Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • Ezekieli 26
  • Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

Habari Zenye Kuwa Katika Ezekieli

      • Unabii juu ya Tiro (1-21)

        • “Kiwanja cha kukaushia nyavu za kukokotwa” (5, 14)

        • Majiwe na udongo vinatupwa ndani ya maji (12)

Ezekieli 26:2

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Yoe 3:4-6; Amo 1:9
  • +Omb 1:1

Ezekieli 26:3

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    “Kila Andiko,” uku. 133

Ezekieli 26:4

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Isa 23:11; Amo 1:10; Zek 9:4

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    “Kila Andiko,” uku. 133

Ezekieli 26:5

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “makila ya.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Eze 27:32

Ezekieli 26:6

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “mabinti wake wenye.”

Ezekieli 26:7

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “Nebukadreza,” njia ingine ya kuandika jina hili.

  • *

    Tnn., “watu wengi.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Yer 25:9; Eze 29:18
  • +Da. 2:37
  • +Hab 1:8
  • +Yer 4:13

Ezekieli 26:9

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “mashine yake ya kushambulia.”

  • *

    Ao “panga.”

Ezekieli 26:10

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “mipeto; pneus.”

Ezekieli 26:11

Maelezo ya Chini

  • *

    Kwato ni sehemu ngumu ya chini ya muguu wa munyama.

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Isa 5:28; Hab 1:8

Ezekieli 26:12

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Eze 27:32, 33; 28:5, 18; Zek 9:3

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Munara wa Mulinzi,

    1/1/2008, uku. 23

    “Kila Andiko,” uku. 133

Ezekieli 26:13

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Isa 23:16

Ezekieli 26:14

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “makila ya.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Eze 26:4, 5

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    “Kila Andiko,” uku. 133

Ezekieli 26:15

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “wenye kuuawa.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Eze 27:28

Ezekieli 26:16

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “koti zao zenye hazina mikono.”

  • *

    Tnn., “watavikwa.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Eze 27:35; 32:10

Ezekieli 26:17

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “wimbo wa maombolezo.”

  • *

    Tnn., “Yeye na wakaaji wake.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Eze 27:32
  • +Amo 1:9, 10
  • +Eze 28:2

Ezekieli 26:18

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Isa 23:5

Ezekieli 26:19

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Eze 27:34

Ezekieli 26:20

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “kaburi.”

  • *

    Ao “nitapamba.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Eze 28:8

Ezekieli 26:21

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Eze 27:36

Maandiko ingine

Eze. 26:2Yoe 3:4-6; Amo 1:9
Eze. 26:2Omb 1:1
Eze. 26:4Isa 23:11; Amo 1:10; Zek 9:4
Eze. 26:5Eze 27:32
Eze. 26:7Yer 25:9; Eze 29:18
Eze. 26:7Da. 2:37
Eze. 26:7Hab 1:8
Eze. 26:7Yer 4:13
Eze. 26:11Isa 5:28; Hab 1:8
Eze. 26:12Eze 27:32, 33; 28:5, 18; Zek 9:3
Eze. 26:13Isa 23:16
Eze. 26:14Eze 26:4, 5
Eze. 26:15Eze 27:28
Eze. 26:16Eze 27:35; 32:10
Eze. 26:17Eze 27:32
Eze. 26:17Amo 1:9, 10
Eze. 26:17Eze 28:2
Eze. 26:18Isa 23:5
Eze. 26:19Eze 27:34
Eze. 26:20Eze 28:8
Eze. 26:21Eze 27:36
  • Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
Ezekieli 26:1-21

Ezekieli

26 Katika mwaka wa kumi na moja (11), siku ya kwanza ya mwezi, neno la Yehova lilikuja kwangu, na kusema: 2 “Mwana wa binadamu, kwa sababu Tiro amesema kuhusu Yerusalemu,+ ‘Aha! Muingilio wa vikundi vya watu umevunjwa!+ Kila kitu kitakuja kwangu, na nitakuwa tajiri kwa sababu ameharibiwa’; 3 kwa hiyo, Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema hivi: ‘Angalia, niko juu yako, Ee Tiro, na nitainua mataifa mengi ili yakushambulie, kama vile bahari inainua mawimbi yake. 4 Wataharibu kuta za Tiro na kubomoa minara yake,+ na nitapalula udongo na kumufanya kuwa mwamba wenye kungaa, wenye kuwa wazi. 5 Atakuwa kiwanja cha kukaushia nyavu za* kukokotwa katikati ya bahari.’+

“‘Kwa maana mimi mwenyewe nimesema,’ ni vile Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema, ‘na atakuwa kitu cha kunyanganywa na mataifa. 6 Na makao yake yenye* kuwa katika eneo la mashamba yatachinjwa kwa upanga, na watu watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.’

7 “Kwa maana Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema hivi: ‘Angalia, ninamuleta Mufalme Nebukadneza* wa Babiloni ili ashambulie Tiro kutoka kaskazini;+ yeye ni mufalme wa wafalme,+ akiwa na farasi,+ magari ya vita,+ wapanda-farasi, na jeshi la maaskari wengi.* 8 Ataharibu kwa upanga makao yako yenye kuwa katika eneo la mashamba, na atajenga ukuta wa kuzunguka kwa ajili ya vita na kusimamisha juu yako boma la kuzunguka kwa ajili ya vita na kuinua ngao kubwa juu yako. 9 Atabomoa kuta zako kwa chombo chake cha kubomolea,* na atabomoa minara yako kwa shoka* zake. 10 Farasi zake watakuwa wengi sana kiasi ya kwamba watakufunika kwa mavumbi, na sauti ya wapanda farasi, magurudumu,* na magari itafanya kuta zako zitikisike wakati ataingia katika milango yako mikubwa, kama vile wanaume wenye kushambulia muji wenye kuta zenye kubomolewa. 11 Kwato* za farasi wake zitakanyanga-kanyanga barabara zako zote;+ ataua watu wako kwa upanga, na nguzo zako zenye nguvu zitaanguka chini. 12 Watanyanganya mali zako, watanyanganya vitu vyako vya biashara,+ watabomoa kuta zako, na watabomoa nyumba zako za muzuri; kisha watatupa majiwe yako na mbao zako na udongo wako katika maji.’

13 “‘Nitanyamazisha makelele ya nyimbo zako, na sauti ya vinubi vyako haitasikiwa tena.+ 14 Na nitakufanya kuwa jiwe lenye kungaa, lenye kuwa wazi, na utakuwa kiwanja cha kukaushia nyavu za* kukokotwa.+ Hakuna siku utajengwa tena, kwa maana mimi mwenyewe, Yehova, nimesema,’ ni vile Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema.

15 “Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anamuambia Tiro hivi: ‘Wakati sauti ya kuanguka kwako itasikika, wakati watu wenye kukaribia kufa* watakuwa wanalia kwa maumivu, wakati kutakuwa uchinjaji katikati yako, je, visiwa havitatetemeka?+ 16 Wakubwa wote wa bahari watashuka kutoka kwenye viti vyao vya ufalme na kutosha kanzu zao* na kuvua nguo zao zenye michoro ya uzi imeshonewa juu yake, na watashikwa na* mutetemeko. Watakaa chini na kuendelea kutetemeka na kukuangalia kwa mushangao.+ 17 Nao watakuimbia wimbo wa huzuni*+ na kukuambia:

“‘“Namna umeangamia,+ wewe mwenye ulikuwa na wakaaji kutoka katika bahari, muji wenye ulisifiwa;

Wewe na wakaaji wako* mulikuwa wenye nguvu kwenye bahari,+

Mulieneza woga mukubwa kwa wakaaji wote wa dunia!

18 Visiwa vitatetemeka siku yenye utaanguka.

Visiwa vya bahari vitavurugika wakati hautakuwa tena.”’+

19 “Kwa maana Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema hivi: ‘Wakati nitakuharibu kama vile miji yenye haikaliwe, wakati nitakulemea kwa maji yenye mawimbi makubwa na maji yenye nguvu yakuwe yamekufunika,+ 20 nitakushusha wewe na wale wenye kushuka katika shimo* pamoja na wewe kwa watu wa zamani sana; nitakufanya ukae mahali pa chini sana, kama vile mahali pa zamani penye paliharibiwa, pamoja na wale wenye kushuka katika shimo,+ ili usiikaliwe. Kisha nitatukuza* inchi ya wazima.

21 “‘Nitaleta woga mukubwa wa kushitukia juu yako, na hautakuwa tena.+ Watakutafuta, lakini hautapatikana tena hata kidogo,’ ni vile Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema.”

Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili (Congo)
  • Tumia Wengine
  • Préférences
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Kanuni za Matumizi
  • Kanuni za Kutunza Siri
  • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
  • JW.ORG
  • Ingia
Tumia Wengine