Ezekieli
47 Kisha akanirudisha kwenye muingilio wa hekalu,+ na kule nikaona maji yakitiririka kuelekea mashariki kutoka chini ya kizingiti* cha hekalu,+ kwa maana upande wa mbele wa hekalu ulielekea mashariki. Maji hayo yalikuwa yanatiririka kutoka chini, upande wa kuume wa hekalu, kusini mwa mazabahu.
2 Kisha akanipeleka inje kupitia mulango mukubwa wa kaskazini+ na akanipeleka inje na kuzunguka mupaka kwenye mulango mukubwa wa inje wenye kuelekea mashariki,+ na kule nikaona maji yakitiririka kutoka upande wa kuume.
3 Wakati mutu huyo alienda inje kuelekea mashariki akiwa na kamba ya kupimia katika mukono wake,+ alipima mikono* elfu moja (1 000) na akanipitisha katika maji; maji hayo yalifika kwenye kifundo cha muguu.
4 Kisha akapima mikono ingine elfu moja (1 000) na akanipitisha katika maji, na maji hayo yakafika mupaka kwenye magoti.
Naye akapima mikono ingine elfu moja na akanipitisha ndani, na maji hayo yakafika kwenye kiuno.
5 Wakati alipima mikono ingine elfu moja (1 000), maji yalikuwa mengi sana kiasi ya kwamba sikuweza kuvuka, kwa maana maji yalikuwa marefu sana kuenda chini na hivyo mutu alilazimika kuogelea, maji mengi yenye mutu hangeweza kuvuka kwa miguu.
6 Akaniuliza: “Mwana wa binadamu, je, umeona jambo hili?”
Kisha akanitembeza na kunirudisha pembeni ya muto mudogo. 7 Wakati nilirudia, nikaona kwamba pembeni ya muto mudogo kulikuwa miti mingi sana kwenye pande zote mbili.+ 8 Halafu akaniambia: “Maji haya yanatiririka kuelekea eneo la mashariki na yanashuka kupitia Araba*+ na kuingia katika bahari. Wakati yataingia katika bahari,+ maji ya bahari yataponyeshwa. 9 Makundi makubwa ya viumbe vyenye uzima yataweza* kuishi kila mahali kwenye maji hayo yanatiririka. Kutakuwa samaki wengi, kwa sababu maji hayo yatatiririka* kule. Maji ya bahari yataponyeshwa, na kila kitu kitaishi mahali kwenye muto huo mudogo unapita.
10 “Wavuvi wa samaki watasimama pembeni yake kutoka En-gedi+ mupaka En-eglaimu, kwenye kutakuwa kiwanja cha kukaushia nyavu za* kukokotwa. Kutakuwa samaki wengi wa aina nyingi, kama samaki wa Bahari Kubwa.*+
11 “Kutakuwa sehemu zenye majimaji na sehemu za tingitingi, na sehemu hizo hazitaponyeshwa. Hakika zitabakia za chumvi.+
12 “Aina zote za miti ya chakula zitakuwa kwenye pande zote mbili za pembeni ya muto huo mudogo. Majani yake hayatakauka; wala matunda yake hayataisha. Kila mwezi itazaa matunda ya mupya, kwa sababu maji yake yanatiririka kutoka patakatifu.+ Matunda yake yatakuwa chakula na majani yake yatakuwa ya kuponyesha.”+
13 Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema hivi: “Hili ndilo eneo lenye mutagawa kuwa uriti wa inchi wa yale makabila kumi na mbili (12) ya Israeli, na Yosefu atapata sehemu mbili.+ 14 Mutairiti na kupata mafungu sawasawa.* Niliapa kwamba nitapatia mababu zenu inchi hii,+ na sasa mumegawiwa inchi hiyo* kuwa uriti wenu.
15 “Huu ndio mupaka wa inchi upande wa kaskazini: Unaanzia kwenye Bahari Kubwa kupitia njia ya Hetloni+ kuelekea Sedadi,+ 16 Hamati,+ Berota,+ na Sibraimu, yenye kuwa kati ya eneo la Damasko na eneo la Hamati, kufikia Haser-hatikoni, yenye kuwa kwenye mupaka wa Haurani.+ 17 Kwa hiyo mupaka utaanzia kwenye bahari kufikia Hasar-enoni,+ kwenye mupaka wa Damasko kuelekea kaskazini, na mupaka wa Hamati.+ Huo ndio mupaka wa kaskazini.
18 “Upande wa mashariki unapita kati ya Haurani na Damasko na pembeni-pembeni ya Yordani kati ya Gileadi+ na inchi ya Israeli. Mutapima kuanzia kwenye mupaka kufikia kwenye bahari ya mashariki.* Huo ndio mupaka wa mashariki.
19 “Mupaka wa kusini* utaanzia Tamari kufikia kwenye maji ya Meribat-kadeshi,+ kisha utaelekea kwenye Bonde la Muto* kufikia kwenye ile Bahari Kubwa.+ Huo ndio mupaka wa kusini.*
20 “Bahari Kubwa iko upande wa mangaribi, kuanzia kwenye mupaka kufikia kwenye nafasi yenye kuangaliana na Lebo-hamati.*+ Huo ndio mupaka wa mangaribi.”
21 “Mutagawanya inchi hii kati yenu, kati ya yale makabila kumi na mbili (12) ya Israeli. 22 Mutaigawanya kuwa uriti kati yenu wenyewe na kwa wageni wenye wanaishi pamoja na ninyi wenye wamepata watoto wakati walikuwa wanaishi kati yenu; watakuwa kwenu kama Waisraeli wenyeji wa kizalikio. Watapewa uriti kati ya makabila ya Israeli pamoja na ninyi. 23 Mutamupatia mugeni uriti katika eneo la kabila kwenye anaishi,” ni vile Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema.