Ezekieli
7 Neno la Yehova likakuja tena kwangu, na kusema: 2 “Sasa wewe, Mwana wa binadamu, Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anaambia inchi ya Israeli hivi: ‘Mwisho! Ule mwisho umekuja juu ya pembe ine (4) za inchi. 3 Sasa mwisho uko juu yako, na nitaachilia kasirani yangu juu yako, na nitakuhukumu kulingana na njia zako na kukuomba utoe hesabu kwa sababu ya matendo yako yote yenye kuchukiza. 4 Jicho langu halitakusikitikia; wala sitasikia huruma,+ kwa maana nitaleta juu yako matokeo ya njia zako mwenyewe, na utapatwa na matokeo ya matendo yako yenye kuchukiza.+ Na ninyi mutalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.’+
5 “Bwana Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi Yehova anasema hivi: ‘Angalia! Musiba, musiba wa pekee, unakuja.+ 6 Mwisho unakuja; ule mwisho utakuja; utainuka wenyewe* juu yako. Angalia! Unakuja. 7 Zamu yako imefika,* wewe mwenye kukaa katika inchi. Wakati unakuja, siku ile iko karibu.+ Kuko muvurugo na haiko makelele ya shangwe kwenye milima.
8 “‘Hivi karibuni nitamwanga kasirani yangu kali juu yako,+ na nitaachilia hasira yangu juu yako,+ na nitakuhukumu kulingana na njia zako na kukuomba utoe hesabu kwa sababu ya matendo yako yote yenye kuchukiza. 9 Jicho langu halitakusikitikia; wala sitasikia huruma.+ Kwa maana nitaleta juu yako matokeo ya njia zako mwenyewe, na utapatwa na matokeo ya matendo yako yenye kuchukiza. Na ninyi mutalazimika kujua kwamba mimi, Yehova, niko nawapiga.+
10 “‘Angalia, ile siku! Angalia, inakuja!+ Zamu yako imefika;* fimbo imetoa maua na kimbelembele kimechipuka. 11 Jeuri imekomaa na kuwa fimbo ya uovu.+ Wao wenyewe wala mali yao wala vikundi vyao vya watu wala sifa yao haitaokoka. 12 Wakati utakuja, siku ile itafika. Mwenye kununua asishangilie, na mwenye kuuzisha asiomboleze, kwa maana kuko kasirani kali juu ya kikundi chao chote cha watu.*+ 13 Kwa maana mwenye kuuzisha hatarudia kwa kitu chenye kiliuzishwa, hata kama uzima wake unaokolewa, kwa maana maono ni juu ya kikundi chote cha watu. Hakuna mwenye atarudia, na kwa sababu ya kosa lake,* hakuna mwenye ataokoa uzima wake.
14 “‘Wamepiga tarumbeta+ na kila mutu iko* tayari, lakini hakuna mwenye anaenda katika vita, kwa sababu niko na gazabu juu ya kikundi chote cha watu.+ 15 Upanga uko inje,+ na ugonjwa wa kuambukiza na njaa viko ndani. Kila mutu mwenye kuwa katika eneo la mashamba atakufa kwa upanga, na njaa na ugonjwa wa kuambukiza vitateketeza wale wenye kuwa katika muji.+ 16 Waokokaji wao wenye wataweza kuponyoka wataenda kwenye milima, na kama vile njiwa wa mabonde, kila mumoja ataomboleza kwa sababu ya kosa lake.+ 17 Mikono yao yote itaninginia kwa uregevu, na magoti yao yote yataangusha matone-matone ya maji.*+ 18 Wamevaa nguo za magunia,+ na kutetemeka kumewashika.* Kila mutu atapatishwa haya, na kila kichwa kitakuwa na upara.*+
19 “‘Watatupa feza yao katika barabara, na zahabu yao itawachukiza. Feza yao wala zahabu yao haitaweza kuwaokoa katika siku ya kasirani kali ya Yehova.+ Hawatashiba,* wala kujaza matumbo yao, kwa maana hiyo* imekuwa kikwazo chenye kinatokeza kosa lao. 20 Walikuwa na kiburi kwa sababu ya uzuri wa mapambo yao, nao wakatumia vitu hivyo* ili kutengeneza mifano yao yenye kuchukiza, sanamu zao zenye kuchukiza.+ Ndiyo sababu nitazifanya kuwa chukizo kwao. 21 Nitatia hiyo* katika mukono wa wageni ili wainyanganye na kwa waovu wa dunia ili waichukue, nao wataichafua.
22 “‘Nitageuza uso wangu kutoka kwao,+ nao watachafua mahali pangu penye kufichwa,* na wanyanganyi watapaingia na kupachafua.+
23 “‘Tengeneza munyororo,*+ kwa maana inchi imejaa hukumu yenye madoa ya damu+ na muji umejaa jeuri.+ 24 Nitaingiza mataifa ya mubaya sana,+ na yatariti nyumba zao,+ na nitamaliza kiburi cha wenye nguvu, na mahali pao patakatifu patachafuliwa.+ 25 Wakati uchungu wao utakuja, watatafuta amani, lakini haitakuwa hata kidogo.+ 26 Musiba utakuja juu ya musiba, na habari moja kisha ingine, na watu watatafuta maono kwa nabii,+ lakini sheria itakosekana* kwa kuhani na shauri kwa wazee.+ 27 Mufalme ataomboleza,+ na mukubwa atavaa hali ya kupoteza tumaini,* na mikono ya watu wa inchi itatetemeka kwa woga. Nitawatendea kulingana na njia zao, na nitawahukumu kama vile wamehukumu. Nao watalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.’”+