Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • Ezekieli 32
  • Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

Habari Zenye Kuwa Katika Ezekieli

      • Wimbo wa huzuni kuhusu Farao na Misri (1-16)

      • Misri atazikwa pamoja na watu wenye hawatahiriwe (17-32)

Ezekieli 32:2

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “wimbo wa maombolezo.”

  • *

    Ao “mwana-simba mwenye manyoya ya murefu kwenye shingo.”

  • *

    Tnn., “mito yao.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Isa 51:9, 10; Eze 29:3

Ezekieli 32:3

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “makila yangu.”

Ezekieli 32:4

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Eze 29:5

Ezekieli 32:5

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Eze 31:12

Ezekieli 32:6

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “Na sehemu za chini za mito midogo zitajazwa kutoka kwako (na wewe).”

Ezekieli 32:7

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Isa 13:1, 10

Ezekieli 32:9

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Eze 29:12; 30:26

Ezekieli 32:11

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Yer 43:10, 11; 46:25, 26; Eze 30:24

Ezekieli 32:12

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Eze 30:10, 11; Hab 1:6
  • +Eze 29:19

Ezekieli 32:13

Maelezo ya Chini

  • *

    Kwato ni sehemu ngumu ya chini ya muguu wa munyama.

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Eze 30:12
  • +Eze 29:8, 11

Ezekieli 32:15

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Zab 107:33, 34; Eze 29:12
  • +Eze 30:26

Ezekieli 32:18

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “kaburi.”

Ezekieli 32:20

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Eze 29:8

Ezekieli 32:21

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “Sheoli,” ni kusema, kaburi la wanadamu wote. Angalia Maana ya Maneno.

Ezekieli 32:22

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “eko.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Isa 37:36; Zek 10:11

Ezekieli 32:23

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “kaburi.”

Ezekieli 32:24

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “eko.”

  • *

    Ao “kaburi.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Mwa 10:22; Yer 49:34, 35

Ezekieli 32:25

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “kaburi.”

Ezekieli 32:26

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “vyake.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Mwa 10:2; Eze 38:2

Ezekieli 32:27

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “Sheoli,” ni kusema, kaburi la wanadamu wote. Angalia Maana ya Maneno.

  • *

    Pengine ni wapiganaji-vita wenye walizikwa wakiwa na upanga wao, kwa heshima za kijeshi.

Ezekieli 32:29

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “eko.”

  • *

    Ao “kaburi.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Mwa 25:30; Isa 34:5; Eze 25:12, 13; Amo 1:11; Oba 1; Mal 1:4
  • +Yer 9:25, 26

Ezekieli 32:30

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “Viongozi.”

  • *

    Ao “kaburi.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Mwa 10:15; Eze 28:21

Ezekieli 32:31

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Eze 31:16

Maandiko ingine

Eze. 32:2Isa 51:9, 10; Eze 29:3
Eze. 32:4Eze 29:5
Eze. 32:5Eze 31:12
Eze. 32:7Isa 13:1, 10
Eze. 32:9Eze 29:12; 30:26
Eze. 32:11Yer 43:10, 11; 46:25, 26; Eze 30:24
Eze. 32:12Eze 30:10, 11; Hab 1:6
Eze. 32:12Eze 29:19
Eze. 32:13Eze 30:12
Eze. 32:13Eze 29:8, 11
Eze. 32:15Zab 107:33, 34; Eze 29:12
Eze. 32:15Eze 30:26
Eze. 32:20Eze 29:8
Eze. 32:22Isa 37:36; Zek 10:11
Eze. 32:24Mwa 10:22; Yer 49:34, 35
Eze. 32:26Mwa 10:2; Eze 38:2
Eze. 32:29Mwa 25:30; Isa 34:5; Eze 25:12, 13; Amo 1:11; Oba 1; Mal 1:4
Eze. 32:29Yer 9:25, 26
Eze. 32:30Mwa 10:15; Eze 28:21
Eze. 32:31Eze 31:16
  • Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
  • 22
  • 23
  • 24
  • 25
  • 26
  • 27
  • 28
  • 29
  • 30
  • 31
  • 32
Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
Ezekieli 32:1-32

Ezekieli

32 Na katika mwaka wa kumi na mbili (12), mwezi wa kumi na mbili, siku ya kwanza ya mwezi huo, neno la Yehova likakuja tena kwangu, na kusema: 2 “Mwana wa binadamu, imba wimbo wa huzuni* kuhusu Farao mufalme wa Misri, na umuambie,

‘Ulikuwa kama mwana-simba* mwenye nguvu wa mataifa,

Lakini umenyamazishwa.

Ulikuwa kama munyama mukubwa wa bahari,+ ukijigeuza-geuza katika mito yako,

Ukivuruga maji kwa miguu yako na kuchafua mito.’*

 3 Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema hivi:

‘Kupitia mukusanyiko wa mataifa mengi nitatupa wavu wangu* juu yako,

Nao watakukokota katika wavu wangu wa kukokotwa.

 4 Nitakuacha juu ya inchi;

Nitakutupa katika eneo lenye kuwa wazi la mashamba.

Nitafanya ndege wote wa anga watue juu yako,

Na nitashibisha wanyama wa pori wa dunia yote kwa nyama yako.+

 5 Nitatupa nyama yako juu ya milima

Na kujaza mabonde kwa masalio yako.+

 6 Nitalowanisha inchi kwa damu yako yenye kutiririka mupaka juu ya milima,

Na itajaza mito ya kidogo.’*

 7 ‘Na wakati utazimwa nitafunika mbingu na kutia giza nyota zake.

Nitafunika jua kwa mawingu,

Na mwezi hautatoa mwangaza wake.+

 8 Nitatia giza vitu vyote vya kutoa mwangaza vyenye kungaa katika mbingu kwa sababu yako,

Na nitafunika inchi yako kwa giza,’ ni vile Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema.

 9 ‘Nitaletea taabu mioyo ya vikundi vingi vya watu wakati nitapeleka watu wako wenye walikamatwa mateka katika mataifa mengine

Katika inchi zenye haukujua.+

10 Nitafanya vikundi vingi vya watu viingiwe na woga,

Nao wafalme wao watatetemeka kwa woga mukubwa kwa sababu yako wakati nitatikisa upanga wangu mbele yao.

Wataendelea kutetemeka, kila mumoja akiogopea uzima wake,

Katika siku yenye utaanguka.’

11 Kwa maana Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema hivi:

‘Upanga wa mufalme wa Babiloni utakuja juu yako.+

12 Nitafanya vikundi vyako vya watu vianguke kwa panga za wapiganaji-vita wenye nguvu,

Wenye hawana huruma kabisa kati ya mataifa, hao wote.+

Watashusha kiburi cha Misri, na vikundi vyake vyote vya watu vitaharibiwa.+

13 Nitaharibu mifugo yake yote pembeni ya maji yake mengi,+

Na hakuna muguu wa mwanadamu ao kwato* ya mifugo yenye itayatia matope tena.’+

14 ‘Wakati huo nitasafisha maji yao,

Na nitafanya mito yao itiririke kama mafuta,’ ni vile Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema.

15 ‘Wakati nitafanya inchi ya Misri kuwa eneo lenye kuwa ukiwa, inchi yenye imeondolewa vitu vyenye viliijaza,+

Wakati nitapiga na kuua wakaaji wote wenye kuwa ndani yake,

Watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.+

16 Huu ni wimbo wa huzuni, na hakika watu watauimba;

Mabinti wa mataifa watauimba.

Watauimbia inchi ya Misri na vikundi vyake vyote vya watu,’ ni vile Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema.”

17 Kisha katika mwaka wa kumi na mbili (12), siku ya kumi na tano (15) ya mwezi huo, neno la Yehova likakuja kwangu, na kusema: 18 “Mwana wa binadamu, ombolezea vikundi vya watu vya Misri na umushushe kwenye inchi ya chini, yeye na mabinti wa mataifa yenye nguvu, pamoja na wale wenye kushuka katika shimo.*

19 “‘Unamupita nani kwa uzuri? Shuka chini, na ulale pamoja na watu wenye hawatahiriwe!’

20 “‘Wataanguka kati ya wale wenye waliuawa kwa upanga.+ Ametolewa auawe kwa upanga; mumukokote mbali pamoja na vikundi vyake vyote vya watu.

21 “‘Kutoka katika sehemu za chini kabisa za Kaburi* wapiganaji-vita wenye nguvu zaidi watazungumuza naye na wasaidizi wake. Hakika watashuka chini na kulala kama vile watu wenye hawatahiriwe, wenye waliuawa kwa upanga. 22 Ashuru iko* kule pamoja na mukusanyiko wake wote. Makaburi yao yamemuzunguka pande zote, wote wameanguka kwa upanga.+ 23 Makaburi yake yako katika sehemu za chini kabisa za shimo,* na mukusanyiko wake umezunguka kaburi lake pande zote, wote wamepigwa na kuuawa kwa upanga, kwa sababu walileta woga mukubwa katika inchi ya wazima.

24 “‘Elamu+ iko* kule pamoja na vikundi vyake vyote vya watu kuzunguka kaburi lake, wote walianguka kwa upanga. Wameshuka chini kwenye inchi ya watu wenye hawatahiriwe, wale wenye walileta woga mukubwa katika inchi ya wazima. Sasa watapata haya yao pamoja na wale wenye kushuka katika shimo.* 25 Wamemutengenezea kitanda kati ya watu wenye waliuawa, pamoja na vikundi vyake vyote vya watu kuzunguka makaburi yake. Wote hawatahiriwe, waliuawa kwa upanga, kwa sababu walileta woga mukubwa katika inchi ya wazima; na watapata haya yao pamoja na wale wenye kushuka katika shimo.* Ametiwa kati ya wale wenye waliuawa.

26 “‘Mesheki na Tubali+ na vikundi vyao* vyote vya watu wako kule. Makaburi yao yamemuzunguka pande zote. Wote hawatahiriwe, wametobolewa kwa upanga, kwa sababu walileta woga mukubwa katika inchi ya wazima. 27 Je, hawatalala pamoja na wapiganaji-vita wenye nguvu wenye hawatahiriwe, na wenye wameanguka na kushuka katika Kaburi* wakiwa na silaha zao za vita? Nao watatia panga zao chini ya vichwa vyao* na zambi zao kwenye mifupa yao, kwa sababu hawa wapiganaji-vita wenye nguvu waliogopesha sana inchi ya wazima. 28 Lakini wewe, utavunjwa kati ya watu wenye hawatahiriwe, na utalala pamoja na wale wenye waliuawa kwa upanga.

29 “‘Edomu+ iko* kule, wafalme wake na wakubwa wake wote, wenye ijapokuwa walikuwa wenye nguvu, walilalishwa kati ya wale wenye waliuawa kwa upanga; wao pia watalala pamoja na watu wenye hawatahiriwe+ na pamoja na wale wenye kushuka katika shimo.*

30 “‘Wakubwa* wote wa kaskazini wako kule, pamoja na Wasidoni wote,+ wenye wameshuka wakiwa wamepatishwa haya pamoja na wenye waliuawa, hata kama walileta woga mukubwa kwa nguvu zao. Watalala wakiwa hawatahiriwe pamoja na wale wenye waliuawa kwa upanga na watapata haya yao pamoja na wale wenye kushuka katika shimo.*

31 “‘Farao ataona hao wote, na atafarijiwa kuhusu mambo yote yenye yalifikia vikundi vyake vya watu;+ Farao na jeshi lake lote watauawa kwa upanga,’ ni vile Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema.

32 “‘Kwa sababu alileta woga mukubwa katika inchi ya wazima, Farao na vikundi vyake vyote vya watu watalalishwa ili wapumuzike pamoja na watu wenye hawatahiriwe, pamoja na wale wenye waliuawa kwa upanga,’ ni vile Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema.”

Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili (Congo)
  • Tumia Wengine
  • Préférences
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Kanuni za Matumizi
  • Kanuni za Kutunza Siri
  • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
  • JW.ORG
  • Ingia
Tumia Wengine