Rutu
3 Basi Naomi mama-mukwe wake akamuambia: “Binti yangu, hauone kama ni muzuri nikutafutie makao,*+ ili mambo yakuendee muzuri? 2 Je, Boazi haiko mutu wa jamaa yetu?+ Vijana wanamuke wenye ulikuwa pamoja nao ni wake. Usiku wa leo anapepua shayiri kwenye kiwanja cha kupigia-pigia nafaka. 3 Basi uoge na ujipakae mafuta yenye marashi; kisha uvae muzuri* na uende kwenye kiwanja cha kupigia-pigia nafaka. Usionekane mbele ya mwanaume huyo mupaka wakati atakuwa amemaliza kula na kunywa. 4 Wakati atalala, angalia kwenye atalala; kisha uende na ufunue miguu yake na ulale. Atakuambia jambo la kufanya.”
5 Basi Rutu akasema: “Mambo yote yenye unaniambia nitafanya.” 6 Kwa hiyo akaenda kwenye kiwanja cha kupigia-pigia nafaka na akafanya mambo yote yenye mama-mukwe wake alimuambia afanye. 7 Basi Boazi akakula, akakunywa, na moyo wake ukachangamuka. Kisha akaenda kulala kwenye mwisho wa rundo la nafaka. Halafu Rutu akakuja polepole akamufunua miguu na akalala. 8 Katikati ya usiku, mwanaume huyo akaanza kutetemeka, na akainuka na akaona mwanamuke amelala kwenye miguu yake. 9 Akasema: “Wewe ni nani?” Akajibu: “Mimi ni Rutu, mutumishi wako. Nyoosha nguo yako* juu ya mutumishi wako, kwa sababu wewe ni mukombozi.”+ 10 Basi Boazi akasema: “Yehova akubariki, binti yangu. Umeonyesha upendo mushikamanifu kwa njia ya muzuri zaidi wakati huu kuliko mara ya kwanza,+ kwa kuwa haukutafuta bwana kati ya vijana, wakuwe matajiri ao maskini. 11 Na sasa, binti yangu, usiogope. Nitakufanyia kila jambo lenye unasema,+ kwa sababu kila mutu katika muji* anajua kwamba wewe ni mwanamuke mwema sana. 12 Ni kweli kwamba mimi ni mukombozi,+ lakini kuko mutu wa jamaa ambaye ni mukombozi wa karibu kuliko mimi.+ 13 Bakia hapa usiku wa leo, na kama atakukomboa asubui, sawa! Akukomboe.+ Lakini kama anakataa kukukomboa, mimi nitakukomboa, kama vile hakika Yehova anaishi. Lala hapa mupaka asubui.”
14 Kwa hiyo akalala kwenye miguu yake mupaka asubui na akaamuka wakati mutu yeyote hangeweza kutambuliwa kwa sababu kulikuwa kungali giza. Kisha Boazi akasema: “Mutu yeyote asijue kama mwanamuke alikuja kwenye kiwanja cha kupigia-pigia nafaka.” 15 Akaendelea kusema: “Leta nguo ya inje yenye unavaa, na uinyooshe.” Basi Rutu akainyoosha, na Boazi akatia vipimo sita (6)* vya shayiri katika nguo hiyo na akamubebesha, kisha Boazi akaenda katika muji.
16 Rutu akaenda kwa mama-mukwe wake, mwenye sasa akasema: “Mambo yalikuendea namna gani,* binti yangu?” Akamuambia mambo yote yenye mwanaume huyo alimufanyia. 17 Akaongezea: “Alinipatia hivi vipimo sita (6) vya shayiri na kuniambia, ‘Usiende kwa mama-mukwe wako mikono wazi.’” 18 Basi Naomi akamuambia: “Kaa hapa, binti yangu mupaka wakati utajua namna jambo hilo litakuwa, kwa sababu mwanaume huyo hatapumuzika mupaka atimize jambo hilo leo.”