Ezekieli
29 Katika mwaka wa kumi (10), mwezi wa kumi, siku ya kumi na mbili (12) ya mwezi huo, neno la Yehova lilikuja kwangu, na kusema: 2 “Mwana wa binadamu, elekeza uso wako kwa Farao mufalme wa Misri, na utoe unabii juu yake na juu ya Misri yote.+ 3 Sema maneno haya: ‘Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema hivi:
“Angalia, nitapigana na wewe, Farao mufalme wa Misri,+
Munyama mukubwa wa bahari mwenye kulala kati ya mito midogo ya muto wake Nile,*+
Mwenye amesema, ‘Muto Nile ni wangu.
Niliufanya kwa ajili yangu mwenyewe.’+
4 Lakini nitatia kulabu* katika mataya* yako na kufanya samaki wa muto wako Nile washikamane na magamba yako.
Nitakutosha katika muto wako Nile pamoja na samaki wa muto wako Nile wenye kushikamana na magamba yako.
5 Nitakuacha katika jangwa, wewe na samaki wote wa muto wako Nile.
Utaanguka katika eneo lenye kuwa wazi la mashamba, na hautakusanywa wala kuokotwa.+
Nitakutoa ili ukuwe chakula cha wanyama wa pori wa dunia na ndege wa anga.+
6 Halafu wakaaji wote wa Misri watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova,
Kwa sababu hawakutegemeza tena nyumba ya Israeli, walikuwa tu kama unyasi.*+
7 Wakati walishika mukono wako, ulipondwa,
Na uliwafanya wapasue bega lao.
8 “‘Kwa hiyo, Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema hivi: “Angalia, ninaleta upanga juu yako,+ na nitaondoa katikati yako mwanadamu na munyama. 9 Inchi ya Misri itakuwa mahali kwenye kuwa ukiwa na kwenye kuharibiwa;+ nao watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova, kwa maana umesema,* ‘Muto Nile ni wangu, mimi ndiye niliufanya.’+ 10 Kwa hiyo nitapigana na wewe na Muto wako Nile, nitafanya inchi ya Misri kuwa mahali kwenye kumeharibiwa na kwenye kukauka, eneo lenye kuwa ukiwa,+ kuanzia Migdoli+ kufikia Sewene+ kwenye mupaka wa Etiopia. 11 Hakuna mwanadamu wala mifugo yenye itapita ndani yake kwa miguu,+ na haitaikaliwa kwa miaka makumi ine (40). 12 Nitafanya inchi ya Misri ikuwe ukiwa kuliko inchi zote, na miji yake itakuwa ukiwa kuliko miji yote kwa miaka makumi ine (40);+ na nitasambaza Wamisri kati ya mataifa na kuwatawanya kati ya inchi mbalimbali.”+
13 “‘Kwa maana Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema hivi: “Kisha miaka makumi ine (40) nitakusanya Wamisri kutoka katika vikundi vya watu kwenye walisambazwa;+ 14 watu wa Misri wenye walikamatwa mateka, nitawarudisha katika inchi ya Patrosi,+ katika inchi yao ya asili, na kule watakuwa ufalme wa hali ya chini. 15 Misri itakuwa chini kuliko zile falme zingine na haitatawala tena yale mataifa mengine,+ na nitawafanya kuwa wadogo sana ili wasiweze kutiisha mataifa mengine.+ 16 Haitakuwa tena chanzo cha tegemeo kwa nyumba ya Israeli,+ lakini itawakumbusha tu kosa lenye walifanya kwa kuendea Wamisri ili kutafuta musaada. Nao watalazimika kujua kwamba mimi ndiye Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova.”’”
17 Sasa katika mwaka wa makumi mbili na saba (27), mwezi wa kwanza, siku ya kwanza ya mwezi huo, neno la Yehova likakuja kwangu, na kusema: 18 “Mwana wa binadamu, Mufalme Nebukadneza*+ wa Babiloni, aliamuru jeshi lake lifanye kazi kubwa juu ya Tiro.+ Kila kichwa kilitiwa upara, na kila bega lilikwaruzwa. Lakini yeye na jeshi lake hawakupata malipo kwa ajili ya kazi yenye alifanya juu ya Tiro.
19 “Kwa hiyo Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema hivi: ‘Angalia, ninamupatia Nebukadneza* mufalme wa Babiloni inchi ya Misri,+ na atabeba utajiri wake na kukamata vitu vingi vyenye vinachukuliwa na vitu vingi vyenye vinanyanganywa katika Misri; na vitakuwa malipo kwa ajili ya jeshi lake.’
20 “‘Kama malipo ya kazi yenye alifanya juu ya kumushambulia,* nitamupatia inchi ya Misri kwa sababu walitenda kwa ajili yangu,’+ ni vile Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema.
21 “Siku hiyo nitafanya pembe ichipuke kwa ajili ya nyumba ya Israeli,*+ na nitakupatia nafasi ya kuzungumuza kati yao; nao watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.”