye imepondwa,
Na hakuna miti mitakatifu* ao vinara vya uvumba vyenye vitabakia.+
10 Kwa maana muji wenye ngome utaachwa,
Malisho yataachwa na kubakia kama jangwa.+
Kitoto-dume cha ngombe kitakulia majani pale na kulala pale
Na kitakula matawi yake.+
Kwa maana watu hawa hawana uelewaji.+
Ndiyo sababu Mutengenezaji wao hatawaonyesha rehema,
Na Ule mwenye aliwafanya hatawaonyesha wema.+
12 Siku hiyo Yehova atapiga-piga matunda kuanzia muto mudogo wenye kutiririka wa ule Muto* mupaka kwenye Bonde la Muto* la Misri,+ na ninyi mutakusanywa mumoja kisha mwingine, Enyi watu wa Israeli.+ 13 Siku hiyo baragumu kubwa itapigwa,+ na wale wenye kuangamia katika inchi ya Ashuru+ na wale wenye walitawanyika katika inchi ya Misri+ watakuja na kumuinamia Yehova kwenye mulima mutakatifu katika Yerusalemu.+