Waamuzi
4 Lakini kisha Ehudi kufa, Waisraeli wakafanya tena mambo ya mubaya mbele ya macho ya Yehova.+ 2 Basi Yehova akawauzisha katika mukono wa Yabini mufalme wa Kanaani,+ mwenye alitawala katika Hasori. Mukubwa wa jeshi lake alikuwa Sisera, na aliishi Harosheti+ ya mataifa.* 3 Waisraeli wakamulilia Yehova+ kwa sababu Yabini alikuwa na magari mia kenda (900) ya vita yenye miundu ya chuma,*+ na kwa miaka makumi mbili (20) alikandamiza Waisraeli kwa ukali.+
4 Basi Debora, nabii mwanamuke,+ bibi ya Lapidoti, alikuwa anahukumu Israeli wakati huo. 5 Alizoea kukaa chini ya muti wa mutende wa Debora wenye ulikuwa kati ya Rama+ na Beteli+ katika eneo lenye milima la Efraimu; Waisraeli walikuwa wanaenda kwake ili awahukumu. 6 Akatuma ujumbe kumuita Baraka+ mwana wa Abinoamu kutoka Kedesh-naftali+ na akamuambia: “Je, Yehova Mungu wa Israeli hakutoa amri? ‘Uende na ujipange* kwenye Mulima Tabori, na uende na wanaume elfu kumi (10 000) wa kabila la Naftali na la Zabuloni. 7 Nitaleta kwako Sisera, mukubwa wa jeshi la Yabini, pamoja na magari yake ya vita na majeshi yake kwenye muto mudogo wa* Kishoni,+ na nitamutia katika mikono yako.’”+
8 Basi Baraka akamuambia: “Ukienda pamoja na mimi, nitaenda; lakini kama hauende pamoja na mimi, sitaenda.” 9 Kisha Debora akamuambia: “Hakika nitaenda pamoja na wewe. Lakini, hautapata sifa katika vita hiyo, kwa maana Yehova atamutia Sisera katika mukono wa mwanamuke.”+ Basi Debora akasimama na kuenda pamoja na Baraka mupaka Kedeshi.+ 10 Baraka akaita watu wa kabila la Zabuloni na la Naftali+ wakuje Kedeshi, na wanaume elfu kumi (10 000) wakamufuata.* Debora pia akapanda pamoja naye.
11 Lakini Heberi Mukeni alikuwa amejitenga na Wakeni,+ wazao wa Hobabu, baba-mukwe wa Musa,+ na hema yake ilikuwa imesimamishwa karibu na muti mukubwa wenye ulikuwa katika Saananimu, kule Kedeshi.
12 Wakamuambia Sisera kwamba Baraka mwana wa Abinoamu alikuwa ameenda kwenye Mulima Tabori.+ 13 Mara moja Sisera akakusanya magari yake yote ya vita—magari mia kenda (900) yenye miundu ya chuma*—na wanajeshi wote wenye walikuwa pamoja naye kutoka Harosheti ya mataifa kuenda kwenye muto mudogo wa* Kishoni.+ 14 Basi Debora akamuambia Baraka: “Simama, kwa maana hii ndiyo siku yenye Yehova atamutia Sisera katika mukono wako. Je, haiko Yehova ndiye anaenda mbele yako?” Na Baraka akashuka kutoka kwenye Mulima Tabori pamoja na wanaume elfu kumi (10 000) wenye kumufuata. 15 Kisha Yehova akavuruga Sisera na magari yake yote ya vita na jeshi lake lote+ na kuwaharibu kwa upanga wa Baraka. Mwishowe, Sisera akashuka kutoka katika gari lake na kukimbia kwa miguu. 16 Basi Baraka akafuatilia yale magari ya vita na lile jeshi mupaka Harosheti ya mataifa. Jeshi lote la Sisera likaharibiwa kwa upanga; hakuna hata mutu mumoja mwenye alibakia.+
17 Lakini Sisera akakimbia kwa miguu mupaka kwenye hema ya Yaeli+ bibi ya Heberi Mukeni,+ kwa maana kulikuwa amani kati ya Yabini+ mufalme wa Hasori na nyumba ya Heberi Mukeni. 18 Kisha Yaeli akatoka inje ili kumupokea Sisera, akamuambia: “Karibu bwana wangu, karibu ndani. Usiogope.” Basi akaingia ndani ya hema yake, na Yaeli akamufunika blangeti. 19 Sisera akamuambia: “Tafazali, unipatie maji kidogo ya kunywa, kwa maana niko na kiu.” Basi Yaeli akafungua chupa ya ngozi ya maziwa na kumupatia akunywe,+ kisha akamufunika tena. 20 Sisera akamuambia: “Simama kwenye muingilio wa hema, na kama mutu fulani anakuja na kukuuliza, ‘Kuko mwanaume yeyote hapa?’ useme, ‘Hapana!’”
21 Lakini Yaeli bibi ya Heberi akakamata musumari wa hema na nyundo* katika mukono wake. Kisha wakati Sisera alikuwa amelala usingizi muzito kwa sababu ya kuchoka, Yaeli akaenda kimya-kimya na kupigilia musumari huo katika mataya yake ya masikio,* na kikaingia mupaka katika udongo, na akakufa.+
22 Baraka akaenda kule kutafuta Sisera, na Yaeli akatoka inje ili kumupokea na akamuambia: “Kuja nikuonyeshe mutu mwenye unatafuta.” Baraka akaingia pamoja naye na akaona Sisera akiwa amekufa, musumari wa hema ulikuwa katika mataya yake ya masikio.*
23 Basi siku hiyo, Mungu akamunyenyekeza Yabini mufalme wa Kanaani mbele ya Waisraeli.+ 24 Mukono wa Waisraeli ukaendelea kuwa mugumu zaidi na zaidi juu ya Yabini mufalme wa Kanaani,+ mupaka wakamuharibu Yabini mufalme wa Kanaani.+