Rutu
4 Sasa Boazi akapanda kuenda kwenye mulango mukubwa wa muji+ na kukaa pale. Na angalia! ule mukombozi mwenye Boazi alitaja+ alikuwa anapita. Basi Boazi akamuita: “Fulani wa fulani, kuja na ukae hapa.” Na akaenda na kukaa. 2 Kisha Boazi akachukua wazee kumi (10) wa muji,+ akawaambia: “Mukae hapa.” Basi wakakaa.
3 Halafu Boazi akamuambia mukombozi huyo:+ “Naomi mwenye alirudia kutoka katika maeneo ya mashamba ya Moabu+ anauzisha shamba lenye lilikuwa la ndugu yetu Elimeleki.+ 4 Kwa hiyo niliona ni muzuri nikujulishe jambo hilo, na kukuambia, ‘Nunua shamba hilo mbele ya wakaaji na wazee wa watu wangu.+ Kama utalikomboa, ulikomboe. Lakini kama hautalikomboa, uniambie ili nijue, kwa sababu uko na haki ya kwanza ya kulikomboa, mimi ni wa pili kisha wewe.’” Mutu huyo akasema: “Niko tayari kulikomboa.”+ 5 Kisha Boazi akamuambia: “Siku yenye utanunua shamba hilo kwa Naomi, utalinunua pia kwa Rutu Mumoabu, bibi ya ule mwanaume mwenye amekwisha kufa, ili urudishe jina la ule mwanaume mwenye amekwisha kufa katika uriti wake.”+ 6 Basi mukombozi huyo akasema: “Sitaweza kulikomboa, kusudi nisiharibu uriti wangu mwenyewe. Wewe ulikomboe kwa haki yangu ya kukomboa, kwa sababu sitaweza kulikomboa.”
7 Basi hii ndiyo ilikuwa desturi zamani katika Israeli kuhusu haki ya kukomboa na kubadilishana vitu ili kuhalalisha kila namna ya jambo: Mutu alipaswa kutosha kiatu chake+ na kukipatia mwingine, na huo ndio utaratibu wenye ulifuatwa ili kuhakikisha* mapatano katika Israeli. 8 Kwa hiyo wakati mukombozi huyo alimuambia Boazi, “Ulinunue kwa ajili yako mwenyewe,” alivua kiatu chake. 9 Kisha Boazi akawaambia wazee na watu wote wenye walikuwa pale: “Muko mashahidi+ leo kwamba ninanunua vitu vyote vyenye vilikuwa vya Elimeleki na vitu vyote vyenye vilikuwa vya Kilioni na Maloni. 10 Ninamuchukua pia Rutu Mumoabu, bibi ya Maloni, akuwe bibi yangu ili kurudisha jina la ule mwanaume mwenye amekwisha kufa katika uriti wake,+ na ili jina lake lisifikie kuondolewa katikati ya ndugu zake na kwenye mulango mukubwa wa muji wa nyumbani kwake. Muko mashahidi leo.”+
11 Basi watu wote wenye walikuwa katika mulango mukubwa wa muji na wale wazee wakasema: “Tuko mashahidi! Yehova abariki bibi mwenye anaingia katika nyumba yako ili akuwe kama Raheli na Lea, wenye walijenga nyumba ya Israeli.+ Ufanikiwe katika Efrata+ na ukuwe na jina la muzuri* katika Betlehemu.+ 12 Nyumba yako ikuwe kama nyumba ya Perezi,+ mwenye Tamari alimuzalia Yuda, kupitia uzao wenye Yehova atakupatia kutoka kwa huyu kijana mwanamuke.”+
13 Basi Boazi akamuchukua Rutu na akakuwa bibi yake. Akalala naye, na Yehova akamuwezesha kupata mimba na akazaa mwana. 14 Kisha wanamuke wakamuambia Naomi: “Yehova asifiwe, mwenye amekupatia mukombozi leo. Jina lake litangazwe katika Israeli! 15 Amekurudishia* uzima wako* na atakutegemeza katika uzee wako, kwa sababu amezaliwa na binti-mukwe wako, mwenye anakupenda+ na ni mwema sana kwako kuliko wana saba (7).” 16 Naomi akachukua mutoto huyo na kumubeba katika kifua chake, na akamuchunga.* 17 Kisha wanamuke majirani wakamupatia jina. Wakasema, “Naomi amezaa mwana,” na wakamupatia jina Obedi.+ Yeye ndiye baba ya Yese,+ baba ya Daudi.
18 Basi huu ndio uzao wa familia ya* Perezi:+ Perezi akamuzaa Hezroni;+ 19 Hezroni akamuzaa Ramu; Ramu akamuzaa Aminadabu;+ 20 Aminadabu+ akamuzaa Nashoni; Nashoni akamuzaa Salmoni; 21 Salmoni akamuzaa Boazi; Boazi akamuzaa Obedi; 22 Obedi akamuzaa Yese;+ na Yese akamuzaa Daudi.+