Isaya
2 Yehova,
Mutengenezaji wako na Mufanyizaji wako,+
Mwenye amekusaidia tangu tumbo la uzazi,* anasema hivi:
4 Na watachipuka kama kati ya majani ya mubichi,+
Kama miti ya mierebi pembeni ya mito midogo ya maji.
5 Mumoja atasema: “Mimi ni wa Yehova.”+
Mwingine atajiita kwa jina la Yakobo,
Na mwingine hata ataandika kwenye mukono wake: “Mali ya Yehova.”
Na atakamata jina la Israeli.’
‘Mimi ndiye wa kwanza na mimi ndiye wa mwisho.+
Hakuna Mungu isipokuwa mimi.+
Aite na atangaze na kunihakikishia jambo hilo!+
Tangu wakati niliweka watu wa zamani sana,
Waseme mambo yenye yatakuja
Na mambo yenye yatatokea.
Je, sikuambia kila mumoja wenu mbele ya wakati na kutangaza jambo hilo?
Muko mashahidi wangu.+
Je, kuko Mungu mwingine isipokuwa mimi?
Hapana, hakuna Mwamba mwingine;+ sijue hata mumoja.’”
9 Wale wote wenye kutengeneza sanamu za kuchongwa hawako kitu,
Na vitu vyao vyenye wanapenda sana havitakuwa na faida yoyote.+
Wakiwa mashahidi wao, hawaone* kitu chochote na hawajue kitu chochote,+
Basi wale wenye walizitengeneza watapatishwa haya.+
10 Ni nani angefanya mungu ao kutengeneza sanamu ya metali?*
Yenye haina faida yoyote?+
11 Angalia! Wenzake wote watapatishwa haya!+
Mafundi ni wanadamu bure.
Wote wakusanyike na kusimama.
Wataogopa sana na kupatishwa haya pamoja.
12 Mufuaji wa metali anatengeneza chuma kwenye makaa kwa kutumia kifaa chake.*
Kisha anasikia njaa na kuishiwa nguvu;
Hakunywe maji na anachoka.
13 Mwenye kuchonga muti ananyoosha kamba ya kupimia, na kuchora umbo kwa kutumia chokaa nyekundu.
Anaitengeneza kwa kifaa cha kuparuza mbao na kifaa cha kuchorea miviringo.
14 Kuko mutu mwenye kazi yake ni kukata miti ya mierezi.
Anachagua muti wa aina fulani, muti wa mwaloni,
Na anauacha ukomae na kuwa wenye nguvu kati ya miti ya pori.+
Anapanda muti wa mulaurusi, na mvua inaufanya ukomae.
15 Kisha ule muti unakuwa kuni zenye mwanadamu anatumia kuwasha moto.
Anakamata sehemu ya muti huo ili aote moto.
Anawasha moto na kupika mukate.
Lakini pia anatengeneza mungu na kumuabudu.
Anatengeneza sanamu ya kuchongwa, na kuinama mbele ya sanamu hiyo.+
16 Nusu yake anaiteketeza katika moto;
Kwa nusu hiyo anachoma nyama yenye anakula, na anashiba.
Pia anaota moto na kusema:
“Aha! Ninasikia joto wakati ninaangalia moto.”
17 Lakini sehemu yenye kubakia anaifanya kuwa mungu, kuwa sanamu yake ya kuchongwa.
Anaiinamia na kuiabudu.
Anasali kwake na kusema:
“Uniokoe, kwa maana wewe ni mungu wangu.”+
18 Hawajue kitu, hawaelewe kitu,+
Kwa sababu macho yao yamefungwa kwa muhuri na hayawezi kuona,
Na moyo wao hauna ufahamu.
19 Hakuna mwenye anafikiri sana katika moyo wake
Wala mwenye kuwa na ujuzi ao uelewaji, mwenye anasema:
“Nusu yake niliiteketeza ndani ya moto,
Na nilipika mukate juu ya makaa yake na kuchoma nyama ya kula.
Basi, je, ninapaswa kutumia sehemu yenye ilibakia ili kutengeneza kitu chenye kuchukiza?+
Je, ninapaswa kuabudu kipande cha muti?”*
20 Anakula majivu.
Moyo wake wenye kudanganywa umemupotosha.
Hawezi kujiokoa,* wala haseme:
“Je, hakuna uongo katika mukono wangu wa kuume?”
21 “Kumbuka mambo haya, Ee Yakobo, na wewe, Ee Israeli,
Kwa maana wewe ni mutumishi wangu.
Nilikufanya, na wewe ni mutumishi wangu.+
Ee Israeli, sitakusahau.+
Rudia kwangu, kwa maana nitakukomboa.+
23 Mupige vigelegele vya shangwe, ninyi mbingu,
Kwa maana Yehova ametenda!
Mupige vigelegele vya ushindi, ninyi sehemu za chini kabisa za dunia!
Mupige vigelegele vya shangwe, ninyi milima,+
Wewe pori na miti yako yote!
Kwa maana Yehova amemukomboa Yakobo,
Na anaonyesha utukufu wake juu ya Israeli.”+
Mwenye alikufanya tangu wakati ulikuwa katika tumbo la uzazi, anasema hivi:
“Mimi ni Yehova, mwenye aliumba kila kitu.
Ni nani alikuwa pamoja na mimi?
25 Ninavuruga alama za wale wenye kuongea maneno yenye hayana maana,*
Na mimi ndiye ninafanya waaguzi watende kama wapumbavu;+
Mwenye kuvuruga watu wenye hekima
Na kugeuza ujuzi wao kuwa upumbavu;+
26 Mwenye kutimiza neno la mutumishi wake,
Na kutimiza kikamili mambo yenye wajumbe wake wametabiri;+
Mwenye kusema kuhusu Yerusalemu, ‘Itaikaliwa,’+
Na kuhusu miji ya Yuda, ‘Itajengwa upya,+
Na nitajenga upya mabomoko yake’;+
27 Mwenye kuambia maji yenye kuenda chini sana, ‘Kauka;
Na nitakausha mito yako yote’;+
28 Mwenye kusema kuhusu Koreshi,+ ‘Yeye ni muchungaji wangu,
Na atatimiza kwa ukamili mapenzi yangu yote’;+
Mwenye kusema kuhusu Yerusalemu, ‘Atajengwa upya,’
Na kuhusu hekalu, ‘Musingi wako utawekwa.’”+