Yoeli
1 Neno la Yehova lenye lilikuja kwa Yoeli* mwana wa Petueli:
2 “Musikie jambo hili, ninyi wazee,
Na mutege sikio, ninyi wakaaji wote wa inchi.*
Je, jambo kama hili limekwisha kutokea katika siku zenu
Ao katika siku za mababu zenu?+
3 Muelezee wana wenu juu ya jambo hilo,
Nao waelezee wana wao,
Na wana wao waelezee kizazi chenye kitafuata.
4 Kitu chenye kiliachwa na nzige mwenye kutafuna kila kitu, kimekuliwa na nzige mwenye kupatikana kwa wingi;+
Na kitu chenye kiliachwa na nzige mwenye kupatikana kwa wingi, kimekuliwa na nzige mwenye hana mabawa;
Na kitu chenye kiliachwa na nzige mwenye hana mabawa, kimekuliwa na nzige mwenye kula sana.+
5 Muamuke, ninyi walevi,+ na mulie!
Mulalamike, ninyi wote wenye munakunywa divai,
Kwa sababu divai tamu imeondolewa katika vinywa vyenu.+
6 Kwa maana taifa limeingia katika inchi yangu, liko na nguvu na halina hesabu.+
Meno yao ni meno ya simba,+ na mataya* yao ni ya simba.
7 Limeharibu muzabibu wangu na kuacha muti wangu wa tini ukiwa kisiki.
Limeondoa juu yake maganda yote na kuyatupa pembeni,
Limefanya matawi yake yabakie meupe.
8 Muomboleze kama bikira* mwenye kuvaa nguo za magunia
Mwenye anaomboleza kwa ajili ya bwana-arusi wake.*
9 Toleo la nafaka+ na toleo la kinywaji+ haviko tena katika nyumba ya* Yehova;
Makuhani, watumishi wa Yehova, wanaomboleza.
10 Mashamba yameharibiwa, udongo unaomboleza;+
Kwa kuwa nafaka imeharibiwa, divai mupya imekauka, mafuta yamekosekana.+
11 Walimaji wameshangaa, watunza-mizabibu wanalalamika,
Kwa sababu ya ngano na shayiri;
Kwa maana mavuno yote ya shamba yameharibika.
12 Muzabibu umekauka,
Muti wa tini umekauka.
Muti wa komamanga, muti wa mutende, na muti wa tofaa,
Miti yote ya shamba imekauka;+
Kwa sababu furaha imegeuka kuwa haya kati ya watu.
13 Muvae nguo za magunia* na muomboleze,* ninyi makuhani.
Mulalamike, ninyi watumishi wa mazabahu.+
Muingie na kulala katika hekalu usiku wote mukiwa na nguo za magunia, ninyi watumishi wa Mungu wangu;
Kwa maana toleo la nafaka+ na toleo la kinywaji+ vimeondolewa katika nyumba ya Mungu wenu.
14 Mutangaze* kufunga; muite watu kwenye mukusanyiko mukubwa.+
Mukusanye wazee pamoja, na wakaaji wote wa inchi,
Kwenye nyumba ya Yehova Mungu wenu,+ na mumulilie Yehova awasaidie.
15 Ole kwa sababu ya ile siku!
Kwa maana siku ya Yehova iko karibu,+
Na itakuja kama uharibifu kutoka kwa Mweza-Yote!
16 Je, chakula hakijaondolewa mbele ya macho yetu,
Na shangwe na furaha kutoka katika nyumba ya Mungu wetu?
17 Mbegu* zimekauka chini ya vipao* vyake.
Madepo yameachwa bila kitu.
Madepo ya nafaka yamebomolewa, kwa maana nafaka imekauka.
18 Hata mifugo inalia kwa maumivu!
Makundi ya ngombe yanatanga-tanga, kwa maana hayana malisho!
Na makundi ya kondoo yanapata azabu.
19 Nitakuita wewe, Ee Yehova;+
Kwa maana moto umeteketeza malisho katika jangwa,
Na mwali wa moto umeteketeza miti yote ya shamba.
20 Hata wanyama wa pori wanakungojea kwa hamu,
Kwa sababu mito midogo ya maji imekauka
Na moto umeteketeza malisho ya jangwa.”