Ezekieli
48 “Haya ndiyo majina ya makabila hayo, kuanzia upande wa kaskazini: Sehemu ya Dani+ inapita kwenye njia ya Hetloni kufikia Lebo-hamati*+ kufikia Hasar-enani, kwenye mupaka wa Damasko kuelekea kaskazini pembeni ya Hamati;+ na inaanzia mashariki kufikia kwenye mupaka wa mangaribi. 2 Sehemu ya Asheri+ iko kwenye mupaka wa Dani, kuanzia mupaka wa mashariki kufikia kwenye mupaka wa mangaribi. 3 Sehemu ya Naftali+ iko kwenye mupaka wa Asheri, kuanzia mupaka wa mashariki kufikia kwenye mupaka wa mangaribi. 4 Sehemu ya Manase+ iko kwenye mupaka wa Naftali, kuanzia mupaka wa mashariki kufikia kwenye mupaka wa mangaribi. 5 Sehemu ya Efraimu iko kwenye mupaka wa Manase,+ kuanzia mupaka wa mashariki kufikia kwenye mupaka wa mangaribi. 6 Sehemu ya Rubeni iko kwenye mupaka wa Efraimu,+ kuanzia mupaka wa mashariki kufikia kwenye mupaka wa mangaribi. 7 Sehemu ya Yuda iko kwenye mupaka wa Rubeni,+ kuanzia mupaka wa mashariki kufikia kwenye mupaka wa mangaribi. 8 Kwenye mupaka wa Yuda, kuanzia mupaka wa mashariki kufikia kwenye mupaka wa mangaribi, muchango wenye mutatia pembeni utakuwa na upana wa mikono* elfu makumi mbili na tano (25 000)+ na utalingana na urefu wa zile sehemu za makabila mengine kuanzia mupaka wa mashariki kufikia kwenye mupaka wa mangaribi. Patakatifu patakuwa katikati yake.
9 “Muchango wenye mutatia pembeni kwa ajili ya Yehova utakuwa na urefu wa mikono elfu makumi mbili na tano (25 000) na upana wa mikono elfu kumi (10 000). 10 Huu ndio utakuwa muchango mutakatifu kwa ajili ya makuhani.+ Upande wa kaskazini utakuwa mikono elfu makumi mbili na tano (25 000), mikono elfu kumi (10 000) upande wa mangaribi, mikono elfu kumi upande wa mashariki, na mikono elfu makumi mbili na tano upande wa kusini. Patakatifu pa Yehova patakuwa katikati yake. 11 Patakuwa pa makuhani wenye kutakaswa kutoka kati ya wana wa Sadoki,+ wale wenye walifanya kazi zao mbalimbali kunielekea na hawakujiendesha mubaya wakati Waisraeli na Walawi walijiendesha mubaya.+ 12 Watakuwa na sehemu ya muchango wa inchi hiyo yenye ilitiwa pembeni ili kuwa kitu kitakatifu zaidi, kwenye mupaka wa Walawi.
13 “Karibu tu na eneo la makuhani, Walawi watakuwa na sehemu yenye urefu wa mikono elfu makumi mbili na tano (25 000), na upana wa mikono elfu kumi (10 000). (Urefu wote utakuwa mikono elfu makumi mbili na tano na upana wa mikono elfu kumi.) 14 Hawapaswe kuuzisha, kubadilisha, wala kumupatia mutu mwingine eneo lolote la sehemu hii ya muzuri sana ya inchi, kwa maana sehemu hiyo ni kitu kitakatifu kwa ajili ya Yehova.
15 “Eneo lenye linabakia lenye liko na upana wa mikono elfu tano (5 000) pembeni-pembeni ya mupaka wenye mikono elfu makumi mbili na tano (25 000), litakuwa la matumizi ya kawaida ya muji,+ kwa ajili ya makao na eneo la malisho. Muji utakuwa katikati yake.+ 16 Vipimo vya muji ni hivi: Mupaka wa kaskazini mikono elfu ine na mia tano (4 500), mupaka wa kusini mikono elfu ine na mia tano, mupaka wa mashariki mikono elfu ine na mia tano, na mupaka wa mangaribi mikono elfu ine na mia tano. 17 Eneo la malisho la muji litakuwa mikono mia mbili makumi tano (250) upande wa kaskazini, mikono mia mbili makumi tano upande wa kusini, mikono mia mbili makumi tano upande wa mashariki, na mikono mia mbili makumi tano upande wa mangaribi.
18 “Urefu wa sehemu yenye inabakia utalingana na muchango mutakatifu,+ mikono elfu kumi (10 000) upande wa mashariki na mikono elfu kumi upande wa mangaribi. Italingana na muchango mutakatifu na mazao yake yatakuwa chakula cha wale wenye wanatumikia muji. 19 Wale wenye kutumikia muji kutoka katika makabila yote ya Israeli watailima.+
20 “Muchango muzima ni mikono elfu makumi mbili na tano (25 000) kwenye kila moja ya pande zote ine (4).* Mutatia eneo hilo pembeni ili likuwe muchango mutakatifu pamoja na eneo la muji.
21 “Sehemu yenye itabakia kwenye pande mbili, upande wa muchango mutakatifu na wa eneo la muji itakuwa ya mukubwa.+ Itakuwa pembeni-pembeni ya mipaka ya mikono elfu makumi mbili na tano (25 000) yenye kuwa upande wa mashariki na mangaribi wa muchango huo. Italingana na sehemu hizo zenye kufuata, na itakuwa ya mukubwa. Muchango mutakatifu na patakatifu pa hekalu patakuwa katikati yake.
22 “Eneo la Walawi na eneo la muji litakuwa kati ya mali ya mukubwa. Eneo la mukubwa litakuwa kati ya mupaka wa Yuda+ na Benyamini.
23 “Na kuhusu makabila yenye yanabakia, sehemu ya Benyamini itaanzia kwenye mupaka wa mashariki kufikia kwenye mupaka wa mangaribi.+ 24 Sehemu ya Simeoni iko karibu na mupaka wa Benyamini,+ kuanzia mupaka wa mashariki kufikia kwenye mupaka wa mangaribi. 25 Sehemu ya Isakari+ iko karibu na mupaka wa Simeoni, kuanzia mupaka wa mashariki kufikia kwenye mupaka wa mangaribi. 26 Sehemu ya Zabuloni iko karibu na mupaka wa Isakari,+ kuanzia mupaka wa mashariki kufikia kwenye mupaka wa mangaribi.+ 27 Sehemu ya Gadi iko karibu na mupaka wa Zabuloni,+ kuanzia mupaka wa mashariki kufikia kwenye mupaka wa mangaribi. 28 Mupaka wa kusini kwenye mupaka wa Gadi utaanzia Tamari+ kufikia kwenye maji ya Meribat-kadeshi,+ utapita kwenye Bonde la Muto*+ kufikia kwenye ile Bahari Kubwa.*
29 “Hiyo ndiyo inchi yenye mutagawanya kuwa uriti kwa makabila ya Israeli,+ na hizo zitakuwa sehemu zao,”+ ni vile Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema.
30 “Hii ndiyo itakuwa milango ya kutokea ya muji: Upande wa kaskazini utakuwa na urefu wa mikono elfu ine mia tano (4 500).+
31 “Milango mikubwa ya muji itaitwa kulingana na makabila ya Israeli. Kati ya milango mikubwa tatu (3) ya kaskazini, kuko mulango mukubwa mumoja wa Rubeni, mulango mukubwa mumoja wa Yuda, na mulango mukubwa mumoja wa Lawi.
32 “Upande wa mashariki utakuwa na urefu wa mikono elfu ine mia tano (4 500), na kutakuwa milango mikubwa tatu (3): mulango mukubwa mumoja wa Yosefu, mulango mukubwa mumoja wa Benyamini, na mulango mukubwa mumoja wa Dani.
33 “Upande wa kusini utakuwa na urefu wa mikono elfu ine mia tano (4 500), na milango mikubwa tatu (3): mulango mukubwa mumoja wa Simeoni, mulango mukubwa mumoja wa Isakari, na mulango mukubwa mumoja wa Zabuloni.
34 “Upande wa mangaribi utakuwa na urefu wa mikono elfu ine mia tano (4 500), na milango mikubwa tatu (3): mulango mukubwa mumoja wa Gadi, mulango mukubwa mumoja wa Asheri, na mulango mukubwa mumoja wa Naftali.
35 “Muzunguko utakuwa mikono elfu kumi na munane (18 000). Na jina la muji huo kuanzia siku hiyo na kuendelea litakuwa, Yehova Iko* Pale.”+