Mika
2 “Ole wao wenye kupanga mambo yenye kuumiza,
Wale wenye kupanga maovu katika vitanda vyao!
Na wakati mwangaza wa asubui unatokea wanayatimiza,
Kwa sababu wako na uwezo wa kufanya vile.+
2 Wanatamani mashamba na kuyanyanganya;+
Pia nyumba, na kuzikamata;
Na wanamunyanganya mutu nyumba yake kwa udanganyifu,+
Na uriti wake.
3 Kwa hiyo Yehova anasema hivi:
‘Angalia, ninapanga kuletea familia hii musiba+ wenye hamutaepuka.*+
Hamutatembea tena kwa kiburi,+ kwa sababu ni wakati wa musiba.+
Watasema: “Tumeharibiwa kabisa!+
Alifanya sehemu ya watu wangu iende katika mikono ya watu wengine—ona namna anaiondoa kwangu!+
Anagawia mashamba yetu mutu mwenye haiko muaminifu.”
5 Kwa hiyo hakuna mwenye atanyoosha kamba ya kupimia,
Na kutugawia inchi kwa kura katika kutaniko la Yehova.
6 “Muache kuhubiri!” ni vile wanahubiri,
“Hawapaswe kuhubiri mambo haya;
Hatutafezeheshwa!”
7 Watu wanasema, Ee nyumba ya Yakobo:
“Roho ya Yehova imeshindwa kuvumilia?
Haya ndiyo matendo yake?”
Je, maneno yangu hayaletee faida wenye kutembea kwa unyoofu?
8 Lakini hivi karibuni watu wangu wamesimama kama adui.
Munaondoa waziwazi mapambo yenye kupendeza pamoja na* nguo,
Juu ya watu wenye kupita bila wasiwasi, kama wale wenye kutoka kwenye vita.
9 Munaondoa wanamuke wa watu wangu katika nyumba zao za muzuri;
Munakamata utukufu wangu kutoka kwa watoto wao milele.
10 Musimame na muende zenu, kwa sababu hapa haiko mahali pa kupumuzikia.
Kwa sababu ya uchafu,+ kutakuwa uharibifu, uharibifu mukubwa.+
11 Kama mutu anafuata upepo na udanganyifu, na kusema uongo huu:
“Nitawahubiria juu ya divai na pombe,”
Basi angekuwa tu muhubiri wa watu hawa!+
12 Kwa kweli nitawakusanya ninyi wote, Ee Yakobo;
Kwa kweli nitakusanya pamoja Waisraeli wote wenye kubakia.+
Nitawaunganisha, kama kondoo katika zizi,*
Kama kundi katika malisho yake;+
Kutakuwa makelele ya watu.’+
13 Mwenye kutoboa tundu ataenda mbele yao;
Na watatoboa tundu na kupita katika mulango mukubwa na kuenda inje kupitia mulango huo.+
Mufalme wao atapita mbele yao,
Na Yehova atawaongoza.”+