Yoshua
7 Lakini Waisraeli hawakukuwa waaminifu kuhusu kitu chenye kilipaswa kuharibiwa, kwa sababu Akani+ mwana wa Karmi, mwana wa Zabdi, mwana wa Zera, wa kabila la Yuda, alikamata sehemu fulani ya vitu vyenye vilipaswa kuharibiwa.+ Kwa hiyo kasirani ya Yehova ikawaka juu ya Waisraeli.+
2 Kisha Yoshua akatuma wanaume kutoka Yeriko kuenda Ai,+ muji wenye kuwa karibu na Bet-aveni na upande wa mashariki wa Beteli,+ akawaambia: “Mupande na mupeleleze inchi hiyo.” Basi wanaume hao wakapanda na kupeleleza Ai. 3 Wakati walirudia kwa Yoshua, wakamuambia: “Haiko lazima watu wote wapande. Wanaume karibu elfu mbili (2 000) ao karibu elfu tatu (3 000) wanatosha ili kushinda Ai. Usichokeshe watu wote kwa kuwatuma kule, kwa maana watu wako kidogo tu.”
4 Basi wanaume karibu elfu tatu (3 000) wakapanda kule, lakini wakakimbia mbele ya watu wa Ai.+ 5 Na watu wa Ai wakapiga na kuua wanaume makumi tatu na sita (36), wakawafuatilia kutoka inje ya mulango mukubwa wa muji mupaka Shebarimu,* na wakaendelea kuwapiga na kuwaua kwenye muteremuko. Basi uhodari* wa watu ukayeyuka na kumwangika kama maji.
6 Kwa hiyo Yoshua akapasua nguo zake na kuanguka uso chini mbele ya Sanduku la Yehova mupaka mangaribi, yeye na wazee wa Israeli, na wakaendelea kutupa mavumbi kwenye vichwa vyao. 7 Yoshua akasema: “Ole wangu, Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova, sababu gani umeleta watu hawa katika njia hiyo yote kuvuka Yordani na kututia katika mikono ya Waamori ili tuharibiwe? Ingekuwa muzuri kama tungeendelea kuishi ngambo ingine ya* Yordani! 8 Unisamehe, Ee Yehova, niseme nini sasa kwa kuwa Israeli amekimbia* mbele ya maadui wake? 9 Wakati Wakanaani na wakaaji wote wa inchi hii watasikia habari hii, watatuzunguka na kuondoa jina letu katika dunia, na utafanya nini juu ya jina lako kubwa?”+
10 Yehova akamujibu Yoshua: “Simama! Sababu gani umelalia uso wako? 11 Israeli wamefanya zambi. Wamevunja agano langu+ lenye niliwaamuru washike. Wamekamata sehemu fulani ya vitu vyenye vilipaswa kuharibiwa,+ wameviiba+ na kuvificha kati ya vitu vyao.+ 12 Kwa hiyo, Waisraeli hawataweza kusimama mbele ya maadui wao. Watageuka na kukimbia maadui wao, kwa sababu wamekuwa kitu chenye kinapaswa kuharibiwa. Sitakuwa tena pamoja na ninyi kama hamuharibu kutoka katikati yenu kitu chenye kinapaswa kuharibiwa.+ 13 Simama na utakase watu!+ Uwaambie, ‘Mujitakase kwa ajili ya kesho, kwa sababu Yehova Mungu wa Israeli anasema hivi: “Kuko kitu chenye kinapaswa kuharibiwa kati yenu, Ee Israeli. Hamutashinda maadui wenu kama hamuondoe katikati yenu kile kitu chenye kinapaswa kuharibiwa. 14 Mutakusanyika asubui, kabila kwa kabila, na kabila lenye Yehova atachagua+ litakaribia, familia kwa familia, na familia yenye Yehova atachagua itakaribia, nyumba kwa nyumba, na nyumba yenye Yehova atachagua itakaribia, mwanaume kwa mwanaume. 15 Na mutu mwenye atapatikana na kile kitu chenye kinapaswa kuharibiwa atateketezwa kwa moto,+ yeye pamoja na vitu vyake vyote, kwa sababu amevunja agano+ la Yehova na kwa sababu amefanya tendo la haya sana katika Israeli.”’”
16 Basi siku yenye ilifuata Yoshua akaamuka asubui sana na kufanya Israeli wakaribie, kabila kwa kabila, na kabila la Yuda likachaguliwa. 17 Kisha akaleta karibu familia za Yuda na familia ya Wazera+ ikachaguliwa, kisha akaleta karibu familia ya Wazera, mwanaume kwa mwanaume, na Zabdi akachaguliwa. 18 Mwishowe akaleta karibu nyumba ya Zabdi, mwanaume kwa mwanaume, na Akani mwana wa Karmi, mwana wa Zabdi, mwana wa Zera, wa kabila la Yuda, akachaguliwa.+ 19 Kisha Yoshua akamuambia Akani: “Tafazali, mwana wangu, umupatie Yehova Mungu wa Israeli heshima na uungame kwake. Tafazali, uniambie jambo lenye umefanya. Usinifiche kitu.”
20 Akani akamujibu Yoshua: “Kwa kweli mimi ndiye nilimutendea zambi Yehova Mungu wa Israeli, na hivi ndivyo nilifanya. 21 Wakati niliona kati ya vitu vya kuchukua nguo ya pekee yenye kupendeza kutoka Shinari+ na shekeli* mia mbili (200) za feza na kipande kimoja cha zahabu chenye uzito wa shekeli makumi tano (50), nilivitamani, kwa hiyo nikavikamata. Kwa sasa vimefichwa katika udongo ndani ya hema yangu, na feza ziko chini yake.”
22 Mara moja Yoshua akatuma wajumbe, na wakakimbia kuenda katika hema, na ile nguo ilikuwa imefichwa katika hema yake, na feza zilikuwa chini ya nguo hiyo. 23 Basi wakakamata vitu hivyo katika hema, wakavipeleka kwa Yoshua na kwa Waisraeli wote na kuvitia mbele ya Yehova. 24 Yoshua na Israeli wote wakamukamata Akani+ mwana wa Zera, zile feza, ile nguo ya pekee yenye kupendeza, na kile kipande cha zahabu,+ pamoja na watoto wake wanaume, watoto wake wanamuke, ngombe-dume zake, punda zake, kundi lake, hema yake, na kila kitu chenye kilikuwa chake, wakavipeleka katika Bonde* la Akori.+ 25 Yoshua akasema: “Sababu gani umetuletea musiba?*+ Leo Yehova atakuletea musiba.” Kisha Israeli wote wakamupiga majiwe,+ kisha wakawateketeza kwa moto.+ Ni vile waliwapiga wote majiwe. 26 Na wakasimamisha rundo kubwa la majiwe juu yake lenye lingali mupaka leo. Basi kasirani kali ya Yehova ikapunguka.+ Ndiyo sababu mupaka leo mahali pale panaitwa Bonde la Akori.*