Cha Pili cha Mambo ya Nyakati
19 Kisha Mufalme Yehoshafati wa Yuda akarudia salama* kabisa+ kwenye nyumba yake mwenyewe* katika Yerusalemu. 2 Yehu+ mwana wa Hanani+ muonaji akaenda kukutana naye na akamuambia Mufalme Yehoshafati: “Je, waovu ndio unapaswa kusaidia,+ na je, wale wenye wanamuchukia Yehova ndio unapaswa kupenda?+ Kwa sababu hiyo kasirani ya Yehova iko juu yako. 3 Hata hivyo, kuko mambo ya muzuri yenye yamepatikana ndani yako,+ kwa sababu uliondoa kabisa miti mitakatifu* katika inchi na umetayarisha moyo wako* ili kumutafuta Mungu wa kweli.”+
4 Yehoshafati akaendelea kuishi katika Yerusalemu, na akatoka tena na kuenda kati ya watu kuanzia Beer-sheba mupaka kwenye eneo lenye milima la Efraimu,+ ili kuwarudisha kwa Yehova Mungu wa mababu zao.+ 5 Pia, aliweka waamuzi katika inchi yote katika miji yote ya Yuda yenye ngome, muji kisha muji.+ 6 Na akaambia waamuzi: “Mukuwe waangalifu juu ya mambo yenye munatenda, kwa maana hamuhukumu kwa ajili ya mwanadamu lakini kwa ajili ya Yehova, na yeye iko* pamoja na ninyi wakati munatoa hukumu.+ 7 Sasa woga wa Yehova ukuwe juu yenu.+ Mukuwe waangalifu juu ya mambo yenye munatenda, kwa maana kwa Yehova Mungu wetu hakuna ukosefu wa haki,+ hakuna ubaguzi,+ hakuna kupokea rushwa.”*+
8 Katika Yerusalemu pia, Yehoshafati aliweka Walawi fulani na makuhani na vichwa fulani vya jamaa za upande wa baba za Israeli ili watumike wakiwa waamuzi kwa ajili ya Yehova na kutatua kesi za hukumu kwa ajili ya wakaaji wa Yerusalemu.+ 9 Na akawaamuru: “Ni hivi munapaswa kufanya katika woga wa Yehova, kwa uaminifu na kwa moyo kamili:* 10 Kila mara wakati ndugu zenu wenye wanaishi katika miji yao wanaleta kesi ya hukumu yenye inahusu umwangaji wa damu+ ao ulizo juu ya sheria fulani, amri, masharti, ao maamuzi, munapaswa kuwaonya ili wasikuwe na hatia mbele ya Yehova; tofauti na hilo kasirani yake itakuja juu yenu na ndugu zenu. Hilo ndilo munapaswa kufanya, ili musikuwe na hatia. 11 Ndiye huyu Amaria mukubwa wa makuhani mwenye anawasimamia ninyi kwa ajili ya kila jambo la Yehova.+ Zebadia mwana wa Ishmaeli ndiye kiongozi wa nyumba ya Yuda kwa ajili ya kila jambo lenye linahusu mufalme. Na Walawi watatumika wakiwa maofisa kwa ajili yenu. Mukuwe wenye nguvu na mutende, na Yehova akuwe pamoja na wale wenye wanafanya mambo ya muzuri.”*+