Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • Ezekieli 47
  • Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

Habari Zenye Kuwa Katika Ezekieli

      • Muto mudogo wenye unatiririka kutoka katika hekalu (1-12)

        • Urefu wa maji kuenda chini unaongezeka pole kwa pole (2-5)

        • Maji ya Bahari ya Chumvi yanaponyeshwa (8-10)

        • Sehemu zenye majimaji haziponyeshwe (11)

        • Miti kwa ajili ya chakula na kuponyesha (12)

      • Mipaka ya inchi (13-23)

Ezekieli 47:1

Maelezo ya Chini

  • *

    Hapa kizingiti ni ubao wenye kuwa chini ya mulango.

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Eze 41:2
  • +Zek 13:1; 14:8; Ufu 22:1

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Munara wa Mulinzi (2007 ),

    1/8/2007, uku. 11

Ezekieli 47:2

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Eze 40:20
  • +Eze 40:6; 44:1, 2

Ezekieli 47:3

Maelezo ya Chini

  • *

    Inamaanisha mikono mirefu. Angalia Nyongeza B14.

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Eze 40:3; Ufu 21:15

Ezekieli 47:7

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Ufu 22:1, 2

Ezekieli 47:8

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “jangwa tambarare.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Kum 4:47, 49
  • +Zek 14:8

Ezekieli 47:9

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “nafsi zenye zitaweza.”

  • *

    Tnn., “mito mbili midogo-midogo inatiririka.”

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Munara wa Mulinzi (2007 ),

    1/8/2007, uku. 11

Ezekieli 47:10

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “makila ya.”

  • *

    Ni kusema, Bahari ya Mediterania.

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Yosh. 15:20, 62; 2Nya 20:2
  • +Hes 34:2, 6

Ezekieli 47:11

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Kum 29:22, 23; Zab 107:33, 34; Yer 17:6

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Munara wa Mulinzi (2007 ),

    1/8/2007, uku. 11

Ezekieli 47:12

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Eze 47:1
  • +Ufu 22:1, 2

Endekse

  • Musaada wa Kutafuta Habari

    Munara wa Mulinzi (2007 ),

    1/8/2007, uku. 11

Ezekieli 47:13

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Mwa 48:5; 1Nya 5:1; Eze 48:5

Ezekieli 47:14

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “mutairiti, kila mutu kama ndugu yake.”

  • *

    Tnn., “inawaangukia.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Mwa 26:3; 28:13

Ezekieli 47:15

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Eze 48:1
  • +Hes 34:2, 8

Ezekieli 47:16

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Hes 13:21
  • +2 Sa. 8:8
  • +Eze 47:18

Ezekieli 47:17

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Hes 34:2, 9
  • +Eze 48:1

Ezekieli 47:18

Maelezo ya Chini

  • *

    Ni kusema, Bahari Yenye Kufa.

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Hes 32:1

Ezekieli 47:19

Maelezo ya Chini

  • *

    Tnn., “Upande wa kusini kuelekea kusini.”

  • *

    Ni kusema, Bonde la Muto la Misri.

  • *

    Tnn., “upande wa kusini kuelekea kusini.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Kum 32:51
  • +Eze 48:28

Ezekieli 47:20

Maelezo ya Chini

  • *

    Ao “muingilio wa Hamati.”

Maelezo Ingine Juu ya Hii Andiko

  • +Hes 34:2, 8

Maandiko ingine

Eze. 47:1Eze 41:2
Eze. 47:1Zek 13:1; 14:8; Ufu 22:1
Eze. 47:2Eze 40:20
Eze. 47:2Eze 40:6; 44:1, 2
Eze. 47:3Eze 40:3; Ufu 21:15
Eze. 47:7Ufu 22:1, 2
Eze. 47:8Kum 4:47, 49
Eze. 47:8Zek 14:8
Eze. 47:10Yosh. 15:20, 62; 2Nya 20:2
Eze. 47:10Hes 34:2, 6
Eze. 47:11Kum 29:22, 23; Zab 107:33, 34; Yer 17:6
Eze. 47:12Eze 47:1
Eze. 47:12Ufu 22:1, 2
Eze. 47:13Mwa 48:5; 1Nya 5:1; Eze 48:5
Eze. 47:14Mwa 26:3; 28:13
Eze. 47:15Eze 48:1
Eze. 47:15Hes 34:2, 8
Eze. 47:16Hes 13:21
Eze. 47:162 Sa. 8:8
Eze. 47:16Eze 47:18
Eze. 47:17Hes 34:2, 9
Eze. 47:17Eze 48:1
Eze. 47:18Hes 32:1
Eze. 47:19Kum 32:51
Eze. 47:19Eze 48:28
Eze. 47:20Hes 34:2, 8
  • Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
  • 1
  • 2
  • 3
  • 4
  • 5
  • 6
  • 7
  • 8
  • 9
  • 10
  • 11
  • 12
  • 13
  • 14
  • 15
  • 16
  • 17
  • 18
  • 19
  • 20
  • 21
  • 22
  • 23
Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
Ezekieli 47:1-23

Ezekieli

47 Kisha akanirudisha kwenye muingilio wa hekalu,+ na kule nikaona maji yakitiririka kuelekea mashariki kutoka chini ya kizingiti* cha hekalu,+ kwa maana upande wa mbele wa hekalu ulielekea mashariki. Maji hayo yalikuwa yanatiririka kutoka chini, upande wa kuume wa hekalu, kusini mwa mazabahu.

2 Kisha akanipeleka inje kupitia mulango mukubwa wa kaskazini+ na akanipeleka inje na kuzunguka mupaka kwenye mulango mukubwa wa inje wenye kuelekea mashariki,+ na kule nikaona maji yakitiririka kutoka upande wa kuume.

3 Wakati mutu huyo alienda inje kuelekea mashariki akiwa na kamba ya kupimia katika mukono wake,+ alipima mikono* elfu moja (1 000) na akanipitisha katika maji; maji hayo yalifika kwenye kifundo cha muguu.

4 Kisha akapima mikono ingine elfu moja (1 000) na akanipitisha katika maji, na maji hayo yakafika mupaka kwenye magoti.

Naye akapima mikono ingine elfu moja na akanipitisha ndani, na maji hayo yakafika kwenye kiuno.

5 Wakati alipima mikono ingine elfu moja (1 000), maji yalikuwa mengi sana kiasi ya kwamba sikuweza kuvuka, kwa maana maji yalikuwa marefu sana kuenda chini na hivyo mutu alilazimika kuogelea, maji mengi yenye mutu hangeweza kuvuka kwa miguu.

6 Akaniuliza: “Mwana wa binadamu, je, umeona jambo hili?”

Kisha akanitembeza na kunirudisha pembeni ya muto mudogo. 7 Wakati nilirudia, nikaona kwamba pembeni ya muto mudogo kulikuwa miti mingi sana kwenye pande zote mbili.+ 8 Halafu akaniambia: “Maji haya yanatiririka kuelekea eneo la mashariki na yanashuka kupitia Araba*+ na kuingia katika bahari. Wakati yataingia katika bahari,+ maji ya bahari yataponyeshwa. 9 Makundi makubwa ya viumbe vyenye uzima yataweza* kuishi kila mahali kwenye maji hayo yanatiririka. Kutakuwa samaki wengi, kwa sababu maji hayo yatatiririka* kule. Maji ya bahari yataponyeshwa, na kila kitu kitaishi mahali kwenye muto huo mudogo unapita.

10 “Wavuvi wa samaki watasimama pembeni yake kutoka En-gedi+ mupaka En-eglaimu, kwenye kutakuwa kiwanja cha kukaushia nyavu za* kukokotwa. Kutakuwa samaki wengi wa aina nyingi, kama samaki wa Bahari Kubwa.*+

11 “Kutakuwa sehemu zenye majimaji na sehemu za tingitingi, na sehemu hizo hazitaponyeshwa. Hakika zitabakia za chumvi.+

12 “Aina zote za miti ya chakula zitakuwa kwenye pande zote mbili za pembeni ya muto huo mudogo. Majani yake hayatakauka; wala matunda yake hayataisha. Kila mwezi itazaa matunda ya mupya, kwa sababu maji yake yanatiririka kutoka patakatifu.+ Matunda yake yatakuwa chakula na majani yake yatakuwa ya kuponyesha.”+

13 Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema hivi: “Hili ndilo eneo lenye mutagawa kuwa uriti wa inchi wa yale makabila kumi na mbili (12) ya Israeli, na Yosefu atapata sehemu mbili.+ 14 Mutairiti na kupata mafungu sawasawa.* Niliapa kwamba nitapatia mababu zenu inchi hii,+ na sasa mumegawiwa inchi hiyo* kuwa uriti wenu.

15 “Huu ndio mupaka wa inchi upande wa kaskazini: Unaanzia kwenye Bahari Kubwa kupitia njia ya Hetloni+ kuelekea Sedadi,+ 16 Hamati,+ Berota,+ na Sibraimu, yenye kuwa kati ya eneo la Damasko na eneo la Hamati, kufikia Haser-hatikoni, yenye kuwa kwenye mupaka wa Haurani.+ 17 Kwa hiyo mupaka utaanzia kwenye bahari kufikia Hasar-enoni,+ kwenye mupaka wa Damasko kuelekea kaskazini, na mupaka wa Hamati.+ Huo ndio mupaka wa kaskazini.

18 “Upande wa mashariki unapita kati ya Haurani na Damasko na pembeni-pembeni ya Yordani kati ya Gileadi+ na inchi ya Israeli. Mutapima kuanzia kwenye mupaka kufikia kwenye bahari ya mashariki.* Huo ndio mupaka wa mashariki.

19 “Mupaka wa kusini* utaanzia Tamari kufikia kwenye maji ya Meribat-kadeshi,+ kisha utaelekea kwenye Bonde la Muto* kufikia kwenye ile Bahari Kubwa.+ Huo ndio mupaka wa kusini.*

20 “Bahari Kubwa iko upande wa mangaribi, kuanzia kwenye mupaka kufikia kwenye nafasi yenye kuangaliana na Lebo-hamati.*+ Huo ndio mupaka wa mangaribi.”

21 “Mutagawanya inchi hii kati yenu, kati ya yale makabila kumi na mbili (12) ya Israeli. 22 Mutaigawanya kuwa uriti kati yenu wenyewe na kwa wageni wenye wanaishi pamoja na ninyi wenye wamepata watoto wakati walikuwa wanaishi kati yenu; watakuwa kwenu kama Waisraeli wenyeji wa kizalikio. Watapewa uriti kati ya makabila ya Israeli pamoja na ninyi. 23 Mutamupatia mugeni uriti katika eneo la kabila kwenye anaishi,” ni vile Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema.

Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili (Congo)
  • Tumia Wengine
  • Préférences
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Kanuni za Matumizi
  • Kanuni za Kutunza Siri
  • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
  • JW.ORG
  • Ingia
Tumia Wengine