Yobu
18 Bildadi+ Mushua akajibu:
2 “Mutaacha kusema maneno kama haya wakati gani?
Mujaribu kuelewa ili na sisi tuseme.
4 Hata kama unajipasua mwenyewe* vipande-vipande katika kasirani yako,
Je, dunia itaachwa kwa sababu yako,
Ao je, mwamba utaondoka mahali pake?
5 Ndiyo, mwangaza wa muovu utazimishwa,
Na mwali wake wa moto hautangaa.+
6 Mwangaza katika hema yake utakuwa giza,
Na taa yenye kuwa juu yake itazimishwa.
7 Hatua zake zenye nguvu zimefupishwa,
Na shauri lake mwenyewe litamwangusha.+
8 Kwa maana miguu yake itamuingiza ndani ya wavu,*
Na atatanga-tanga kwenye kamba za wavu.
9 Mutego utamunasa kwenye kisigino;
Na mutego utamukamata.+
10 Kamba imefichwa katika udongo kwa ajili yake,
Na mutego uko katika njia yake.
11 Vitu vyenye kuogopesha vinamutisha pande zote,+
Na vinamufuatilia karibu na miguu yake.
13 Ngozi yake imekuliwa;
Ugonjwa hatari sana unakula* viungo vya mwili wake.
15 Wageni watakaa katika hema yake;
Kiberiti kitasambazwa juu ya makao yake.+
16 Mizizi yake itakauka chini yake,
Na matawi yake yatakauka juu yake.
17 Hakuna mwenye atamukumbuka katika dunia,
Na jina lake halitajulikana* katika barabara.
18 Atatoshwa kwenye mwangaza na kupelekwa katika giza
Na atafukuzwa mbali na inchi yenye kuzaa.
19 Hatakuwa na mutoto wala wazao kati ya watu wake,
Na hatakuwa na mutu mwenye ataokoka mahali kwenye anaishi.*
20 Wakati siku yake itafika, watu wa Mangaribi watashituka
Na watu wa Mashariki wataogopa sana.
21 Hayo ndiyo mambo yenye yanatokea kwenye mahema ya mukosaji
Na kwenye makao ya mutu mwenye hamujue Mungu.”