Yobu
39 “Je, unajua ni wakati gani mbuzi wa milima wanazaa?+
Je, umekwisha kuona wakati paa wanazaa vitoto vyao?+
2 Je, unahesabia miezi yenye wanapaswa kutimiza wakiwa na mimba?
Je, unajua ni wakati gani wanazaa?
3 Wanashutama wakati wanazaa vitoto vyao,
Na maumivu yao ya kuzaa yanaisha.
4 Vitoto vyao vinapata nguvu na kukomalia katika eneo lenye kuwa wazi la mashamba;
Vinaenda na havirudie tena kwa mama zao.
5 Ni nani alimuachilia punda wa pori akuwe huru,+
Na ni nani alifungua kamba za punda wa pori?
6 Nimefanya jangwa kuwa makao yake
Na inchi yenye chumvi kuwa mahali pake pa kuishi.
7 Yeye anazarau fujo za muji;
Na hasikie makelele za muendeshaji.
8 Anatanga-tanga kwenye milima, akitafuta malisho,
Akitafuta kila mumea wenye majani ya mubichi.
9 Je, ngombe-dume wa pori iko* tayari kukutumikia?+
Je, atalala usiku katika kibanda chako?*
10 Je, utafunga ngombe-dume wa pori kwa kamba katika mufereji,
Ao atakufuata nyuma ili alime* bonde?
11 Je, utategemea nguvu zake nyingi
Na kumuacha afanye kazi yako ya nguvu?
12 Je, utamutegemea akuletee mavuno* yako,
Na atayakusanya kwenye kiwanja chako cha kupigia-pigia nafaka?
13 Mabawa ya mbuni yanapiga-piga kwa furaha,
Lakini, je, mabawa na manyoya yake yanaweza kulinganishwa na ya korongo?+
14 Kwa maana yeye anaacha mayai yake juu ya udongo,
Na anayatia joto katika mavumbi.
15 Yeye anasahau kwamba muguu fulani unaweza kuyavunja
Ao kwamba munyama wa pori anaweza kuyakanyanga.
16 Anatendea wana wake kwa ukali, kama vile hawako wake;+
Haogope kwamba kazi yake inaweza kuwa ya bure.
18 Lakini wakati anasimama na kupiga-piga mabawa yake,
Yeye anachekelea farasi na mupandaji wake.
19 Je, ni wewe unapatia farasi nguvu yake?+
Je, ni wewe unavalisha shingo yake manyoya ya murefu yenye kutetemeka?
20 Je, unaweza kumufanya aruke kama nzige?
Mulio wake mukubwa wa kungoroma unaogopesha sana.+
22 Anachekelea woga na haogope kitu.+
Harudie nyuma kwa sababu ya upanga.
23 Mufuko wa mishale unafanya makelele juu yake,
Mukuki mukubwa na mukuki mudogo vinangaa.
25 Wakati baragumu inalia, yeye anasema, ‘Aha!’
Anasikia harufu ya mapigano akiwa mbali
Na anasikia sauti ya makamanda na makelele ya vita.+
26 Je, ni uelewaji wako ndio unawezesha kipanga kuruka,
Na kukunjua mabawa yake kuelekea kusini?