Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • Ezekieli 30
  • Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

Habari Zenye Kuwa Katika Ezekieli

      • Unabii juu ya Misri (1-19)

        • Shambulizi la Nebukadneza linatabiriwa (10)

      • Nguvu za Farao zinavunjwa (20-26)

Ezekieli 30:3

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Oba 15
  • +Eze 32:7
  • +Zab 110:6

Ezekieli 30:4

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Eze 32:11, 12

Ezekieli 30:5

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “wale wote wenye walitoka katika mataifa mengine.”

  • *

    Pengine ni Waisraeli wenye walifanya muungano na Misri.

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Sef 2:12
  • +Nah 3:8, 9

Ezekieli 30:6

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Eze 30:18
  • +Yer 44:1
  • +Eze 29:10

Ezekieli 30:7

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Yer 46:19; Eze 29:12; 32:18

Ezekieli 30:9

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “mashua za maji; bateaux.”

Ezekieli 30:10

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “Nebukadreza,” njia ingine ya kuandika jina hili.

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Eze 29:19; 32:11

Ezekieli 30:11

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Hab 1:6
  • +Eze 29:5

Ezekieli 30:12

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Eze 29:3
  • +Eze 31:12

Ezekieli 30:13

Maelezo ya Chini

  • *

    Pengine neno la Kiebrania lenye linatumiwa hapa linahusiana na maneno “mavi ya wanyama” na linatumiwa ili kuonyesha zarau.

  • *

    Ao “Memfisi.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Yer 43:12; 46:14
  • +Yer 46:5

Ezekieli 30:14

Maelezo ya Chini

  • *

    Ni kusema, Tebesi.

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Mwa 10:13, 14; Yer 44:1
  • +Yer 46:25

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Munara wa Mulinzi,

    1/7/2003, uku. 32

Ezekieli 30:15

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Munara wa Mulinzi,

    1/7/2003, uku. 32

Ezekieli 30:16

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “Memfisi.”

Ezekieli 30:17

Maelezo ya Chini

  • *

    Ni kusema, Heliopolisi.

Ezekieli 30:18

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Eze 30:8
  • +Yer 46:20; Eze 31:18
  • +Yer 46:19

Ezekieli 30:22

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Yer 46:25; Eze 29:3
  • +2 Fal. 24:7; Yer 46:2
  • +Yer 46:21

Ezekieli 30:23

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Eze 29:12

Ezekieli 30:24

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “Nitaongeza nguvu za.”

  • *

    Ni kusema, mbele ya mufalme wa Babiloni.

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Yer 27:6
  • +Eze 32:11, 12

Ezekieli 30:25

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Eze 29:19, 20

Ezekieli 30:26

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Eze 29:12

Maandiko ingine

Eze. 30:3Oba 15
Eze. 30:3Eze 32:7
Eze. 30:3Zab 110:6
Eze. 30:4Eze 32:11, 12
Eze. 30:5Sef 2:12
Eze. 30:5Nah 3:8, 9
Eze. 30:6Eze 30:18
Eze. 30:6Yer 44:1
Eze. 30:6Eze 29:10
Eze. 30:7Yer 46:19; Eze 29:12; 32:18
Eze. 30:10Eze 29:19; 32:11
Eze. 30:11Hab 1:6
Eze. 30:11Eze 29:5
Eze. 30:12Eze 29:3
Eze. 30:12Eze 31:12
Eze. 30:13Yer 43:12; 46:14
Eze. 30:13Yer 46:5
Eze. 30:14Mwa 10:13, 14; Yer 44:1
Eze. 30:14Yer 46:25
Eze. 30:18Eze 30:8
Eze. 30:18Yer 46:20; Eze 31:18
Eze. 30:18Yer 46:19
Eze. 30:22Yer 46:25; Eze 29:3
Eze. 30:222 Fal. 24:7; Yer 46:2
Eze. 30:22Yer 46:21
Eze. 30:23Eze 29:12
Eze. 30:24Yer 27:6
Eze. 30:24Eze 32:11, 12
Eze. 30:25Eze 29:19, 20
Eze. 30:26Eze 29:12
  • Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
  • 22
  • 23
  • 24
  • 25
  • 26
Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
Ezekieli 30:1-26

Ezekieli

30 Na neno la Yehova likakuja tena kwangu, na kusema: 2 “Mwana wa binadamu, toa unabii na useme, ‘Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema hivi:

“Omboleza, ‘Ole, ile siku inakuja!’

 3 Kwa maana siku iko karibu, ndiyo, siku ya Yehova iko karibu.+

Itakuwa siku ya mawingu,+ wakati wenye uliwekwa wa mataifa.+

 4 Upanga utakuja juu ya Misri, na Etiopia itapatwa na woga mukubwa wakati wale wenye kuuawa wataanguka kule Misri;

Utajiri wake umekamatwa na misingi yake imebomolewa.+

 5 Etiopia,+ Putu,+ Ludi na watu wote wenye kuchanganyika,*

Na Kubu, pamoja na wana wa inchi ya agano,*

Wote wataanguka kwa upanga.”’

 6 Yehova anasema hivi:

‘Wenye kuunga mukono Misri wataanguka pia,

Na nguvu zake zenye majivuno zitashushwa.’+

“‘Kuanzia Migdoli+ mupaka Sewene+ wataanguka kwa upanga katika inchi,’ ni vile Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema. 7 ‘Watafanywa kuwa inchi yenye ukiwa kuliko inchi zote, na miji yake itakuwa miji yenye imeharibiwa zaidi.+ 8 Nao watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova wakati nitawasha moto kule Misri na wakati wale wenye waliungana naye watapondwa. 9 Katika siku hiyo nitatuma wajumbe katika mashua* ili kufanya Etiopia yenye kujitegemea itetemeke; woga mukubwa utawashika katika siku yenye inakuja juu ya Misri, kwa maana hakika itakuja.’

10 “Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema hivi: ‘Nitakomesha vikundi vya watu vya Misri kupitia mukono wa Mufalme Nebukadneza* wa Babiloni.+ 11 Yeye na wanajeshi wake, taifa lenye halina huruma kabisa kati ya mataifa,+ wataletwa ili kuharibu inchi. Watachomoa panga zao juu ya Misri na kujaza inchi watu wenye kuuawa.+ 12 Nitageuza mifereji ya Muto Nile+ kuwa inchi kavu na kuuzisha inchi katika mukono wa watu waovu. Kupitia mukono wa wageni,+ nitaharibu inchi na kila kitu chenye kuwa ndani yake. Mimi mwenyewe, Yehova, nimesema.’

13 “Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema hivi: ‘Nitaharibu pia sanamu zenye kuchukiza* na kuharibu miungu yenye haina mafaa yoyote ya Nofu.*+ Hakutakuwa tena mukubwa katika inchi ya Misri, na nitatia woga katika inchi ya Misri.+ 14 Nitafanya Patrosi+ kuwa ukiwa na nitawasha moto katika Soani na kuleta hukumu juu ya No.*+ 15 Nitamwanga kasirani yangu kali juu ya Sini, ngome ya Misri, na kuharibu wakaaji wa No. 16 Nitawasha moto katika Misri; na Sini itashikwa na woga mukubwa na No itatobolewa na Nofu* itashambuliwa wakati wa muchana! 17 Vijana wa Oni* na Pibeseti wataanguka kwa upanga, na miji itaenda katika utekwa. 18 Katika Tehafnehesi siku itakuwa na giza wakati nitavunja nira za Misri kule.+ Nguvu zake zenye majivuno zitaisha,+ mawingu yatamufunika, na miji yake itaenda katika utekwa.+ 19 Nitaleta hukumu juu ya Misri, nao watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.’”

20 Na katika mwaka wa kumi na moja (11), mwezi wa kwanza, siku ya saba (7) ya mwezi huo, neno la Yehova likakuja kwangu, na kusema: 21 “Mwana wa binadamu, nimevunja mukono wa Farao mufalme wa Misri; hautafungwa ili upone ao kufungwa kwa kitambaa ili ukuwe na nguvu za kushika upanga.”

22 “Kwa hiyo Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema hivi: ‘Angalia, niko juu ya Farao mufalme wa Misri,+ na nitavunja mikono yake, mukono wenye nguvu na ule wenye kuvunjika,+ na nitafanya upanga uanguke kutoka kwenye mukono wake.+ 23 Kisha nitasambaza Wamisri kati ya mataifa na kuwasambaza kati ya inchi mbalimbali.+ 24 Nitatia nguvu mikono ya* mufalme wa Babiloni+ na kutia upanga wangu katika mukono wake,+ na nitavunja mikono ya Farao, naye atalia kwa maumivu kwa sauti kubwa kama vile mutu mwenye anakaribia kufa mbele yake.* 25 Nitatia nguvu mikono ya mufalme wa Babiloni, lakini mikono ya Farao itaninginia kwa uregevu; nao watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova wakati nitatia upanga wangu katika mukono wa mufalme wa Babiloni na atautumia juu ya inchi ya Misri.+ 26 Na nitasambaza Wamisri kati ya mataifa na kuwasambaza kati ya inchi mbalimbali,+ nao watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.’”

Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili (Congo)
  • Tumia Wengine
  • Préférences
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Kanuni za Matumizi
  • Kanuni za Kutunza Siri
  • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
  • JW.ORG
  • Ingia
Tumia Wengine