Zaburi
135 Mumusifu Yah!*
Musifu jina la Yehova;
Mutoe sifa, ninyi watumishi wa Yehova,+
2 Ninyi wenye kusimama katika nyumba ya Yehova,
Katika viwanja vya nyumba ya Mungu wetu.+
3 Mumusifu Yah, kwa maana Yehova ni mwema.+
Muimbie jina lake sifa,* kwa maana ni lenye kupendeza.
5 Kwa maana ninajua muzuri kwamba Yehova ni mukubwa;
Bwana wetu ni mukubwa kuliko miungu mingine yote.+
6 Yehova anafanya kila kitu chenye anapenda kufanya+
Katika mbingu na juu ya dunia, katika bahari na katika sehemu za chini kabisa.
7 Anafanya mawingu yapande* kutoka kwenye miisho ya dunia;
Anatokeza umeme wa radi kwa ajili ya* mvua;
Analeta upepo kutoka katika madepo yake.+
8 Alipiga na kuua muzaliwa wa kwanza wa Misri,
Mwanadamu na munyama pia.+
10 Alipiga na kuua mataifa mengi+
Na kuua wafalme wenye nguvu+
11 —Sihoni mufalme wa Waamori,+
Ogu mufalme wa Bashani,+
Na falme zote za Kanaani.
12 Alitoa inchi yao kuwa uriti,
Uriti kwa watu wake Israeli.+
13 Ee Yehova, jina lako linadumu milele.
Ee Yehova, sifa yako inadumu* katika vizazi vyote.+
15 Sanamu za mataifa ni feza na zahabu,
Kazi ya mikono ya mwanadamu.+
16 Ziko na kinywa, lakini haziwezi kusema;+
Ziko na macho, lakini haziwezi kuona;
17 Ziko na masikio, lakini haziwezi kusikia.
Hakuna pumuzi katika kinywa chao.+
19 Ee nyumba ya Israeli, mumusifu Yehova.
Ee nyumba ya Haruni, mumusifu Yehova.
20 Ee nyumba ya Lawi, mumusifu Yehova.+
Ninyi wenye kumuogopa Yehova, mumusifu Yehova.
Mumusifu Yah!+