Ezekieli
32 Na katika mwaka wa kumi na mbili (12), mwezi wa kumi na mbili, siku ya kwanza ya mwezi huo, neno la Yehova likakuja tena kwangu, na kusema: 2 “Mwana wa binadamu, imba wimbo wa huzuni* kuhusu Farao mufalme wa Misri, na umuambie,
‘Ulikuwa kama mwana-simba* mwenye nguvu wa mataifa,
Lakini umenyamazishwa.
Ulikuwa kama munyama mukubwa wa bahari,+ ukijigeuza-geuza katika mito yako,
Ukivuruga maji kwa miguu yako na kuchafua mito.’*
3 Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema hivi:
‘Kupitia mukusanyiko wa mataifa mengi nitatupa wavu wangu* juu yako,
Nao watakukokota katika wavu wangu wa kukokotwa.
4 Nitakuacha juu ya inchi;
Nitakutupa katika eneo lenye kuwa wazi la mashamba.
Nitafanya ndege wote wa anga watue juu yako,
Na nitashibisha wanyama wa pori wa dunia yote kwa nyama yako.+
5 Nitatupa nyama yako juu ya milima
Na kujaza mabonde kwa masalio yako.+
6 Nitalowanisha inchi kwa damu yako yenye kutiririka mupaka juu ya milima,
Na itajaza mito ya kidogo.’*
7 ‘Na wakati utazimwa nitafunika mbingu na kutia giza nyota zake.
Nitafunika jua kwa mawingu,
Na mwezi hautatoa mwangaza wake.+
8 Nitatia giza vitu vyote vya kutoa mwangaza vyenye kungaa katika mbingu kwa sababu yako,
Na nitafunika inchi yako kwa giza,’ ni vile Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema.
9 ‘Nitaletea taabu mioyo ya vikundi vingi vya watu wakati nitapeleka watu wako wenye walikamatwa mateka katika mataifa mengine
Katika inchi zenye haukujua.+
10 Nitafanya vikundi vingi vya watu viingiwe na woga,
Nao wafalme wao watatetemeka kwa woga mukubwa kwa sababu yako wakati nitatikisa upanga wangu mbele yao.
Wataendelea kutetemeka, kila mumoja akiogopea uzima wake,
Katika siku yenye utaanguka.’
11 Kwa maana Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema hivi:
‘Upanga wa mufalme wa Babiloni utakuja juu yako.+
12 Nitafanya vikundi vyako vya watu vianguke kwa panga za wapiganaji-vita wenye nguvu,
Wenye hawana huruma kabisa kati ya mataifa, hao wote.+
Watashusha kiburi cha Misri, na vikundi vyake vyote vya watu vitaharibiwa.+
13 Nitaharibu mifugo yake yote pembeni ya maji yake mengi,+
Na hakuna muguu wa mwanadamu ao kwato* ya mifugo yenye itayatia matope tena.’+
14 ‘Wakati huo nitasafisha maji yao,
Na nitafanya mito yao itiririke kama mafuta,’ ni vile Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema.
15 ‘Wakati nitafanya inchi ya Misri kuwa eneo lenye kuwa ukiwa, inchi yenye imeondolewa vitu vyenye viliijaza,+
Wakati nitapiga na kuua wakaaji wote wenye kuwa ndani yake,
Watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.+
16 Huu ni wimbo wa huzuni, na hakika watu watauimba;
Mabinti wa mataifa watauimba.
Watauimbia inchi ya Misri na vikundi vyake vyote vya watu,’ ni vile Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema.”
17 Kisha katika mwaka wa kumi na mbili (12), siku ya kumi na tano (15) ya mwezi huo, neno la Yehova likakuja kwangu, na kusema: 18 “Mwana wa binadamu, ombolezea vikundi vya watu vya Misri na umushushe kwenye inchi ya chini, yeye na mabinti wa mataifa yenye nguvu, pamoja na wale wenye kushuka katika shimo.*
19 “‘Unamupita nani kwa uzuri? Shuka chini, na ulale pamoja na watu wenye hawatahiriwe!’
20 “‘Wataanguka kati ya wale wenye waliuawa kwa upanga.+ Ametolewa auawe kwa upanga; mumukokote mbali pamoja na vikundi vyake vyote vya watu.
21 “‘Kutoka katika sehemu za chini kabisa za Kaburi* wapiganaji-vita wenye nguvu zaidi watazungumuza naye na wasaidizi wake. Hakika watashuka chini na kulala kama vile watu wenye hawatahiriwe, wenye waliuawa kwa upanga. 22 Ashuru iko* kule pamoja na mukusanyiko wake wote. Makaburi yao yamemuzunguka pande zote, wote wameanguka kwa upanga.+ 23 Makaburi yake yako katika sehemu za chini kabisa za shimo,* na mukusanyiko wake umezunguka kaburi lake pande zote, wote wamepigwa na kuuawa kwa upanga, kwa sababu walileta woga mukubwa katika inchi ya wazima.
24 “‘Elamu+ iko* kule pamoja na vikundi vyake vyote vya watu kuzunguka kaburi lake, wote walianguka kwa upanga. Wameshuka chini kwenye inchi ya watu wenye hawatahiriwe, wale wenye walileta woga mukubwa katika inchi ya wazima. Sasa watapata haya yao pamoja na wale wenye kushuka katika shimo.* 25 Wamemutengenezea kitanda kati ya watu wenye waliuawa, pamoja na vikundi vyake vyote vya watu kuzunguka makaburi yake. Wote hawatahiriwe, waliuawa kwa upanga, kwa sababu walileta woga mukubwa katika inchi ya wazima; na watapata haya yao pamoja na wale wenye kushuka katika shimo.* Ametiwa kati ya wale wenye waliuawa.
26 “‘Mesheki na Tubali+ na vikundi vyao* vyote vya watu wako kule. Makaburi yao yamemuzunguka pande zote. Wote hawatahiriwe, wametobolewa kwa upanga, kwa sababu walileta woga mukubwa katika inchi ya wazima. 27 Je, hawatalala pamoja na wapiganaji-vita wenye nguvu wenye hawatahiriwe, na wenye wameanguka na kushuka katika Kaburi* wakiwa na silaha zao za vita? Nao watatia panga zao chini ya vichwa vyao* na zambi zao kwenye mifupa yao, kwa sababu hawa wapiganaji-vita wenye nguvu waliogopesha sana inchi ya wazima. 28 Lakini wewe, utavunjwa kati ya watu wenye hawatahiriwe, na utalala pamoja na wale wenye waliuawa kwa upanga.
29 “‘Edomu+ iko* kule, wafalme wake na wakubwa wake wote, wenye ijapokuwa walikuwa wenye nguvu, walilalishwa kati ya wale wenye waliuawa kwa upanga; wao pia watalala pamoja na watu wenye hawatahiriwe+ na pamoja na wale wenye kushuka katika shimo.*
30 “‘Wakubwa* wote wa kaskazini wako kule, pamoja na Wasidoni wote,+ wenye wameshuka wakiwa wamepatishwa haya pamoja na wenye waliuawa, hata kama walileta woga mukubwa kwa nguvu zao. Watalala wakiwa hawatahiriwe pamoja na wale wenye waliuawa kwa upanga na watapata haya yao pamoja na wale wenye kushuka katika shimo.*
31 “‘Farao ataona hao wote, na atafarijiwa kuhusu mambo yote yenye yalifikia vikundi vyake vya watu;+ Farao na jeshi lake lote watauawa kwa upanga,’ ni vile Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema.
32 “‘Kwa sababu alileta woga mukubwa katika inchi ya wazima, Farao na vikundi vyake vyote vya watu watalalishwa ili wapumuzike pamoja na watu wenye hawatahiriwe, pamoja na wale wenye waliuawa kwa upanga,’ ni vile Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema.”