Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • Yeremia 27
  • Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

Habari Zenye Kuwa Katika Yeremia

      • Nira ya Babiloni (1-11)

      • Sedekia anaambiwa ajitiishe kwa Babiloni (12-22)

Yeremia 27:1

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Yeremia, uku. 27

Yeremia 27:3

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Eze 25:12, 13; Oba 1
  • +Yer 48:1; Eze 25:8, 9
  • +Yer 49:1, 2; Eze 25:2
  • +Isa 23:1; Yer 47:4; Eze 26:3
  • +Isa 23:4; Eze 28:21; Yoe 3:4

Yeremia 27:5

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “ule mwenye ni sawa katika macho yangu.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Da. 4:17

Yeremia 27:6

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Yer 25:9; 28:14; 43:10; Da. 2:37, 38

Yeremia 27:7

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Zab 137:8; Yer 50:14, 27; Da. 5:26, 30
  • +Yer 25:12, 14; 51:11

Yeremia 27:8

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Eze 26:7, 8

Yeremia 27:11

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “lipumuzike.”

Yeremia 27:12

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +2 Fal. 24:17; 1Nya 3:15; Yer 37:1
  • +Yer 38:2, 20

Yeremia 27:13

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +2 Fal. 25:7
  • +2 Fal. 25:3
  • +Yer 21:9; Eze 14:21

Yeremia 27:14

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Yer 28:1, 2, 11; 37:19
  • +Yer 14:14; 23:21; 28:15; 29:8, 9; Eze 13:6

Yeremia 27:15

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Yer 20:6; 29:21; Eze 13:3

Yeremia 27:16

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +2 Fal. 24:11, 13; 2Nya 36:7; Yer 28:1-3; Da. 1:1, 2
  • +Yer 14:13

Yeremia 27:17

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Yer 27:11; 38:17

Yeremia 27:19

Maelezo ya Chini

  • *

    Ni kusema, “Bahari ya shaba ya hekalu.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +1 Fal. 7:15; 2 Fal. 25:17; 2Nya 4:11, 12; Yer 52:21
  • +1 Fal. 7:23
  • +1 Fal. 7:27; 2 Fal. 25:16; 2Nya 4:11, 14

Yeremia 27:20

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +2 Fal. 24:14, 15; 2Nya 36:10; Yer 24:1; Da. 1:2, 3

Yeremia 27:22

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +2 Fal. 25:13, 14; 2Nya 36:18; Yer 52:17, 18; Da. 5:3
  • +Ezr 1:7; 5:14

Maandiko ingine

Yer. 27:3Eze 25:12, 13; Oba 1
Yer. 27:3Yer 48:1; Eze 25:8, 9
Yer. 27:3Yer 49:1, 2; Eze 25:2
Yer. 27:3Isa 23:1; Yer 47:4; Eze 26:3
Yer. 27:3Isa 23:4; Eze 28:21; Yoe 3:4
Yer. 27:5Da. 4:17
Yer. 27:6Yer 25:9; 28:14; 43:10; Da. 2:37, 38
Yer. 27:7Zab 137:8; Yer 50:14, 27; Da. 5:26, 30
Yer. 27:7Yer 25:12, 14; 51:11
Yer. 27:8Eze 26:7, 8
Yer. 27:122 Fal. 24:17; 1Nya 3:15; Yer 37:1
Yer. 27:12Yer 38:2, 20
Yer. 27:132 Fal. 25:7
Yer. 27:132 Fal. 25:3
Yer. 27:13Yer 21:9; Eze 14:21
Yer. 27:14Yer 28:1, 2, 11; 37:19
Yer. 27:14Yer 14:14; 23:21; 28:15; 29:8, 9; Eze 13:6
Yer. 27:15Yer 20:6; 29:21; Eze 13:3
Yer. 27:162 Fal. 24:11, 13; 2Nya 36:7; Yer 28:1-3; Da. 1:1, 2
Yer. 27:16Yer 14:13
Yer. 27:17Yer 27:11; 38:17
Yer. 27:191 Fal. 7:15; 2 Fal. 25:17; 2Nya 4:11, 12; Yer 52:21
Yer. 27:191 Fal. 7:23
Yer. 27:191 Fal. 7:27; 2 Fal. 25:16; 2Nya 4:11, 14
Yer. 27:202 Fal. 24:14, 15; 2Nya 36:10; Yer 24:1; Da. 1:2, 3
Yer. 27:222 Fal. 25:13, 14; 2Nya 36:18; Yer 52:17, 18; Da. 5:3
Yer. 27:22Ezr 1:7; 5:14
  • Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
  • 22
Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
Yeremia 27:1-22

Yeremia

27 Katika mwanzo wa utawala wa Yehoyakimu mwana wa Yosia, mufalme wa Yuda, neno hili lilikuja kwa Yeremia kutoka kwa Yehova: 2 “Yehova ameniambia hivi: ‘Ujitengenezee kamba na nira, na uviweke kwenye shingo yako. 3 Kisha uvitume kwa mufalme wa Edomu,+ mufalme wa Moabu,+ mufalme wa Waamoni,+ mufalme wa Tiro,+ na mufalme wa Sidoni+ kupitia mukono wa wajumbe wenye wamekuja Yerusalemu kwa Mufalme Sedekia wa Yuda. 4 Uwapatie amri hii kwa ajili ya mabwana wao:

“‘“Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: muambie hivi mabwana wenu: 5 ‘Mimi ndiye nilifanya dunia, wanadamu, na wanyama wenye kuwa juu ya uso wa dunia kwa nguvu zangu kubwa na kwa mukono wangu wenye kunyooshwa; na nimeipatia mutu yeyote mwenye ninapenda.*+ 6 Na sasa nimetia inchi hizi zote katika mukono wa mutumishi wangu Mufalme Nebukadneza+ wa Babiloni; nimemupatia hata wanyama wa pori ili wamutumikie. 7 Mataifa yote yatamutumikia yeye na mwana wake na mujukuu wake mupaka wakati wa inchi yake mwenyewe utafika,+ wakati mataifa mengi na wafalme wakubwa watamufanya kuwa mutumwa wao.’+

8 “‘“‘Kama taifa lolote ao ufalme unakataa kumutumikia Mufalme Nebukadneza wa Babiloni na unakataa kuweka shingo yake chini ya nira ya mufalme wa Babiloni, nitapatia taifa hilo azabu kwa upanga,+ kwa njaa, na kwa ugonjwa wa kuambukiza,’ ni vile Yehova anasema, ‘mupaka wakati nitakuwa nimewamaliza kabisa kupitia mukono wake.’

9 “‘“‘Kwa hiyo, musisikilize manabii wenu, waaguzi wenu, waota-ndoto wenu, wachawi wenu, na walozi wenu, wenye wanawaambia ninyi: “Hamutamutumikia mufalme wa Babiloni.” 10 Kwa maana wanawatolea ninyi unabii wa uongo, na hivyo mutapelekwa mbali na inchi yenu na nitawatawanya ninyi na mutaangamia.

11 “‘“‘Lakini taifa lenye linaweka shingo yake chini ya nira ya mufalme wa Babiloni na kumutumikia, nitaliruhusu libakie* kwenye inchi yake,’ ni vile Yehova anasema, ‘ili kuilima na kukaa ndani yake.’”’”

12 Pia Mufalme Sedekia+ wa Yuda nilimuambia maneno yaleyale, kwa kusema: “Muweke shingo zenu chini ya nira ya mufalme wa Babiloni na mumutumikie yeye na watu wake, na mutaendelea kuishi.+ 13 Sababu gani wewe na watu wako mukufe kwa upanga,+ kwa njaa,+ na kwa ugonjwa wa kuambukiza,+ kama vile Yehova alisema kuhusu taifa lenye halitamutumikia mufalme wa Babiloni? 14 Musisikilize maneno ya manabii wenye wanawaambia ninyi, ‘Hamutamutumikia mufalme wa Babiloni,’+ kwa sababu wanawatolea ninyi unabii wa uongo.+

15 “‘Kwa maana sikuwatuma,’ ni vile Yehova anasema, ‘lakini wanatoa unabii wa uongo katika jina langu, ili mwishowe niwatawanye ninyi na muangamie, ninyi na manabii wenye wanawatolea ninyi unabii.’”+

16 Na nikaambia makuhani na watu hawa wote: “Yehova anasema hivi: ‘Musisikilize maneno ya manabii wenu wenye wanawatolea ninyi unabii: “Muangalie! Karibuni vyombo vya nyumba ya Yehova vitarudishwa kutoka Babiloni!”+ kwa maana wanawatolea ninyi unabii wa uongo.+ 17 Musiwasikilize. Mumutumikie mufalme wa Babiloni na mutaendelea kuishi.+ Sababu gani muji huu ukuwe mabomoko? 18 Lakini kama wao ni manabii na kama neno la Yehova liko pamoja nao, tafazali acha waombe Yehova wa majeshi kwamba vyombo vyenye vilibakia katika nyumba ya Yehova, katika nyumba ya mufalme wa Yuda, na katika Yerusalemu visipelekwe Babiloni.’

19 “Kwa maana Yehova wa majeshi anasema hivi kuhusu zile nguzo,+ ile Bahari,*+ yale magari,+ na vyombo vyenye vilibakia vyenye viliachwa katika muji huu, 20 vyenye Mufalme Nebukadneza wa Babiloni hakukamata wakati alimupeleka katika uhamisho Yekonia mwana wa Yehoyakimu, mufalme wa Yuda, kutoka Yerusalemu mupaka Babiloni, pamoja na watu wote wenye vyeo wa Yuda na Yerusalemu;+ 21 ndiyo, Yehova wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi kuhusu vyombo vyenye vilibakia kwenye nyumba ya Yehova, katika nyumba ya mufalme wa Yuda, na katika Yerusalemu: 22 ‘“Vitapelekwa Babiloni,+ na vitabakia kule mupaka siku nitavikazia uangalifu,” ni vile Yehova anasema. “Kisha nitavileta na kuvirudisha mahali hapa.”’”+

Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili (Congo)
  • Tumia Wengine
  • Préférences
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Kanuni za Matumizi
  • Kanuni za Kutunza Siri
  • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
  • JW.ORG
  • Ingia
Tumia Wengine