Isaya
4 Na wanamuke saba (7) watamushika mwanaume mumoja siku hiyo,+ na kusema:
“Tutakula mukate wetu wenyewe
Na kuvaa nguo zetu wenyewe;
Uturuhusu tu tuitwe kwa jina lako
2 Siku hiyo kile chenye Yehova anachipusha kitakuwa kizuri sana na chenye utukufu, na mazao ya inchi yatakuwa kitu cha kujivunia na uzuri kwa ajili ya waokokaji wa Israeli.+ 3 Kila mutu mwenye atabakia katika Sayuni na kuachwa katika Yerusalemu ataitwa mutakatifu, wale wote katika Yerusalemu wenye kuandikwa kwa ajili ya uzima.+
4 Wakati Yehova atasafisha uchafu wa* mabinti wa Sayuni+ na kusafisha umwangaji wa damu wa Yerusalemu kutoka ndani yake kwa roho ya hukumu na kwa roho ya kuteketeza kwa moto,*+ 5 juu ya eneo lote la mulima Sayuni na juu ya mahali pa mikusanyiko yake, Yehova ataumba wingu na moshi wakati wa muchana na moto wenye kungaa wenye unawaka usiku;+ kwa maana juu ya utukufu wote kutakuwa mahali pa kujificha. 6 Na kutakuwa kibanda kwa ajili ya kivuli wakati wa muchana kutokana na joto,+ na kwa ajili ya kimbilio na ulinzi kutokana na zoruba na mvua.+