Yobu
10 “Ninachukia* maisha yangu.+
Nitaonyesha malalamiko yangu.
Nitasema kwa sababu ya uchungu wangu mwingi!*
2 Nitamuambia Mungu: ‘Usinitangaze kuwa na hatia.
Uniambie sababu gani unashindana na mimi.
3 Je, unapata faida kwa kunikandamiza,
Kwa kuzarau kazi ya mikono yako+
Na kupendelea mashauri ya waovu?
4 Je, uko na macho ya kimwili,
Ao je, unaonaka kama vile mwanadamu mwenye anaweza kufa anaonaka?
5 Je, siku zako ni kama siku za wanadamu wenye wanaweza kufa,
Ao miaka yako ni kama ya mwanadamu,+
6 Ili utafute kosa langu
Na kuendelea kutafuta zambi yangu?+
8 Mikono yako mwenyewe ilinitengeneza na kunifanya,+
Lakini sasa unataka kuniharibu kabisa.
11 Ulinivalisha ngozi na nyama,
Ukanisuka kwa mifupa na mishipa.+
13 Lakini ulikusudia kwa siri kufanya mambo haya.*
Ninajua kwamba mambo haya yametoka kwako.
14 Kama nilifanya zambi, ungeniangalia,+
Na ungekataa kunisamehe kosa langu.
15 Kama niko na hatia, ole wangu!
16 Kama ninainua kichwa changu, unaniwinda kama simba+
Na tena unaonyesha nguvu zako ili kuniumiza.
17 Unaleta mashahidi wapya ili kunipinga
Na kuongeza kasirani yako juu yangu,
Wakati magumu juu ya magumu yanakuja juu yangu.
18 Basi sababu gani ulinitosha ndani ya tumbo la uzazi?+
Afazali ningekufa mbele jicho lolote linione.
19 Ingekuwa kama vile sijapata kuwa hata siku moja;
Ningekamatwa kutoka katika tumbo la uzazi na kupelekewa moja kwa moja ndani ya kaburi.’