NEHEMIA
1 Maneno ya Nehemia*+ mwana wa Hakalia: Sasa katika mwezi wa Kislevu,* katika mwaka wa makumi mbili (20), nilikuwa katika ngome* ya Shushani.*+ 2 Wakati huo Hanani,+ mumoja wa ndugu zangu, akakuja pamoja na wanaume wengine kutoka Yuda, na nikawauliza kuhusu Wayahudi wenye walibakia wenye walikuwa wameponyoka utekwa,+ na pia kuhusu Yerusalemu. 3 Wakajibu: “Wale wenye wamebakia kule katika jimbo* wenye waliponyoka utekwa, wako katika hali ya mubaya sana na yenye kuleta haya.+ Kuta za Yerusalemu zimebomoka,+ na milango yake mikubwa imeteketezwa kwa moto.”+
4 Wakati tu nilisikia maneno hayo, nikakaa chini na kuanza kulia na kuomboleza kwa siku nyingi, na nikaendelea kufunga+ na kusali mbele ya Mungu wa mbinguni. 5 Nikasema: “Ee Yehova Mungu wa mbinguni, Mungu mukubwa na mwenye kuogopesha sana, mwenye kushika agano lake na kuonyesha upendo mushikamanifu kwa wale wenye wanamupenda na kushika amri zake,+ 6 tafazali, tega sikio lako na ufungue macho yako ili kusikiliza sala ya mutumishi wako yenye ninakutolea leo, muchana na usiku,+ kuhusu watumishi wako Waisraeli, wakati ninaungama zambi zenye watu wa Israeli wamekutendea. Tumetenda zambi, mimi pamoja na nyumba ya baba yangu.+ 7 Kwa kweli tumekutendea kwa upotovu+ kwa kukosa kushika amri, masharti, na maamuzi ya hukumu yenye ulimupatia Musa mutumishi wako.+
8 “Tafazali, kumbuka lile neno lenye ulimuamuru* Musa mutumishi wako: ‘Kama hamutakuwa waaminifu, nitawasambaza kati ya vikundi vya watu.+ 9 Lakini mukirudia kwangu na kushika amri zangu na kuzitii, hata kama watu wenu wenye kutawanywa wangekuwa kwenye mwisho wa mbingu, nitawakusanya+ na kuwaleta mahali kwenye nimechagua jina langu likae.’+ 10 Wao ni watumishi wako na watu wako, wenye ulikomboa kwa uwezo wako mukubwa na kwa mukono wako wenye nguvu.+ 11 Ee Yehova, tafazali, tega sikio lako lisikilize sala ya mutumishi wako na sala ya watumishi wako wenye wanafurahia kuogopa jina lako, na tafazali, ufanye mutumishi wako apate matokeo ya muzuri leo, na mwanaume huyu anionyeshe rehema.”+
Wakati huo nilikuwa munyweshaji wa mufalme.+
2 Katika mwezi wa Nisani,* katika mwaka wa makumi mbili (20)+ wa Mufalme Artashasta,+ divai ilikuwa imetiwa mbele yake, na kama kawaida, nikakamata divai na kuipatia mufalme.+ Lakini hakuna siku nilikuwa nimeonekana mwenye huzuni mbele yake. 2 Kwa hiyo mufalme akaniambia: “Sababu gani unaonekana kuwa na huzuni na hauko mugonjwa? Hii haiko kitu kingine, ni huzuni tu ya moyo.” Basi nikaogopa sana.
3 Halafu nikamuambia mufalme: “Mufalme aishi siku nyingi! Sababu gani nisikuwe na huzuni wakati ule muji, mahali kwenye mababu zangu wamezikwa, umebomoka, na milango yake mikubwa imeteketezwa kwa moto?”+ 4 Kisha mufalme akaniambia: “Basi unataka nini?” Mara moja nikasali kwa Mungu wa mbinguni.+ 5 Kisha nikamuambia mufalme: “Kama inamupendeza mufalme na kama mutumishi wako amekubaliwa na wewe, unitume Yuda, muji kwenye mababu zangu wamezikwa, kusudi niujenge upya.”+ 6 Kisha mufalme akaniambia, malkia wake akiwa amekaa pembeni yake: “Safari yako itakuwa ya siku ngapi, na utarudia wakati gani?” Kwa hiyo ikamupendeza mufalme kunituma,+ na nikamupatia muda wenye nitafanya.+
7 Kisha nikamuambia mufalme: “Kama inamupendeza mufalme, ninaomba nipewe barua kwa ajili ya magavana wa eneo la Ngambo ya ule Muto,*+ ili waniruhusu nipite salama mupaka nifike Yuda, 8 na pia barua ya kumupelekea Asafu mutunzaji wa Bustani ya Mufalme,* ili anipatie miti kwa ajili ya nguzo za milango mikubwa ya Ngome+ ya Nyumba* na kwa ajili ya kuta za muji+ na kwa ajili ya nyumba yenye nitakaa ndani.” Kwa hiyo mufalme akanipatia barua hizo,+ kwa sababu mukono mwema wa Mungu wangu ulikuwa juu yangu.+
9 Mwishowe nikafika kwa magavana wa eneo la Ngambo ya ule Muto na nikawapatia barua za mufalme. Pia, mufalme alinituma pamoja na wakubwa wa jeshi na wapanda-farasi. 10 Wakati Sanbalati+ Muhoroni na Tobia+ ofisa* Mwamoni+ walisikia jambo hilo, hawakufurahi kabisa kwamba mutu fulani alikuwa amekuja kuwatendea mema watu wa Israeli.
11 Mwishowe nikafika Yerusalemu, na nikakaa kule siku tatu (3). 12 Nilisimama usiku, mimi na wanaume kidogo, na sikuambia mutu yeyote mambo yenye Mungu wangu alikuwa ametia katika moyo wangu ili kufanya kwa ajili ya Yerusalemu, na sikukuwa na munyama yeyote isipokuwa ule mwenye nilikuwa nimepanda juu yake. 13 Na nilitoka inje usiku kupitia Mulango Mukubwa wa Bonde,+ nikapita mbele ya Chemchemi ya Nyoka Mukubwa mupaka kwenye Mulango Mukubwa wa Marundo ya Majivu,+ na nikachunguza kuta za Yerusalemu zenye zilikuwa zimebomolewa na milango yake mikubwa yenye ilikuwa imeteketezwa kwa moto.+ 14 Na nikapita kwenye Mulango Mukubwa wa Chemchemi+ na kuelekea kwenye Kiziwa cha Maji cha Mufalme, na hapakukuwa nafasi ya kutosha kwenye munyama mwenye nilikuwa nimepanda juu yake angeweza kupita. 15 Lakini, nikaendelea kupita katika bonde*+ usiku, na nikaendelea kuchunguza ukuta; kisha nikarudia na kuingia kupitia Mulango Mukubwa wa Bonde, na kisha nikarudia.
16 Watawala-wasaidizi+ hawakujua mahali nilikuwa nimeenda na jambo lenye nilikuwa ninafanya, kwa sababu nilikuwa sijawaambia jambo lolote Wayahudi, makuhani, watu wenye vyeo, watawala-wasaidizi, na wafanyakazi wengine. 17 Mwishowe niliwaambia: “Munaona hali ya mubaya yenye tuko ndani, muji wa Yerusalemu umeharibiwa na milango yake mikubwa imeteketezwa kwa moto. Mukuje, tujenge upya kuta za Yerusalemu, kusudi hali hii yenye kuleta haya isiendelee.” 18 Kisha nikawaambia namna mukono mwema wa Mungu wangu ulikuwa juu yangu,+ na pia maneno yenye mufalme alikuwa ameniambia.+ Kwa hiyo wakasema: “Tusimame na kujenga.” Basi wakajitia nguvu* ili kufanya kazi hiyo ya muzuri.+
19 Sasa wakati Sanbalati Muhoroni, Tobia+ ofisa* Mwamoni,+ na Geshemu Mwarabu+ walisikia jambo hilo, wakaanza kutuchekelea+ na kutuzarau na kusema: “Muko munafanya nini? Je, munamuasi mufalme?”+ 20 Basi nikajibu: “Mungu wa mbinguni ndiye atafanya tufanikiwe,+ na sisi watumishi wake tutasimama na kujenga; lakini ninyi hamuna fungu wala haki ya kuomba jambo lolote wala ukumbusho* katika Yerusalemu.”+
3 Eliashibu+ kuhani mukubwa na ndugu zake makuhani wakasimama na kuanza kujenga Mulango Mukubwa wa Kondoo.+ Wakautakasa*+ na kuweka milango yake; wakautakasa mupaka kwenye Munara wa Mea,+ mupaka kwenye Munara wa Hananeli.+ 2 Na karibu nao watu wa Yeriko+ walikuwa wanajenga; na karibu nao Zakuri mwana wa Imri alikuwa anajenga.
3 Wana wa Hasenaa wakajenga Mulango Mukubwa wa Samaki;+ wakautengeneza kwa mbao+ na kisha wakaweka milango yake, makomeo yake, na mapingo* yake. 4 Na karibu nao Meremoti+ mwana wa Uriya mwana wa Hakozi akafanya kazi ya kutengeneza nafasi zenye kuharibika, na karibu nao Meshulamu+ mwana wa Berekia mwana wa Meshezabeli akafanya kazi ya kutengeneza nafasi zenye kuharibika, na karibu nao Sadoki mwana wa Baana akafanya kazi ya kutengeneza nafasi zenye kuharibika. 5 Na karibu nao Watekoa+ wakafanya kazi ya kutengeneza nafasi zenye kuharibika, lakini watu wao wa maana hawakutaka kujishusha ili kushiriki katika* kazi za mabwana wao.
6 Yoyada mwana wa Pasea na Meshulamu mwana wa Besodeya wakatengeneza Mulango Mukubwa wa Muji wa Zamani+ wenye ulikuwa umeharibika, wakautengeneza kwa mbao, wakaweka milango yake, makomeo yake, na mapingo* yake. 7 Karibu nao Melatia Mugibeoni+ na Yadoni Mumeronoti wakafanya kazi ya kutengeneza nafasi zenye kuharibika, watu wa Gibeoni na Mispa,+ wenye walikuwa chini ya mamlaka ya* gavana wa eneo la Ngambo ya ule Muto.*+ 8 Karibu nao Uzieli mwana wa Harhaya, mumoja wa mafundi wa zahabu, akafanya kazi ya kutengeneza nafasi zenye kuharibika, na karibu naye Hanania, mumoja wa watu wenye kuchanganya mafuta yenye marashi;* wakafanya kazi ya kutengeneza nafasi zenye kuharibika; wakatandika majiwe Yerusalemu mupaka kwenye Ukuta Mupana.+ 9 Na karibu nao Refaya mwana wa Huru, mukubwa wa nusu ya wilaya ya Yerusalemu, akafanya kazi ya kutengeneza nafasi zenye kuharibika. 10 Na karibu nao Yedaya mwana wa Harumafu akafanya kazi ya kutengeneza nafasi zenye kuharibika mbele ya nyumba yake mwenyewe, na karibu naye Hatushi mwana wa Hashabneya akafanya kazi ya kutengeneza nafasi zenye kuharibika.
11 Malkiya mwana wa Harimu+ na Hashubu mwana wa Pahat-moabu+ wakatengeneza sehemu ingine yenye kuharibika,* na vilevile Munara wa Majiko.+ 12 Na karibu nao Shalumu mwana wa Haloheshi, mukubwa wa nusu ya wilaya ya Yerusalemu, akafanya kazi ya kutengeneza nafasi zenye kuharibika, pamoja na mabinti wake.
13 Hanuni na wakaaji wa Zanoa+ wakatengeneza Mulango Mukubwa wa Bonde+ wenye ulikuwa umeharibika; wakaujenga na kisha wakaweka milango yake, makomeo yake, na mapingo* yake, na wakatengeneza sehemu ya ukuta yenye urefu wa mikono* elfu moja (1 000) mupaka kwenye Mulango Mukubwa wa Marundo ya Majivu.+ 14 Malkiya mwana wa Rekabu, mukubwa wa wilaya ya Bet-hakeremu+ alitengeneza Mulango Mukubwa wa Marundo ya Majivu wenye ulikuwa umeharibika; aliujenga na kuweka milango yake, makomeo yake, na mapingo* yake.
15 Shaluni mwana wa Kolhoze, mukubwa wa wilaya ya Mispa,+ alitengeneza Mulango Mukubwa wa Chemchemi+ wenye ulikuwa umeharibika; aliujenga na pia sehemu yake ya juu, akaweka milango yake, makomeo yake, na mapingo* yake, na pia akatengeneza ukuta wenye ulikuwa umeharibika wa Kiziwa cha Maji+ cha Mufereji wenye unaelekea kwenye Bustani ya Mufalme+ mupaka kwenye Ngazi+ yenye kushuka kutoka kwenye Muji wa Daudi.+
16 Kisha yeye, Nehemia mwana wa Azbuki, mukubwa wa nusu ya wilaya ya Bet-suri,+ akafanya kazi ya kutengeneza nafasi zenye kuharibika kuanzia mbele ya Makaburi ya Daudi+ mupaka kwenye kiziwa cha maji+ chenye kilikuwa kimetengenezwa na mupaka kwenye Nyumba ya Wenye Nguvu.
17 Kisha yeye, Walawi wakafanya kazi ya kutengeneza nafasi zenye kuharibika: Rehumu mwana wa Bani; na karibu naye Hashabia, mukubwa wa nusu ya wilaya ya Keila,+ akafanya kazi ya kutengeneza nafasi zenye kuharibika kwa ajili ya wilaya yake. 18 Kisha yeye, ndugu zao wakafanya kazi ya kutengeneza nafasi zenye kuharibika: Bavai mwana wa Henadadi, mukubwa wa nusu ya wilaya ya Keila.
19 Na karibu naye, Ezeri mwana wa Yeshua,+ mukubwa wa Mispa, alikuwa anatengeneza sehemu ingine yenye kuharibika mbele ya mupando wenye kuenda kwenye Depo ya Silaha karibu na Nguzo.+
20 Kisha yeye, Baruku mwana wa Zabai+ akafanya kazi kwa bidii na akatengeneza sehemu ingine yenye ilikuwa imeharibika, kuanzia kwenye Nguzo mupaka muingilio wa nyumba ya Eliashibu,+ kuhani mukubwa.
21 Kisha yeye, Meremoti+ mwana wa Uriya mwana wa Hakozi akatengeneza sehemu ingine yenye ilikuwa imeharibika, kuanzia muingilio wa nyumba ya Eliashibu mupaka mwisho wa nyumba ya Eliashibu.
22 Na kisha yeye, makuhani, wanaume wa Wilaya ya Yordani,*+ wakafanya kazi ya kutengeneza nafasi zenye zilikuwa zimeharibika. 23 Kisha wao, Benyamini na Hashubu wakafanya kazi ya kutengeneza nafasi zenye zilikuwa zimeharibika mbele ya nyumba yao wenyewe. Na kisha wao, Azaria mwana wa Maaseya mwana wa Ananiya akafanya kazi ya kutengeneza nafasi zenye zilikuwa zimeharibika karibu na nyumba yake mwenyewe. 24 Kisha yeye, Binui mwana wa Henadadi akatengeneza sehemu ingine yenye ilikuwa imeharibika, kuanzia kwenye nyumba ya Azaria mupaka kwenye Nguzo+ na mupaka kwenye pembe.
25 Kisha yeye, Palali mwana wa Uzai akafanya kazi ya kutengeneza nafasi zenye zilikuwa zimeharibika mbele ya Nguzo na munara wenye unaanzia kwenye Nyumba ya Mufalme,+ ule wa juu wenye kuwa kwenye Kiwanja cha Walinzi.+ Kisha yeye, kulikuwa Pedaya mwana wa Paroshi.+
26 Na watumishi wa hekalu*+ wenye waliishi Ofeli+ wakafanya kazi ya kutengeneza nafasi zenye zilikuwa zimeharibika mupaka mbele ya Mulango Mukubwa wa Maji+ upande wa mashariki na munara wenye kutokea inje.
27 Kisha wao, Watekoa+ walitengeneza sehemu ingine yenye ilikuwa imeharibika, kuanzia mbele ya ule munara mukubwa wenye kutokea inje mupaka kwenye ukuta wa Ofeli.
28 Makuhani wakafanya kazi ya kutengeneza nafasi zenye zilikuwa zimeharibika juu ya Mulango Mukubwa wa Farasi,+ kila mumoja mbele ya nyumba yake mwenyewe.
29 Kisha wao, Sadoki+ mwana wa Imeri akafanya kazi ya kutengeneza nafasi zenye zilikuwa zimeharibika mbele ya nyumba yake mwenyewe.
Na kisha yeye, Shemaya mwana wa Shekania, mulinzi wa Mulango Mukubwa wa Mashariki,+ akafanya kazi ya kutengeneza nafasi zenye zilikuwa zimeharibika.
30 Kisha yeye, Hanania mwana wa Shelemia na Hanuni mwana wa sita (6) wa Zalafu wakatengeneza sehemu ingine yenye ilikuwa imeharibika.
Na kisha yeye, Meshulamu+ mwana wa Berekia akafanya kazi ya kutengeneza sehemu yenye ilikuwa imeharibika mbele ya jumba lake mwenyewe.
31 Kisha yeye, Malkiya, mushiriki wa chama cha mafundi wa zahabu akafanya kazi ya kutengeneza nafasi zenye zilikuwa zimeharibika mupaka kwenye nyumba ya watumishi wa hekalu*+ na wafanyabiashara, mbele ya Mulango Mukubwa wa Uchunguzi mupaka kwenye chumba cha juu cha pembe.
32 Na kati ya chumba cha juu cha pembe na Mulango Mukubwa wa Kondoo,+ mafundi wa zahabu na wafanyabiashara walifanya kazi ya kutengeneza nafasi zenye zilikuwa zimeharibika.
4 Sasa wakati tu Sanbalati+ alisikia kwamba tulikuwa tunajenga upya ukuta, akakasirika na kuwa na uchungu sana,* na akaendelea kuchekelea Wayahudi. 2 Na akasema mbele ya ndugu zake na jeshi la Samaria: “Wayahudi hawa wazaifu wako wanafanya nini? Je, watafanya jambo hili wao wenyewe? Je, watatoa zabihu? Je, watamaliza kwa siku moja? Je, watafanya majiwe yenye yalichomwa na moto na yenye kuwa katika marundo ya mabomoko yenye kuwa na vumbi yakuwe na uzima?”+
3 Sasa Tobia+ Mwamoni,+ mwenye alikuwa anasimama pembeni yake, akasema: “Hata mbweha akipanda juu ya kile chenye wako wanajenga, atabomoa ukuta wao wa majiwe.”
4 Sikia, Ee Mungu wetu, kwa maana tumezarauliwa;+ na urudishe haya yao juu ya vichwa vyao wenyewe,+ na uwatoe kuwa kitu cha kunyanganywa katika inchi ya utekwa. 5 Na usifunike hatia yao wala kuruhusu zambi yao ifutwe mbele yako,+ kwa sababu wametukana wajenzi.
6 Kwa hiyo tukaendelea kujenga ukuta, na ukuta wote ukaunganishwa pamoja na kujengwa kufikia nusu ya urefu wake kuenda juu, na watu wakaendelea kufanya kazi kwa moyo wao wote.
7 Sasa wakati tu Sanbalati, Tobia,+ Waarabu,+ Waamoni, na Waashdodi+ walisikia kwamba kazi ya kutengeneza kuta za Yerusalemu zenye zilikuwa zimeharibika inaendelea na kwamba matundu yalikuwa yanaendelea kufunikwa, wakakasirika sana. 8 Wakafanya shauri pamoja ili kuja na kushambulia Yerusalemu na kuleta fujo ndani yake. 9 Lakini tulisali kwa Mungu wetu na kuweka walinzi muchana na usiku kwa sababu yao.
10 Lakini, watu wa Yuda walikuwa wanasema: “Nguvu za wafanyakazi* zimeisha, na kuko mabomoko mengi sana; hatutaweza kujenga ukuta hata kidogo.”
11 Na maadui wetu waliendelea kusema: “Mbele wajue jambo hilo ao kutuona, tutaingia kati yao na kuwaua na kusimamisha ile kazi.”
12 Kila mara wakati Wayahudi wenye waliishi karibu nao waliingia, walikuwa wanatuambia mara kwa mara:* “Watatushambulia kutoka kila upande.”
13 Kwa hiyo nilipanga wanaume kwenye sehemu za chini zenye kuwa wazi nyuma ya ukuta, na niliwapanga kulingana na familia zao, walikuwa na panga zao, mikuki yao, na pinde zao. 14 Wakati niliona kwamba wameogopa, mara moja nikasimama na kuambia watu wenye vyeo+ na watawala-wasaidizi na watu wengine wote: “Musiwaogope.+ Mumukumbuke Yehova, yeye ni mukubwa na mwenye kuogopesha sana;+ na mupigane kwa ajili ya ndugu zenu, watoto wenu wanaume na watoto wenu wanamuke, bibi zenu na nyumba zenu.”
15 Sasa wakati maadui wetu walisikia kwamba tumejua mambo yenye walikuwa wanafanya na kwamba Mungu wa kweli alikuwa amevunja mipango yao, sisi wote tukarudia kufanya kazi ya kujenga ukuta. 16 Kuanzia siku hiyo, nusu ya wanaume wangu walikuwa wanafanya kazi+ na nusu ingine walikuwa wanashika mikuki, ngao, pinde na makoti ya chuma. Na wakubwa+ walisimama nyuma ya watu wa nyumba yote ya Yuda 17 wenye walikuwa wanajenga ukuta. Wale wenye walikuwa wanabeba mizigo walifanya kazi kwa mukono mumoja na mukono mwingine ulikuwa unakamata silaha. 18 Na kila mujenzi alikuwa amejifunga upanga kwenye kiuno wakati alikuwa anajenga, na mupiga-baragumu+ alikuwa amesimama pembeni yangu.
19 Kisha niliambia watu wenye vyeo na watawala-wasaidizi na watu wengine wote: “Kazi hii ni kubwa na imeenea sehemu kubwa, na sisi tumesambazwa kwenye ukuta kila mumoja mbali na mwenzake. 20 Wakati mutasikia sauti ya baragumu, mujikusanye pamoja mahali kwenye tuko. Mungu wetu atatupigania.”+
21 Kwa hiyo tuliendelea kufanya kazi na wakati huo nusu ya wanaume walikuwa wamekamata mikuki, kuanzia wakati kulipambazuka* mupaka wakati nyota zilitokea. 22 Wakati huo niliambia watu: “Wanaume wakae katikati ya Yerusalemu usiku, kila mwanaume na mutumishi wake, na watatulinda usiku na kufanya kazi muchana.” 23 Lakini mimi, ndugu zangu, watumishi wangu,+ na walinzi wenye walinifuata hatukuvua nguo zetu, na kila mumoja wetu aliendelea kukamata silaha yake kwa mukono wa kuume.
5 Lakini, kulitokea kilio kikubwa cha watu na bibi zao kwa sababu ya ndugu zao Wayahudi.+ 2 Wamoja walikuwa wanasema: “Tuko wengi, sisi na watoto wetu wanaume na watoto wetu wanamuke. Tunapaswa kupata nafaka ili tukule na kuendelea kuishi.” 3 Wengine walikuwa wanasema: “Tunatoa mashamba yetu na mashamba yetu ya mizabibu na nyumba zetu kuwa kitu chenye kinawekeshwa kwa ajili ya mukopo ili tupate nafaka wakati wa njaa.” 4 Na wengine walikuwa wanasema: “Tumekopa feza kwa kutoa mashamba yetu na mashamba yetu ya mizabibu ili tulipe kodi ya mufalme.+ 5 Sasa tuko wa mwili na damu moja sawasawa na ndugu zetu,* na watoto wetu wako sawasawa tu na watoto wao; hata hivyo tumelazimika kutia watoto wetu wanaume na watoto wetu wanamuke katika utumwa, na wamoja kati ya watoto wetu wanamuke wamekwisha kuwa watumwa.+ Lakini hatuna nguvu ya kuzuia jambo hili, kwa sababu mashamba yetu na mashamba yetu ya mizabibu yamekuwa ya watu wengine.”
6 Nilikasirika sana wakati nilisikia kilio chao na maneno hayo. 7 Kwa hiyo nikafikiria mambo hayo katika moyo wangu, na nikakemea watu wenye vyeo na watawala-wasaidizi na kuwaambia: “Kila mumoja wenu iko* anamuomba ndugu yake mwenyewe faida.”*+
Tena, nikapanga kufanyike mukusanyiko mukubwa kwa sababu yao. 8 Na nikawaambia: “Kwa kadiri ya uwezo wetu, tumenunua ndugu zetu Wayahudi wenye waliuzishwa kwa mataifa; lakini sasa mutauzisha ndugu zenu,+ na itafaa tuwauze tena?” Kwa hiyo wakanyamaza kimya na hawakupata neno la kusema. 9 Kisha nikasema: “Jambo lenye muko munafanya haliko la muzuri. Hamuone kama ni muzuri mutembee katika woga wa Mungu wetu+ ili mataifa, maadui wetu, wasitulaumu? 10 Tena, mimi, ndugu zangu, na watumishi wangu tunakopesha watu feza na nafaka. Tafazali, tuache kukopesha ili kupata faida.+ 11 Tafazali, muwarudishie leo hii mashamba yao na mashamba yao ya mizabibu,+ mashamba yao ya mizeituni, na nyumba zao, na pia sehemu moja ya mia (1/100)* ya feza, nafaka, divai mupya, na mafuta yenye muko munawaomba kama faida.”
12 Kwa hiyo wakasema: “Tutawarudishia vitu hivyo na hatutawaomba kitu. Tutafanya sawasawa na vile unasema.” Basi nikaita makuhani na kuomba wanaume hao waape kwamba watatimiza ahadi yao. 13 Pia, nikakunguta mikunjo ya nguo yangu* na kusema: “Mungu wa kweli amukungute hivi ili kumuondoa katika nyumba yake na katika mali yake kila mutu mwenye hatatimiza ahadi hii; mutu huyo akungutwe hivi na abakie bila kitu.” Kwa hiyo kutaniko lote likasema: “Amina!”* Na wakamusifu Yehova, na watu wakafanya kama vile waliahidi.
14 Pia, tangu siku mufalme alinichagua kuwa gavana+ katika inchi ya Yuda, kuanzia mwaka wa makumi mbili (20)+ mupaka mwaka wa makumi tatu na mbili (32)+ wa Mufalme Artashasta,+ miaka kumi na mbili (12), mimi na ndugu zangu hatukukula posho la chakula lenye gavana alikuwa na haki ya kupewa.+ 15 Lakini magavana wa zamani wenye walinitangulia walikuwa muzigo kwa watu na kila siku walikuwa wanakamata kutoka kwa watu shekeli* makumi ine (40) za feza kwa ajili ya mukate na divai. Pia, watumishi wao walikandamiza watu. Lakini mimi sikufanya vile+ kwa sababu ya kumuogopa Mungu.+
16 Tena, nilisaidia kufanya kazi ya kujenga ukuta huu, na hatukukamata hata shamba moja;+ watumishi wangu wote walikusanyika pale ili kufanya kazi. 17 Kulikuwa Wayahudi na watawala-wasaidizi mia moja makumi tano (150) wenye walikuwa wanakula kwenye meza yangu, na pia watu wenye walitoka katika mataifa na kuja kwetu. 18 Kila siku ngombe-dume mumoja, kondoo wazuri sita (6), na ndege wengi walikuwa wanatayarishwa kwa ajili yangu,* na kila mara kisha siku kumi (10) tulitayarishiwa kila namna ya divai kwa wingi. Ijapokuwa mambo hayo yote sikuomba posho la chakula lenye gavana alikuwa na haki ya kupewa, kwa sababu kazi yenye watu walikuwa wanafanya ilikuwa tayari muzigo kwao. 19 Unikumbuke kwa wema, Ee Mungu wangu, kwa sababu ya mambo yote yenye nimetendea watu hawa.+
6 Sasa wakati tu Sanbalati, Tobia,+ Geshemu Mwarabu,+ na maadui wetu wengine waliambiwa kwamba nilikuwa nimejenga upya ukuta+ na kwamba hapakukuwa matundu yenye yalibakia ndani yake (hata kama kufikia wakati huo nilikuwa sijatia milango katika ile milango mikubwa),+ 2 mara moja Sanbalati na Geshemu wakanitumia ujumbe huu: “Kuja, tupange wakati ili kukutana kwenye vijiji vya Bonde Tambarare la Ono.”+ Lakini walikuwa wanapanga kunifanya mubaya. 3 Kwa hiyo nikatuma wajumbe kwao, na kusema: “Niko nafanya kazi kubwa, na siwezi kushuka. Sababu gani kazi isimame wakati ninaiacha ili nikuje kwenu?” 4 Walinitumia ujumbe uleule mara ine (4), na kila wakati niliwapatia jibu lilelile.
5 Kisha Sanbalati akatuma mutumishi wake na ujumbe uleule mara ya tano (5), alikuwa na barua yenye kuwa wazi katika mukono wake. 6 Ilikuwa imeandikwa hivi: “Habari zimesikiwa kati ya mataifa, na Geshemu+ pia anasema habari hizo, kwamba wewe na Wayahudi muko munapanga kuasi.+ Ndiyo sababu uko unajenga ukuta; na kulingana na habari hizo unataka kuwa mufalme wao. 7 Pia, umeweka manabii ili watangaze kukuhusu katika Yerusalemu yote, ‘Kuko mufalme katika Yuda!’ Na sasa mufalme ataambiwa mambo haya. Basi kuja, tuyazungumuzie pamoja.”
8 Lakini, nilimutumia jibu hili: “Mambo yenye unasema hayajafanyika; uko unayatunga katika mawazo yako* mwenyewe.” 9 Kwa maana wote walikuwa wanajaribu kutuogopesha, kwa kusema: “Mikono yao itaregea katika kazi, na haitafanywa.”+ Sasa, ninaomba, utie nguvu mikono yangu.+
10 Kisha nikaenda kwenye nyumba ya Shemaya mwana wa Delaya mwana wa Mehetabeli na alikuwa amejifungia ndani. Alisema: “Tupange wakati ili tukutane katika nyumba ya Mungu wa kweli, ndani ya hekalu, na tufunge milango ya hekalu, kwa maana wanakuja kukuua. Wanakuja kukuua usiku.” 11 Lakini nikasema: “Je, mutu kama mimi anapaswa kukimbia? Je, mutu kama mimi anaweza kuingia katika hekalu na kuishi?+ Sitaingia!” 12 Kisha nikatambua kwamba Mungu hakumutuma, lakini Tobia na Sanbalati+ walikuwa wamemulipa ili atoe unabii huu juu yangu. 13 Alikuwa amelipwa ili aniogopeshe na kunifanya nitende zambi, ili wakuwe na sababu ya kuniharibishia jina na kunilaumu.
14 Umukumbuke Tobia+ na Sanbalati na matendo haya, Ee Mungu wangu, na pia Noadia nabii mwanamuke na wale manabii wengine wenye walikuwa wanajaribu mara kwa mara kuniogopesha.
15 Kwa hiyo ukuta ukamalizika kujengwa siku ya makumi mbili na tano (25) ya mwezi wa Eluli,* kwa siku makumi tano na mbili (52).
16 Wakati tu maadui wetu walisikia habari hii na wakati mataifa yote yenye kutuzunguka yaliona jambo hilo, wakasikia haya sana,*+ na wakatambua kwamba kazi hii ilimalizika kwa musaada wa Mungu wetu. 17 Katika siku hizo watu wenye vyeo+ wa Yuda walikuwa wanamutumia Tobia barua nyingi, na Tobia alikuwa anawajibu. 18 Watu wengi kule Yuda waliapa kumuunga mukono, kwa sababu alikuwa mwana-mukwe wa Shekania mwana wa Ara,+ na Yehohanani mwana wake alikuwa amemuoa binti ya Meshulamu+ mwana wa Berekia. 19 Pia, walikuwa wananiambia-ambia mambo mema kumuhusu na kisha walikuwa wanamujulisha mambo yenye nilisema. Halafu Tobia alikuwa ananitumia barua za kuniogopesha.+
7 Wakati tu ukuta ulikuwa umejengwa upya,+ nilitia milango;+ kisha walinzi wa milango mikubwa,+ waimbaji,+ na Walawi+ wakawekwa. 2 Kisha nikachagua ndugu yangu Hanani+ asimamie Yerusalemu, pamoja na Hanania mukubwa wa Ngome,+ kwa maana alikuwa mwanaume mwenye kutumainika sana na alimuogopa Mungu wa kweli+ kuliko wengine wengi. 3 Kwa hiyo nikawaambia: “Milango mikubwa ya Yerusalemu isifunguliwe mupaka wakati wa joto la muchana, na wakati watakuwa wanalinda, wanapaswa kufunga milango na kutia makomeo. Na muweke wakaaji wa Yerusalemu kuwa walinzi, kila mumoja mahali pake pa kufanyia ulinzi na kila mutu mbele ya nyumba yake mwenyewe.” 4 Sasa muji ulikuwa mukubwa na mupana, na kulikuwa watu kidogo ndani yake,+ na nyumba zilikuwa hazijajengwa upya.
5 Lakini Mungu wangu akatia katika moyo wangu wazo la kukusanya pamoja watu wenye vyeo na watawala-wasaidizi na watu ili waandikishwe kulingana na ukoo.+ Basi nikapata kitabu cha maandikisho ya ukoo ya wale wenye walikuwa wa kwanza kupanda, na ndani yake nikakuta imeandikwa:
6 Na hawa ndio watu wa jimbo* wenye walipanda kutoka katika utekwa wa wale wenye walikuwa wamepelekwa katika uhamisho, wale wenye Mufalme Nebukadneza+ wa Babiloni alikuwa amepeleka katika uhamisho,+ wenye kisha wakati fulani, walirudia Yerusalemu na Yuda, kila mutu katika muji wake mwenyewe,+ 7 wale wenye walikuja pamoja na Zerubabeli,+ Yeshua,+ Nehemia, Azaria, Raamia, Nahamani, Mordekai, Bilshani, Mispereti, Bigvai, Nehumu, na Baana.
Katika hesabu ya wanaume Waisraeli kulikuwa:+ 8 wana wa Paroshi, elfu mbili mia moja makumi saba na mbili (2 172); 9 wana wa Shefatia, mia tatu makumi saba na mbili (372); 10 wana wa Ara,+ mia sita makumi tano na mbili (652); 11 wana wa Pahat-moabu,+ kati ya wana wa Yeshua na Yoabu,+ elfu mbili mia munane kumi na munane (2 818); 12 wana wa Elamu,+ elfu moja mia mbili makumi tano na ine (1 254); 13 wana wa Zatu, mia munane makumi ine na tano (845); 14 wana wa Zakai, mia saba makumi sita (760); 15 wana wa Binui, mia sita makumi ine na munane (648); 16 wana wa Bebai, mia sita makumi mbili na munane (628); 17 wana wa Azgadi, elfu mbili mia tatu makumi mbili na mbili (2 322); 18 wana wa Adonikamu, mia sita makumi sita na saba (667); 19 wana wa Bigvai, elfu mbili makumi sita na saba (2 067); 20 wana wa Adini, mia sita makumi tano na tano (655); 21 wana wa Ateri, wa Hezekia, makumi kenda na munane (98); 22 wana wa Hashumu, mia tatu makumi mbili na munane (328); 23 wana wa Besai, mia tatu makumi mbili na ine (324); 24 wana wa Harifu, mia moja kumi na mbili (112); 25 wana wa Gibeoni,+ makumi kenda na tano (95); 26 wanaume wa Betlehemu na Netofa, mia moja makumi munane na munane (188); 27 wanaume wa Anatoti,+ mia moja makumi mbili na munane (128); 28 wanaume wa Bet-azmaveti, makumi ine na mbili (42); 29 wanaume wa Kiriat-yearimu,+ Kefira, na Beeroti,+ mia saba makumi ine na tatu (743); 30 wanaume wa Rama na Geba,+ mia sita makumi mbili na moja (621); 31 wanaume wa Mikmasi,+ mia moja makumi mbili na mbili (122); 32 wanaume wa Beteli+ na Ai,+ mia moja makumi mbili na tatu (123); 33 wanaume wa ile Nebo ingine, makumi tano na mbili (52); 34 wana wa Elamu mwingine, elfu moja mia mbili makumi tano na ine (1 254); 35 wana wa Harimu, mia tatu makumi mbili (320); 36 wana wa Yeriko, mia tatu makumi ine na tano (345); 37 wana wa Lodi, Hadidi na Ono,+ mia saba makumi mbili na moja (721); 38 wana wa Senaa, elfu tatu mia kenda makumi tatu (3 930).
39 Makuhani:+ wana wa Yedaya wa nyumba ya Yeshua, mia kenda makumi saba na tatu (973); 40 wana wa Imeri, elfu moja makumi tano na mbili (1 052); 41 wana wa Pashuri,+ elfu moja mia mbili makumi ine na saba (1 247); 42 wana wa Harimu,+ elfu moja kumi saba (1 017).
43 Walawi:+ wana wa Yeshua, wa nyumba ya Kadmieli,+ kati ya wana wa Hodeva, makumi saba na ine (74). 44 Waimbaji:+ wana wa Asafu,+ mia moja makumi ine na munane (148). 45 Walinzi wa milango mikubwa:+ wana wa Shalumu, wana wa Ateri, wana wa Talmoni, wana wa Akubu,+ wana wa Hatita, wana wa Shobai, mia moja makumi tatu na munane (138).
46 Watumishi wa hekalu:*+ wana wa Siha, wana wa Hasufa, wana wa Tabaoti, 47 wana wa Kerosi, wana wa Sia, wana wa Padoni, 48 wana wa Lebana, wana wa Hagaba, wana wa Salmai, 49 wana wa Hanani, wana wa Gideli, wana wa Gahari, 50 wana wa Reaya, wana wa Resini, wana wa Nekoda, 51 wana wa Gazamu, wana wa Uza, wana wa Pasea, 52 wana wa Besai, wana wa Meunimu, wana wa Nefushesimu, 53 wana wa Bakbuki, wana wa Hakufa, wana wa Harhuri, 54 wana wa Basliti, wana wa Mehida, wana wa Harsha, 55 wana wa Barkosi, wana wa Sisera, wana wa Tema, 56 wana wa Nezia, wana wa Hatifa.
57 Wana wa watumishi wa Sulemani:+ wana wa Sotai, wana wa Sofereti, wana wa Perida, 58 wana wa Yaala, wana wa Darkoni, wana wa Gideli, 59 wana wa Shefatia, wana wa Hatili, wana wa Pokeret-hazebaimu, wana wa Amoni. 60 Watumishi wote wa hekalu*+ na wana wa watumishi wa Sulemani walikuwa mia tatu makumi kenda na mbili (392).
61 Na hawa ndio walipanda kutoka Tel-mela, Tel-harsha, Kerubi, Adoni, na Imeri, lakini hawakuweza kuonyesha jamaa yao ya upande wa baba na asili yao, kama walikuwa Waisraeli:+ 62 wana wa Delaya, wana wa Tobia, wana wa Nekoda, mia sita makumi ine na mbili (642). 63 Na wana wa makuhani: wana wa Habaya, wana wa Hakozi,+ wana wa Barzilai, mwenye alioa mumoja kati ya mabinti wa Barzilai+ Mugileadi na akaitwa kwa jina lao. 64 Hao walitafuta maandishi yao ya zamani ili wajue ukoo wao, lakini hawakuyapata, kwa hiyo hawakustahili kuwa makuhani.*+ 65 Gavana*+ akawaambia kwamba hawakupaswa kula vitu vitakatifu zaidi+ mupaka kukuwe kuhani mwenye angechunguza Urimu na Tumimu.+
66 Hesabu yote ya kutaniko nzima ilikuwa elfu makumi ine na mbili mia tatu makumi sita (42 360),+ 67 zaidi ya watumwa wao wanaume na watumwa wao wanamuke,+ wenye walikuwa elfu saba mia tatu makumi tatu na saba (7 337); walikuwa pia na waimbaji mia mbili makumi ine na tano (245) wanaume na wanamuke.+ 68 Farasi wao walikuwa mia saba makumi tatu na sita (736), nyumbu wao mia mbili makumi ine na tano (245), 69 ngamia wao mia ine makumi tatu na tano (435), na punda wao elfu sita mia saba makumi mbili (6 720).
70 Wamoja kati ya vichwa vya jamaa za upande wa baba walitoa muchango kwa ajili ya kazi.+ Gavana* alitoa kwa ajili ya hazina drakma* elfu moja (1 000) za zahabu, mabakuli makumi tano (50), kanzu mia tano makumi tatu (530) za makuhani.+ 71 Na wamoja kati ya vichwa vya jamaa za upande wa baba walitoa kwa ajili ya hazina ya kazi drakma elfu makumi mbili (20 000) za zahabu na mina* elfu mbili mia mbili (2 200) za feza. 72 Na wale watu wengine walitoa drakma elfu makumi mbili (20 000) za zahabu, mina elfu mbili (2 000) za feza, na kanzu makumi sita na saba (67) za makuhani.
73 Na makuhani, Walawi, walinzi wa milango mikubwa, waimbaji,+ wamoja kati ya watu, watumishi wa hekalu,* na Israeli wengine wote* wakaanza kuishi katika miji yao.+ Wakati mwezi wa saba (7) ulifika,+ Waisraeli wote walikuwa wamekwisha kukaa katika miji yao.+
8 Kisha watu wote wakakusanyika kwa kusudi moja katika kiwanja cha watu wote chenye kilikuwa mbele ya Mulango Mukubwa wa Maji,+ wakamuambia Ezra+ mwandikaji* alete kitabu cha Sheria ya Musa,+ yenye Yehova alikuwa ameamuru Israeli wafuate.+ 2 Basi Ezra kuhani akaleta Sheria mbele ya kutaniko+ la wanaume, wanamuke, na wote wenye wangeweza kusikiliza na kuelewa, katika siku ya kwanza ya mwezi wa saba (7).+ 3 Na akawasomea kwa sauti kubwa+ Sheria hiyo wanaume, wanamuke, na wote wenye wangeweza kuelewa, katika kiwanja cha watu wote chenye kilikuwa mbele ya Mulango Mukubwa wa Maji, kuanzia asubui sana mupaka katikati ya muchana; na watu wakasikiliza kwa uangalifu+ kitabu cha Sheria. 4 Na Ezra mwandikaji* alikuwa amesimama juu ya jukwaa la mbao lenye lilitengenezwa kwa ajili ya tukio hilo; na Matitia, Shema, Anaya, Uria, Hilkia, na Maaseya walisimama pembeni yake kwenye upande wake wa kuume; na Pedaya, Mishaeli, Malkiya,+ Hashumu, Hash-badana, Zekaria, na Meshulamu kwenye upande wake wa kushoto.
5 Ezra akafungua kitabu mbele ya macho ya watu wote, kwa maana alikuwa mwenye kusimama juu kuliko watu wote. Wakati alifungua kitabu hicho, watu wote wakasimama. 6 Kisha Ezra akamusifu Yehova Mungu wa kweli, mwenye ni Mukubwa, kisha watu wote wakajibu, “Amina!* Amina!”+ nao wakainua mikono yao juu. Kisha wakainama na kushusha nyuso chini mbele ya Yehova. 7 Na Yeshua, Bani, Sherebia,+ Yamini, Akubu, Shabetai, Hodia, Maaseya, Kelita, Azaria, Yozabadi,+ Hanani, na Pelaya, wenye walikuwa Walawi, walikuwa wanafasiria watu Sheria,+ wakati watu walikuwa wamesimama. 8 Na wakaendelea kusoma kwa sauti kubwa katika kile kitabu, katika Sheria ya Mungu wa kweli, wakaifasiria waziwazi na kueleza maana yake; kwa hiyo wakasaidia watu kuelewa mambo yenye yalikuwa yanasomwa.*+
9 Na Nehemia, mwenye alikuwa gavana* wakati huo, Ezra+ kuhani na mwandikaji,* na Walawi wenye walikuwa wanafundisha watu wakaambia watu wote: “Siku hii ni takatifu kwa Yehova Mungu wenu.+ Musiomboleze wala kulia.” Kwa maana watu wote walikuwa wanalia wakati walikuwa wanasikia maneno ya Sheria. 10 Akawaambia: “Muende, mukule vitu vya muzuri* na kunywa vitu vitamu, na mutume mafungu ya chakula+ kwa wale wenye hawana kitu; kwa kuwa siku hii ni takatifu kwa Bwana wetu, musihuzunike, kwa maana shangwe ya Yehova ni ngome yenu.”* 11 Na Walawi walikuwa wanatuliza watu wote, kwa kusema: “Munyamaze! kwa maana siku hii ni siku takatifu; wala musihuzunike.” 12 Kwa hiyo watu wote wakaenda kula na kunywa na kutumia wengine mafungu ya chakula na kushangilia sana,+ kwa maana walielewa maneno yenye walikuwa wamejulishwa.+
13 Na siku ya pili, vichwa vya jamaa za upande wa baba za watu wote, makuhani, na Walawi wakakusanyika kumuzunguka Ezra mwandikaji* ili wapate kuelewa zaidi maneno ya Sheria. 14 Kisha wakavumbua kwamba ilikuwa imeandikwa katika Sheria kwamba Yehova alikuwa ameamuru kupitia Musa kwamba Waisraeli walipaswa kukaa katika vibanda* wakati wa sikukuu katika mwezi wa saba (7),+ 15 na kwamba walipaswa kutangaza+ na kujulisha katika miji yao yote na Yerusalemu yote, na kusema: “Muende katika eneo lenye milima na mulete matawi ya mizeituni, ya miti ya misonobari, ya miti ya mihadasi na ya miti ya mitende, na matawi ya miti ingine ili kujenga vibanda, kama vile imeandikwa.”
16 Kwa hiyo watu wakaenda na kuleta matawi ili kujijengea vibanda, kila mutu kwenye sehemu ya juu ya nyumba yake, na pia katika viwanja vyao, na katika viwanja vya nyumba ya Mungu wa kweli,+ na katika kiwanja cha watu wote cha Mulango Mukubwa wa Maji,+ na katika kiwanja cha watu wote cha Mulango Mukubwa wa Efraimu.+ 17 Basi kutaniko lote la wale wenye walikuwa wamerudia kutoka katika utekwa wakajenga vibanda na kukaa katika vibanda hivyo; kwa maana Waisraeli walikuwa hawajafanya vile tangu siku za Yoshua+ mwana wa Nuni mupaka siku hiyo, kwa hiyo kukakuwa furaha kubwa sana.+ 18 Na kitabu cha Sheria ya Mungu wa kweli kikasomwa kila siku,+ tangu siku ya kwanza mupaka siku ya mwisho. Na wakafanya sikukuu hiyo kwa siku saba (7), na kukakuwa mukusanyiko mukubwa siku ya munane (8), kama vile iliombwa.+
9 Siku ya makumi mbili na ine (24) ya mwezi huo Waisraeli wakakusanyika; walikuwa wamefunga na walikuwa wamevaa nguo za magunia na kujitia mavumbi juu yao.+ 2 Kisha wazao wa Waisraeli wakajitenga na wageni wote,+ na wakasimama na kuungama zambi zao na makosa ya baba zao.+ 3 Wakaendelea kusimama mahali walikuwa na kusoma kwa sauti kubwa kitabu cha Sheria+ ya Yehova Mungu wao kwa saa tatu (3);* na kwa saa tatu zingine walikuwa wanaungama na kumuinamia Yehova Mungu wao.
4 Yeshua, Bani, Kadmieli, Shebania, Buni, Sherebia,+ Bani, na Kenani wakasimama kwenye jukwaa lenye kuinuliwa+ la Walawi, na wakasema na Yehova Mungu wao kwa sauti. 5 Na Walawi, Yeshua, Kadmieli, Bani, Hashabneya, Sherebia, Hodia, Shebania, na Petahia wakasema: “Musimame na mumusifu Yehova Mungu wenu kwa umilele wote.*+ Na wasifu jina lako lenye tukufu na lenye kuinuliwa juu ya baraka na sifa zote.
6 “Wewe peke yako ndiye Yehova;+ uliumba mbingu, ndiyo, mbingu za mbingu na jeshi lao lote, dunia na vyote vyenye kuwa juu yake, bahari na vyote vyenye kuwa ndani yake. Na unalinda uzima wa hivyo vyote, na jeshi la mbinguni linakuinamia wewe. 7 Wewe ndiye Yehova Mungu wa kweli, mwenye alimuchagua Abramu+ na kumutosha katika muji wa Uru+ wa Wakaldayo na kumupatia jina Abrahamu.+ 8 Na uliona moyo wake kuwa muaminifu mbele yako;+ kwa hiyo ukafanya agano pamoja naye ili umupatie inchi ya Wakanaani, Wahiti, Waamori, Waperizi, Wayebusi, na Wagirgashi, ili uipatie wazao wake;+ na ulitimiza ahadi yako, kwa sababu wewe ni mwenye haki.
9 “Kwa hiyo uliona mateso ya mababu zetu kule Misri,+ na ulisikia kilio chao kwenye Bahari Nyekundu. 10 Kisha ukafanya alama na miujiza juu ya Farao na watumishi wake wote na watu wote wa inchi yake,+ kwa maana ulijua kwamba walitesa+ watu wako. Ulijifanyia jina lenye lingali mupaka leo.+ 11 Na uligawanya bahari mbele yao, kusudi wavuke bahari juu ya inchi kavu,+ na wale wenye waliwafuatilia uliwatupa katika sehemu za chini kabisa kama vile jiwe lenye kutupwa ndani ya bahari yenye kuchafuka.+ 12 Uliwaongoza muchana kwa nguzo ya wingu, na usiku kwa nguzo ya moto, ili kuwaangazia njia yenye walipaswa kufuata.+ 13 Na ulishuka kwenye Mulima Sinai+ na kuzungumuza nao kutoka mbinguni+ na kuwapatia hukumu zenye haki, sheria za kweli,* masharti ya muzuri na amri.+ 14 Uliwajulisha Sabato yako takatifu,+ na uliwapatia amri, masharti, na sheria kupitia mutumishi wako Musa. 15 Uliwapatia mukate kutoka mbinguni wakati walikuwa na njaa,+ na ulitosha maji katika mwamba wakati walikuwa na kiu,+ na uliwaambia waingie na kukamata inchi yenye ulikuwa umeapa* kwamba utawapatia.
16 “Lakini, mababu zetu, walitenda kwa kimbelembele+ na walikuwa kichwa-nguvu,*+ na hawakukuwa wanasikiliza amri zako. 17 Walikataa kusikiliza,+ na hawakukumbuka matendo yako ya ajabu yenye ulifanya kati yao, lakini walikuwa kichwa-nguvu* na walichagua kichwa ili warudie katika utumwa wao kule Misri.+ Lakini wewe ni Mungu mwenye kuwa tayari kusamehe,* mwenye rehema* na huruma nyingi, mwenye hakasirike haraka na mwenye upendo mwingi mushikamanifu,*+ na wewe haukuwaacha.+ 18 Hata wakati walijitengenezea sanamu ya metali* ya kitoto-dume cha ngombe na kusema, ‘Huyu ndiye Mungu wako mwenye alikupandisha kutoka Misri,’+ na walitenda matendo makubwa ya kukosa heshima, 19 hata hivyo wewe, kwa rehema yako kubwa, haukuwaacha katika jangwa.+ Nguzo ya wingu haikutoka juu yao wakati wa muchana ili kuwaongoza katika njia, wala nguzo ya moto haikutoka juu yao wakati wa usiku ili kuwaangazia njia yenye walipaswa kufuata.+ 20 Na uliwapatia roho yako ya muzuri ili kuwapatia ufahamu,+ na haukukosa kutia mana katika vinywa vyao,+ na uliwapatia maji wakati walisikia kiu.+ 21 Kwa miaka makumi ine (40) uliwapatia chakula katika jangwa.+ Hawakukosa kitu. Nguo zao hazikuzeeka,+ na miguu yao haikuvimba.
22 “Uliwapatia falme na vikundi vya watu, ukawagawia sehemu kwa sehemu;+ kwa hiyo wakakamata inchi ya Sihoni,+ ni kusema, inchi ya mufalme wa Heshboni,+ na pia inchi ya Ogu+ mufalme wa Bashani. 23 Na ulifanya wana wao kuwa wengi kama nyota za mbinguni.+ Kisha uliwaingiza katika inchi yenye ulikuwa umeahidi mababu zao kwamba wanapaswa kuingia na kuikamata.+ 24 Kwa hiyo wana wao waliingia na kukamata inchi hiyo,+ na ulinyenyekeza mbele yao Wakanaani,+ wenye walikuwa wakaaji wa inchi hiyo, na uliwatia katika mukono wao, wao pamoja na wafalme wao na vikundi vya watu wa inchi, ili wawatendee namna walitaka. 25 Na walikamata miji yenye ngome+ na inchi yenye mbolea,*+ na walikamata nyumba zenye kujaa aina yote ya vitu vya muzuri, matangi yenye yalikuwa tayari yamechimbwa, mashamba ya mizabibu, mashamba ya mizeituni,+ na miti mingi ya matunda. Kwa hiyo walikula na kushiba na kunenepa, na walifurahia wema wako mwingi.
26 “Lakini, hawakutii na walikuasi+ na waligeuzia Sheria yako mugongo wao.* Waliua manabii wako wenye waliwaonya ili wawarudishe kwako, na walitenda matendo makubwa ya kukosa heshima.+ 27 Kwa hiyo uliwatia katika mukono wa wapinzani wao,+ wenye waliendelea kuwatesa.+ Lakini walikuwa wanakulilia wakati wa taabu yao, na wewe ulikuwa unasikia ukiwa kule mbinguni; na kwa sababu ya rehema yako kubwa, ulikuwa unatuma wakombozi ili kuwaokoa katika mukono wa wapinzani wao.+
28 “Lakini wakati tu walipata kitulizo, walitenda tena mambo ya mubaya mbele yako,+ na uliwaacha katika mukono wa maadui wao, wenye waliwatawala.*+ Kisha walikuwa wanarudia na kukuomba musaada,+ na wewe ulikuwa unasikia kule mbinguni na kuwakomboa tena na tena kwa sababu ya rehema yako kubwa.+ 29 Hata kama ulikuwa unawaonya ili warudilie Sheria yako, walijiendesha kwa kimbelembele na walikataa kusikiliza amri zako;+ na walitenda zambi juu ya masharti yako, yenye kama mutu anayafuata ataishi.+ Lakini kwa kichwa-nguvu waligeuza mugongo wao na kufanya shingo zao zikuwe nguvu, na walikataa kusikiliza. 30 Uliwavumilia+ kwa miaka mingi na uliendelea kuwaonya kwa roho yako kupitia manabii wako, lakini walikataa kusikiliza. Mwishowe uliwatia katika mukono wa vikundi vya watu wa inchi hizo.+ 31 Na kwa sababu ya rehema yako kubwa haukuwaharibu+ wala kuwaacha, kwa maana wewe ni Mungu mwenye huruma* na mwenye rehema.+
32 “Na sasa, Ee Mungu wetu, Mungu mukubwa, mwenye nguvu, mwenye kuogopesha sana, mwenye kushika agano lake na kuonyesha upendo mushikamanifu,+ usione kuwa jambo la kidogo mateso yenye yametupata sisi, wafalme wetu, wakubwa wetu,+ makuhani wetu,+ manabii wetu,+ mababu zetu, na watu wako wote tangu siku za wafalme wa Ashuru+ mupaka leo. 33 Umekuwa mwenye haki katika mambo yote yenye yametupata, kwa maana umetenda kwa uaminifu; lakini sisi ndio tumetenda kwa uovu.+ 34 Wafalme wetu, wakubwa wetu, makuhani wetu, na mababu zetu hawakufuata Sheria yako wala kusikiliza amri zako na vikumbusho* vyenye ulitumia ili kuwaonya. 35 Hata wakati walikuwa katika ufalme wao na kufurahia wema mwingi wenye uliwaonyesha na walikuwa katika inchi kubwa na yenye mbolea* yenye uliwapatia, hawakukutumikia+ na hawakuacha matendo yao mabaya. 36 Sasa leo sisi tuko watumwa+—ndiyo, watumwa katika inchi yenye ulipatia mababu zetu ili wakule matunda yake na vitu vyake vya muzuri. 37 Mazao yake mengi ni ya wafalme wenye umetia juu yetu kwa sababu ya zambi zetu.+ Wanatawala juu ya miili yetu na juu ya mifugo yetu namna wanapenda, na sisi tuko katika taabu kubwa.
38 “Kwa hiyo kwa sababu ya mambo hayo yote, tunafanya mapatano yenye kutegemeka+ na kuyaandika, na yanashuhudiwa kwa muhuri wa wakubwa wetu, Walawi wetu, na makuhani wetu.”+
10 Wale wenye walishuhudia kwa kutia muhuri juu ya mapatano hayo+ walikuwa:
Nehemia gavana,* mwana wa Hakalia,
Na Sedekia, 2 Seraya, Azaria, Yeremia, 3 Pashuri, Amaria, Malkiya, 4 Hatushi, Shebania, Maluku, 5 Harimu,+ Meremoti, Obadia, 6 Danieli,+ Ginetoni, Baruku, 7 Meshulamu, Abiya, Miyamini, 8 Maazia, Bilgai, na Shemaya; hao walikuwa makuhani.
9 Pia Walawi: Yeshua mwana wa Azania, Binui wa wana wa Henadadi, Kadmieli,+ 10 na ndugu zao Shebania, Hodia, Kelita, Pelaya, Hanani, 11 Mika, Rehobu, Hashabia, 12 Zakuri, Sherebia,+ Shebania, 13 Hodia, Bani, na Beninu.
14 Vichwa vya watu: Paroshi, Pahat-moabu,+ Elamu, Zatu, Bani, 15 Buni, Azgadi, Bebai, 16 Adoniya, Bigvai, Adini, 17 Ateri, Hezekia, Azuri, 18 Hodia, Hashumu, Besai, 19 Harifu, Anatoti, Nebai, 20 Magpiashi, Meshulamu, Heziri, 21 Meshezabeli, Sadoki, Yadua, 22 Pelatia, Hanani, Anaya, 23 Hoshea, Hanania, Hashubu, 24 Haloheshi, Pilha, Shobeki, 25 Rehumu, Hashabna, Maaseya, 26 Ahiya, Hanani, Anani, 27 Maluku, Harimu, na Baana.
28 Watu wengine—makuhani, Walawi, walinzi wa milango mikubwa, waimbaji, watumishi wa hekalu,* na watu wote wenye walijitenga na watu wa inchi hizo ili wafuate Sheria ya Mungu wa kweli,+ pamoja na bibi zao, watoto wao wanaume, na watoto wao wanamuke, wale wote wenye ujuzi na uelewaji*— 29 wakajiunga na ndugu zao, watu wao wa maana, wakajifunga kwa laana na kiapo, ili kutembea katika Sheria ya Mungu wa kweli, yenye ilikuwa imetolewa kupitia Musa mutumishi wa Mungu wa kweli, na kufuata kwa uangalifu amri zote za Yehova Bwana wetu, hukumu zake, na masharti yake. 30 Hatutapatia watu wa inchi watoto wetu wanamuke, na hatutachukua watoto wao wanamuke kwa ajili ya watoto wetu wanaume.+
31 Kama watu wa inchi wanaleta vitu vyao na kila namna ya nafaka ili kuuzisha siku ya Sabato, hatutanunua kitu chao chochote siku ya Sabato+ ao siku takatifu.+ Pia, tutaachilia mazao ya mwaka wa saba (7)+ na hatutalipisha kila deni lenye halijalipwa.+
32 Pia, tuliweka amri juu yetu wenyewe kwamba kila mumoja wetu anapaswa kutoa sehemu moja ya tatu (1/3) ya shekeli* kila mwaka kwa ajili ya utumishi wa nyumba ya* Mungu wetu,+ 33 na kwa ajili ya mikate yenye kupangwa moja juu ya ingine,*+ toleo la nafaka lenye linatolewa kwa ukawaida,+ toleo la kuteketezwa lenye linatolewa kwa ukawaida la Sabato mbalimbali+ na miezi mipya,+ na kwa ajili ya sikukuu zenye kuwekwa,+ kwa ajili ya vitu vitakatifu, kwa ajili ya matoleo ya zambi+ ili kufunika zambi kwa ajili ya Israeli, na kwa ajili ya kazi zote za nyumba ya Mungu wetu.
34 Pia, tulipiga kura kuhusu kiasi cha kuni zenye makuhani, Walawi na watu walipaswa kuleta kwenye nyumba ya Mungu kulingana na jamaa zetu za upande wa baba, kwa nyakati zenye kuwekwa, mwaka kwa mwaka, ili kuwasha moto kwenye mazabahu ya Yehova Mungu wetu, kulingana na mambo yenye kuandikwa katika Sheria.+ 35 Pia, tutaleta matunda ya kwanza yenye kukomaa ya mashamba yetu na matunda ya kwanza yenye kuivya ya kila aina ya muti wa matunda, mwaka kwa mwaka, kwenye nyumba ya Yehova,+ 36 na pia muzaliwa wa kwanza wa wana wetu na wa mifugo yetu+—kulingana na mambo yenye kuandikwa katika Sheria—na muzaliwa wa kwanza wa mifugo yetu na makundi yetu. Tutawaleta kwenye nyumba ya Mungu wetu, kwa makuhani wenye wanatumikia kwenye nyumba ya Mungu wetu.+ 37 Pia, matunda ya kwanza ya unga wetu wa chenga-chenga,+ michango yetu, matunda ya kila aina ya muti,+ divai mupya, na mafuta,+ tunapaswa kupelekea makuhani kwenye madepo ya* nyumba ya Mungu wetu,+ na kupelekea Walawi sehemu moja ya kumi (1/10)*+ ya mazao ya mashamba yetu, kwa maana wao ndio wanakusanya sehemu moja za kumi za miji yetu yote ya kilimo.
38 Na kuhani, mwana wa Haruni, anapaswa kuwa pamoja na Walawi wakati Walawi wanakusanya sehemu moja ya kumi (1/10); na Walawi wanapaswa kutoa sehemu moja ya kumi ya ile sehemu moja ya kumi kwa nyumba ya Mungu wetu,+ kwenye vyumba* vya depo. 39 Kwa maana Waisraeli na wana wa Walawi wanapaswa kuleta muchango+ wa nafaka, divai mupya, na mafuta+ kwenye madepo,* ni pale vyombo vya patakatifu vinapatikana, na pia makuhani wenye kutumikia, walinzi wa milango mikubwa, na waimbaji. Hatutapuuza nyumba ya Mungu wetu.”+
11 Sasa wakubwa wa watu walikuwa wanaishi Yerusalemu;+ lakini watu wengine walipiga kura+ ili kuleta mutu mumoja kati ya watu kumi (10) aishi Yerusalemu, ule muji mutakatifu, wakati huo wale wengine kenda (9) walibakia katika miji ingine. 2 Zaidi ya hilo, watu walibariki watu wote wenye walijitolea ili kuishi Yerusalemu.
3 Na hawa ndio vichwa vya jimbo* wenye waliishi Yerusalemu. (Israeli wengine, makuhani, Walawi, watumishi wa hekalu,*+ na wana wa watumishi wa Sulemani,+ waliishi katika miji ingine ya Yuda, kila mumoja katika uriti wake mwenyewe katika muji wake.+
4 Pia, wamoja kati ya watu wa Yuda na Benyamini waliishi Yerusalemu.) Kati ya watu wa Yuda kulikuwa Ataya mwana wa Uzia mwana wa Zekaria mwana wa Amaria mwana wa Shefatia mwana wa Mahalaleli wa wana wa Perezi;+ 5 na Maaseya mwana wa Baruku mwana wa Kolhoze mwana wa Hazaya mwana wa Adaya mwana wa Yoyaribu mwana wa Zekaria mwana wa Mushela. 6 Wana wote wa Perezi wenye walikuwa wanaishi Yerusalemu walikuwa wanaume mia ine makumi sita na munane (468) wenye uwezo.
7 Na hawa ndio walikuwa watu wa Benyamini: Salu+ mwana wa Meshulamu mwana wa Yoedi mwana wa Pedaya mwana wa Kolaya mwana wa Maaseya mwana wa Itieli mwana wa Yeshaya; 8 na kisha yeye Gabai na Salai, watu mia kenda makumi mbili na munane (928); 9 na Yoeli mwana wa Zikri, alikuwa musimamizi wao, na Yuda mwana wa Hasenua alikuwa wa pili katika kusimamia muji.
10 Kati ya makuhani: Yedaya mwana wa Yoyaribu, Yakini,+ 11 Seraya mwana wa Hilkia mwana wa Meshulamu mwana wa Sadoki mwana wa Merayoti mwana wa Ahitubu,+ kiongozi wa nyumba ya* Mungu wa kweli; 12 na ndugu zao wenye walifanya kazi ya ile nyumba, watu mia munane makumi mbili na mbili (822); na Adaya mwana wa Yerohamu mwana wa Pelalia mwana wa Amzi mwana wa Zekaria mwana wa Pashuri+ mwana wa Malkiya, 13 na ndugu zake, vichwa vya jamaa za upande wa baba, watu mia mbili makumi ine na mbili (242), na Amashisai mwana wa Azareli mwana wa Azai mwana wa Meshilemoti mwana wa Imeri, 14 na ndugu zao wenye walikuwa wanaume wenye nguvu, na hodari, watu mia moja makumi mbili na munane (128), na musimamizi wao alikuwa Zabdieli, mutu wa familia ya watu wa maana.
15 Na kati ya Walawi: Shemaya+ mwana wa Hashubu mwana wa Azrikamu mwana wa Hashabia mwana wa Buni, 16 na Shabetai+ na Yozabadi,+ wa vichwa vya Walawi, wenye walisimamia kazi za inje ya nyumba ya Mungu wa kweli; 17 na Matania,+ mwana wa Mika mwana wa Zabdi mwana wa Asafu,+ kiongozi wa nyimbo, mwenye aliongoza nyimbo za sifa wakati wa sala,+ na Bakbukia, wa pili kati ya ndugu zake, na Abda mwana wa Shamua mwana wa Galali mwana wa Yedutuni.+ 18 Walawi wote katika muji mutakatifu walikuwa mia mbili makumi munane na ine (284).
19 Na walinzi wa milango mikubwa walikuwa Akubu, Talmoni,+ na ndugu zao wenye walikuwa wanalinda milango mikubwa, watu mia moja makumi saba na mbili (172).
20 Israeli wengine, makuhani, na Walawi wenye walikuwa katika miji ingine yote ya Yuda, kila mutu katika sehemu yake ya uriti.* 21 Watumishi wa hekalu*+ walikuwa wanaishi Ofeli,+ na Siha na Gishpa walisimamia watumishi wa hekalu.*
22 Na musimamizi wa Walawi katika Yerusalemu alikuwa Uzi mwana wa Bani mwana wa Hashabia mwana wa Matania+ mwana wa Mika, wa wana wa Asafu, waimbaji; alisimamia kazi ya nyumba ya Mungu wa kweli. 23 Kwa maana mufalme alikuwa ametoa amri kwa ajili yao,+ na kulikuwa mupango fulani kwa ajili ya mahitaji ya kila siku ya waimbaji. 24 Na Petahia mwana wa Meshezabeli wa wana wa Zera mwana wa Yuda alikuwa mushauri* wa mufalme kwa kila jambo lenye lilihusu watu.
25 Kuhusu makao katika maeneo yao ya mashamba, wamoja kati ya watu wa Yuda waliishi Kiriat-arba,+ na miji yake ya pembeni-pembeni,* Diboni na miji yake ya pembeni-pembeni, Yekabzeeli+ na makao yake. 26 katika Yeshua, katika Molada,+ katika Bet-peleti+ 27 katika Hasar-shuali,+ katika Beer-sheba na miji yake ya pembeni-pembeni,* 28 katika Siklagi,+ katika Mekona na miji yake ya pembeni-pembeni,* 29 katika En-rimoni,+ katika Sora,+ na katika Yarmuti, 30 katika Zanoa,+ katika Adulamu na makao yake, katika Lakishi+ na maeneo yake ya mashamba, na katika Azeka+ na miji yake ya pembeni-pembeni.* Wakaishi* kuanzia Beer-sheba mupaka Bonde la Hinomu.+
31 Na watu wa kabila la Benyamini waliishi Geba,+ Mikmashi, Aiya, Beteli+ na miji yake ya pembeni-pembeni,* 32 Anatoti,+ Nobu,+ Ananiya, 33 Hasori, Rama,+ Gitaimu, 34 Hadidi, Seboimu, Nebalati, 35 Lodi, na Ono,+ bonde la mafundi. 36 Na vikundi fulani vya Walawi kutoka Yuda viliombwa kuishi katika eneo la Benyamini.
12 Hawa ndio makuhani na Walawi wenye walipanda pamoja na Zerubabeli+ mwana wa Shealtieli+ na Yeshua:+ Seraya, Yeremia, Ezra, 2 Amaria, Maluku, Hatushi, 3 Shekania, Rehumu, Meremoti, 4 Ido, Ginetoi, Abiya, 5 Miyamini, Maadia, Bilga, 6 Shemaya, Yoyaribu, Yedaya, 7 Salu, Amoki, Hilkia, na Yedaya. Hao ndio walikuwa vichwa vya makuhani na ndugu zao katika siku za Yeshua.
8 Walawi walikuwa Yeshua, Binui, Kadmieli,+ Sherebia, Yuda, na Matania,+ mwenye aliongoza nyimbo za shukrani pamoja na ndugu zake. 9 Na Bakbukia na Uni ndugu zao walisimama kwa kuangaliana nao ili kufanya kazi za ulinzi.* 10 Yeshua akamuzaa Yoyakimu, Yoyakimu akamuzaa Eliashibu,+ Eliashibu akamuzaa Yoyada,+ 11 Yoyada akamuzaa Yonatani, naye Yonatani akamuzaa Yadua.
12 Katika siku za Yoyakimu, hawa walikuwa makuhani, vichwa vya jamaa za upande wa baba: kwa ajili ya Seraya,+ Meraya; kwa ajili ya Yeremia, Hanania; 13 kwa ajili ya Ezra,+ Meshulamu; kwa ajili ya Amaria, Yehohanani; 14 kwa ajili ya Maluki, Yonatani; kwa ajili ya Shebania, Yosefu; 15 kwa ajili ya Harimu,+ Adna; kwa ajili ya Merayoti, Helkai; 16 kwa ajili ya Ido, Zekaria; kwa ajili ya Ginetoni, Meshulamu; 17 kwa ajili ya Abiya,+ Zikri; kwa ajili ya Miniamini, . . . ;* kwa ajili ya Moadia, Piltai; 18 kwa ajili ya Bilga,+ Shamua; kwa ajili ya Shemaya, Yehonatani; 19 kwa ajili ya Yoyaribu, Matenai; kwa ajili ya Yedaya,+ Uzi; 20 kwa ajili ya Salai, Kalai; kwa ajili ya Amoki, Eberi; 21 kwa ajili ya Hilkia, Hashabia; kwa ajili ya Yedaya, Netaneli.
22 Vichwa vya jamaa za upande wa baba za Walawi katika siku za Eliashibu, Yoyada, Yohanani, na Yadua+ waliandikishwa, sawasawa na makuhani, mupaka wakati wa ufalme wa Dario Mwajemi.
23 Walawi wenye walikuwa vichwa vya jamaa za upande wa baba waliandikishwa katika kitabu cha historia za nyakati hizo, mupaka siku za Yohanani mwana wa Eliashibu. 24 Vichwa vya Walawi walikuwa Hashabia, Sherebia, na Yeshua+ mwana wa Kadmieli,+ na ndugu zao walisimama kwa kuangaliana nao ili kutoa sifa na shukrani kulingana na maagizo ya Daudi+ mutu wa Mungu wa kweli, kikundi cha ulinzi kwa kikundi cha ulinzi. 25 Matania,+ Bakbukia, Obadia, Meshulamu, Talmoni, na Akubu+ walikuwa walinzi wa milango mikubwa,+ walilinda madepo karibu na milango mikubwa. 26 Hao walitumika katika siku za Yoyakimu mwana wa Yeshua+ mwana wa Yozadaki na katika siku za Nehemia gavana na Ezra+ mwenye alikuwa kuhani na mwandikaji.*
27 Wakati wa kuzindua kuta za Yerusalemu, walitafuta Walawi na kuwatosha kila mahali kwenye waliishi ili kuwaleta Yerusalemu kusudi wazindue kwa kushangilia, kwa nyimbo za shukrani,+ na kwa matoazi, vyombo vya kamba, na vinubi. 28 Na wana wa waimbaji* walikusanyika kutoka katika Wilaya,* kutoka sehemu zote zenye zilizunguka Yerusalemu pande zote, na makao ya Wanetofa,+ 29 kutoka Bet-gilgali,+ na kutoka katika maeneo ya mashamba ya Geba+ na Azmaveti,+ kwa maana waimbaji walikuwa wamejijengea makao kuzunguka Yerusalemu pande zote. 30 Na makuhani na Walawi walijitakasa, na walitakasa watu,+ milango mikubwa,+ na ukuta.+
31 Kisha nilipandisha wakubwa wa Yuda kwenye sehemu ya juu ya ukuta. Tena, nikatia vikundi mbili vikubwa vya waimbaji wa kutoa shukrani na vikundi vya kuwafuata, na kikundi kimoja kilitembea kuelekea upande wa kuume juu ya ukuta, kuelekea kwenye Mulango Mukubwa wa Marundo ya Majivu.+ 32 Hoshaya na nusu ya wakubwa wa Yuda walitembea nyuma yao, 33 pamoja na Azaria, Ezra, Meshulamu, 34 Yuda, Benyamini, Shemaya, na Yeremia. 35 Walikuwa pamoja na wamoja kati ya wana wa makuhani wenye walikuwa na tarumbeta:+ Zekaria mwana wa Yonatani mwana wa Shemaya mwana wa Matania mwana wa Mikaya mwana wa Zakuri mwana wa Asafu,+ 36 na ndugu zake Shemaya, Azareli, Milalai, Gilalai, Maai, Netaneli, Yuda, na Hanani, walikuwa na vyombo vya muziki vya Daudi+ ule mutu wa Mungu wa kweli; na Ezra+ mwandikaji* aliwatangulia. 37 Kwenye Mulango Mukubwa wa Chemchemi+ walienda moja kwa moja mbele yao, wakapanda Ngazi+ ya Muji wa Daudi+ kupitia njia yenye kupanda kwenye ukuta, juu ya Nyumba ya Daudi na mupaka kwenye Mulango Mukubwa wa Maji,+ upande wa mashariki.
38 Kikundi cha pili cha waimbaji wa kutoa shukrani kilitembea kuelekea upande mwingine,* na mimi nilikifuata pamoja na nusu ya watu, kwenye ukuta, juu ya Munara wa Majiko,+ na mupaka kwenye Ukuta Mupana,+ 39 na juu ya Mulango Mukubwa wa Efraimu,+ na mupaka kwenye Mulango Mukubwa wa Muji wa Zamani,+ na mupaka kwenye Mulango Mukubwa wa Samaki,+ Munara wa Hananeli,+ Munara wa Mea, na mupaka kwenye Mulango Mukubwa wa Kondoo;+ na wakakuja kusimama kwenye Mulango Mukubwa wa Mulinzi.
40 Mwishowe vikundi hivyo mbili vya waimbaji wa kutoa shukrani vikasimama mbele ya nyumba ya Mungu wa kweli; na mimi pia nikafanya vile na nusu ya watawala-wasaidizi wenye walikuwa pamoja na mimi, 41 na makuhani Eliakimu, Maaseya, Miniamini, Mikaya, Elioenai, Zekaria, na Hanania, wenye walikuwa na tarumbeta, 42 na Maaseya, Shemaya, Eleazari, Uzi, Yehohanani, Malkiya, Elamu, na Ezeri. Na waimbaji wakaimba kwa sauti kubwa na Izrahia alikuwa musimamizi wao.
43 Siku hiyo walitoa zabihu nyingi na kushangilia,+ kwa maana Mungu wa kweli aliwafanya wafurahi sana. Wanamuke na watoto pia walishangilia,+ mupaka sauti za kushangilia za Yerusalemu zikasikika mbali sana.+
44 Siku hiyo wanaume waliwekwa ili kusimamia madepo + ya michango,+ matunda ya kwanza,+ na sehemu moja za kumi (1/10).*+ Kutoka katika maeneo ya mashamba ya miji, walipaswa kukusanya ndani ya madepo hayo sehemu zenye Sheria iliomba+ kwa ajili ya makuhani na Walawi,+ kwa maana kulikuwa furaha nyingi katika Yuda kwa sababu ya makuhani na Walawi wenye walikuwa wanatumikia. 45 Na walianza kutimiza kazi za Mungu wao na sharti la kutakasa, kama vile waimbaji na walinzi wa milango mikubwa walifanya, kulingana na maagizo ya Daudi na Sulemani mwana wake. 46 Kwa maana zamani sana katika siku za Daudi na Asafu, kulikuwa viongozi wa* waimbaji na wa nyimbo za kumusifu na kumushukuru Mungu.+ 47 Na katika siku za Zerubabeli+ na siku za Nehemia, Israeli wote walipatia waimbaji+ na walinzi wa milango mikubwa mafungu yao,+ kulingana na mahitaji yao ya kila siku. Pia, walitia pembeni fungu la Walawi,+ na Walawi nao wakatia pembeni fungu la wazao wa Haruni.
13 Siku hiyo kitabu cha Musa kilisomwa katika masikio ya watu,+ na ndani yake ikavumbuliwa kwamba ilikuwa imeandikwa kuwa Mwamoni ao Mumoabu+ hawapaswe hata kidogo kuingia katika kutaniko la Mungu wa kweli,+ 2 kwa maana hawakuenda kupokea Waisraeli na mukate na maji, lakini walimulipa Balaamu ili awalaani.+ Hata hivyo, Mungu wetu aligeuza laana hiyo kuwa baraka.+ 3 Wakati tu walisikia Sheria hiyo, wakaanza kutenga kutoka katika Israeli wale wote wenye walikuwa wa asili ya kigeni.*+
4 Sasa mbele ya mambo hayo, kuhani mwenye alisimamia madepo ya* nyumba ya* Mungu wetu+ alikuwa Eliashibu,+ mutu wa jamaa ya Tobia.+ 5 Eliashibu alikuwa amemupatia Tobia depo kubwa,* mahali kwenye kulikuwa kunatumiwa zamani ili kuweka toleo la nafaka, ubani, na vyombo na sehemu moja ya kumi (1/10)* ya nafaka, divai mupya, na mafuta,+ vyenye Walawi,+ waimbaji, na walinzi wa milango mikubwa walikuwa na haki ya kupewa, pamoja na michango kwa ajili ya makuhani.+
6 Na wakati huo wote mimi sikukuwa Yerusalemu, kwa maana nilienda kwa mufalme katika mwaka wa makumi tatu na mbili (32)+ wa Mufalme Artashasta+ wa Babiloni; na kisha wakati fulani nilimuomba mufalme ruhusa ya kuondoka. 7 Kisha nikafika Yerusalemu na kuona jambo la kuchukiza lenye Eliashibu+ alikuwa amefanya kwa ajili ya Tobia,+ kwa kumupatia depo katika kiwanja cha nyumba ya Mungu wa kweli. 8 Jambo hilo lilinichukiza sana, kwa hiyo nikatupa vitu vyote vya nyumba ya Tobia inje ya depo hiyo.* 9 Kisha jambo hilo nikatoa amri, na wakatakasa madepo;* na nikarudisha ndani vyombo vya nyumba ya Mungu wa kweli,+ pamoja na toleo la nafaka na ubani.+
10 Pia, nikavumbua kwamba Walawi+ hawakukuwa wanapewa tena mafungu yao,+ kwa hiyo Walawi na waimbaji wenye walikuwa wanafanya kazi walikuwa wameenda, kila mumoja kwenye shamba lake.+ 11 Kwa hiyo nikakemea watawala-wasaidizi+ na kusema: “Sababu gani nyumba ya Mungu wa kweli imepuuzwa?”+ Kisha nikawakusanya pamoja na kuwarudisha kwenye kazi zao. 12 Na watu wote wa Yuda wakaleta kwenye madepo sehemu moja ya kumi (1/10)+ ya nafaka, divai mupya, na mafuta.+ 13 Kisha nikaweka Shelemia kuhani, Sadoki mwandikaji,* na Pedaya Mulawi wasimamie madepo, na Hanani mwana wa Zakuri mwana wa Matania alikuwa musaidizi wao, kwa maana wanaume hao walionwa kuwa wenye kutegemeka. Walikuwa na daraka la kugawia ndugu zao.
14 Unikumbuke,+ Ee Mungu wangu, juu ya jambo hili, na usifute matendo yangu ya upendo mushikamanifu yenye nimetenda kwa ajili ya nyumba ya Mungu wangu na utumishi wake mbalimbali.*+
15 Katika siku hizo niliona watu kule Yuda wakikanyanga-kanyanga katika vikamulio vya divai siku ya Sabato,+ walileta marundo ya nafaka na kuyapakiza juu ya punda, na walileta divai, zabibu, tini, na kuingiza kila aina ya muzigo katika Yerusalemu siku ya Sabato.+ Kwa hiyo, niliwaonya wasiuzishe vyakula siku hiyo.* 16 Na Watiro wenye waliishi katika muji walikuwa wanaleta samaki na kila namna ya vitu vya biashara, waliviuzisha kwa watu wa Yuda na katika Yerusalemu siku ya Sabato.+ 17 Kwa hiyo nikakemea watu wenye vyeo wa Yuda na kuwaambia: “Ni jambo gani hili la mubaya lenye muko munafanya, kwa kuchafua hata siku ya Sabato? 18 Je, mababu zenu hawakufanya vile, na kwa hiyo Mungu wetu alileta musiba wote huu juu yetu na juu ya muji huu? Sasa munaendelea kuongeza kasirani yenye kuwaka juu ya Israeli kwa kuchafua Sabato.”+
19 Kwa hiyo wakati tu giza lilianza kuingia juu ya milango mikubwa ya Yerusalemu mbele ya Sabato kuanza, nikatoa amri milango ifungwe. Pia nikasema hawapaswe kuifungua mupaka kisha Sabato, na niliweka wamoja kati ya watumishi wangu kwenye milango mikubwa ili muzigo wowote usiingizwe ndani ya muji siku ya Sabato. 20 Kwa hiyo wafanyabiashara na wenye kuuzisha kila aina ya vitu vya biashara walilala inje ya Yerusalemu mara moja ao mara mbili. 21 Kisha nikawapatia angalisho na kuwaambia: “Sababu gani munalala mbele ya ukuta usiku? Mukifanya hivi tena, nitawafukuza kwa nguvu.” Tangu wakati huo na kuendelea hawakukuja tena siku ya Sabato.
22 Na nikaambia Walawi kwamba wanapaswa kujitakasa kwa ukawaida na kuja na kulinda milango mikubwa ili kuendelea kufanya siku ya Sabato kuwa takatifu.+ Kwa ajili ya jambo hili pia, Ee Mungu wangu, unikumbuke, na unisikilie huruma kwa sababu ya wingi wa upendo wako mushikamanifu.+
23 Katika siku hizo pia niliona Wayahudi wenye walikuwa wameoa* wanamuke+ Waashdodi,+ Waamoni, na Wamoabu.+ 24 Nusu ya wana wao walizungumuza Kiashdodi na nusu walizungumuza luga za vikundi vingine vya watu, lakini hakuna mumoja kati yao mwenye alijua kuzungumuza luga ya Wayahudi. 25 Kwa hiyo nikawakemea na kuwalaani na kupiga wamoja kati ya wanaume hao+ na nikangoa nywele zao na kuwaapisha katika jina la Mungu: “Hamupaswe kupana watoto wenu wanamuke kwa watoto wao wanaume, na hamupaswe kukubali hata mumoja wa watoto wao wanamuke kwa ajili ya watoto wenu wanaume ao kwa ajili yenu wenyewe.+ 26 Je, haikukuwa kwa sababu yao kwamba Mufalme Sulemani wa Israeli alitenda zambi? Kati ya mataifa mengi hapakukuwa mufalme kama yeye;+ na alipendwa na Mungu wake,+ hata Mungu akamufanya kuwa mufalme juu ya Israeli wote. Lakini wanamuke wa kigeni walimufanya hata yeye atende zambi.+ 27 Je, hili haliko jambo lenye halijapata kusikiwa kwamba muko munatenda uovu huu mukubwa wa kukosa kuwa waaminifu kwa Mungu wetu kwa kuoa wanamuke wa kigeni?”+
28 Mumoja wa wana wa Yoyada+ mwana wa Eliashibu+ kuhani mukubwa alikuwa amekuwa mwana-mukwe wa Sanbalati+ Muhoroni. Kwa hiyo nikamufukuza atoke mbele yangu.
29 Uwakumbuke, Ee Mungu wangu, kwa sababu wamechafua ukuhani na agano la ukuhani+ na Walawi.+
30 Na niliwatakasa kutokana na kila uchafu wa kigeni, na nilipatia makuhani na Walawi kazi zao, kila mutu katika utumishi wake,+ 31 na nilifanya mipango kwa ajili ya kuleta kuni+ wakati wenye ulichaguliwa na kwa ajili ya matunda ya kwanza yenye kukomaa.
Unikumbuke kwa wema, Ee Mungu wangu.+
Maana yake “Yah Anafariji.”
Angalia Nyongeza B15.
Ao “nyumba ya mufalme.”
Ao “Susa.”
Ao “wilaya ya utawala.”
Ao “onyo lenye ulimupatia.”
Angalia Nyongeza B15.
Ao “Eneo la Ngambo Ingine ya Efrati.”
Ao “pori la mufalme.”
Ao “Hekalu.”
Tnn., “mutumishi.”
Ao “bonde la muto.”
Tnn., “wakatia nguvu mikono yao.”
Tnn., “mutumishi.”
Ao “haki ya kuwa na kitu fulani.”
Ao “Wakautolea Mungu.”
Pingo ni kipande cha muti ao cha chuma cha kufungia mulango kwa ndani.
Tnn., “hawakutia shingo zao katika.”
Pingo ni kipande cha muti ao cha chuma cha kufungia mulango kwa ndani.
Tnn., “wa kiti cha ufalme cha.”
Ao “Eneo la Ngambo Ingine ya Efrati.”
Ao “watengenezaji wa marashi.”
Ao “sehemu ingine yenye kupimwa.”
Pingo ni kipande cha muti ao cha chuma cha kufungia mulango kwa ndani.
Karibu metre 445 (futi 1 460).
Pingo ni kipande cha muti ao cha chuma cha kufungia mulango kwa ndani.
Pingo ni kipande cha muti ao cha chuma cha kufungia mulango kwa ndani.
Ao pengine, “wilaya ya pembeni-pembeni.”
Ao “Wanetini.” Tnn., “wenye walitolewa.”
Ao “Wanetini.” Tnn., “wenye walitolewa.”
Ao “akauzika.”
Ao “wabeba-mizigo.”
Tnn., “mara kumi.”
Ni kusema, wakati mwangaza wa jua ulianza kutokea.
Tnn., “nyama ya mwili wa ndugu zetu ni sawa nyama ya mwili wetu.”
Ao “eko.”
Ao “faida ya juu sana.”
Ao “asilimia moja,” ni kusema, kila mwezi.
Tnn., “nikakunguta kifua changu.”
Ao “Ikuwe vile!”
Shekeli moja ilikuwa sawa na grame 11.4 (aunsi troi 0.367). Angalia Nyongeza B14.
Ao “kwa feza zangu.”
Tnn., “katika moyo wako.”
Angalia Nyongeza B15.
Tnn., “wakaanguka sana katika macho yao wenyewe.”
Ao “wilaya ya utawala.”
Ao “Wanetini.” Tnn., “wenye walitolewa.”
Ao “Wanetini.” Tnn., “wenye walitolewa.”
Ao “hawakustahili utumishi wa kikuhani kwa sababu hawakukuwa safi.”
Ao “Tirshata,” jina la cheo cha Kiajemi cha gavana wa jimbo.
Ao “Tirshata,” jina la cheo cha Kiajemi cha gavana wa jimbo.
Kwa kawaida ilikuwa sawa na dariki ya zahabu ya Uajemi yenye uzito wa grame 8.4 (aunsi troi 0.27). Ni tofauti na drakma yenye kutajwa katika Maandiko ya Kigiriki. Angalia Nyongeza B14.
Mina yenye inatajwa katika Maandiko ya Kiebrania ilikuwa sawa na grame 570 (aunsi troi 18.35). Angalia Nyongeza B14.
Ao “Wanetini.” Tnn., “wenye walitolewa.”
Tnn., “Israeli wote.”
Ao “mwandishi.”
Ao “mwandishi.”
Ao “Ikuwe vile!”
Ao “wakaeleza maana ya usomaji huo.”
Ao “Tirshata,” jina la cheo cha Kiajemi cha gavana wa jimbo.
Ao “mwandishi.”
Tnn., “vitu vinono.”
Ao “nguvu yenu.”
Ao “mwandishi.”
Ao “makao ya muda.”
Ao “sehemu moja ya ine ya siku.”
Ao “tangu milele mupaka milele.”
Ao “sheria zenye kutegemeka.”
Tnn., “umeinua mukono wako.”
Tnn., “walifanya shingo yao kuwa ngumu.”
Tnn., “walifanya shingo yao kuwa ngumu.”
Ao “Mungu mwenye matendo ya kusamehe.”
Ao “neema.”
Ao “fazili zenye upendo.”
Ao “sanamu ya kuyeyushwa.”
Ao “tajiri.”
Tnn., “na walitupa Sheria yako nyuma ya mugongo wao.”
Ao “waliwaponda.”
Ao “neema.”
Ao “maonyo.”
Ao “tajiri.”
Ao “Tirshata,” jina la cheo cha Kiajemi cha gavana wa jimbo.
Ao “Wanetini.” Tnn., “wenye walitolewa.”
Ao pengine, “wote wenye miaka ya kuelewa.”
Shekeli moja ilikuwa sawa na grame 11.4 (aunsi troi 0.367). Angalia Nyongeza B14.
Ao “hekalu la.”
Ni kusema, mikate ya wonyesho.
Ao “vyumba vya kukulia chakula vya.”
Ao “zaka.”
Ao “vyumba vya kukulia chakula.”
Ao “vyumba vya kukulia chakula.”
Ao “wilaya ya utawala.”
Ao “Wanetini.” Tnn., “wenye walitolewa.”
Ao “hekalu la.”
Ao “uriti wake mwenyewe.”
Ao “Wanetini.” Tnn., “wenye walitolewa.”
Ao “Wanetini.” Tnn., “wenye walitolewa.”
Tnn., “alikuwa kwenye mukono wa mufalme.”
Ao “yenye kuizunguka.”
Ao “yenye kuizunguka.”
Ao “yenye kuizunguka.”
Ao “yenye kuizunguka.”
Ao “Wakapiga kambi.”
Ao “yenye kuizunguka.”
Ao pengine, “wakati wa kazi.”
Inaonekana jina fulani limeondolewa hapa katika maandishi ya Kiebrania.
Ao “mwandishi.”
Ao “Na waimbaji wenye kuzoezwa.”
Ni kusema, wilaya yenye ilizunguka Yordani.
Ao “mwandishi.”
Ao “mbele.”
Ao “zaka.”
Tnn., “vichwa vya.”
Ao “asili yenye kuchangamana.”
Ao “vyumba vya kukulia chakula vya.”
Ao “hekalu la.”
Ao “chumba kikubwa cha kukulia chakula.”
Ao “zaka.”
Ao “chumba hicho cha kukulia chakula.”
Ao “vyumba vya kukulia chakula.”
Ao “mwandishi.”
Ao “kazi yake ya kulinda.”
Ao pengine, “niliwaonya siku hiyo wasiuzishe vyakula.”
Ao “walikuwa wameingiza katika nyumba zao.”