MEZALI
1 Mezali za Sulemani,+ mwana wa Daudi,+ mufalme wa Israeli:+
2 Ili kujifunza* hekima+ na nizamu;
Ili kuelewa maneno ya hekima;
3 Ili kupata nizamu+ yenye inaleta ufahamu,
Haki,+ uwezo wa kuchukua maamuzi ya muzuri,*+ na unyoofu;*
4 Ili kumupatia werevu+ mutu mwenye hana uzoefu;
Ili kumupatia kijana ujuzi na uwezo wa kufikiri.+
5 Mutu mwenye hekima anasikiliza na kujifunza mengi zaidi;+
Mutu mwenye uelewaji anapata ufundi wa kuongoza*+
6 Ili kuelewa mezali na neno la fumbo,*
Maneno ya wenye hekima na vitendawili vyao.+
7 Kumuogopa* Yehova ndio mwanzo wa ujuzi.+
Ni wapumbavu tu ndio wanazarau hekima na nizamu.+
9 Ni taji la maua lenye kuvutia kwa ajili ya kichwa chako+
Na pambo la muzuri kwa ajili ya shingo yako.+
10 Mwana wangu, kama watenda-zambi wanajaribu kukushawishi, usikubali.+
11 Kama wanasema: “Kuja tuende.
Tuvizie ili kumwanga damu.
Tutajificha, tukingojea kushambulia bila sababu watu wenye hawana kosa.
12 Tutawameza wakiwa wazima kama vile Kaburi* linameza,
Wazima-wazima, kama wale wenye kushuka katika shimo.
13 Tukamate hazina zao zote zenye samani;
Nyumba zetu tutazijaza vitu vyenye vinachukuliwa katika vita.
15 Mwana wangu, usiwafuate.
Epusha miguu yako na njia yao.+
16 Kwa maana miguu yao inakimbilia kutenda uovu;
Wanaenda haraka kumwanga damu.+
17 Kwa kweli ni kazi bure kutandika wavu* wakati ndege iko* anaona.
18 Ndio sababu wanavizia ili kumwanga damu;
Wanajificha ili waondoe uzima wa* wengine.
19 Hizo ndizo njia za wale wenye kutafuta faida yenye haiko ya haki,
20 Hekima ya kweli+ inaita kwa sauti kubwa katika barabara.+
Inaendelea kupandisha sauti yake katika viwanja vya watu wote.+
21 Inaita kwa sauti kubwa kwenye makutano ya* barabara zenye watu wengi.
Inasema hivi kwenye milango mikubwa ya muji:+
22 “Ninyi wenye kukosa uzoefu mutaendelea kupenda kukosa uzoefu mupaka wakati gani?
Ninyi wazihaki mutaendelea kufurahia zihaka mupaka wakati gani?
Na ninyi wapumbavu mutaendelea kuchukia ujuzi mupaka wakati gani?+
Halafu nitawamwangia roho yangu;
Nitawajulisha maneno yangu.+
24 Kwa sababu niliwaita, lakini muliendelea kukataa,
Nilinyoosha mukono wangu, lakini hakuna mwenye alikazia uangalifu,+
25 Muliendelea kupuuza mashauri yangu yote
Na kukataa karipio langu,
26 Mimi pia nitacheka wakati musiba utawapata;
Nitafanya zihaka wakati jambo lenye munaogopa sana litakuja,+
27 Wakati jambo lenye munaogopa sana litakuja kama zoruba,
Na wakati musiba wenu utafika kama upepo wa zoruba,
Wakati shida na taabu vitakuja juu yenu.
28 Wakati huo wataendelea kuniita, lakini sitajibu;
Watanitafuta kwa bidii, lakini hawatanipata,+
29 Kwa sababu walichukia ujuzi,+
Na hawakuchagua kumuogopa Yehova.+
30 Walikataa shauri langu;
Walizarau makaripio yangu yote.
32 Kwa maana upotovu wa wajinga utawaua,
Na kukosa kujali kwa wapumbavu kutawaharibu.
2 Mwana wangu, kama unakubali maneno yangu
Na kuweka amri zangu kama hazina,+
2 Kwa kutega sikio lako ili usikilize hekima+
Na kuelekeza moyo wako kwenye utambuzi;+
3 Pia, kama unaita uelewaji kwa sauti+
Na kupandisha sauti yako ili upate utambuzi;+
4 Kama unaendelea kuutafuta kama feza,+
Na kuendelea kuutafuta sana kama hazina zenye kufichwa;+
5 Basi utaelewa maana ya kumuogopa Yehova,+
Na utapata ujuzi juu ya Mungu.+
7 Anaweka kama hazina hekima yenye kutenda kwa ajili ya wanyoofu;
Yeye ni ngao kwa wale wenye kutembea katika uaminifu-mushikamanifu.+
8 Analinda njia za haki,
Na atalinda njia ya washikamanifu wake.+
10 Wakati hekima itaingia katika moyo wako+
Na wakati ujuzi utapendeza nafsi* yako,+
11 Uwezo wa kufikiri utakulinda,+
Na utambuzi utakuchunga,
12 Ili kukuokoa kutoka katika njia ya mubaya,
Kutoka kwa mutu mwenye kusema mambo mapotovu,+
13 Kutoka kwa wale wenye kuacha njia zenye kunyooka
Ili kutembea katika njia za giza,+
14 Kutoka kwa wale wenye kufurahia kutenda mabaya,
Wenye kufurahia upotovu wa uovu,
15 Wale wenye njia zao ni zenye kujikunja-kunja
Na wenye mwenendo wao wote ni mudanganyifu.
16 Utakuokoa kutoka kwa mwanamuke mwenye kupotoka,*
Kutokana na maneno laini* ya mwanamuke mwasherati,*+
17 Mwenye anaacha rafiki wa karibu* wa ujana wake+
Na kusahau agano la Mungu wake;
18 Kwa maana nyumba yake inazama katika kifo,
Na njia zake* zinaongoza kwa wale wenye hawana uwezo katika kifo.+
19 Kati ya wale wenye kulala naye,* hakuna mutu yeyote mwenye atarudia,
Wala hawatarudia kwenye njia za uzima.+
20 Basi fuata njia ya watu wema
Na ubakie kwenye njia za wenye haki,+
21 Kwa maana ni watu wenye kufanya mambo yenye kunyooka tu ndio watakaa katika dunia,
3 Mwana wangu, usisahau mafundisho* yangu,
Na moyo wako ushike amri zangu,
2 Kwa sababu zitakuongezea siku nyingi
Na miaka ya uzima na amani.+
3 Usiruhusu upendo mushikamanifu na uaminifu* vikuache.+
Uvifunge kuzunguka shingo yako;
Uviandike kwenye kibao cha moyo wako;+
4 Halafu utakubaliwa na kupata ufahamu muzuri
Mbele ya macho ya Mungu na ya mwanadamu.+
7 Usikuwe mwenye hekima mbele ya macho yako mwenyewe.+
Umuogope Yehova na ujiepushe na ubaya.
9 Umuheshimie Yehova kupitia vitu vyako vyenye samani,+
Kupitia matunda ya kwanza ya* mazao* yako yote;+
10 Halafu madepo yako yatajazwa kabisa,+
Na mashimo yako ya kukamulia divai yatajaa sana* divai mupya.
11 Mwana wangu, usikatae nizamu ya Yehova,+
Na usichukie karipio lake,+
12 Kwa maana wale wenye Yehova anapenda anawakaripia,+
Kama vile baba anamukaripia mwana mwenye anafurahia sana.+
13 Mwenye furaha ni mutu mwenye anapata hekima+
Na mutu mwenye anapata utambuzi;
14 Kupata hekima ni muzuri kuliko kupata feza,
Na kuipata kama faida ni muzuri kuliko kupata zahabu.+
15 Ni yenye samani kuliko marijani;*
Hakuna kitu chenye unatamani chenye kinaweza kulinganishwa nayo.
16 Maisha ya murefu yanapatikana katika mukono wake wa kuume;
Utajiri na utukufu viko katika mukono wake wa kushoto.
17 Njia zake ni zenye kupendeza,
Na njia zake zote ni zenye amani.+
18 Ni muti wa uzima kwa wale wenye kuishika,
Na wale wenye kuishika sana wataitwa wenye furaha.+
19 Yehova aliweka musingi wa dunia kwa hekima.+
Kwa utambuzi alifanya mbingu zikuwe imara kabisa.+
20 Kwa ujuzi wake maji mengi yalitenganishwa
Na anga zenye mawingu ziliangusha matone-matone ya umande.+
21 Mwana wangu, zisiondoke mbele ya macho yako.*
Linda hekima yenye kutenda na uwezo wa kufikiri;
22 Zitakupatia* uzima
Na zitakuwa pambo kwa ajili ya shingo yako;
23 Halafu utatembea kwa usalama katika njia yako,
25 Hautaogopa jambo lolote lenye kuogopesha sana lenye linatokea bila kutazamia+
Wala zoruba yenye inakuja juu ya waovu.+
28 Usimuambie jirani yako, “Uende; urudie wakati mwingine! Nitakupatia kesho,”
Kama unaweza kumupatia kitu hicho sasa.
29 Usipange kumutendea mubaya jirani yako+
Wakati anafikiri kwamba anaishi kwa usalama karibu na wewe.
31 Usimusikilie wivu mutu mwenye jeuri+
Wala kuchagua yoyote kati ya njia zake,
32 Kwa maana Yehova anachukia mutu mudanganyifu,+
Lakini anafanya urafiki wa karibu pamoja na watu wanyoofu.+
35 Wenye hekima watariti heshima,
Lakini wajinga wanatukuza haya.+
4 Wana wangu, musikilize nizamu ya baba;+
Musikilize kwa uangalifu ili mupate uelewaji,
2 Kwa maana nitawapatia mafundisho ya muzuri;
4 Baba alinifundisha na kusema: “Moyo wako ushike kabisa maneno yangu.+
Shika amri zangu na uendelee kuishi.+
5 Pata hekima, pata uelewaji.+
Usisahau, na usigeuke na kuacha mambo yenye ninasema.
6 Usiiache, nayo itakulinda.
Uipende, nayo itakuchunga.
7 Hekima ndilo jambo la maana zaidi,*+ kwa hiyo pata hekima,
Na pamoja na vyote vyenye unapata, pata uelewaji.+
8 Uione kuwa ya maana sana, nayo itakuinua.+
Itakuheshimia kwa sababu unaikumbatia.+
9 Itatia taji la maua lenye kuvutia kwenye kichwa chako;
Itakupamba kwa taji la uzuri.”
12 Wakati unatembea, hatua zako hazitazuiwa;
Na kama unakimbia, hautajikwaa.
13 Shika kabisa nizamu; usiiache.+
Uilinde, kwa maana ni uzima wako.+
16 Kwa maana hawawezi kulala kama hawajafanya mambo ya mubaya.
Hawapate usingizi kama hawajaangusha mutu.
17 Wanajilisha mukate wa uovu,
Na kunywa divai ya jeuri.
18 Lakini njia ya wenye haki iko kama mwangaza wenye kungaa wa asubui
Wenye kungaa zaidi na zaidi mupaka muchana kamili.+
19 Njia ya waovu iko kama giza;
Hawajue ni nini kinawafanya wajikwae.
20 Mwana wangu, sikiliza maneno yangu;
Sikiliza kwa uangalifu* mambo yenye ninasema.
21 Yasiondoke mbele ya macho yako;
Uyaweke ndani kabisa ya moyo wako,+
22 Kwa maana ni uzima kwa wale wenye kuyapata+
Na afya ya muzuri kwa mwili wao wote.
23 Linda moyo wako kuliko vitu vyote vyenye unalinda,+
Kwa maana ni mule munatoka chemchemi za uzima.
25 Macho yako yanapaswa kuangalia mbele moja kwa moja,
27 Usielekee kuume wala kushoto.+
Epusha miguu yako na mambo ya mubaya.
5 Mwana wangu, sikiliza hekima yangu.
Sikiliza kwa uangalifu* utambuzi wangu,+
2 Ili uweze kulinda uwezo wako wa kufikiri
Na kulinda ujuzi kwa midomo yako.+
3 Kwa maana midomo ya mwanamuke mwenye kupotoka* inaangusha matone-matone kama sega la asali,+
Na kinywa chake ni laini kuliko mafuta.+
4 Lakini mwishowe ni muchungu kama pakanga+
Na mwenye makali kama upanga wenye kukata pande zote mbili.+
5 Miguu yake inashuka kwenye kifo.
Hatua zake zinaongoza moja kwa moja katika Kaburi.*
6 Hafikiriake njia ya uzima.
Njia yake inaenda huku na huku, lakini hajue kwenye inaelekea.
7 Sasa, wana wangu, munisikilize
Na musiache mambo yenye ninasema.
8 Mukae mbali naye;
Musikaribie muingilio wa nyumba yake,+
9 Ili musipatie wengine heshima yenu+
Wala kuvuna miaka ya ukali;+
10 Ili wageni wasimalize mali* zenu+
Na ili vitu vyenye mulifanyia kazi ya jasho visiende katika nyumba ya mugeni.
11 Mukifanya vile, mutalia kwa maumivu kwenye mwisho wa maisha yenu
Wakati nyama yenu na mwili wenu vitakuwa zaifu+
12 Na utasema: “Nilichukia sana nizamu!
Moyo wangu ulizarau sana karipio!
13 Sikusikiliza sauti ya wafundishaji wangu
Wala kusikiliza kwa uangalifu walimu wangu.
17 Yakuwe yako peke yako,
Na yasikuwe ya wageni pamoja na wewe.+
Na ufurahi pamoja na bibi wa ujana wako,+
19 Paa-dike mwenye kupendeza, mbuzi wa milima* mwenye kuvutia.+
Maziwa yake yakushibishe* nyakati zote.
Upendo wake ukuvutie sana kila wakati.+
22 Muovu ananaswa na makosa yake mwenyewe,
Na atashikwa katika kamba za zambi yake mwenyewe.+
23 Atakufa kwa sababu ya kukosa nizamu
Na kupotea njia kwa sababu ya upumbavu wake wenye kupita kiasi.
6 Mwana wangu, kama umeahidi kulipia jirani yako mukopo,+
Kama umepatiana mukono na mugeni,*+
2 Kama umenaswa na ahadi yako,
Kama umekamatwa na maneno ya kinywa chako,+
3 Mwana wangu, fanya hivi na ujiokoe,
Kwa maana umeanguka katika mukono wa jirani yako:
Uende na ujinyenyekeze mwenyewe na kumulilia haraka jirani yako.+
4 Usiruhusu macho yako yapate usingizi,
Wala kope zako kusinzia.
5 Ujiokoe kama swala kutoka katika mukono wa muwindaji,
Kama ndege kutoka katika mukono wa muwindaji wa ndege.
7 Hata kama hana kamanda, ofisa, wala mutawala,
8 Anatayarisha chakula chake wakati wa kipindi cha joto,+
Na kukusanya chakula chake wakati wa mavuno.
9 Wewe muvivu, utaendelea kulala pale mupaka wakati gani?
Utaamuka wakati gani katika usingizi wako?
10 Kulala kidogo, kusinzia kidogo,
Kukunja mikono kidogo ili kupumuzika,+
11 Na umaskini wako utakuja kama munyanganyi,
Na uhitaji wako kama mwanaume mwenye silaha.+
12 Mutu muovu mwenye hana mafaa yoyote anazunguka-zunguka akisema maneno yenye kupotoka;+
13 Anafinya jicho lake,+ anafanya alama kwa muguu wake, na kufanya alama kwa vidole vyake.
17 Macho yenye majivuno,+ ulimi wa uongo,+ na mikono yenye kumwanga damu yenye haina kosa,+
18 Moyo wenye kufanya mipango ya uovu,+ na miguu yenye kukimbilia haraka kwenye uovu,
19 Shahidi wa uongo mwenye kusema uongo kila wakati anapumua,+
Na mutu yeyote mwenye kupanda ugomvi kati ya ndugu.+
21 Uvifunge sikuzote kuzunguka moyo wako;
Uvifunge kuzunguka shingo yako.
22 Wakati utatembea huku na huku, itakuongoza;
Wakati utalala, itakulinda;
Na wakati utaamuka, itasema na wewe.*
24 Yatakulinda na mwanamuke mubaya,+
Yatakulinda na ulimi wenye kushawishi wa mwanamuke mwasherati.*+
25 Usitamani uzuri wake katika moyo wako+
Wala kukubali akuvute kupitia macho yake yenye kuvutia,
26 Kwa maana kahaba anafanya mutu abakie na kipande kimoja tu cha mukate,+
Lakini bibi ya mwanaume mwingine anawinda uzima wenye* samani.
27 Je, mutu anaweza kukusanya moto kwenye kifua chake na nguo zake zisiungue?+
28 Ao je, mutu anaweza kutembea juu ya makaa yenye kuwaka moto na miguu yake isiungue?
29 Ni vile kuhusu mutu yeyote mwenye analala na bibi ya jirani yake;
Hakuna mutu yeyote mwenye kugusa bibi huyo mwenye atakosa kupewa azabu.+
32 Mutu yeyote mwenye kufanya uzinifu na mwanamuke hana akili ya muzuri;*
Ule mwenye kufanya vile analeta uharibifu juu yake mwenyewe.+
4 Ambia hekima, “Wewe ni dada yangu,”
Na uite uelewaji “mutu wa jamaa yangu,”
6 Nikiwa kwenye dirisha la nyumba yangu,
Niliangalia chini kupitia kayungio ya dirisha langu,
7 Na wakati nilikuwa ninachunguza wajinga,*
Nilitambua kati ya vijana, kijana mumoja mwanaume mwenye kukosa akili ya muzuri.*+
8 Alipita katika barabara karibu na makutano ya barabara katika njia yenye kupeleka kwa mwanamuke huyo
Na alishika njia ya kuenda kwenye nyumba ya mwanamuke huyo
9 Mangaribi, wakati giza linaanza,+
Wakati usiku na giza vinaingia.
11 Ni mwenye makelele na iko* kichwa-nguvu.+
Habakiake* katika nyumba yake.
12 Wakati fulani iko* inje, wakati mwingine iko* katika viwanja vya watu wote,
Anajificha karibu na kila makutano ya barabara.+
13 Kisha anamukamata kwa nguvu kijana huyo na kumupatia busu;
Bila haya, mwanamuke huyo anamuambia:
14 “Nilipaswa kutoa zabihu za ushirika.+
Leo nilitimiza naziri zangu.
15 Ndiyo sababu nimekuja kukutana na wewe,
Kukutafuta, na nimekupata!
17 Nimenyunyiza* manemane, udi, na mudalasini juu ya kitanda changu.+
18 Kuja, tukunywe na kushiba upendo mupaka asubui;
Na tujifurahishe pamoja kwa mapendo,
19 Kwa maana bwana yangu haiko nyumbani;
Ameenda safari ya mbali.
20 Alibeba mufuko wa feza,
Na hatarudia mupaka siku ya mwezi wenye kuenea.”
21 Anamupotosha kwa ushawishi mukubwa.+
Anamutongoza kwa maneno laini.
22 Mara moja kijana huyo anamufuata, kama ngombe-dume mwenye anaenda kuchinjwa,
Kama mupumbavu mwenye anaenda kupewa azabu katika mikatale,*+
23 Mupaka wakati mushale unatoboa maini yake;
Kama ndege mwenye anakimbia kuingia katika mutego, hajue kwamba hilo litamufanya apoteze uzima wake.*+
24 Na sasa, wana wangu, munisikilize;
Musikilize kwa uangalifu maneno yenye ninasema.
25 Musiruhusu moyo wenu ugeuke na kufuata njia zake.
Musipotee njia na kufuata njia zake,+
26 Kwa maana amefanya wengi waanguke wakiwa wameuawa,+
Na wale wenye ameua ni wengi sana.+
27 Nyumba yake inaongoza katika Kaburi;*
Inashuka chini kwenye vyumba vya ndani vya kifo.
8 Je, hekima haiite kwa sauti kubwa?
Je, utambuzi haupandishe sauti yake?+
3 Karibu na milango mikubwa yenye kupeleka kwenye muji,
Kwenye miingilio ya milango,
Inaendelea kulia kwa sauti kubwa:+
6 Musikilize, kwa maana mambo yenye ninasema ni ya maana,
Midomo yangu inasema mambo yenye kuwa sawa;
7 Kwa maana kinywa changu kinasema ukweli kwa sauti ya chini,
Na midomo yangu inachukia sana jambo lenye uovu.
8 Maneno yote ya kinywa changu ni yenye haki.
Kati ya maneno hayo, hakuna neno moja lenye kupengama ao lenye kupotoka.
9 Yote yako wazi kabisa kwa mutu mwenye utambuzi
Na yako sawa kwa wale wenye wamepata ujuzi.
10 Mukamate nizamu yangu pa nafasi ya feza,
Na ujuzi pa nafasi ya zahabu safi sana,+
11 Kwa maana hekima ni ya muzuri kuliko marijani;*
Vitu vingine vyote vyenye kutamanika haviwezi kulinganishwa nayo.
13 Kumuogopa Yehova kunamaanisha kuchukia ubaya.+
Ninachukia kujiinua na kiburi+ na njia ya uovu na maneno yenye kupotoka.+
16 Kwa musaada wangu wakubwa wanaendelea kutawala,
Na watu wenye vyeo wanahukumu kwa haki.
19 Matunda yangu ni ya muzuri kuliko zahabu, hata kuliko zahabu yenye kusafishwa,
Na mazao yangu ni ya muzuri kuliko feza ya muzuri kabisa.+
20 Ninatembea katika njia ya uadilifu,*
Katikati ya njia za haki;
21 Ninapatia wale wenye kunipenda uriti mwingi,
Na ninajaza madepo yao.
24 Wakati hapakukuwa maji yenye kuenda chini sana,+ nilizaliwa,*
Wakati hapakukuwa chemchemi zenye kujaa sana maji.
25 Mbele milima haijawekwa mahali pake,
Mbele vilima vikuwe, nilizaliwa,
26 Wakati alikuwa hajaumba dunia na maeneo yake ya mashamba
Wala madonge ya kwanza ya udongo wa dunia.
27 Wakati alitayarisha mbingu,+ nilikuwa pale;
Wakati alichora mwisho* kwenye uso wa maji,+
28 Wakati alifanya imara* mawingu yenye kuwa juu,
Wakati aliweka musingi wa chemchemi za mahali kwenye maji yenye kuenda chini sana,
29 Wakati alitilia bahari sheria
Kwamba maji yake yasipite agizo lake,+
Wakati aliweka* misingi ya dunia,
Mimi ndiye alipenda sana+ siku kwa siku;
Nilifurahi mbele yake wakati wote;+
31 Nilifurahia dunia yake yenye kuikaliwa na watu,
Na wana wa binadamu* ndio nilipenda zaidi sana.
32 Na sasa, wana wangu, munisikilize;
Ndiyo, wenye furaha ni wale wenye wanashika njia zangu.
34 Mwenye furaha ni mutu mwenye ananisikiliza
Kwa kuja mbele ya wakati* kwenye milango yangu siku kwa siku,
Kwa kungojea karibu na miimo ya milango yangu;
35 Kwa maana mwenye kunipata atapata uzima,+
Na anakubaliwa na Yehova.
9 Hekima ya kweli imejenga nyumba yake;
Imechonga nguzo zake saba (7).
4 “Mutu yeyote mwenye hana uzoefu, aingie humu.”
Anamuambia ule mwenye hana akili ya muzuri:*
5 “Kuja, ukule mukate wangu
Na ukunywe divai yenye nilichanganya.
7 Ule mwenye kumurekebisha mutu mwenye zihaka anaalika haya,+
Na mutu yeyote mwenye kumukaripia mutu muovu ataumia.
8 Usimukaripie mutu mwenye zihaka, kwa maana atakuchukia.+
Karipia mwenye hekima, naye atakupenda.+
9 Patia mwenye hekima, na atakuwa mwenye hekima zaidi.+
Fundisha mwenye haki, na elimu yake itaongezeka.
12 Kama unakuwa mwenye hekima, unakuwa mwenye hekima kwa faida yako mwenyewe,
Lakini kama uko mwenye zihaka, utabeba zihaka hiyo peke yako.
13 Mwanamuke mujinga ni mwenye fujo.+
Yeye ni mujinga na hajue kitu.
14 Anakaa kwenye muingilio wa nyumba yake
Kwenye kiti katika mahali pa juu pa muji,+
15 Anaita kwa sauti kubwa wale wenye kupita karibu naye,
Wale wenye kuenda mbele moja kwa moja katika njia yao:
16 “Mutu yeyote mwenye hana uzoefu, aingie humu.”
Anaambia wale wenye hawana akili ya muzuri:*+
18 Lakini hawajue kwamba wale wenye hawana uwezo katika kifo wako pale,
Kwamba wageni wake wanapatikana katika sehemu za chini kabisa za Kaburi.*+
Mwana mwenye hekima anamufurahisha baba yake,+
Lakini mwana mupumbavu ni huzuni kwa mama yake.
2 Mali zenye zilipatikana kwa uovu hazitakuwa na faida yoyote,
Lakini haki ndiyo inaokoa katika kifo.+
5 Mwana mwenye kutenda kwa ufahamu anakusanya mazao wakati wa kipindi cha joto,
Lakini mwana mwenye kutenda kwa haya analala usingizi muzito wakati wa mavuno.+
8 Mutu mwenye moyo wa hekima atakubali mafundisho,*+
Lakini mwenye kuzungumuza maneno ya ujinga atakanyangiwa chini.+
9 Mwenye kutembea kwa uaminifu-mushikamanifu atatembea kwa usalama,+
Lakini mwenye kupotosha njia zake atajulikana.+
10 Mwenye kufinya jicho lake kwa udanganyifu anatokeza huzuni,+
Na ule mwenye kuzungumuza maneno ya ujinga atakanyangiwa chini.+
13 Hekima inapatikana kwenye midomo ya mutu mwenye utambuzi,+
Lakini fimbo ni kwa ajili ya mugongo wa mutu mwenye hana akili ya muzuri.*+
15 Mali ya* tajiri ni muji wake wenye ngome.
Uharibifu wa maskini ni umaskini wao.+
17 Mwenye kutii nizamu ni njia yenye inapeleka kwenye uzima,*
Lakini mwenye anapuuza karipio anapoteza wengine.
19 Wakati maneno ni mengi, kosa haliwezi kuepukwa,+
Lakini mutu yeyote mwenye anazuia midomo yake anatenda kwa busara.+
23 Kujiingiza katika mwenendo wa haya ni kama muchezo kwa mujinga,
Lakini hekima ni ya mutu mwenye utambuzi.+
31 Kinywa cha mwenye haki kinatokeza* hekima,
Lakini ulimi wenye kupotoka utakatwa.
32 Midomo ya mwenye haki inajua mambo yenye kupendeza,
Lakini kinywa cha waovu kimepotoka.
5 Haki ya mwenye hana lawama inanyoosha njia yake,
Lakini muovu ataanguka kwa sababu ya uovu wake mwenyewe.+
7 Wakati mutu muovu anakufa, tumaini lake linapotea;
Na matumaini yenye kutegemea nguvu zake yanapotea pia.+
10 Wema wa wenye haki unafanya muji ushangilie,
Na wakati waovu wanaangamia, kunakuwa vigelegele vya shangwe.+
12 Mutu yeyote mwenye hana akili ya muzuri* anamuzarau jirani yake,
Lakini mutu mwenye utambuzi wa kweli anabakia kimya.+
15 Mutu yeyote mwenye anaahidi kulipia mugeni mukopo hakika ataumia,+
Lakini mutu yeyote mwenye anaepuka* kupana mukono katika kiapo atakuwa salama.
18 Mutu muovu anapata mushahara wa udanganyifu,+
Lakini mutu mwenye kupanda haki anapata zawabu ya kweli.+
19 Mwenye kutetea haki bila kuyumba-yumba atapata uzima,+
Lakini mwenye kufuatilia uovu anaelekea kwenye kifo.
20 Wale wenye kupotoka katika moyo ni chukizo kwa Yehova,+
Lakini wale wenye njia yao haina lawama wanamufurahisha.+
21 Ukuwe hakika na jambo hili:* Mutu muovu hatakosa kupewa azabu,+
Lakini watoto wa mwenye haki wataponyoka.
22 Kama pete ya zahabu katika pua ya nguruwe
Ni vile pia mwanamuke mwenye sura na umbo ya muzuri mwenye anakataa akili ya muzuri.
23 Tamaa ya wenye haki inaongoza kwenye mema,+
Lakini tumaini la waovu linaongoza kwenye kasirani kali.
24 Mutu mumoja anatoa kwa ukarimu* na kujikuta na vitu vingi zaidi;+
Mwingine anaima wengine kile wanapaswa kupewa, lakini anakuwa maskini.+
26 Watu watalaani mwenye anaficha nafaka,
Lakini watabariki mwenye anaiuzisha.
27 Mwenye anatafuta kwa bidii kutenda mema anatafuta kukubaliwa,+
Lakini mwenye anatafuta ubaya—hakika ubaya ndio utamupata.+
29 Mutu yeyote mwenye kuleta taabu* juu ya watu wa nyumba yake atariti upepo,+
Na mupumbavu atakuwa mutumishi wa mutu mwenye moyo wa hekima.
31 Kama, kwa kweli, mwenye haki katika dunia anapewa zawabu,
Itakuwa namna gani kwa muovu na kwa mutenda-zambi!+
3 Hakuna mutu mwenye anakuwa na usalama kwa kutenda uovu,+
Lakini wenye haki hawatangolewa hata kidogo.
4 Bibi mwenye uwezo ni taji kwa bwana yake,+
Lakini bibi mwenye kutenda mambo ya haya ni kama kuoza katika mifupa ya bwana yake.+
5 Mawazo ya wenye haki ni ya haki,
Lakini muongozo wa waovu ni udanganyifu.
8 Mutu anasifiwa kwa sababu ya busara ya kinywa chake,+
Lakini mutu mwenye kuwa na moyo wenye kupotoka atatendewa kwa zarau.+
11 Mwenye analima shamba lake atakuwa na chakula kingi,+
Lakini mwenye kufuatilia vitu vyenye havina mafaa yoyote hana akili ya muzuri.*
12 Mutu muovu anatamani kitu chenye kilikamatwa na watu wengine waovu,
Lakini muzizi wa wenye haki unazaa matunda.
14 Mutu anashiba mema kutokana na matunda ya maneno yake,*+
Na kazi ya mikono yake itamupatia zawabu.
17 Mwenye anatoa ushuhuda kwa uaminifu atasema kweli,*
Lakini shahidi wa uongo anasema mambo ya udanganyifu.
18 Maneno yenye kusemwa bila kufikiri yanatoboa kama upanga,
Lakini ulimi wa mwenye hekima unaponyesha.+
19 Midomo yenye kusema kweli itadumu milele,+
Lakini ulimi wenye kusema uongo utadumu wakati kidogo tu.+
20 Udanganyifu uko katika moyo wa wale wenye kufanya mipango mibaya,
21 Hakuna mambo yenye kuumiza yenye yatamupata mwenye haki,+
Lakini waovu watapatwa na misiba mingi.+
22 Midomo yenye kusema uongo ni chukizo kwa Yehova,+
Lakini wale wenye kutenda kwa uaminifu wanamufurahisha.
23 Mutu mwerevu anaficha mambo yenye anajua,
Lakini moyo wa mupumbavu unasema-sema mambo ya upumbavu.+
26 Mwenye haki anatafuta malisho yake,
Lakini njia ya waovu inawapoteza.
28 Njia ya haki inaongoza kwenye uzima;+
Hakuna kifo katika njia hiyo.
13 Mwana mwenye hekima anakubali nizamu ya baba yake,+
Lakini mwenye kuchekelea wengine hasikilize wakati anakemewa.*+
2 Mutu atakula mambo ya muzuri kutokana na matunda ya maneno yake,*+
Lakini tamaa kabisa* ya wadanganyifu ni jeuri.
3 Mwenye analinda kinywa chake* analinda uzima wake,*+
Lakini mwenye anafungua wazi midomo yake ataharibiwa.+
7 Kuko mutu mwenye anajifanya kama tajiri ijapokuwa hana kitu;+
Kuko mwingine mwenye anajifanya kama maskini ijapokuwa iko* na mali nyingi.
11 Mali yenye kupatikana haraka* itapunguka,+
Lakini mali ya ule mwenye anaikusanya kidogo-kidogo* itaongezeka.
12 Tazamio* lenye kucheleweshwa linafanya moyo ugonjwe,+
Lakini tamaa yenye imetimizwa ni muti wa uzima.+
13 Mutu yeyote mwenye anazarau mafundisho* atalipia kosa lake,+
Lakini mwenye anaheshimia amri atapewa zawabu.+
15 Ufahamu mwingi unafanya mutu akubaliwe,
Lakini njia ya wadanganyifu iko nguvu sana.
18 Mutu yeyote mwenye anapuuza nizamu anakuwa maskini na anapata haya,
20 Mwenye anatembea na wenye hekima atakuwa na hekima,+
Lakini mwenye kufanya urafiki na wajinga ataumia.+
22 Mutu mwema anaachia wajukuu wake uriti,
Lakini mali ya mutenda-zambi itawekwa akiba kwa ajili ya mwenye haki.+
23 Shamba la maskini lenye kulimwa linazaa chakula kingi,
Lakini ukosefu wa haki unaweza kuliharibu.*
14 Mwanamuke mwenye hekima kabisa anajenga nyumba yake,+
Lakini mwanamuke mupumbavu anaibomoa kwa mikono yake mwenyewe.
2 Mutu mwenye kutembea katika unyoofu wake anamuogopa Yehova,
Lakini ule mwenye njia zake ni za udanganyifu* anamuzarau Yeye.
3 Fimbo ya kiburi iko katika kinywa cha mupumbavu,
Lakini midomo ya wenye hekima itawalinda.
4 Kwenye hakuna ngombe, chombo cha kukulishia wanyama kiko safi,
Lakini nguvu za ngombe-dume zinaleta mavuno mengi.
6 Mutu mwenye kuchekelea wengine anatafuta hekima lakini haipate hata kidogo,
Lakini ujuzi unakuja kwa urahisi kwa mutu mwenye uelewaji.+
8 Kwa hekima, mutu mwerevu anaelewa njia yenye anafuata,
10 Moyo unajua uchungu wake mwenyewe,*
Na hakuna mutu wa inje mwenye anaweza kushiriki katika furaha yake.
12 Kuko njia yenye inaonekana kuwa sawa mbele ya macho ya mutu,+
Lakini mwishowe inaongoza kwenye kifo.+
13 Hata katika kicheko moyo unaweza kusikia maumivu,
Na shangwe inaweza kuishia katika huzuni.
14 Mutu mwenye kupotoka katika moyo atavuna matokeo ya njia zake,+
Lakini mutu muzuri anavuna zawabu ya matendo yake.+
17 Mutu mwenye kukasirika haraka anatenda kwa ujinga,+
Lakini mutu mwenye kufikiri sana juu ya mambo* anachukiwa.
19 Watu wabaya watalazimika kuinama mbele ya watu wema,
Na waovu watainama kwenye milango mikubwa ya wenye haki.
21 Mwenye anazarau jirani yake anatenda zambi,
Lakini mutu yeyote mwenye anaonyesha huruma watu wa hali ya chini ni mwenye furaha.+
22 Je, wale wenye kufanya mipango mibaya hawatapotea njia?
Lakini wale wenye nia ya kutenda mema watapata upendo mushikamanifu na uaminifu.+
27 Kumuogopa Yehova ni chemchemi ya uzima,
Ili kuepusha mutu na mitego ya kifo.
29 Mutu mwenye hakasirike haraka iko* na utambuzi mwingi,+
Lakini mwenye hana uvumilivu anaonyesha upumbavu wake.+
31 Mwenye anapunja mutu wa hali ya chini anatukana Mutengenezaji wake,+
Lakini mutu yeyote mwenye anasikilia maskini huruma anamutukuza Mungu.+
32 Uovu wa muovu utamushusha chini,
Lakini mwenye haki atapata kimbilio katika uaminifu-mushikamanifu wake.+
33 Hekima inakaa kimya katika moyo wa mutu mwenye uelewaji,+
Lakini inapaswa kujijulisha kati ya wajinga.
35 Mufalme anafurahia mutumishi mwenye anatenda kwa ufahamu,+
Lakini kasirani yake inawaka juu ya ule mwenye kutenda kwa haya.+
10 Nizamu inaonekana kuwa mubaya* kwa mutu mwenye anaacha njia,+
Lakini mutu yeyote mwenye anachukia karipio atakufa.+
11 Kaburi* na mahali pa uharibifu* viko wazi kabisa mbele ya macho ya Yehova.+
Namna gani mioyo ya wanadamu!+
12 Mutu mwenye kuchekelea wengine hapendi mutu mwenye anamurekebisha.*+
Hatatafuta shauri kwa wenye hekima.+
15 Siku zote za mutu mwenye kuteseka ziko mubaya,+
Lakini mutu mwenye moyo wa furaha* iko* na karamu sikuzote.+
17 Ni muzuri zaidi kula mboga za majani mahali kwenye kuko upendo+
Kuliko kula ngombe-dume mwenye kunenepa* mahali kwenye kuko chuki.+
18 Mutu mwenye kukasirika-kasirika anachochea muzozo,+
Lakini mutu mwenye hakasirike haraka anatuliza ugomvi.+
19 Njia ya muvivu ni kama lupango ya miiba,+
Lakini njia ya watu wanyoofu ni kama barabara kubwa yenye kusawazika.+
21 Mutu mwenye hana akili ya muzuri* anafurahia upumbavu,+
Lakini mutu mwenye utambuzi anaenda mbele bila kugeuka.+
22 Mipango inashindikana wakati hakuna mazungumuzo,*
Lakini mambo yanatimizwa kupitia washauri wengi.+
23 Mutu anafurahi sana wakati anatoa jibu lenye kufaa,*+
Na neno lenye kusemwa wakati wenye kufaa—ni la muzuri sana!+
26 Yehova anachukia sana mipango ya mubaya ya mutu muovu,+
Lakini maneno yenye kupendeza ni safi Kwake.+
28 Moyo wa mwenye haki unafikiri sana mbele ya kujibu,*+
Lakini kinywa cha waovu kinasema-sema mambo ya mubaya.
32 Mutu yeyote mwenye anakataa nizamu anazarau uzima wake,*+
Lakini kila mutu mwenye anasikiliza karipio anapata uelewaji.*+
5 Kila mutu mwenye kiburi katika moyo ni chukizo kwa Yehova.+
Ukuwe hakika kwamba* hatakosa kupewa azabu.
6 Kwa upendo mushikamanifu na uaminifu, kosa linafunikwa,+
Na kwa kumuogopa Yehova mutu anajiepusha na ubaya.+
10 Uamuzi wenye kuongozwa na roho* unapaswa kuwa kwenye midomo ya mufalme;+
Hapaswe hata kidogo kusaliti haki.+
11 Mizani* na vipimo vyenye kuwa sawa vinatoka kwa Yehova;
Majiwe yote ya kupimia yenye kuwa katika mufuko ni kazi yake.+
12 Matendo maovu yanachukiza wafalme,+
Kwa maana kiti cha ufalme kinafanywa kuwa imara kabisa kupitia haki.+
13 Maneno ya haki yanafurahisha wafalme.
Wanapenda mutu mwenye anasema kweli.+
15 Katika mwangaza wa uso wa mufalme kuko uzima;
Kukubaliwa naye ni kama wingu la mvua wakati wa kipindi cha mvua ya mwisho.+
16 Ni muzuri sana kupata hekima kuliko zahabu!+
Inafaa kuchagua uelewaji kuliko kuchagua feza.+
17 Barabara kubwa ya watu wanyoofu inaepuka mambo ya mubaya.
Kila mutu mwenye analinda njia yake analinda uzima wake.*+
19 Ni muzuri zaidi kuwa munyenyekevu* kati ya wapole+
Kuliko kupata sehemu ya vitu vyenye watu wenye majivuno walichukua katika vita.
20 Mutu mwenye anaonyesha ufahamu katika jambo atapata mafanikio,*
Na mwenye furaha ni ule mwenye anamutegemea Yehova.
22 Ufahamu ni chemchemi ya uzima kwa wenye kuwa nao,
Lakini wapumbavu wanapewa nizamu kwa upumbavu wao wenyewe.
25 Kuko njia yenye inaonekana kuwa sawa mbele ya macho ya mutu,
Lakini mwishowe inaongoza kwenye kifo.+
27 Mutu mwenye hana mafaa yoyote anachimbua mambo ya mubaya;+
Na maneno yake ni kama moto wenye kuunguza.+
29 Mutu mwenye jeuri anashawishi jirani yake
Na kumuongoza katika njia ya mubaya.
30 Anafinya jicho lake wakati anafanya mipango yenye kuumiza.
Anakaza midomo yake pamoja wakati anafanya jambo lenye kuumiza.
32 Mutu mwenye hakasirike haraka+ ni muzuri zaidi kuliko mwanaume mwenye nguvu,
Na mutu mwenye kuzuia kasirani yake* ni muzuri zaidi kuliko mutu mwenye anashinda muji.+
33 Kura inapigwa katika sehemu ya nguo yenye kufunika mapaja,+
Lakini kila uamuzi wenye unafanywa kwa kura hiyo unatoka kwa Yehova.+
2 Mutumishi mwenye ufahamu atatawala juu ya mwana mwenye anatenda kwa haya;
Atapokea uriti kama mumoja wa ndugu za mwana huyo.
3 Chungu cha kusafishia ni kwa ajili ya feza na tanuru ni kwa ajili ya zahabu,+
Lakini Yehova ndiye anachunguza mioyo.+
4 Mutu muovu anasikiliza maneno yenye kuumiza,
Na mutu mudanganyifu anasikiliza ulimi wenye uovu.+
5 Mutu yeyote mwenye kuchekelea maskini anatukana Mutengenezaji wake,+
Na kila mutu mwenye anafurahia musiba wa mwingine hatakosa kupewa azabu.+
7 Maneno manyoofu* hayamufae mupumbavu.+
Namna gani maneno ya uongo kwa mutawala!*+
8 Zawadi ni kama jiwe lenye samani kwa mwenye kuwa nayo;*+
Kila mahali kwenye anageukia, linamuletea mafanikio.+
9 Kila mutu mwenye anasamehe* kosa anatafuta upendo,+
Lakini ule mwenye anaendelea kuongea juu ya jambo anatenganisha marafiki wa karibu.+
11 Mutu mubaya anatafuta uasi tu,
Lakini mujumbe mwenye hana huruma atatumwa ili kumupatia azabu.+
12 Ni muzuri zaidi kukutana na dubu mwenye amepoteza vitoto vyake
Kuliko kukutana na mujinga katika upumbavu wake.+
13 Kama mutu analipa ubaya kwa wema,
Ubaya hautaondoka katika nyumba yake.+
15 Mutu yeyote mwenye kumuhesabia muovu kuwa hana kosa na mutu yeyote mwenye kumuhukumu mwenye haki kuwa na kosa+
—Wote wawili ni chukizo kwa Yehova.
17 Rafiki wa kweli anapenda nyakati zote+
Naye ni ndugu mwenye amezaliwa kwa ajili ya nyakati za taabu.+
18 Mutu mwenye hana akili ya muzuri* anapana mukono na kukubali
Kulipia mwingine mukopo mbele ya jirani yake.+
19 Mutu mwenye anapenda ugomvi anapenda kosa.+
Kila mutu mwenye anainua mahali pake pa kuingilia anaalika taabu.+
20 Mutu mwenye kupotoka katika moyo hatapata mafanikio,*+
Na ule mwenye kusema maneno ya udanganyifu ataanguka katika uharibifu.
21 Baba mwenye anazaa mutoto mwenye hana akili atakuwa na huzuni;
Na baba ya mutoto mwenye hana akili hana furaha.+
24 Hekima iko kabisa mbele ya mutu mwenye utambuzi,
Lakini macho ya mujinga yanaenda huku na huku mupaka kwenye miisho ya dunia.+
26 Haiko muzuri kumupatia mwenye haki azabu,*
Na kupiga viboko watu wenye kuheshimiwa ni kinyume na mambo yenye kuwa sawa.
28 Hata mupumbavu mwenye anabakia kimya ataonwa kuwa mwenye hekima,
Na ule mwenye anafunga midomo yake, ataonwa kuwa mwenye utambuzi.
18 Kila mutu mwenye anajitenga na wengine anafuatilia tamaa zake mwenyewe za uchoyo;
Anakataa* hekima yote yenye kutumika.
2 Mutu mujinga hafurahie uelewaji;
Lakini anafurahia kufunua mambo yenye kuwa katika moyo wake.+
3 Wakati mutu muovu anakuja, zarau inakuja pia,
Na kukosa heshima kunakuja pamoja na haya.+
4 Maneno ya kinywa cha mutu ni maji yenye kuenda chini sana.+
Chemchemi ya hekima ni muto mudogo wenye kububujika.
9 Kila mutu mwenye kuwa muvivu katika kazi yake
Ni ndugu ya mutu mwenye kuleta uharibifu.+
10 Jina la Yehova ni munara wenye nguvu.+
Mwenye haki anakimbilia ndani na kupata ulinzi.*+
12 Mbele ya kuanguka kwa kishindo moyo wa mutu ni wenye kiburi,+
Na mbele ya utukufu kuko unyenyekevu.+
13 Wakati mutu anajibu mbele ya kusikia ukweli wa mambo,
Huo ni upumbavu na haya.+
14 Roho ya mutu inaweza kumutegemeza katika ugonjwa,+
16 Zawadi ya mwanadamu inamufungulia njia;+
Inamuwezesha kufika mbele ya wakubwa.
23 Maskini anabembeleza wakati anaongea,
Lakini tajiri anajibu kwa ukali.
24 Kuko marafiki wenye kuwa tayari kuumizana,+
Lakini kuko rafiki mwenye anashikamana sana na mutu kuliko ndugu.+
19 Ni muzuri zaidi kuwa maskini na kutembea katika uaminifu-mushikamanifu+
Kuliko kuwa mujinga na kusema uongo.+
3 Upumbavu wa mutu ndio unapotosha njia yake,
Na moyo wake unamukasirikia sana Yehova.
4 Mali inavuta marafiki wengi,
Lakini hata rafiki ya maskini atamuacha.+
5 Shahidi wa uongo hatakosa kupewa azabu,+
Na ule mwenye anasema uongo kila wakati anapumua hataponyoka.+
6 Wengi wanatafuta kukubaliwa na mutu mwenye cheo,*
Na kila mutu ni rafiki ya mutu mwenye kutoa zawadi.
Anawafuatilia ili awaombe mambo fulani, lakini hakuna mwenye anamusikiliza.
8 Kila mutu mwenye anapata akili ya muzuri* anajipenda mwenyewe.*+
Kila mutu mwenye anapendezwa sana na utambuzi atapata mafanikio.*+
9 Shahidi wa uongo hatakosa kupewa azabu,
Na ule mwenye anasema uongo kila wakati anapumua ataangamia.+
10 Mupumbavu hastahili kuishi maisha ya raha;
Namna gani mutumishi kutawala wakubwa!+
12 Kasirani kali ya mufalme ni kama mungurumo wa simba,*+
Lakini kukubaliwa naye ni kama umande juu ya majani.
13 Mwana mujinga anamuletea baba yake shida,+
Na bibi mugomvi* ni kama sehemu ya juu ya nyumba yenye haiache kuvuya hata kidogo.+
14 Nyumba na mali vinaritiwa kutoka kwa baba,
Lakini bibi mwenye busara anatoka kwa Yehova.+
15 Uvivu unaleta usingizi muzito,
Na mutu muregevu atakuwa na njaa.+
19 Mutu mwenye kukasirika-kasirika atalipia kosa lake;
Ukijaribu kumuokoa, utalazimika kufanya vile tena na tena.+
22 Kitu chenye kutamanika ndani ya mutu ni upendo wake mushikamanifu;+
Na ni muzuri zaidi kuwa maskini kuliko kuwa muongo.
23 Kumuogopa Yehova kunaongoza kwenye uzima;+
Ule mwenye kuwa na woga huo atapumuzika muzuri, hatapatwa na mambo yenye kuumiza.+
24 Muvivu anazika mukono wake katika bakuli la karamu,
Lakini hajikaze hata kuurudisha katika kinywa chake.+
25 Piga mwenye zihaka,+ ili mwenye hana uzoefu akuwe mwerevu,+
Karipia mwenye uelewaji, ili aongeze ujuzi wake.+
26 Mwenye anatendea baba yake mubaya na kufukuza mama yake
Ni mwana mwenye kuleta haya na aibu.+
27 Mwana wangu, ukiacha kusikiliza nizamu,
Utakengeuka na kuacha maneno ya ujuzi.
20 Divai ni muzihaki,+ pombe inamufanya mutu kuwa kichwa-nguvu;+
Kila mutu mwenye anapotoshwa navyo hana hekima.+
2 Kuogopesha sana kwa mufalme ni kama mungurumo wa simba;*+
Kila mutu mwenye anaamusha kasirani yake anatia uzima wake mwenyewe katika hatari.+
4 Muvivu halime wakati wa kipindi cha baridi,
Kwa hiyo atakuwa anaomba-omba katika kipindi cha mavuno wakati hatakuwa na kitu.*+
5 Mawazo* ya moyo wa mutu ni kama maji yenye kuenda chini sana,
Lakini mutu mwenye utambuzi anayashota.
6 Watu wengi wanatangaza upendo wao mushikamanifu,
Lakini ni nani anaweza kupata mutu muaminifu?
7 Mwenye haki anatembea katika uaminifu-mushikamanifu wake.+
Watoto* wake wenye kuja kisha yeye watakuwa na furaha.+
8 Wakati mufalme anakaa kwenye kiti cha ufalme ili kuhukumu,+
Anayungulula uovu wote kwa macho yake.+
12 Sikio lenye linasikia na jicho lenye linaona
—Yehova ameumba vyote viwili.+
13 Usipende usingizi, ukiupenda utakuwa maskini.+
Fungua macho yako, na utashiba mukate.+
14 “Haiko kizuri, haiko kizuri!” ni vile mwenye kununua anasema;
Kisha anaenda zake na kujisifu.+
16 Kamata nguo ya mutu ikiwa ameahidi kulipia mugeni mukopo;+
Umunyanganye kitu chenye aliwekesha kwa ajili ya mukopo ikiwa alifanya vile kwa ajili ya mwanamuke mugeni.*+
17 Mukate wenye ulipatikana kwa udanganyifu ni mutamu kwa mutu,
Lakini kisha, kinywa chake kitajaa majiwe ya kidogo-kidogo.+
19 Muchongezi anaenda huku na huku akifunua mazungumuzo ya siri;+
Usishirikiane na mutu mwenye anapenda kupiga porojo.*
20 Kila mutu mwenye analaani baba yake na mama yake,
Taa yake itazimwa wakati giza litaingia.+
21 Uriti wenye unapatikana kwanza kwa pupa
Mwishowe hautakuwa baraka.+
22 Usiseme: “Nitalipiza uovu!”+
Tumainia Yehova,+ naye atakuokoa.+
25 Ni mutego kwa mutu kutangaza haraka-haraka, “Ni kitakatifu!”+
Na kisha tu wakati fulani anachunguza kile aliwekea naziri.+
27 Pumuzi ya mutu ni taa ya Yehova,
Inachunguza kabisa utu wake wa ndani sana.
28 Upendo mushikamanifu na uaminifu vinamulinda mufalme;+
Kwa upendo mushikamanifu anafanya kiti chake cha ufalme kikuwe imara.+
21 Moyo wa mufalme ni kama mito midogo ya maji katika mukono wa Yehova.+
Anauongoza mahali popote kwenye anapenda.+
2 Njia zote za mwanadamu zinaonekana kuwa sawa mbele ya macho yake,+
3 Kufanya mambo yenye kuwa sawa na ya haki
Kunamupendeza Yehova zaidi kuliko zabihu.+
4 Macho yenye kiburi na moyo wenye majivuno
—Taa yenye inaongoza waovu ni zambi.+
5 Mipango ya wenye bidii hakika inaleta mafanikio,*+
Lakini wale wote wenye kutenda haraka-haraka hakika watakuwa maskini.+
6 Kupata hazina kupitia ulimi wenye kusema uongo
7 Jeuri ya waovu itawaharibu,+
Kwa maana wanakataa kutenda haki.
8 Njia ya mutu mwenye hatia ni yenye kujikunja-kunja,
Lakini matendo ya mutu safi ni yenye kunyooka.+
9 Ni muzuri zaidi kuishi kwenye pembe ya sehemu ya juu ya nyumba
11 Wakati mwenye zihaka anapewa azabu, mwenye hana uzoefu anakuwa na hekima zaidi,
Na wakati mutu mwenye hekima anapata ufahamu, anapata ujuzi.*+
12 Mwenye Haki anachunguza nyumba ya muovu;
Anapindua waovu na kuwaharibu.+
13 Kila mutu mwenye anafunga sikio lake ili asisikie kilio cha mutu wa hali ya chini
Yeye mwenyewe ataita naye hatajibiwa.+
14 Zawadi yenye kutolewa kwa uficho inatuliza hasira,+
15 Mwenye haki anafurahia kutenda kwa haki,+
Lakini ni jambo la mubaya sana kwa wale wenye kutenda uovu.
16 Mutu mwenye anakengeuka na kuacha njia ya ufahamu
Atapumuzika katika kikundi cha wale wenye hawana uwezo katika kifo.+
18 Muovu ni bei ya ukombozi kwa ajili ya mwenye haki,
Na mudanganyifu atakamatwa pa nafasi ya watu wanyoofu.+
19 Ni muzuri zaidi kuishi katika jangwa
Kuliko kuishi na bibi mugomvi* na mwenye kukasirika-kasirika.+
20 Hazina yenye samani na mafuta vinapatikana katika nyumba ya mwenye hekima,+
Lakini mutu mujinga atatumia mubaya* vitu vyenye iko* navyo.+
22 Mutu mwenye hekima anaweza kupanda katika* muji wa watu wenye nguvu
Na kupunguza nguvu zenye wanategemea.+
24 Mutu mwenye kimbelembele, mwenye kujisifu-sifu, ni vile unamuita
Mutu mwenye kutenda kwa kimbelembele bila kujali.+
25 Kile mutu muvivu anatamani sana kitamuua,
Kwa maana mikono yake inakataa kufanya kazi.+
26 Anatamani sana kwa pupa muchana wote,
Lakini mwenye haki anatoa, haime wengine kitu.+
27 Zabihu ya muovu inachukiza.+
Namna gani wakati anaitoa na nia yenye uovu!*
28 Shahidi mwenye kusema uongo ataangamia,+
Lakini mutu mwenye anasikiliza atatoa ushuhuda kwa mafanikio.*
30 Hakuna hekima, wala utambuzi wowote, wala shauri katika kumupinga Yehova.+
22 Inafaa kuchagua jina la muzuri* kuliko kuchagua mali nyingi;+
Kuheshimiwa* ni muzuri kuliko feza na zahabu.
2 Matajiri na maskini wanafanana katika jambo hili:*
Yehova aliwaumba wote.+
3 Mutu mwerevu anaona hatari na kujificha,
Lakini wenye hawana uzoefu wanaendelea mbele na kupata matokeo ya mubaya.*
4 Matokeo ya unyenyekevu na kumuogopa Yehova
Ni utajiri na utukufu na uzima.+
5 Miiba na mitego iko kwenye njia ya mutu mwenye kupotoka,
Lakini kila mutu mwenye anaona uzima wake kuwa wa* maana anakaa mbali nayo.+
8 Kila mutu mwenye anapanda ukosefu wa haki atavuna musiba,+
Na fimbo ya kasirani yake kali itafikia mwisho wake.+
11 Mutu mwenye anapenda moyo safi na mwenye anasema maneno yenye kupendeza
Atakuwa rafiki ya mufalme.+
12 Macho ya Yehova yanalinda ujuzi,
Lakini Yeye anapindua maneno ya wadanganyifu.+
13 Muvivu anasema: “Simba iko* inje!
Nitauawa katikati ya kiwanja cha watu wote!”+
14 Kinywa cha wanamuke wenye kupotoka* ni shimo la murefu.+
Mwenye anahukumiwa na Yehova ataangukia ndani yake.
15 Upumbavu umefungwa katika moyo wa mutoto mwanaume,*+
Lakini fimbo ya nizamu itauondolea mbali naye.+
16 Mwenye anamupunja maskini ili aongeze mali yake+
Na ule mwenye anapatia matajiri zawadi
Mwishowe watakuwa maskini.
17 Tega sikio lako na usikilize maneno ya wenye hekima,+
Ili ufanye moyo wako uzame katika ujuzi wangu,+
18 Kwa maana inapendeza kuchunga maneno hayo ndani yako kabisa,+
Ili yote yakuwe kwenye midomo yako kila wakati.+
19 Ili umutumainie Yehova,
Ninakupatia ujuzi leo.
20 Je, tayari sijakuandikia,
Ili kukupatia mashauri na ujuzi,
21 Ili nikufundishe maneno ya kweli yenye kutegemeka,
Kusudi uweze kumupelekea habari ya kweli ule mwenye alikutuma?
22 Usinyanganye vitu vya mutu maskini kwa sababu yeye ni maskini,+
Wala usiponde mutu wa hali ya chini katika mulango mukubwa wa muji,+
23 Kwa maana Yehova mwenyewe atatetea mashitaka yao+
Na ataondoa uzima wa* wale wenye kuwapunja.
24 Usishirikiane na mutu mwenye kukasirika-kasirika
Wala kujiunga na mutu mwenye muelekeo wa kukasirika sana,
25 Ili usijifunze hata kidogo njia zake
Na kujitia katika mutego.+
26 Usikuwe kati ya wale wenye kupana mikono wakati wanaahidi kulipia wengine mukopo,
Wenye wanaahidi kulipa mikopo.+
27 Kama hauna kitu cha kulipa,
Kitanda chako kitapelekwa moja kwa moja inje kutoka chini yako!
29 Je, umemuona mutu mwenye ufundi katika kazi yake?
Atasimama mbele ya wafalme;+
Hatasimama mbele ya watu wa kawaida.
23 Wakati unakaa ili kula pamoja na mufalme,
Chunguza kwa uangalifu kile chenye kuwa mbele yako;
2 Tia kisu kwenye koo lako*
Kama uko na hamu kubwa ya kula.*
3 Usitamani vyakula vyake vitamu,
Kwa maana ni vyakula vya udanganyifu.
4 Usijichokeshe ili kupata utajiri.+
Acha na uonyeshe uelewaji.*
5 Wakati unautupia jicho, hauko pale,+
Kwa maana hakika utaota mabawa kama tai na kuruka mbali katika anga.+
6 Usikule chakula cha mutu muchoyo;*
Usitamani vyakula vyake vitamu,
7 Kwa maana yeye ni kama mutu mwenye kuweka hesabu.*
Anakuambia: “Kula na ukunywe,” lakini haiko vile anamaanisha.*
8 Utatapika matonge yenye ulikula
Na utakuwa umepoteza maneno yako ya kumusifu.
10 Usihamishe alama ya zamani ya mupaka+
Wala kuingia katika shamba la wenye hawana baba.
12 Fanya moyo wako uzame katika nizamu
Na sikio lako katika maneno ya ujuzi.
13 Usiime mutoto mwanaume* nizamu.+
Kama unamupiga kwa fimbo, hatakufa.
17 Moyo wako usisikilie wivu watenda-zambi,+
Lakini umuogope Yehova muchana wote,+
18 Kwa maana ukifanya vile utakuwa na wakati muzuri wenye kuja+
Na tumaini lako halitaondolewa.
19 Mwana wangu, sikiliza na ukuwe na hekima,
Na uelekeze moyo wako katika njia yenye kufaa.
20 Usikuwe kati ya wale wenye kunywa divai nyingi sana,+
Kati ya wale wenye kula nyama nyingi sana,+
21 Kwa maana mulevi na mulafi watakuwa maskini,+
Na kusinzia kutavalisha mutu nguo zenye kupasuka-pasuka.
24 Baba ya mwenye haki hakika atakuwa na furaha;
Kila baba mwenye anazaa mwana mwenye hekima atamufurahia sana.
25 Baba yako na mama yako watafurahi sana,
Na mama mwenye alikuzaa atakuwa na shangwe.
26 Mwana wangu, unipatie moyo wako,
Na macho yako yafurahie njia zangu.+
28 Anavizia kama munyanganyi;+
Anaongeza hesabu ya wanaume wenye hawako waaminifu.
29 Ni nani mwenye ole? Ni nani mwenye wasiwasi?
Ni nani mwenye ugomvi? Ni nani mwenye malalamiko?
Ni nani mwenye vidonda bila sababu? Ni nani mwenye macho mekundu?*
30 Ni wale wenye kupitisha wakati mwingi kwenye divai;+
Wale wenye kutafuta* divai yenye kuchanganywa.
31 Usiangalie rangi nyekundu ya divai
Wakati inangaa katika kikombe na kushuka kwa urahisi,
32 Kwa maana mwishowe inauma kama nyoka,
Na inatoa sumu kama nyoka-kipiri.
34 Na utakuwa kama mutu mwenye kulala katikati ya bahari,
Kama mutu mwenye kulala kwenye sehemu ya juu ya mulingoti wa mashua.*
35 Utasema: “Wamenipiga, lakini sikusikia kitu.*
Walinipiga, lakini sikujua.
Nitaamuka wakati gani?+
Ninahitaji kinywaji kingine.”*
24 Usisikilie waovu wivu,
Na usitamani kushirikiana nao,+
2 Kwa maana moyo wao unafikiri sana juu ya jeuri,
Na midomo yao inaongea juu ya kuleta matata.
7 Mupumbavu hawezi kupata hekima ya kweli;+
Hana jambo la kusema katika mulango mukubwa wa muji.
8 Kila mutu mwenye anapanga uovu
Ataitwa fundi wa kufanya mipango ya mubaya.+
11 Okoa wale wenye kupelekwa kwenye kifo,
Na uzuie wale wenye kuyumba-yumba wakienda kuchinjwa.+
13 Mwana wangu, kula asali, kwa sababu ni ya muzuri;
Asali ya sega ni tamu kuonja.
14 Vilevile, jua kwamba hekima ni ya muzuri kwako.*+
Kama unaipata, utakuwa na wakati muzuri wenye kuja
Na tumaini lako halitaondolewa.+
15 Usivizie kwa uovu karibu na makao ya mwenye haki;
Usiharibu mahali pake pa kupumuzikia.
16 Kwa maana mwenye haki anaweza kuanguka mara saba (7), na atasimama tena,+
Lakini musiba utafanya waovu wajikwae.+
17 Wakati adui yako anaanguka, usishangilie,
Na wakati anajikwaa, usiache moyo wako ufurahi;+
18 Kama unafanya vile, Yehova ataona jambo hilo na hatafurahi,
19 Usikasirike* kwa sababu ya waovu;
Usisikilie watu waovu wivu,
20 Kwa maana hakuna wakati muzuri wenye kuja kwa ajili ya muovu hata mumoja;+
Taa ya waovu itazimwa.+
21 Mwana wangu, ogopa Yehova na mufalme.+
Ni nani anajua ni uharibifu gani wote wawili* wataleta juu ya waasi hao?+
23 Haya pia ni maneno ya wenye hekima:
Kuonyesha upendeleo katika hukumu haiko muzuri.+
24 Mutu yeyote mwenye anamuambia muovu, “Wewe ni mwenye haki,”+
Atalaaniwa na vikundi vya watu na kulaumiwa na mataifa.
26 Watu watabusu midomo ya mutu mwenye kujibu kwa unyoofu.*+
28 Usitoe ushuhuda juu ya jirani yako bila kuwa na sababu za kweli.+
Usitumie midomo yako ili kudanganya wengine.+
30 Nilipita karibu na shamba la muvivu,+
Karibu na shamba la mizabibu la mutu mwenye hana akili ya muzuri.*
31 Niliona limejaa magugu;
Udongo ulikuwa umefunikwa na mimea yenye kuwasha,
Na ukuta wake wa majiwe ulikuwa umebomoka.+
32 Niliangalia hilo na kulitia katika moyo;
Nililiona na kujifunza somo hili:*
33 Kulala kidogo, kusinzia kidogo,
Kukunja mikono kidogo ili kupumuzika,
34 Na umaskini wako utakuja kama munyanganyi,
Na uhitaji wako kama mwanaume mwenye silaha.+
25 Hizi pia ni mezali za Sulemani,+ zenye watu wa Hezekia+ mufalme wa Yuda waliandika:*
2 Ni utukufu wa Mungu kuweka jambo likiwa siri,+
Na utukufu wa wafalme ni kuchunguza jambo kwa undani.
3 Kama vile mbingu ziko juu na kama vile dunia iko na urefu kuenda chini,
Vilevile moyo wa wafalme hauchunguzike.
4 Ondoa takataka kwenye feza,
Nayo itatoka ikiwa imesafishwa kabisa.+
5 Ondoa muovu mbele ya mufalme,
Na kiti chake cha ufalme kitafanywa kuwa imara kabisa katika haki.+
6 Usijipatie heshima mbele ya mufalme,+
Na usikae kati ya watu wa maana,+
7 Kwa maana ni muzuri zaidi yeye akuambie, “Kuja hapa juu,”
Kuliko akupatishe haya mbele ya mutu mwenye cheo.+
8 Usipeleke haraka-haraka mashitaka kwenye tribinali,
Kwa maana utafanya nini kisha kama jirani yako anakupatisha haya?+
9 Utetee shida yako pamoja na jirani yako,+
Lakini usifunue mambo yenye uliambiwa kwa siri,*+
10 Ili mwenye kukusikiliza asikupatishe haya
Na ili usieneze habari ya mubaya* yenye haiwezi kukusanywa tena.
11 Kama matunda ya mutofaa ya zahabu kwenye vyombo vya feza vyenye kupambwa*
Ni vile pia neno lenye kusemwa wakati wenye kufaa.+
12 Kama hereni la sikio la zahabu na pambo la zahabu safi
Ni vile pia mukaripiaji mwenye hekima kwa sikio lenye kusikia.+
13 Kama baridi ya teluji* siku ya mavuno
Ni vile pia mujumbe muaminifu kwa wale wenye walimutuma
14 Kama mawingu na upepo wenye haulete mvua
Ni vile pia mutu mwenye anajisifu kuhusu zawadi yenye haijatolewa hata kidogo.*+
16 Ukipata asali, kula tu yenye unahitaji,
Kwa maana ukikula nyingi sana, unaweza kuitapika.+
17 Muguu wako usifike mara nyingi katika nyumba ya jirani yako,
Ili asikuchoke na kukuchukia.
18 Kama gongo* ya vita na upanga na mushale wenye kuwa na makali
Ni vile pia mutu mwenye anatoa ushahidi wa uongo juu ya jirani yake.+
19 Kama jino lenye kuvunjika ao muguu wenye kuyumba-yumba
Ni vile pia kutumainia mutu mwenye hategemeke* nyakati za taabu.
20 Kama mutu mwenye anatosha nguo siku ya baridi
Na kama siki* yenye kumwangwa kwenye chumvi ya asili
Ni vile pia mutu mwenye kuimbia moyo wenye huzuni nyimbo.+
21 Kama adui yako* iko* na njaa, umupatie mukate akule;
Kama iko* na kiu, umupatie maji akunywe,+
22 Kwa maana utakuwa unakusanya makaa yenye kuwaka juu ya kichwa chake,*+
Na Yehova atakupatia zawabu.
23 Upepo wa kaskazini unaleta mvua kubwa,
Na ulimi wenye kupiga porojo unaleta uso wenye kasirani.+
24 Ni muzuri zaidi kuishi kwenye pembe ya sehemu ya juu ya nyumba
25 Kama maji ya baridi juu ya nafsi* yenye kuchoka
Ni vile pia habari ya muzuri yenye inatoka katika inchi ya mbali.+
26 Kama chemchemi yenye matope na kisima chenye kuharibika
Ni vile pia mwenye haki ambaye anakubali kufuata* muovu.
28 Kama muji wenye umebomolewa, wenye hauna ukuta
26 Kama vile teluji* wakati wa kipindi cha joto na mvua wakati wa mavuno,
Vilevile heshima haistahili mujinga.+
2 Kama vile ndege iko* na sababu ya kukimbia na mbaruwayu sababu ya kuruka,
Vilevile laana haiwezi kuja bila sababu fulani.*
3 Mujeledi ni kwa ajili ya farasi, lijamu* ni kwa ajili ya punda,+
Na fimbo ni kwa ajili ya mugongo wa watu wajinga.+
4 Usijibu mujinga kulingana na upumbavu wake,
Ili usikuwe kama yeye.*
6 Kama mutu mwenye anajivunja miguu yake mwenyewe na kujiumiza mwenyewe*
Ni vile pia mutu mwenye anatia mambo katika mikono ya mujinga.
8 Kama kufunga jiwe kwenye kombeo,
Ni vile pia kumupatia mutu mujinga utukufu.+
9 Kama mumea wa miiba katika mukono wa mulevi,
Ni vile pia mezali katika kinywa cha watu wajinga.
10 Kama mupiga-mishale mwenye anaumiza ovyo-ovyo,*
Ni vile pia mutu mwenye anapatia mujinga ao wapita-njia kazi.
11 Kama vile imbwa anarudilia matapiko yake,
Mujinga anarudilia upumbavu wake.+
12 Je, umemuona mutu mwenye anafikiri kama iko* na hekima?+
Kuko tumaini zaidi kwa mujinga kuliko kwa mutu huyo.
15 Muvivu anazika mukono wake katika bakuli la karamu,
Lakini amechoka sana kuurudisha katika kinywa chake.+
16 Muvivu anafikiri kwamba iko* na hekima zaidi
Kuliko watu saba (7) wenye wanajibu kwa busara.
17 Kama mutu mwenye kukamata masikio ya imbwa
Ni vile pia mupita-njia mwenye anakasirishwa* na ugomvi wenye hauko wake.+
18 Kama mwenda-wazimu mwenye anatupa silaha zenye kuwaka moto, mishale, na kifo*
19 Ni vile pia mutu mwenye anamudanganya jirani yake na kusema, “Nilikuwa ninafanya muzaha tu!”+
20 Kwenye hakuna kuni, moto unazimika,
Na kwenye hakuna muchongezi, ugomvi unaisha.+
21 Kama vile makaa yanaongezwa kwenye makaa yenye kuwaka na kuni kwenye moto
Ni vile mutu wa ugomvi anachochea ugomvi.+
23 Kama feza yenye kupakwa juu ya chombo cha udongo
24 Mwenye anachukia wengine anaficha chuki hiyo kwa midomo yake,
Lakini ndani anaweka udanganyifu.
25 Hata kama anasema maneno yenye kupendeza, usimuamini,
Kwa maana kuko mambo saba (7) yenye kuchukiza katika moyo wake.*
26 Hata kama chuki yake imefichwa kwa udanganyifu,
Uovu wake utafunuliwa katika kutaniko.
27 Mwenye anachimba shimo ataangukia ndani,
Na kila mutu mwenye anaviringisha jiwe—litamurudilia.+
28 Ulimi wenye kusema uongo unachukia watu wenye uliponda,
Na kinywa chenye kusifu-sifu kinaleta uharibifu.+
3 Jiwe ni nzito na muchanga ni muzito,
Lakini usumbufu wenye unaletwa na mupumbavu ni muzito zaidi kuliko vyote viwili.+
4 Kuko ukali wa hasira na mafuriko ya kasirani kali,
Lakini ni nani anaweza kuvumilia wivu?+
5 Karipio lenye kuwa wazi ni muzuri zaidi kuliko upendo wenye kufichwa.+
7 Mwenye hamu yake ya kula imetoshelezwa anazarau* asali ya sega,
Lakini kwa mwenye njaa, hata kitu kichungu ni kitamu.
8 Kama ndege mwenye anaenda* mbali na chicha yake*
Ni vile pia mutu mwenye anaenda mbali na nyumba yake.
9 Mafuta na uvumba vinafurahisha moyo;
Ni vile pia urafiki mutamu wenye unatokana na shauri la unyoofu.*+
10 Usimuache rafiki yako ao rafiki ya baba yako,
Na usiingie katika nyumba ya ndugu yako siku yenye uko na musiba;
Jirani wa karibu anashindia ndugu wa mbali.+
11 Ukuwe na hekima, mwana wangu, na ufurahishe moyo wangu,+
Ili niweze kumujibu ule mwenye ananichokoza.+
12 Mutu mwerevu anaona hatari na kujificha,+
Lakini wenye hawana uzoefu wanaendelea mbele na kupata matokeo ya mubaya.*
13 Kamata nguo ya mutu ikiwa ameahidi kulipia mugeni mukopo;
Umunyanganye kitu chenye aliwekesha kwa ajili ya mukopo ikiwa alifanya vile kwa ajili ya mwanamuke mugeni.*+
14 Wakati mutu anabariki jirani yake kwa sauti kubwa asubui sana,
Itaonwa kuwa laana kwake.
15 Bibi mugomvi* ni kama sehemu ya juu ya nyumba yenye inavuya bila kuacha katika siku ya mvua.+
16 Kila mutu mwenye anaweza kumuzuia anaweza kuzuia upepo
Na anaweza kukamata mafuta kwa mukono wake wa kuume.
19 Kama vile maji yanaonyesha uso wa mutu,
Ni vile pia moyo wa mutu unaonyesha moyo wa mwingine.
20 Kaburi na mahali pa uharibifu* havitosheke hata kidogo,+
Wala macho ya mwanadamu hayatosheke hata kidogo.
21 Chungu cha kusafishia ni kwa ajili ya feza na tanuru ni kwa ajili ya zahabu,+
Vilevile mutu anapimwa kupitia sifa yenye anapokea.*
22 Hata kama unatwanga mupumbavu kwa mutwangio
Kama vile nafaka yenye kupondwa katika kinu,
Upumbavu wake hautamutoka.
23 Unapaswa kujua muzuri hali ya kundi lako.
25 Majani ya mubichi yanaisha, na majani ya mupya yanatokea,
Na majani ya milima yanakusanywa.
26 Wana-kondoo dume wanakupatia nguo zako,
Na mbuzi-dume wanakupatia bei ya shamba.
27 Na kutakuwa maziwa ya kutosha ya mbuzi ya kukulisha wewe,
Kukulisha familia yako, na kutegemeza watumishi wako wanamuke.
28 Waovu wanakimbia hata kama hakuna mwenye anawafuatilia,
2 Wakati kuko kosa* katika inchi, inchi inakuwa na mukubwa mumoja kisha mwingine,+
Lakini kwa musaada wa mutu mwenye utambuzi na ujuzi, mukubwa* atadumu wakati murefu.+
3 Mutu maskini mwenye anapunja mutu wa hali ya chini+
Ni kama mvua yenye inaharibu chakula chote.
4 Wale wenye kuacha sheria wanasifu mutu muovu,
Lakini wale wenye kushika sheria wanawakasirikia.+
6 Maskini mwenye kutembea kwa uaminifu-mushikamanifu wake ni muzuri zaidi
Kuliko tajiri mwenye njia zake zimepotoka.+
7 Mwana mwenye uelewaji anashika sheria,
Lakini rafiki ya walafi analetea baba yake haya.+
8 Mwenye anaongeza mali yake kwa faida+ na faida ya juu sana
Anaikusanyia ule mwenye anaonyesha maskini wema.+
9 Mwenye anakataa kusikiliza sheria
—Hata sala yake inachukiza.+
10 Mwenye anapoteza watu wanyoofu ili wafuate njia ya uovu ataanguka katika shimo lake mwenyewe,+
Lakini wenye hawana lawama watariti mambo ya muzuri.+
11 Tajiri anajiona mwenyewe kuwa mwenye hekima,+
Lakini mutu maskini mwenye utambuzi anaweza kumuchunguza kwa undani.+
12 Wakati wenye haki wanashinda, kunakuwa utukufu mwingi,
Lakini wakati waovu wanapata mamlaka, watu wanajificha.+
13 Mwenye anafunika makosa yake hatafanikiwa,+
Lakini kila mutu mwenye anayaungama na kuyaacha ataonyeshwa rehema.+
14 Mwenye furaha ni mutu mwenye kuwa muangalifu sikuzote,*
Lakini kila mutu mwenye anafanya moyo wake kuwa mugumu ataanguka katika musiba.+
15 Kama simba mwenye kunguruma na dubu mwenye kushambulia
Ni vile pia mutawala muovu mwenye anatawala juu ya watu wenye hawana uwezo.+
16 Kiongozi mwenye hana utambuzi anatumia mubaya mamlaka yake,+
Lakini mutu mwenye anachukia faida yenye haiko ya haki atarefusha maisha yake.+
17 Mutu mwenye kulemewa na hatia ya damu kwa sababu ya kuondoa uzima wa mutu* ataendelea kukimbia mupaka katika kaburi.*+
Mutu yeyote asimusaidie.
18 Mwenye anatembea bila kosa ataokolewa,+
Lakini ule mwenye njia zake zimepotoka ataanguka bila kutazamia.+
19 Mwenye analima udongo wake atakuwa na mikate mingi,
Lakini mwenye anafuatilia vitu vyenye havina mafaa yoyote atakuwa maskini sana.+
20 Mutu muaminifu atapata baraka nyingi,+
Lakini mwenye anaharakisha kupata utajiri hatakosa kuwa na hatia.+
21 Haiko muzuri kuonyesha upendeleo;+
Lakini mutu anaweza kukosea kwa sababu ya kipande cha mukate.
22 Mutu mwenye wivu* anajikaza sana kupata mali,
Lakini hajue kwamba umaskini utamupata.
23 Kila mutu mwenye anakaripia mwingine+ atafikia kukubaliwa zaidi+
Kuliko mutu mwenye anasifu-sifu kwa ulimi wake.
24 Kila mutu mwenye anaiba vitu vya baba yake na vya mama yake na kusema, “Haiko kosa,”+
Ni rafiki ya mutu mwenye analeta uharibifu.+
25 Mutu mwenye pupa anachochea* mugawanyiko,
Lakini kila mutu mwenye anamutegemea Yehova atapata mafanikio.*+
26 Kila mutu mwenye anategemea moyo wake mwenyewe ni mujinga,+
Lakini ule mwenye anatembea kwa hekima ataponyoka.+
27 Kila mutu mwenye anapatia maskini hatakosa kitu,+
Lakini ule mwenye anawafungia macho atapata laana nyingi.
28 Wakati waovu wanapata mamlaka, mutu anajificha,
Lakini wakati wanaangamia, wenye haki wanaongezeka.+
29 Mutu mwenye anafanya shingo yake ikuwe nguvu* kisha kukaripiwa mara nyingi+
Atavunjwa bila kutazamia na hataweza kupona.+
2 Wakati wenye haki ni wengi, watu wanafurahi sana,
Lakini wakati muovu anatawala, watu wanalia kwa maumivu.+
3 Mutu mwenye anapenda hekima anamufurahisha baba yake,+
Lakini mwenye anashirikiana na makahaba anatumia mubaya mali yake.+
6 Kosa la mutu mubaya linamunasa yeye mwenyewe,+
Lakini mwenye haki anapiga vigelegele vya shangwe na kufurahi sana.+
9 Wakati mutu mwenye hekima anabishana na mupumbavu,
Kutakuwa makelele na zihaka, lakini hawatatosheka.+
12 Wakati mutawala anasikiliza uongo,
Watumishi wake wote watakuwa waovu.+
13 Maskini na mukandamizaji wanafanana katika jambo hili:*
Yehova anapatia macho ya wote wawili mwangaza.*
16 Wakati waovu wanaongezeka, makosa yanaongezeka,
Lakini wenye haki wataona kuanguka kwao.+
18 Wakati hakuna maono,* watu wanafanya kile wanapenda,+
Lakini wenye furaha ni wale wenye wanashika sheria.+
19 Mutumishi hatajiacha arekebishwe na maneno,
Kwa maana hata kama anaelewa, hatii.+
20 Je, umemuona mutu mwenye kuwa haraka kusema?+
Kuko tumaini zaidi kwa mupumbavu kuliko yeye.+
21 Kama mutumishi anabembelezwa tangu ujana wake,
Kisha wakati fulani atakuwa mutu mwenye hana shukrani.
22 Mutu mwenye kukasirika haraka anachochea ugomvi;+
Kila mutu mwenye kukasirika-kasirika sana anafanya makosa mengi.+
24 Mwenye kushirikiana na mwizi anajichukia mwenyewe.*
Anaweza kusikia mwito wa kutoa ushahidi,* lakini hatoe habari yoyote.+
27 Mutu mwenye hatende haki anachukiza mwenye haki,+
Lakini ule mwenye njia yake imenyooka anachukiza muovu.+
30 Ujumbe muzito wenye kuwa katika maneno ya Aguri mwana wa Yake, wenye alimuambia Itieli, ndiyo, Itieli na Ukali.
2 Mimi ni mujinga kuliko mutu mwingine yeyote,+
Na sina uelewaji wenye mwanadamu anapaswa kuwa nao.
3 Sijajifunza hekima,
Na sina ujuzi kuhusu Mwenye Kuwa Mutakatifu Zaidi.
4 Ni nani amepanda mbinguni na kisha akashuka?+
Ni nani amekusanya upepo katika viganja vya mikono mbili?
Ni nani amefunga maji katika nguo yake?+
Ni nani amefanya miisho yote ya dunia kuwa imara?*+
Jina lake ni nani na jina la mwana wake ni nani—kama unajua?
5 Kila neno la Mungu ni safi.+
Yeye ni ngao kwa wale wenye kumukimbilia.+
7 Ninakuomba mambo mbili.
Usiniime mambo hayo mbele nikufe.
8 Ondolea mbali na mimi mambo yenye hayako ya kweli na ya uongo.+
Usinipatie umaskini wala utajiri.
Wala usiruhusu nikuwe maskini, niibe na kuletea haya* jina la Mungu wangu.
10 Usimuchongee mutumishi kwa bwana wake,
Ukifanya vile anaweza kukulaani na utapatikana na hatia.+
11 Kuko kizazi cha watu wenye wanamulaani baba yao
Na hawamubariki mama yao.+
13 Kuko kizazi cha watu wenye macho yenye kujaa kiburi
Na wenye macho yao yanaangalia kwa majivuno mengi!+
14 Kuko kizazi cha watu wenye meno yao ni panga
Na wenye mataya* yao ni visu vya kuchinjia;
Wanameza watu wa hali ya chini wa dunia
Na maskini kutoka kati ya wanadamu.+
15 Vidudu-ruba viko na mabinti wawili wenye kulia, “Nipatie! Nipatie!”
Kuko vitu tatu (3) vyenye havishibake,
Vitu ine (4) vyenye havisemake, “Inaenea!”
17 Jicho lenye linamuchekelea baba na kuzarau kumutii mama+
—Kunguru wa bonde* watalingoa,
Na tai wadogo watalikula.+
18 Kuko mambo tatu (3) yenye kunipita uelewaji,*
Na mambo ine (4) yenye sielewe:
19 Njia ya tai katika mbingu,
Njia ya nyoka juu ya mwamba,
Njia ya mashua* katika bahari kubwa,
Na njia ya mwanaume pamoja na kijana mwanamuke.
20 Hii ndiyo njia ya mwanamuke muzinifu:
Anakula, anapangusa kinywa chake;
Kisha anasema, “Sikufanya kosa lolote.”+
21 Kuko mambo tatu (3) yenye kutetemesha dunia
Na mambo ine (4) yenye dunia haiwezi kuvumilia:
22 Wakati mutumwa anatawala akiwa mufalme,+
Wakati mupumbavu anashiba sana,
23 Wakati mwanamuke mwenye kuchukiwa* anaolewa,
Na wakati mutumishi mwanamuke anachukua nafasi ya bimukubwa wake.+
24 Kuko vitu ine (4) katika dunia vyenye kuwa kati ya vitu vidogo zaidi,
29 Kuko vitu tatu (3) vyenye mwendo wa kuvutia,
Vitu ine (4) vyenye kuvutia wakati vinatembea:
30 Simba, munyama mwenye nguvu zaidi kuliko wanyama wote,
Mwenye hamukimbie mutu yeyote;+
31 Imbwa-muwindaji; mbuzi-dume;
Na mufalme mwenye kuwa pamoja na jeshi lake.
33 Kwa maana kama vile kupiga-piga maziwa kunatokeza siagi
Na kufinya pua kunafanya damu itoke,
Ni vile pia kuchochea kasirani kunatokeza magomvi.+
31 Maneno ya Mufalme Lemueli, ujumbe muzito wenye mama yake alimupatia ili kumufundisha:+
2 Nikuambie nini, Ee mwana wangu,
Nikuambie nini, Ee mwana wa tumbo langu la uzazi,
Na nikuambie nini, Ee mwana wa naziri zangu?+
4 Haiko muzuri kwa wafalme, Ee Lemueli,
Haiko muzuri kwa wafalme kunywa divai
Wala watawala kusema, “Kinywaji changu kiko wapi?”+
5 Ili wasikunywe na kusahau mambo yenye yameagizwa
Na kupotosha haki za watu wa hali ya chini.
7 Acha wakunywe na kusahau umaskini wao;
Na wasikumbuke tena taabu yao.
8 Semea wale wenye hawana uwezo wa kusema;
Tetea haki za wote wenye kuangamia.+
א [Aleph]
10 Ni nani anaweza kupata bibi mwenye uwezo?*+
Samani yake inapita sana samani ya marijani.*
ב [Beth]
11 Bwana yake anamutumainia katika moyo wake,
Na hakose kitu chochote chenye samani.
ג [Gimel]
12 Anamupatia bwana yake zawabu ya mema, hapana mabaya,
Siku zote za maisha yake.
ד [Daleth]
13 Anapata manyoya ya kondoo na kitani;
Anafurahia sana kufanya kazi kwa mikono yake.+
ה [He]
ו [Waw]
15 Tena, anaamuka wakati ingali usiku,
Na kupatia watu wa nyumba yake chakula
Na kupatia mafungu watumishi wake wanamuke.+
ז [Zayin]
ח [Heth]
ט [Teth]
18 Anahakikisha kwamba biashara yake iko na faida;
Taa yake haizimike usiku.
י [Yod]
19 Mikono yake inashika kipande cha muti cha kufungia uzi,
Na mikono yake inashika kipande cha muti cha kusukia uzi.+
כ [Kaph]
20 Ananyooshea mukono mutu wa hali ya chini,
Anafungulia maskini mikono yake.+
ל [Lamed]
21 Hana wasiwasi kuhusu watu wa nyumba yake kwa sababu ya teluji,*
Kwa sababu watu wote wa nyumba yake wamevaa nguo za kuleta joto.*
מ [Mem]
22 Anajitengenezea matandiko ya kufunika kitanda.
Nguo zake ni za kitani na manyoya ya kondoo ya rangi ya zambarau.
נ [Nun]
23 Bwana yake anajulikana sana katika milango mikubwa ya muji,+
Kwenye anakaa kati ya wazee wa inchi.
ס [Samekh]
ע [Ayin]
פ [Pe]
צ [Tsade]
ק [Qoph]
28 Watoto wake wanasimama na kumutangaza kuwa mwenye furaha;
Bwana yake anasimama na kumusifu.
ר [Resh]
ש [Shin]
30 Uvutio unaweza kudanganya, na uzuri unaweza kupita haraka,*+
Lakini bibi mwenye anamuogopa Yehova atasifiwa.+
ת [Taw]
31 Mumupatie zawabu kwa sababu ya mambo yenye anafanya,*+
Na kazi zake zimusifu katika milango mikubwa ya muji.+
Tnn., “kujua.”
Ao “mambo ya haki.”
Ao “haki.”
Ao “muongozo wenye hekima.”
Ao “mufano.”
Ao “Kumuheshimia.”
Ao “sheria.”
Ao “Sheoli,” ni kusema, kaburi la wanadamu wote. Angalia Maana ya Maneno.
Ao “Tupa kura yako pamoja na sisi.”
Ao “tutakuwa na mufuko mumoja.”
Ao “makila.”
Ao “eko.”
Ao “nafsi za.”
Ao “nafsi ya.”
Tnn., “kichwa cha.”
Ao “Mugeuke wakati ninawakaripia.”
Tnn., “watakula matunda.”
Ao “mipango yao wenyewe ya mubaya.”
Angalia Maana ya Maneno.
Angalia Maana ya Maneno.
Tnn., “mugeni.” Inaonekana ni mutu mwenye amejitenga na Mungu kwa sababu ya mwenendo mupotovu.
Ao “maneno yenye ushawishi.”
Tnn., “mugeni.” Inaonekana ni mutu mwenye amemuacha Mungu kwa sababu ya mwenendo mupotovu.
Ao “bwana.”
Tnn., “mapito yake.”
Tnn., “wenye wanaingia kwake.”
Ao “wenye kushika uaminifu-mushikamanifu.”
Ao “sheria.”
Ao “kweli.”
Tnn., “usiegemee.”
Tnn., “kitofu chako.”
Ao “vitu vya muzuri sana vya.”
Ao “mapato.”
Ao “vikamulio vyako vya divai vitajaa sana.”
Angalia Maana ya Maneno.
Inaonekana mustari huu unazungumuzia sifa za Mungu zenye kutajwa katika mistari yenye kutangulia.
Ao “Zitapatia nafsi yako.”
Ao “hautagonga kitu chochote.”
Ao “wale wenye kustahili mema hayo.”
Ao “Kama mukono wako uko na nguvu za kusaidia.”
Ao “sheria.”
Ao “la kwanza.”
Tnn., “Tegea sikio.”
Ao “macho yako yenye kungaa.”
Ao pengine, “Chunguza kwa uangalifu.”
Tnn., “Tegea sikio lako.”
Tnn., “mugeni.” Angalia Mez 2:16.
Ao “Sheoli,” ni kusema, kaburi la wanadamu wote. Angalia Maana ya Maneno.
Ao “nguvu.”
Tnn., “Katikati ya mukusanyiko na kutaniko.”
Ao “safi.”
Ao “Chanzo chako cha maji kibarikiwe.”
Ao “mbuzi wa pori.”
Ao “yakuleweshe.”
Tnn., “mugeni.” Angalia Mez 2:16.
Tnn., “mugeni.” Angalia Mez 2:16.
Ni kusema, wakati unaahidi kumulipia mukopo.
Ao “vyenye nafsi yake inachukia.”
Ao “sheria.”
Ao “itakufundisha.”
Tnn., “mugeni.” Angalia Mez 2:16.
Ao “nafsi yenye.”
Ao “ajaze nafsi yake.”
Tnn., “iko katika ukosefu wa moyo.”
Ao “bei yoyote ya ukombozi.”
Ao “sheria.”
Tnn., “mugeni.” Angalia Mez 2:16.
Tnn., “mugeni.” Angalia Mez 2:16.
Ao “yenye kushawishi.”
Ao “wenye hawana uzoefu.”
Tnn., “iko katika ukosefu wa moyo.”
Ao “Alikuwa na nguo ya.”
Ao “eko.”
Tnn., “Miguu yake haibakiake.”
Ao “eko.”
Ao “eko.”
Kunyunyiza ni kumwanga kidogo-kidogo kitu cha majimaji ao ungaunga.
Ao “pingu.”
Ao “nafsi yake.”
Ao “Sheoli,” ni kusema, kaburi la wanadamu wote. Angalia Maana ya Maneno.
Tnn., “wana wa binadamu.”
Tnn., “muelewe moyo.”
Angalia Maana ya Maneno.
Ao “Kanuni zenye kuritiwa.”
Angalia Maana ya Maneno.
Ao “zamani za kale.”
Ao “nilizaliwa kama vile kwa maumivu ya kuzaa.”
Tnn., “muzunguko.”
Tnn., “alifanya nguvu.”
Ao “alitunga sheria kuhusu.”
Ao “wanadamu.”
Ao “Kwa kukesha.”
Ao “anaumiza nafsi yake.”
Tnn., “Amechinja machinjo yake.”
Tnn., “iko katika ukosefu wa moyo.”
Ao “watu wenye hawana uzoefu.”
Tnn., “wako katika ukosefu wa moyo.”
Ao “Sheoli,” ni kusema, kaburi la wanadamu wote. Angalia Maana ya Maneno.
Ao “nafsi ya mwenye haki ikae.”
Ao “Sifa ya.”
Tnn., “amri.”
Tnn., “iko katika ukosefu wa moyo.”
Ao “Kitu cha maana cha.”
Ao pengine, “iko kwenye njia yenye inapeleka kwenye uzima.”
Ao “habari zenye haziko hakika.”
Ao “inaongoza.”
Ao “huzuni; magumu.”
Ao “vinaigre.”
Ao “eko.”
Ao “bwana wake wa kazi.”
Ao “Tarajio.”
Ao “kinazaa tunda la.”
Ao “Kilo.”
Ao “udanganyifu.”
Ao “jiwe kamili la kupimia.”
Ao “Vitu vya maana havitakuwa.”
Ao “mutu mwenye hamuogope Mungu.”
Tnn., “iko katika ukosefu wa moyo.”
Tnn., “muaminifu katika roho.”
Tnn., “anafunika jambo.”
Ao “muongozo wa hekima.”
Ao “wokovu.”
Tnn., “anachukia.”
Ao “mwenye kuvutia.”
Ao “Mutu mwenye upendo mushikamanifu.”
Ao “anatendea mema nafsi yake.”
Ao “haya.”
Tnn., “Mukono kwa mukono.”
Tnn., “anasambaza.”
Ao “Nafsi yenye ukarimu.”
Tnn., “atanenepeshwa.”
Tnn., “mwenye kunywesha wengine kwa ukarimu.”
Ao “haya.”
Angalia Maana ya Maneno.
Ao “hana ufahamu.”
Tnn., “yanavizia ili kumwanga damu.”
Tnn., “mukate.”
Ao “nafsi ya munyama wake wa kufugwa.”
Tnn., “iko katika ukosefu wa moyo.”
Tnn., “kinywa chake.”
Ao “siku ileile.”
Tnn., “anafunika.”
Tnn., “mambo yenye haki.”
Tnn., “Lakini washauri wa.”
Ao “yanamufanya ashuke moyo.”
Ao “anarekebishwa.”
Tnn., “kinywa chake.”
Ao “Lakini nafsi kabisa.”
Ao “mambo yenye anasema.”
Ao “nafsi yake.”
Ao “nafsi yake haina.”
Ao “nafsi ya mwenye bidii.”
Tnn., “atanenepeshwa.”
Ao “eko.”
Ao “nafsi ya mutu.”
Tnn., “hawasikie kemeo lolote.”
Tnn., “unashangilia.”
Ao “wenye kupatiana mawazo.”
Ao “Mali yenye inatokana na ubatili.”
Tnn., “mwenye anaikusanya kwa mukono.”
Ao “Tumaini.”
Ao “neno.”
Ao “Sheria.”
Ao “karipio.”
Ao “nafsi.”
Ao “kumuharibu.”
Ao “hatoe nizamu; azabu.”
Ao pengine, “bila kukawia.”
Ao “nafsi.”
Ao “zenye kupotoka.”
Ao pengine, “wajinga wanadanganya wengine.”
Ao “wanafanya muzaha wakati wanaombwa kufanya marekebisho.”
Ao “Lakini kuko nia njema kati ya watu wanyoofu.”
Ao “uchungu wa nafsi yake.”
Ao “Mwenye hana uzoefu.”
Ao “iko na kasirani kali.”
Ao “mutu mwenye uwezo wa kufikiri.”
Ao “Mwenye hana uzoefu.”
Ao “eko.”
Ao “nafsi.”
Ao “eko.”
Ao “afya ya muzuri.”
Ao “lenye utulivu.”
Ao “lenye kuumiza.”
Ao “Ulimi wenye kuponyesha.”
Tnn., “ni kupondeka kwa roho.”
Ao “karipio.”
Ao “mapato.”
Ao “kali.”
Ao “Sheoli,” ni kusema, kaburi la wanadamu wote. Angalia Maana ya Maneno.
Ao “na Abadoni.”
Ao “mwenye anamukaripia.”
Ao “kinafuatia.”
Ao “muzuri.”
Ao “eko.”
Ao “muvurugo.”
Tnn., “mwenye alikulishwa katika chombo cha kukulishia wanyama.”
Tnn., “iko katika ukosefu wa moyo.”
Ao “mazungumuzo ya siri.”
Tnn., “anafurahia sana jibu la kinywa chake.”
Ao “Sheoli,” ni kusema, kaburi la wanadamu wote. Angalia Maana ya Maneno.
Ao “haya.”
Ao “kata-midomo.”
Ao “unafikiria kwa uangalifu namna ya kujibu; unawaza mbele ya kusema.”
Ao “eko.”
Ao “Kumutupia mutu jicho kwa furaha.”
Tnn., “inanenepesha mifupa.”
Ao “nafsi yake.”
Tnn., “moyo.”
Tnn., “Mipangilio ya moyo ni ya mutu.”
Ao “jibu lenye kufaa.” Tnn., “jibu la ulimi.”
Tnn., “safi.”
Tnn., “roho.”
Tnn., “Umuviringishie Yehova kazi zako.”
Tnn., “Mukono kwa mukono.”
Angalia Maana ya Maneno.
Ao “Uamuzi wenye kuongozwa na Mungu.”
Ao “Kilo.”
Ao “anaiepuka.”
Ao “nafsi yake.”
Tnn., “munyenyekevu wa roho.”
Tnn., “mema.”
Ao “Na maneno yenye kuvutia yanaongeza.” Tnn., “Na utamu wa midomo unaongeza.”
Ao “Yako na onjo tamu.” Angalia Maana ya Maneno.
Ao “Nafsi.”
Tnn., “kinywa chake kinamuchochea.”
Ao “Mwenye kufanya mipango ya mubaya.”
Ao “utukufu.”
Tnn., “anatawala juu ya roho yake.”
Ao “utulivu.”
Tnn., “zabihu.”
Ao “wazazi.”
Ao “watoto.”
Ao “ya muzuri.”
Ao “mutu mwenye cheo.”
Ao “ni jiwe lenye kufanya mwenye kuwa nalo akubaliwe.”
Tnn., “mwenye anafunika.”
Ao “kufungua ukuta wa maji.” Tnn., “kuachilia maji.”
Ao “Wakati hana akili ya muzuri?”
Tnn., “iko katika ukosefu wa moyo.”
Tnn., “mema.”
Ao “unasaidia mutu kupona.”
Ao “inakausha kabisa mifupa.”
Ao “kata-midomo.”
Tnn., “rushwa kutoka katika kifua.”
Tnn., “uchungu.”
Ao “kulipisha mwenye haki amande.”
Tnn., “atabakia na roho yenye kutulia.”
Ao “Anazarau.”
Ao “nafsi yake.”
Ao “ni kama vitu vya kumezwa kwa pupa.”
Tnn., “na kuinuliwa juu,” ni kusema, hawezi kufikiwa, iko salama.
Ao “hali ya kupoteza kabisa tumaini?”
Ao “kumuchunguza kwa undani.”
Tnn., “kunatenganisha.”
Pingu ni kipande cha muti ao cha chuma cha kufungia mulango kwa ndani.
Tnn., “kinywa chake.”
Ao “anapata nia njema ya.”
Ao “Nafsi yenye haina ujuzi haiko nafsi ya muzuri.”
Tnn., “mwenye anaenda haraka kwa miguu yake.”
Ao “mutu mukarimu.”
Tnn., “anapata moyo.”
Ao “anapenda nafsi yake.”
Tnn., “mema.”
Tnn., “kupita juu ya.”
Ao “mwana-simba mwenye manyoya ya murefu kwenye shingo.”
Ao “musumbufu.”
Ao “nafsi yake.”
Ao “atamupatia zawabu.”
Ao “usitamani.” Tnn., “usiinue nafsi yako ili.”
Ao “kusudi.”
Ao “mwana-simba mwenye manyoya ya murefu kwenye shingo.”
Ao pengine, “Ataangalia wakati wa mavuno lakini hatapata kitu.”
Ao “Nia.” Tnn., “Shauri.”
Tnn., “Wana.”
Ao “kilo.”
Ao “Majiwe mbili ya kupimia yenye kuwa tofauti na pia vyombo mbili vya kupimia vyenye kuwa tofauti.”
Ao “kijana mwanaume.”
Angalia Maana ya Maneno.
Ao “mugeni.”
Ao “itafanywa kuwa imara.”
Ao “shauri.”
Ao “muongozo wenye hekima.”
Ao “mwenye anashawishi kwa midomo yake.”
Ao “Majiwe mbili ya kupimia yenye kuwa tofauti.”
Ao “kilo.”
Ao “njia ya kufuata.”
Ao “mupeto; pneu.”
Ao “vinasugua na kuondoa.”
Ao “nia.”
Ao “faida.”
Ao pengine, “kwa wale wenye kutafuta kifo.”
Ao “musumbufu.”
Ao “anajua jambo la kufanya.”
Ao “kata-midomo.”
Tnn., “yenye kuwa katika kifua.”
Ao “mwenye anapenda raha.”
Ao “musumbufu.”
Tnn., “atameza.”
Ao “eko.”
Ao “kushinda.”
Ao “Anaepusha nafsi yake.”
Ao “pamoja na mwenendo wa haya!”
Tnn., “atazungumuza milele.”
Ao “mutu munyoofu anafanya njia yake kuwa hakika.”
Ao “sifa ya muzuri.” Tnn., “jina.”
Tnn., “Kukubaliwa.”
Tnn., “wanakutana pamoja.”
Ao “azabu.”
Ao “nafsi yake kuwa ya.”
Ao “mutoto; kijana.”
Tnn., “Mwenye kuwa na jicho la muzuri.”
Ao “Mashitaka ya kisheria.”
Ao “eko.”
Tnn., “wageni.” Angalia Mez 2:16.
Ao “mutoto; kijana.”
Ao “atanyanganya nafsi ya.”
Ao “Jizuie.”
Ao “nafsi yenye kujaa tamaa.”
Ao pengine, “Acha kufuata uelewaji wako mwenyewe.”
Ao “cha mutu yeyote mwenye jicho lenye uovu.”
Ao “mwenye kuhesabia katika nafsi yake.”
Tnn., “moyo wake hauko pamoja na wewe.”
Tnn., “Mukombozi.”
Ao “eko.”
Ao “mutoto; kijana.”
Ao “uokoe nafsi yake isiingie.”
Ao “Sheoli,” ni kusema, kaburi la wanadamu wote. Angalia Maana ya Maneno.
Tnn., “Figo zangu zitafurahi.”
Ao “Ujipatie.”
Tnn., “mugeni.” Angalia Mez 2:16.
Ao “macho mazito.”
Ao “wenye wanakusanyika ili kuonja-onja.”
Ao “mashua ya maji; bateau.”
Ao “sikusikia maumivu yoyote.”
Ao “Nitakitafuta tena.”
Ao “Familia.”
Ao “eko.”
Ao “muongozo wenye hekima.”
Ao “mafanikio; wokovu.”
Ao “Mipango ya mubaya ya mupumbavu.”
Ao “nyakati za taabu.”
Ao “nia.”
Ao “kuangalia nafsi yako.”
Ao “ni tamu kwa nafsi yako.”
Ni kusema, juu ya ule adui.
Ao “Usijionyeshe umewaka kasirani.”
Ao “wale wenye kutaka mabadiliko.”
Ni kusema, Yehova na mufalme.
Ao pengine, “Kujibu kwa njia yenye kuwa wazi ni kama kubusu mutu.”
Ao “familia.”
Ao “Nitamulipa sawasawa na matendo yake.”
Tnn., “iko katika ukosefu wa moyo.”
Tnn., “Nilipokea nizamu.”
Ao “walifanya kopi na kukusanya.”
Ao “siri za wengine.”
Ao “habari ya mubaya yenye haiko hakika.”
Ao “vikalio vya feza.”
Ao “neige.”
Ao “nafsi ya bwana wake.”
Tnn., “anajisifu kuhusu zawadi ya uongo.”
Ao “wenye upole.”
Gongo ni fimbo yenye kuvimba kwenye mwisho wake mumoja.
Ao pengine, “mudanganyifu.”
Ao “vinaigre.”
Tnn., “mwenye anakuchukia.”
Ao “eko.”
Ao “eko.”
Ni kusema, kupunguza uadui wake na kuyeyusha ugumu wake.
Ao “musumbufu.”
Angalia Maana ya Maneno.
Ao “mwenye anakubaliana na.” Tnn., “mwenye anayumba-yumba mbele ya.”
Ao “mwenye anashindwa kuzuia roho yake.”
Ao “neige.”
Ao “eko.”
Ao pengine, “Vilevile laana yenye mutu hastahili haimupatake.”
Lijamu ni kipande cha chuma chenye kinawekwa kwenye kinywa cha munyama ili kumuongoza na kumuzuia.
Ao “Ili usijifanye kuwa kama yeye.”
Ao “eko.”
Tnn., “kunywa jeuri.”
Ao “yenye kuninginia.”
Ao “mwenye anaumiza kila mutu.”
Ao “eko.”
Ao “eko.”
Ao “eko.”
Ao “maegemeo yake.”
Ao “eko.”
Ao pengine, “mwenye anajiingiza katika.”
Ao “mishale yenye kuua.”
Ao “ni kama vitu vya kumezwa kwa pupa.”
Tnn., “midomo yenye shauku pamoja na.”
Ao “Kwa maana moyo wake ni wenye kuchukiza kabisa.”
Tnn., “itazaa nini.”
Tnn., “mugeni.”
Tnn., “Mugeni.”
Ao pengine, “haziko za kweli; ni za kulazimishwa.”
Ao “Nafsi yenye kutosheka inazarau.” Tnn., “anakanyangia chini.”
Ao “mwenye anakimbia.”
Ao “nyumba yake; kiota chake.”
Ao “shauri la nafsi.”
Ao “azabu.”
Ao “mugeni.”
Ao “musumbufu.”
Tnn., “uso wa rafiki.”
Ao “Sheoli na Abadoni.”
Ao “Vilevile mutu ni kulingana na sifa yake.”
Ao “Weka moyo juu ya; Kazia uangalifu.”
Ao “mwana-simba.”
Ao “uasi.”
Tnn., “yeye.”
Ao “mwenye anaogopa kila wakati.”
Ao “mwenye kulemewa na damu ya nafsi.”
Ao “shimo.”
Ao “pupa.”
Ao pengine, “Nafsi yenye kiburi inachochea.”
Tnn., “atanenepeshwa.”
Ao “mwenye anaendelea kuwa kichwa-nguvu.”
Ao “kata-midomo.”
Ao “makila ya.”
Ao “mwenye hana lawama.”
Ao “nafsi ya.”
Ao pengine, “Lakini mutu munyoofu anatafuta kulinda uzima wake.”
Tnn., “roho yake yote.”
Tnn., “wanakutana pamoja.”
Ni kusema, Yeye anawapatia uzima.
Ao “Nizamu; Azabu.”
Ao “atafurahisha sana nafsi yako.”
Ao “maono ya unabii; ufunuo.”
Ao “anachukia nafsi yake mwenyewe.”
Ao “kiapo chenye laana.”
Ao “Kuogopa.”
Ao “kunatega.”
Ao pengine, “wanatafuta kukubaliwa na.” Tnn., “wanatafuta uso wa.”
Tnn., “ameinua miisho yote ya dunia.”
Ao “kushambulia.”
Tnn., “mavi yao.”
Mataya ni mifupa ya kinywa yenye kubeba meno.
Ao “Sheoli,” ni kusema, kaburi la wanadamu wote. Angalia Maana ya Maneno.
Ao “bonde la muto.”
Ao “yenye kuwa ya ajabu sana kwangu.”
Ao “mashua ya maji; bateau.”
Ao “mwenye hapendwe.”
Ao “viko na hekima nyingi sana.”
Tnn., “hawako kikundi cha watu wenye nguvu.”
Ao “Pelele.”
Tnn., “hawako kikundi cha watu wenye nguvu.”
Ao “wakiwa wamegawanywa vikundi-vikundi.”
Ao “wenye uchungu wa nafsi.”
Ao “Tetea mashitaka ya.”
Ao “bibi muzuri.”
Angalia Maana ya Maneno.
Ao “mashua za maji; bateaux.”
Ao “kwa mapato yake.” Tnn., “kutokana na matunda ya mikono yake.”
Tnn., “Anafunga nguvu kwenye viuno vyake.”
Ao “neige.”
Tnn., “nguo mbili.”
Ao “nguo za ndani.”
Ao “mishipi.”
Ao “eko.”
Ao “anacheka siku yenye kuja.”
Ao “Mafundisho ya upendo yako; Sheria ya upendo mushikamanifu iko.”
Ao “wazuri.”
Ao “unaweza kuwa kitu bure.”
Tnn., “Mumupatie kutokana na matunda ya mikono yake.”