Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • nwt Mithali 1:1-31:31
  • Mezali

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Mezali
  • Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
Mezali

MEZALI

1 Mezali za Sulemani,+ mwana wa Daudi,+ mufalme wa Israeli:+

 2 Ili kujifunza* hekima+ na nizamu;

Ili kuelewa maneno ya hekima;

 3 Ili kupata nizamu+ yenye inaleta ufahamu,

Haki,+ uwezo wa kuchukua maamuzi ya muzuri,*+ na unyoofu;*

 4 Ili kumupatia werevu+ mutu mwenye hana uzoefu;

Ili kumupatia kijana ujuzi na uwezo wa kufikiri.+

 5 Mutu mwenye hekima anasikiliza na kujifunza mengi zaidi;+

Mutu mwenye uelewaji anapata ufundi wa kuongoza*+

 6 Ili kuelewa mezali na neno la fumbo,*

Maneno ya wenye hekima na vitendawili vyao.+

 7 Kumuogopa* Yehova ndio mwanzo wa ujuzi.+

Ni wapumbavu tu ndio wanazarau hekima na nizamu.+

 8 Mwana wangu, sikiliza nizamu ya baba yako,+

Na usiache mafundisho* ya mama yako.+

 9 Ni taji la maua lenye kuvutia kwa ajili ya kichwa chako+

Na pambo la muzuri kwa ajili ya shingo yako.+

10 Mwana wangu, kama watenda-zambi wanajaribu kukushawishi, usikubali.+

11 Kama wanasema: “Kuja tuende.

Tuvizie ili kumwanga damu.

Tutajificha, tukingojea kushambulia bila sababu watu wenye hawana kosa.

12 Tutawameza wakiwa wazima kama vile Kaburi* linameza,

Wazima-wazima, kama wale wenye kushuka katika shimo.

13 Tukamate hazina zao zote zenye samani;

Nyumba zetu tutazijaza vitu vyenye vinachukuliwa katika vita.

14 Unapaswa kujiunga na sisi,*

Na sisi wote tutagawana sawasawa vitu vyenye tunaiba.”*

15 Mwana wangu, usiwafuate.

Epusha miguu yako na njia yao.+

16 Kwa maana miguu yao inakimbilia kutenda uovu;

Wanaenda haraka kumwanga damu.+

17 Kwa kweli ni kazi bure kutandika wavu* wakati ndege iko* anaona.

18 Ndio sababu wanavizia ili kumwanga damu;

Wanajificha ili waondoe uzima wa* wengine.

19 Hizo ndizo njia za wale wenye kutafuta faida yenye haiko ya haki,

Yenye itaondoa uzima wa* wale wenye kuipata.+

20 Hekima ya kweli+ inaita kwa sauti kubwa katika barabara.+

Inaendelea kupandisha sauti yake katika viwanja vya watu wote.+

21 Inaita kwa sauti kubwa kwenye makutano ya* barabara zenye watu wengi.

Inasema hivi kwenye milango mikubwa ya muji:+

22 “Ninyi wenye kukosa uzoefu mutaendelea kupenda kukosa uzoefu mupaka wakati gani?

Ninyi wazihaki mutaendelea kufurahia zihaka mupaka wakati gani?

Na ninyi wapumbavu mutaendelea kuchukia ujuzi mupaka wakati gani?+

23 Mukubali karipio langu.*+

Halafu nitawamwangia roho yangu;

Nitawajulisha maneno yangu.+

24 Kwa sababu niliwaita, lakini muliendelea kukataa,

Nilinyoosha mukono wangu, lakini hakuna mwenye alikazia uangalifu,+

25 Muliendelea kupuuza mashauri yangu yote

Na kukataa karipio langu,

26 Mimi pia nitacheka wakati musiba utawapata;

Nitafanya zihaka wakati jambo lenye munaogopa sana litakuja,+

27 Wakati jambo lenye munaogopa sana litakuja kama zoruba,

Na wakati musiba wenu utafika kama upepo wa zoruba,

Wakati shida na taabu vitakuja juu yenu.

28 Wakati huo wataendelea kuniita, lakini sitajibu;

Watanitafuta kwa bidii, lakini hawatanipata,+

29 Kwa sababu walichukia ujuzi,+

Na hawakuchagua kumuogopa Yehova.+

30 Walikataa shauri langu;

Walizarau makaripio yangu yote.

31 Basi watapata matokeo* ya njia yao,+

Na watashiba kabisa shauri lao wenyewe.*

32 Kwa maana upotovu wa wajinga utawaua,

Na kukosa kujali kwa wapumbavu kutawaharibu.

33 Lakini ule mwenye kunisikiliza ataishi kwa usalama+

Na hatasumbuliwa na woga wa musiba.”+

2 Mwana wangu, kama unakubali maneno yangu

Na kuweka amri zangu kama hazina,+

 2 Kwa kutega sikio lako ili usikilize hekima+

Na kuelekeza moyo wako kwenye utambuzi;+

 3 Pia, kama unaita uelewaji kwa sauti+

Na kupandisha sauti yako ili upate utambuzi;+

 4 Kama unaendelea kuutafuta kama feza,+

Na kuendelea kuutafuta sana kama hazina zenye kufichwa;+

 5 Basi utaelewa maana ya kumuogopa Yehova,+

Na utapata ujuzi juu ya Mungu.+

 6 Kwa maana Yehova mwenyewe anatoa hekima;+

Katika kinywa chake munatoka ujuzi na utambuzi.

 7 Anaweka kama hazina hekima yenye kutenda kwa ajili ya wanyoofu;

Yeye ni ngao kwa wale wenye kutembea katika uaminifu-mushikamanifu.+

 8 Analinda njia za haki,

Na atalinda njia ya washikamanifu wake.+

 9 Halafu utaelewa mambo ya uadilifu* na ya haki na yenye kunyooka;

Njia yote ya mambo ya muzuri.+

10 Wakati hekima itaingia katika moyo wako+

Na wakati ujuzi utapendeza nafsi* yako,+

11 Uwezo wa kufikiri utakulinda,+

Na utambuzi utakuchunga,

12 Ili kukuokoa kutoka katika njia ya mubaya,

Kutoka kwa mutu mwenye kusema mambo mapotovu,+

13 Kutoka kwa wale wenye kuacha njia zenye kunyooka

Ili kutembea katika njia za giza,+

14 Kutoka kwa wale wenye kufurahia kutenda mabaya,

Wenye kufurahia upotovu wa uovu,

15 Wale wenye njia zao ni zenye kujikunja-kunja

Na wenye mwenendo wao wote ni mudanganyifu.

16 Utakuokoa kutoka kwa mwanamuke mwenye kupotoka,*

Kutokana na maneno laini* ya mwanamuke mwasherati,*+

17 Mwenye anaacha rafiki wa karibu* wa ujana wake+

Na kusahau agano la Mungu wake;

18 Kwa maana nyumba yake inazama katika kifo,

Na njia zake* zinaongoza kwa wale wenye hawana uwezo katika kifo.+

19 Kati ya wale wenye kulala naye,* hakuna mutu yeyote mwenye atarudia,

Wala hawatarudia kwenye njia za uzima.+

20 Basi fuata njia ya watu wema

Na ubakie kwenye njia za wenye haki,+

21 Kwa maana ni watu wenye kufanya mambo yenye kunyooka tu ndio watakaa katika dunia,

Na wenye hawana lawama* ndio watabakia ndani yake.+

22 Lakini waovu, wataondolewa katika dunia,+

Na wadanganyifu watangolewa kutoka ndani yake.+

3 Mwana wangu, usisahau mafundisho* yangu,

Na moyo wako ushike amri zangu,

 2 Kwa sababu zitakuongezea siku nyingi

Na miaka ya uzima na amani.+

 3 Usiruhusu upendo mushikamanifu na uaminifu* vikuache.+

Uvifunge kuzunguka shingo yako;

Uviandike kwenye kibao cha moyo wako;+

 4 Halafu utakubaliwa na kupata ufahamu muzuri

Mbele ya macho ya Mungu na ya mwanadamu.+

 5 Umutegemee Yehova+ kwa moyo wako wote,

Na usitegemee* uelewaji wako mwenyewe.+

 6 Umutambue katika njia zako zote,+

Naye atanyoosha mapito yako.+

 7 Usikuwe mwenye hekima mbele ya macho yako mwenyewe.+

Umuogope Yehova na ujiepushe na ubaya.

 8 Hilo litaponyesha mwili wako*

Na kuburudisha mifupa yako.

 9 Umuheshimie Yehova kupitia vitu vyako vyenye samani,+

Kupitia matunda ya kwanza ya* mazao* yako yote;+

10 Halafu madepo yako yatajazwa kabisa,+

Na mashimo yako ya kukamulia divai yatajaa sana* divai mupya.

11 Mwana wangu, usikatae nizamu ya Yehova,+

Na usichukie karipio lake,+

12 Kwa maana wale wenye Yehova anapenda anawakaripia,+

Kama vile baba anamukaripia mwana mwenye anafurahia sana.+

13 Mwenye furaha ni mutu mwenye anapata hekima+

Na mutu mwenye anapata utambuzi;

14 Kupata hekima ni muzuri kuliko kupata feza,

Na kuipata kama faida ni muzuri kuliko kupata zahabu.+

15 Ni yenye samani kuliko marijani;*

Hakuna kitu chenye unatamani chenye kinaweza kulinganishwa nayo.

16 Maisha ya murefu yanapatikana katika mukono wake wa kuume;

Utajiri na utukufu viko katika mukono wake wa kushoto.

17 Njia zake ni zenye kupendeza,

Na njia zake zote ni zenye amani.+

18 Ni muti wa uzima kwa wale wenye kuishika,

Na wale wenye kuishika sana wataitwa wenye furaha.+

19 Yehova aliweka musingi wa dunia kwa hekima.+

Kwa utambuzi alifanya mbingu zikuwe imara kabisa.+

20 Kwa ujuzi wake maji mengi yalitenganishwa

Na anga zenye mawingu ziliangusha matone-matone ya umande.+

21 Mwana wangu, zisiondoke mbele ya macho yako.*

Linda hekima yenye kutenda na uwezo wa kufikiri;

22 Zitakupatia* uzima

Na zitakuwa pambo kwa ajili ya shingo yako;

23 Halafu utatembea kwa usalama katika njia yako,

Na muguu wako hautajikwaa* hata kidogo.+

24 Wakati utalala, hautaogopa;+

Utalala, na usingizi wako utakuwa mutamu.+

25 Hautaogopa jambo lolote lenye kuogopesha sana lenye linatokea bila kutazamia+

Wala zoruba yenye inakuja juu ya waovu.+

26 Kwa maana Yehova atakuwa chanzo cha tumaini lako;+

Atalinda muguu wako usinaswe.+

27 Usiime mema wale wenye unapaswa kutendea mema*+

Kama uko na uwezo wa kusaidia.*+

28 Usimuambie jirani yako, “Uende; urudie wakati mwingine! Nitakupatia kesho,”

Kama unaweza kumupatia kitu hicho sasa.

29 Usipange kumutendea mubaya jirani yako+

Wakati anafikiri kwamba anaishi kwa usalama karibu na wewe.

30 Usigombane na mutu bila sababu+

Kama hakukutendea jambo lolote la mubaya.+

31 Usimusikilie wivu mutu mwenye jeuri+

Wala kuchagua yoyote kati ya njia zake,

32 Kwa maana Yehova anachukia mutu mudanganyifu,+

Lakini anafanya urafiki wa karibu pamoja na watu wanyoofu.+

33 Laana ya Yehova iko juu ya nyumba ya muovu,+

Lakini anabariki makao ya wenye haki.+

34 Kwa maana yeye anachekelea wale wenye kuchekelea wengine,+

Lakini anaonyesha wapole wema.+

35 Wenye hekima watariti heshima,

Lakini wajinga wanatukuza haya.+

4 Wana wangu, musikilize nizamu ya baba;+

Musikilize kwa uangalifu ili mupate uelewaji,

 2 Kwa maana nitawapatia mafundisho ya muzuri;

Musiache mafundisho* yangu.+

 3 Nilikuwa kabisa mwana wa baba yangu+

Na mama yangu alinipenda sana.+

 4 Baba alinifundisha na kusema: “Moyo wako ushike kabisa maneno yangu.+

Shika amri zangu na uendelee kuishi.+

 5 Pata hekima, pata uelewaji.+

Usisahau, na usigeuke na kuacha mambo yenye ninasema.

 6 Usiiache, nayo itakulinda.

Uipende, nayo itakuchunga.

 7 Hekima ndilo jambo la maana zaidi,*+ kwa hiyo pata hekima,

Na pamoja na vyote vyenye unapata, pata uelewaji.+

 8 Uione kuwa ya maana sana, nayo itakuinua.+

Itakuheshimia kwa sababu unaikumbatia.+

 9 Itatia taji la maua lenye kuvutia kwenye kichwa chako;

Itakupamba kwa taji la uzuri.”

10 Sikiliza, mwana wangu, na ukubali maneno yangu,

Na miaka ya maisha yako itakuwa mingi.+

11 Nitakufundisha katika njia ya hekima;+

Nitakuongoza katika njia za unyoofu.+

12 Wakati unatembea, hatua zako hazitazuiwa;

Na kama unakimbia, hautajikwaa.

13 Shika kabisa nizamu; usiiache.+

Uilinde, kwa maana ni uzima wako.+

14 Usiingie katika njia ya waovu,

Na usitembee katika njia ya watu wabaya.+

15 Uiepuke, usiifuate;+

Ujiepushe nayo, na upite mbali nayo.+

16 Kwa maana hawawezi kulala kama hawajafanya mambo ya mubaya.

Hawapate usingizi kama hawajaangusha mutu.

17 Wanajilisha mukate wa uovu,

Na kunywa divai ya jeuri.

18 Lakini njia ya wenye haki iko kama mwangaza wenye kungaa wa asubui

Wenye kungaa zaidi na zaidi mupaka muchana kamili.+

19 Njia ya waovu iko kama giza;

Hawajue ni nini kinawafanya wajikwae.

20 Mwana wangu, sikiliza maneno yangu;

Sikiliza kwa uangalifu* mambo yenye ninasema.

21 Yasiondoke mbele ya macho yako;

Uyaweke ndani kabisa ya moyo wako,+

22 Kwa maana ni uzima kwa wale wenye kuyapata+

Na afya ya muzuri kwa mwili wao wote.

23 Linda moyo wako kuliko vitu vyote vyenye unalinda,+

Kwa maana ni mule munatoka chemchemi za uzima.

24 Ujiepushe kabisa na maneno yenye kupotoka,+

Na ujitenge mbali na mazungumuzo yenye udanganyifu.

25 Macho yako yanapaswa kuangalia mbele moja kwa moja,

Ndiyo, kaza macho yako* moja kwa moja mbele yako.+

26 Sawazisha* mahali miguu yako itapita,+

Na njia zako zote zitakuwa hakika.

27 Usielekee kuume wala kushoto.+

Epusha miguu yako na mambo ya mubaya.

5 Mwana wangu, sikiliza hekima yangu.

Sikiliza kwa uangalifu* utambuzi wangu,+

 2 Ili uweze kulinda uwezo wako wa kufikiri

Na kulinda ujuzi kwa midomo yako.+

 3 Kwa maana midomo ya mwanamuke mwenye kupotoka* inaangusha matone-matone kama sega la asali,+

Na kinywa chake ni laini kuliko mafuta.+

 4 Lakini mwishowe ni muchungu kama pakanga+

Na mwenye makali kama upanga wenye kukata pande zote mbili.+

 5 Miguu yake inashuka kwenye kifo.

Hatua zake zinaongoza moja kwa moja katika Kaburi.*

 6 Hafikiriake njia ya uzima.

Njia yake inaenda huku na huku, lakini hajue kwenye inaelekea.

 7 Sasa, wana wangu, munisikilize

Na musiache mambo yenye ninasema.

 8 Mukae mbali naye;

Musikaribie muingilio wa nyumba yake,+

 9 Ili musipatie wengine heshima yenu+

Wala kuvuna miaka ya ukali;+

10 Ili wageni wasimalize mali* zenu+

Na ili vitu vyenye mulifanyia kazi ya jasho visiende katika nyumba ya mugeni.

11 Mukifanya vile, mutalia kwa maumivu kwenye mwisho wa maisha yenu

Wakati nyama yenu na mwili wenu vitakuwa zaifu+

12 Na utasema: “Nilichukia sana nizamu!

Moyo wangu ulizarau sana karipio!

13 Sikusikiliza sauti ya wafundishaji wangu

Wala kusikiliza kwa uangalifu walimu wangu.

14 Nilikuwa karibu kuangamia kabisa

Katikati ya kutaniko lote.”*+

15 Kunywa maji ya tangi lako mwenyewe

Na maji yenye kutiririka* ya kisima chako mwenyewe.+

16 Je, chemchemi zako zisambae inje,

Na mito yako midogo ya maji katika viwanja vya watu wote?+

17 Yakuwe yako peke yako,

Na yasikuwe ya wageni pamoja na wewe.+

18 Chemchemi yako ibarikiwe,*

Na ufurahi pamoja na bibi wa ujana wako,+

19 Paa-dike mwenye kupendeza, mbuzi wa milima* mwenye kuvutia.+

Maziwa yake yakushibishe* nyakati zote.

Upendo wake ukuvutie sana kila wakati.+

20 Basi mwana wangu, sababu gani uvutiwe sana na mwanamuke mwenye kupotoka*

Ao kukumbatia kifua cha mwanamuke mwasherati?*+

21 Kwa maana njia za mwanadamu ziko mbele ya macho ya Yehova;

Anachunguza njia zake zote.+

22 Muovu ananaswa na makosa yake mwenyewe,

Na atashikwa katika kamba za zambi yake mwenyewe.+

23 Atakufa kwa sababu ya kukosa nizamu

Na kupotea njia kwa sababu ya upumbavu wake wenye kupita kiasi.

6 Mwana wangu, kama umeahidi kulipia jirani yako mukopo,+

Kama umepatiana mukono na mugeni,*+

 2 Kama umenaswa na ahadi yako,

Kama umekamatwa na maneno ya kinywa chako,+

 3 Mwana wangu, fanya hivi na ujiokoe,

Kwa maana umeanguka katika mukono wa jirani yako:

Uende na ujinyenyekeze mwenyewe na kumulilia haraka jirani yako.+

 4 Usiruhusu macho yako yapate usingizi,

Wala kope zako kusinzia.

 5 Ujiokoe kama swala kutoka katika mukono wa muwindaji,

Kama ndege kutoka katika mukono wa muwindaji wa ndege.

 6 Uende kwa siafu, wewe muvivu;+

Chunguza njia zake na ukuwe na hekima.

 7 Hata kama hana kamanda, ofisa, wala mutawala,

 8 Anatayarisha chakula chake wakati wa kipindi cha joto,+

Na kukusanya chakula chake wakati wa mavuno.

 9 Wewe muvivu, utaendelea kulala pale mupaka wakati gani?

Utaamuka wakati gani katika usingizi wako?

10 Kulala kidogo, kusinzia kidogo,

Kukunja mikono kidogo ili kupumuzika,+

11 Na umaskini wako utakuja kama munyanganyi,

Na uhitaji wako kama mwanaume mwenye silaha.+

12 Mutu muovu mwenye hana mafaa yoyote anazunguka-zunguka akisema maneno yenye kupotoka;+

13 Anafinya jicho lake,+ anafanya alama kwa muguu wake, na kufanya alama kwa vidole vyake.

14 Kwa moyo wenye kupotoka,

Anafanya sikuzote mipango ya uovu+ na kueneza ugomvi.+

15 Kwa hiyo, musiba wake utakuja bila kutazamia;

Atavunjwa kwa kushitukia na hataweza kupona.+

16 Kuko vitu sita (6) vyenye Yehova anachukia;

Ndiyo, vitu saba (7) vyenye anachukia* sana:

17 Macho yenye majivuno,+ ulimi wa uongo,+ na mikono yenye kumwanga damu yenye haina kosa,+

18 Moyo wenye kufanya mipango ya uovu,+ na miguu yenye kukimbilia haraka kwenye uovu,

19 Shahidi wa uongo mwenye kusema uongo kila wakati anapumua,+

Na mutu yeyote mwenye kupanda ugomvi kati ya ndugu.+

20 Mwana wangu, shika amri ya baba yako,

Na usiache mafundisho* ya mama yako.+

21 Uvifunge sikuzote kuzunguka moyo wako;

Uvifunge kuzunguka shingo yako.

22 Wakati utatembea huku na huku, itakuongoza;

Wakati utalala, itakulinda;

Na wakati utaamuka, itasema na wewe.*

23 Kwa maana amri hiyo ni taa,+

Na sheria ni mwangaza,+

Na makaripio ya nizamu ni njia ya uzima.+

24 Yatakulinda na mwanamuke mubaya,+

Yatakulinda na ulimi wenye kushawishi wa mwanamuke mwasherati.*+

25 Usitamani uzuri wake katika moyo wako+

Wala kukubali akuvute kupitia macho yake yenye kuvutia,

26 Kwa maana kahaba anafanya mutu abakie na kipande kimoja tu cha mukate,+

Lakini bibi ya mwanaume mwingine anawinda uzima wenye* samani.

27 Je, mutu anaweza kukusanya moto kwenye kifua chake na nguo zake zisiungue?+

28 Ao je, mutu anaweza kutembea juu ya makaa yenye kuwaka moto na miguu yake isiungue?

29 Ni vile kuhusu mutu yeyote mwenye analala na bibi ya jirani yake;

Hakuna mutu yeyote mwenye kugusa bibi huyo mwenye atakosa kupewa azabu.+

30 Watu hawamuzarau mwizi

Kama anaiba ili ajishibishe* wakati anasikia njaa.

31 Lakini, akipatikana, atalipa mara saba (7);

Atatoa vitu vyote vya maana vya nyumba yake.+

32 Mutu yeyote mwenye kufanya uzinifu na mwanamuke hana akili ya muzuri;*

Ule mwenye kufanya vile analeta uharibifu juu yake mwenyewe.+

33 Atapata tu vidonda na hataheshimiwa,+

Na haya yake haitafutwa.+

34 Kwa maana wivu unafanya bwana akasirike sana;

Hataonyesha huruma wakati atalipiza kisasi.+

35 Hatakubali malipo yoyote;*

Hatatulizwa, hata ukimupatia zawadi kubwa kadiri gani.

7 Mwana wangu, shika maneno yangu,

Na uweke amri zangu kama hazina.+

 2 Shika amri zangu na uishi;+

Linda mafundisho* yangu kama mboni ya jicho lako.

 3 Uvifunge kuzunguka vidole vyako;

Uviandike kwenye kibao cha moyo wako.+

 4 Ambia hekima, “Wewe ni dada yangu,”

Na uite uelewaji “mutu wa jamaa yangu,”

 5 Ili vikulinde na mwanamuke mwenye kupotoka,*+

Na mwanamuke mwasherati* na maneno yake laini.*+

 6 Nikiwa kwenye dirisha la nyumba yangu,

Niliangalia chini kupitia kayungio ya dirisha langu,

 7 Na wakati nilikuwa ninachunguza wajinga,*

Nilitambua kati ya vijana, kijana mumoja mwanaume mwenye kukosa akili ya muzuri.*+

 8 Alipita katika barabara karibu na makutano ya barabara katika njia yenye kupeleka kwa mwanamuke huyo

Na alishika njia ya kuenda kwenye nyumba ya mwanamuke huyo

 9 Mangaribi, wakati giza linaanza,+

Wakati usiku na giza vinaingia.

10 Kisha nikamuona mwanamuke akikutana naye,

Alikuwa amevaa kama* kahaba,+ mwenye moyo mujanja.

11 Ni mwenye makelele na iko* kichwa-nguvu.+

Habakiake* katika nyumba yake.

12 Wakati fulani iko* inje, wakati mwingine iko* katika viwanja vya watu wote,

Anajificha karibu na kila makutano ya barabara.+

13 Kisha anamukamata kwa nguvu kijana huyo na kumupatia busu;

Bila haya, mwanamuke huyo anamuambia:

14 “Nilipaswa kutoa zabihu za ushirika.+

Leo nilitimiza naziri zangu.

15 Ndiyo sababu nimekuja kukutana na wewe,

Kukutafuta, na nimekupata!

16 Nimetandika matandiko ya muzuri kwenye kitanda changu,

Kitani cha Misri chenye rangi mbalimbali.+

17 Nimenyunyiza* manemane, udi, na mudalasini juu ya kitanda changu.+

18 Kuja, tukunywe na kushiba upendo mupaka asubui;

Na tujifurahishe pamoja kwa mapendo,

19 Kwa maana bwana yangu haiko nyumbani;

Ameenda safari ya mbali.

20 Alibeba mufuko wa feza,

Na hatarudia mupaka siku ya mwezi wenye kuenea.”

21 Anamupotosha kwa ushawishi mukubwa.+

Anamutongoza kwa maneno laini.

22 Mara moja kijana huyo anamufuata, kama ngombe-dume mwenye anaenda kuchinjwa,

Kama mupumbavu mwenye anaenda kupewa azabu katika mikatale,*+

23 Mupaka wakati mushale unatoboa maini yake;

Kama ndege mwenye anakimbia kuingia katika mutego, hajue kwamba hilo litamufanya apoteze uzima wake.*+

24 Na sasa, wana wangu, munisikilize;

Musikilize kwa uangalifu maneno yenye ninasema.

25 Musiruhusu moyo wenu ugeuke na kufuata njia zake.

Musipotee njia na kufuata njia zake,+

26 Kwa maana amefanya wengi waanguke wakiwa wameuawa,+

Na wale wenye ameua ni wengi sana.+

27 Nyumba yake inaongoza katika Kaburi;*

Inashuka chini kwenye vyumba vya ndani vya kifo.

8 Je, hekima haiite kwa sauti kubwa?

Je, utambuzi haupandishe sauti yake?+

 2 Kwenye nafasi za juu+ pembeni ya barabara,

Inasimama kwenye makutano ya barabara.

 3 Karibu na milango mikubwa yenye kupeleka kwenye muji,

Kwenye miingilio ya milango,

Inaendelea kulia kwa sauti kubwa:+

 4 “Ninawaita, Enyi watu;

Ninalalamikia kila mutu.*

 5 Ninyi watu wenye hawana uzoefu, mujifunze werevu;+

Ninyi wajinga, mujipatie moyo wenye uelewaji.*

 6 Musikilize, kwa maana mambo yenye ninasema ni ya maana,

Midomo yangu inasema mambo yenye kuwa sawa;

 7 Kwa maana kinywa changu kinasema ukweli kwa sauti ya chini,

Na midomo yangu inachukia sana jambo lenye uovu.

 8 Maneno yote ya kinywa changu ni yenye haki.

Kati ya maneno hayo, hakuna neno moja lenye kupengama ao lenye kupotoka.

 9 Yote yako wazi kabisa kwa mutu mwenye utambuzi

Na yako sawa kwa wale wenye wamepata ujuzi.

10 Mukamate nizamu yangu pa nafasi ya feza,

Na ujuzi pa nafasi ya zahabu safi sana,+

11 Kwa maana hekima ni ya muzuri kuliko marijani;*

Vitu vingine vyote vyenye kutamanika haviwezi kulinganishwa nayo.

12 Mimi, hekima, ninakaa pamoja na werevu;

Nimepata ujuzi na uwezo wa kufikiri.+

13 Kumuogopa Yehova kunamaanisha kuchukia ubaya.+

Ninachukia kujiinua na kiburi+ na njia ya uovu na maneno yenye kupotoka.+

14 Niko na shauri la muzuri na hekima yenye kutenda;+

Uelewaji+ na nguvu+ ni vyangu.

15 Kwa musaada wangu wafalme wanaendelea kutawala,

Na maofisa wakubwa wanatunga sheria za haki.+

16 Kwa musaada wangu wakubwa wanaendelea kutawala,

Na watu wenye vyeo wanahukumu kwa haki.

17 Ninapenda wale wenye kunipenda,

Na wale wenye kunitafuta watanipata.+

18 Niko na utajiri na utukufu,

Mali yenye kudumu* na haki.

19 Matunda yangu ni ya muzuri kuliko zahabu, hata kuliko zahabu yenye kusafishwa,

Na mazao yangu ni ya muzuri kuliko feza ya muzuri kabisa.+

20 Ninatembea katika njia ya uadilifu,*

Katikati ya njia za haki;

21 Ninapatia wale wenye kunipenda uriti mwingi,

Na ninajaza madepo yao.

22 Yehova aliniumba nikiwa mwanzo wa njia yake,+

Mwanzo kabisa wa kazi zake za zamani sana.+

23 Niliwekwa tangu nyakati za zamani,*+

Tangu mwanzo, nyakati za zamani mbele dunia ikuwe.+

24 Wakati hapakukuwa maji yenye kuenda chini sana,+ nilizaliwa,*

Wakati hapakukuwa chemchemi zenye kujaa sana maji.

25 Mbele milima haijawekwa mahali pake,

Mbele vilima vikuwe, nilizaliwa,

26 Wakati alikuwa hajaumba dunia na maeneo yake ya mashamba

Wala madonge ya kwanza ya udongo wa dunia.

27 Wakati alitayarisha mbingu,+ nilikuwa pale;

Wakati alichora mwisho* kwenye uso wa maji,+

28 Wakati alifanya imara* mawingu yenye kuwa juu,

Wakati aliweka musingi wa chemchemi za mahali kwenye maji yenye kuenda chini sana,

29 Wakati alitilia bahari sheria

Kwamba maji yake yasipite agizo lake,+

Wakati aliweka* misingi ya dunia,

30 Wakati huo nilikuwa pembeni yake nikiwa fundi wa kazi.+

Mimi ndiye alipenda sana+ siku kwa siku;

Nilifurahi mbele yake wakati wote;+

31 Nilifurahia dunia yake yenye kuikaliwa na watu,

Na wana wa binadamu* ndio nilipenda zaidi sana.

32 Na sasa, wana wangu, munisikilize;

Ndiyo, wenye furaha ni wale wenye wanashika njia zangu.

33 Musikilize nizamu+ na mukuwe na hekima,

Na musiipuuze hata kidogo.

34 Mwenye furaha ni mutu mwenye ananisikiliza

Kwa kuja mbele ya wakati* kwenye milango yangu siku kwa siku,

Kwa kungojea karibu na miimo ya milango yangu;

35 Kwa maana mwenye kunipata atapata uzima,+

Na anakubaliwa na Yehova.

36 Lakini mwenye kunipuuza anajiumiza yeye mwenyewe,*

Na wale wenye kunichukia wanapenda kifo.”+

9 Hekima ya kweli imejenga nyumba yake;

Imechonga nguzo zake saba (7).

 2 Imetayarisha kabisa nyama yake;*

Imechanganya divai yake;

Imepanga pia meza yake.

 3 Imetuma watumishi wake wanamuke

Ili waite kwa sauti kubwa kutoka nafasi za juu za muji:+

 4 “Mutu yeyote mwenye hana uzoefu, aingie humu.”

Anamuambia ule mwenye hana akili ya muzuri:*

 5 “Kuja, ukule mukate wangu

Na ukunywe divai yenye nilichanganya.

 6 Acha ukosefu wako wa uzoefu* na uishi;+

Tembea moja kwa moja katika njia ya uelewaji.”+

 7 Ule mwenye kumurekebisha mutu mwenye zihaka anaalika haya,+

Na mutu yeyote mwenye kumukaripia mutu muovu ataumia.

 8 Usimukaripie mutu mwenye zihaka, kwa maana atakuchukia.+

Karipia mwenye hekima, naye atakupenda.+

 9 Patia mwenye hekima, na atakuwa mwenye hekima zaidi.+

Fundisha mwenye haki, na elimu yake itaongezeka.

10 Kumuogopa Yehova ndio mwanzo wa hekima,+

Na kumujua Mwenye Kuwa Mutakatifu Zaidi+ ni uelewaji.

11 Kwa maana nitafanya siku zako zikuwe nyingi,+

Na miaka ya maisha yako itaongezwa.

12 Kama unakuwa mwenye hekima, unakuwa mwenye hekima kwa faida yako mwenyewe,

Lakini kama uko mwenye zihaka, utabeba zihaka hiyo peke yako.

13 Mwanamuke mujinga ni mwenye fujo.+

Yeye ni mujinga na hajue kitu.

14 Anakaa kwenye muingilio wa nyumba yake

Kwenye kiti katika mahali pa juu pa muji,+

15 Anaita kwa sauti kubwa wale wenye kupita karibu naye,

Wale wenye kuenda mbele moja kwa moja katika njia yao:

16 “Mutu yeyote mwenye hana uzoefu, aingie humu.”

Anaambia wale wenye hawana akili ya muzuri:*+

17 “Maji yenye yaliibwa ni matamu,

Na chakula chenye kukuliwa kwa uficho ni chenye kupendeza.”+

18 Lakini hawajue kwamba wale wenye hawana uwezo katika kifo wako pale,

Kwamba wageni wake wanapatikana katika sehemu za chini kabisa za Kaburi.*+

10 Mezali za Sulemani.+

Mwana mwenye hekima anamufurahisha baba yake,+

Lakini mwana mupumbavu ni huzuni kwa mama yake.

 2 Mali zenye zilipatikana kwa uovu hazitakuwa na faida yoyote,

Lakini haki ndiyo inaokoa katika kifo.+

 3 Yehova hataacha mwenye haki akae* na njaa,+

Lakini ataima waovu mambo yenye wanatamani sana.

 4 Mikono yenye uvivu italeta umaskini,+

Lakini mikono yenye bidii inaleta utajiri.+

 5 Mwana mwenye kutenda kwa ufahamu anakusanya mazao wakati wa kipindi cha joto,

Lakini mwana mwenye kutenda kwa haya analala usingizi muzito wakati wa mavuno.+

 6 Baraka ziko juu ya kichwa cha mwenye haki,+

Lakini kinywa cha muovu kinaficha jeuri.

 7 Kumbukumbu la* mwenye haki litabarikiwa,+

Lakini jina la muovu litaoza.+

 8 Mutu mwenye moyo wa hekima atakubali mafundisho,*+

Lakini mwenye kuzungumuza maneno ya ujinga atakanyangiwa chini.+

 9 Mwenye kutembea kwa uaminifu-mushikamanifu atatembea kwa usalama,+

Lakini mwenye kupotosha njia zake atajulikana.+

10 Mwenye kufinya jicho lake kwa udanganyifu anatokeza huzuni,+

Na ule mwenye kuzungumuza maneno ya ujinga atakanyangiwa chini.+

11 Kinywa cha mwenye haki ni chemchemi ya uzima,+

Lakini kinywa cha muovu kinaficha jeuri.+

12 Chuki ndiyo inachochea ugomvi,

Lakini upendo unafunika makosa yote.+

13 Hekima inapatikana kwenye midomo ya mutu mwenye utambuzi,+

Lakini fimbo ni kwa ajili ya mugongo wa mutu mwenye hana akili ya muzuri.*+

14 Watu wenye hekima wanaweka ujuzi kama hazina,+

Lakini kinywa cha mupumbavu kinaalika uharibifu.+

15 Mali ya* tajiri ni muji wake wenye ngome.

Uharibifu wa maskini ni umaskini wao.+

16 Kazi ya mwenye haki inaongoza kwenye uzima;

Lakini mazao ya muovu yanaongoza kwenye zambi.+

17 Mwenye kutii nizamu ni njia yenye inapeleka kwenye uzima,*

Lakini mwenye anapuuza karipio anapoteza wengine.

18 Mwenye kuficha chuki yake anasema uongo,+

Na mwenye kueneza habari zenye kuumiza* ni mujinga.

19 Wakati maneno ni mengi, kosa haliwezi kuepukwa,+

Lakini mutu yeyote mwenye anazuia midomo yake anatenda kwa busara.+

20 Ulimi wa mwenye haki uko kama feza ya muzuri kabisa,+

Lakini moyo wa muovu uko na mafaa kidogo.

21 Midomo ya mwenye haki inakulisha* wengi,+

Lakini wapumbavu wanakufa kwa sababu ya kukosa akili.+

22 Baraka ya Yehova ndiyo inamufanya mutu kuwa tajiri,+

Naye haongeze maumivu* yoyote pamoja nayo.

23 Kujiingiza katika mwenendo wa haya ni kama muchezo kwa mujinga,

Lakini hekima ni ya mutu mwenye utambuzi.+

24 Kile muovu anaogopa kitamufikia;

Lakini tamaa ya mwenye haki itatimizwa.+

25 Wakati zoruba itapita, muovu hatakuwa tena,+

Lakini mwenye haki ni musingi milele.+

26 Kama siki* kwenye meno na moshi katika macho,

Ni vile mutu muvivu iko* kwa ule mwenye kumutuma.*

27 Kumuogopa Yehova kunarefusha maisha,+

Lakini miaka ya waovu itafupishwa.+

28 Tumaini* la wenye haki linaleta shangwe,+

Lakini tumaini la waovu litapotea.+

29 Njia ya Yehova ni ngome kwa mutu mwenye hana lawama,+

Lakini ni uharibifu kwa watenda maovu.+

30 Mwenye haki hataangushwa hata siku moja,+

Lakini waovu hawatakaa tena katika dunia.+

31 Kinywa cha mwenye haki kinatokeza* hekima,

Lakini ulimi wenye kupotoka utakatwa.

32 Midomo ya mwenye haki inajua mambo yenye kupendeza,

Lakini kinywa cha waovu kimepotoka.

11 Mizani* za uongo* ni chukizo kwa Yehova,

Lakini kipimo chenye kuwa sawa* kinamufurahisha.+

 2 Wakati kimbelembele kinakuja, haya itafuata,+

Lakini wenye kiasi wako na hekima.+

 3 Uaminifu-mushikamanifu wa wanyoofu ndio unawaongoza,+

Lakini ujanja wa wadanganyifu utawaharibu.+

 4 Mali haitakuwa* na faida yoyote siku ya kasirani kali,+

Lakini haki ndiyo itaokoa katika kifo.+

 5 Haki ya mwenye hana lawama inanyoosha njia yake,

Lakini muovu ataanguka kwa sababu ya uovu wake mwenyewe.+

 6 Haki ya watu wanyoofu itawaokoa,+

Lakini wadanganyifu watanaswa na tamaa zao wenyewe.+

 7 Wakati mutu muovu anakufa, tumaini lake linapotea;

Na matumaini yenye kutegemea nguvu zake yanapotea pia.+

 8 Mwenye haki anaokolewa katika taabu,

Na muovu anakamata nafasi yake.+

 9 Kwa kinywa chake muasi-imani* anamuharibu jirani yake,

Lakini wenye haki wanaokolewa kwa ujuzi.+

10 Wema wa wenye haki unafanya muji ushangilie,

Na wakati waovu wanaangamia, kunakuwa vigelegele vya shangwe.+

11 Muji unainuliwa kwa sababu ya baraka ya watu wanyoofu,+

Lakini kinywa cha waovu kinaubomoa.+

12 Mutu yeyote mwenye hana akili ya muzuri* anamuzarau jirani yake,

Lakini mutu mwenye utambuzi wa kweli anabakia kimya.+

13 Muchongezi anazunguka-zunguka akifunua mazungumuzo ya siri,+

Lakini mutu mwenye kutumainika* anachunga siri.*

14 Wakati hakuna ufundi wa kuongoza,* watu wanaanguka,

Lakini kuko mafanikio* kupitia washauri wengi.+

15 Mutu yeyote mwenye anaahidi kulipia mugeni mukopo hakika ataumia,+

Lakini mutu yeyote mwenye anaepuka* kupana mukono katika kiapo atakuwa salama.

16 Mwanamuke mwema* anapata utukufu,+

Lakini watu wenye hawana huruma wanajikamatia utajiri.

17 Mutu mwenye fazili* anajiletea faida,*+

Lakini mutu mwenye hana huruma anajiletea shida.*+

18 Mutu muovu anapata mushahara wa udanganyifu,+

Lakini mutu mwenye kupanda haki anapata zawabu ya kweli.+

19 Mwenye kutetea haki bila kuyumba-yumba atapata uzima,+

Lakini mwenye kufuatilia uovu anaelekea kwenye kifo.

20 Wale wenye kupotoka katika moyo ni chukizo kwa Yehova,+

Lakini wale wenye njia yao haina lawama wanamufurahisha.+

21 Ukuwe hakika na jambo hili:* Mutu muovu hatakosa kupewa azabu,+

Lakini watoto wa mwenye haki wataponyoka.

22 Kama pete ya zahabu katika pua ya nguruwe

Ni vile pia mwanamuke mwenye sura na umbo ya muzuri mwenye anakataa akili ya muzuri.

23 Tamaa ya wenye haki inaongoza kwenye mema,+

Lakini tumaini la waovu linaongoza kwenye kasirani kali.

24 Mutu mumoja anatoa kwa ukarimu* na kujikuta na vitu vingi zaidi;+

Mwingine anaima wengine kile wanapaswa kupewa, lakini anakuwa maskini.+

25 Mutu mukarimu* atafanikiwa,*+

Na ule mwenye kuburudisha wengine* yeye mwenyewe ataburudishwa.+

26 Watu watalaani mwenye anaficha nafaka,

Lakini watabariki mwenye anaiuzisha.

27 Mwenye anatafuta kwa bidii kutenda mema anatafuta kukubaliwa,+

Lakini mwenye anatafuta ubaya⁠—​hakika ubaya ndio utamupata.+

28 Mwenye kutegemea utajiri wake ataanguka,+

Lakini wenye haki watasitawi kama majani.+

29 Mutu yeyote mwenye kuleta taabu* juu ya watu wa nyumba yake atariti upepo,+

Na mupumbavu atakuwa mutumishi wa mutu mwenye moyo wa hekima.

30 Tunda la mwenye haki ni muti wa uzima,+

Na ule mwenye anapata nafsi* ni mwenye hekima.+

31 Kama, kwa kweli, mwenye haki katika dunia anapewa zawabu,

Itakuwa namna gani kwa muovu na kwa mutenda-zambi!+

12 Mwenye anapenda nizamu anapenda ujuzi,+

Lakini mwenye anachukia karipio hana akili.*+

 2 Mutu mwema anakubaliwa na Yehova,

Lakini Yeye anamuhukumu mutu mwenye kufanya mipango ya uovu.+

 3 Hakuna mutu mwenye anakuwa na usalama kwa kutenda uovu,+

Lakini wenye haki hawatangolewa hata kidogo.

 4 Bibi mwenye uwezo ni taji kwa bwana yake,+

Lakini bibi mwenye kutenda mambo ya haya ni kama kuoza katika mifupa ya bwana yake.+

 5 Mawazo ya wenye haki ni ya haki,

Lakini muongozo wa waovu ni udanganyifu.

 6 Maneno ya waovu yanavizia ili kuua,*+

Lakini kinywa cha watu wanyoofu kinawaokoa.+

 7 Wakati waovu wanapinduliwa, hawako tena,

Lakini nyumba ya wenye haki itaendelea kusimama.+

 8 Mutu anasifiwa kwa sababu ya busara ya kinywa chake,+

Lakini mutu mwenye kuwa na moyo wenye kupotoka atatendewa kwa zarau.+

 9 Afazali usiheshimiwe sana lakini ukuwe na mutumishi

Kuliko kujitukuza mwenyewe na ukose chakula.*+

10 Mwenye haki anatunza wanyama wake wa kufugwa,*+

Lakini hata rehema ya waovu ni yenye ukali.

11 Mwenye analima shamba lake atakuwa na chakula kingi,+

Lakini mwenye kufuatilia vitu vyenye havina mafaa yoyote hana akili ya muzuri.*

12 Mutu muovu anatamani kitu chenye kilikamatwa na watu wengine waovu,

Lakini muzizi wa wenye haki unazaa matunda.

13 Mutu muovu ananaswa na mazungumuzo yake ya zambi,+

Lakini mwenye haki anaponyoka katika taabu.

14 Mutu anashiba mema kutokana na matunda ya maneno yake,*+

Na kazi ya mikono yake itamupatia zawabu.

15 Njia ya mupumbavu iko sawa mbele ya macho yake mwenyewe,+

Lakini mwenye hekima anakubali shauri.+

16 Mupumbavu anaonyesha pale pale* kwamba ameuzika,+

Lakini mutu mwerevu anapuuza* matusi.

17 Mwenye anatoa ushuhuda kwa uaminifu atasema kweli,*

Lakini shahidi wa uongo anasema mambo ya udanganyifu.

18 Maneno yenye kusemwa bila kufikiri yanatoboa kama upanga,

Lakini ulimi wa mwenye hekima unaponyesha.+

19 Midomo yenye kusema kweli itadumu milele,+

Lakini ulimi wenye kusema uongo utadumu wakati kidogo tu.+

20 Udanganyifu uko katika moyo wa wale wenye kufanya mipango mibaya,

Lakini wale wenye kuendeleza* amani wako na furaha.+

21 Hakuna mambo yenye kuumiza yenye yatamupata mwenye haki,+

Lakini waovu watapatwa na misiba mingi.+

22 Midomo yenye kusema uongo ni chukizo kwa Yehova,+

Lakini wale wenye kutenda kwa uaminifu wanamufurahisha.

23 Mutu mwerevu anaficha mambo yenye anajua,

Lakini moyo wa mupumbavu unasema-sema mambo ya upumbavu.+

24 Mukono wa wenye bidii utatawala,+

Lakini mikono yenye uvivu itafanyishwa kazi ya kulazimishwa.+

25 Mahangaiko katika moyo wa mutu yanalemea moyo,*+

Lakini neno la muzuri linauchangamusha.+

26 Mwenye haki anatafuta malisho yake,

Lakini njia ya waovu inawapoteza.

27 Wavivu hawafuatilie mawindo,+

Lakini bidii ni hazina yenye samani ya mutu.

28 Njia ya haki inaongoza kwenye uzima;+

Hakuna kifo katika njia hiyo.

13 Mwana mwenye hekima anakubali nizamu ya baba yake,+

Lakini mwenye kuchekelea wengine hasikilize wakati anakemewa.*+

 2 Mutu atakula mambo ya muzuri kutokana na matunda ya maneno yake,*+

Lakini tamaa kabisa* ya wadanganyifu ni jeuri.

 3 Mwenye analinda kinywa chake* analinda uzima wake,*+

Lakini mwenye anafungua wazi midomo yake ataharibiwa.+

 4 Kuko vitu vyenye mutu muvivu anatamani sana, ijapokuwa hana* kitu,+

Lakini mwenye bidii* atatoshelezwa kabisa.*+

 5 Mwenye haki anachukia uongo,+

Lakini matendo ya waovu yanaleta haya na aibu.

 6 Haki inalinda mutu mwenye njia yake haina kosa,+

Lakini uovu unamushusha mutenda-zambi.

 7 Kuko mutu mwenye anajifanya kama tajiri ijapokuwa hana kitu;+

Kuko mwingine mwenye anajifanya kama maskini ijapokuwa iko* na mali nyingi.

 8 Utajiri ni bei ya ukombozi ya uzima wa mutu,*+

Lakini maskini hawaogopeshwe hata kidogo.*+

 9 Mwangaza wa wenye haki unangaa sana,*+

Lakini taa ya waovu itazimishwa.+

10 Kimbelembele kinaongoza tu kwenye mabishano,+

Lakini hekima ni ya wale wenye kutafuta shauri.*+

11 Mali yenye kupatikana haraka* itapunguka,+

Lakini mali ya ule mwenye anaikusanya kidogo-kidogo* itaongezeka.

12 Tazamio* lenye kucheleweshwa linafanya moyo ugonjwe,+

Lakini tamaa yenye imetimizwa ni muti wa uzima.+

13 Mutu yeyote mwenye anazarau mafundisho* atalipia kosa lake,+

Lakini mwenye anaheshimia amri atapewa zawabu.+

14 Mafundisho* ya mwenye hekima ni chemchemi ya uzima+

Ili kuepusha mutu na mitego ya kifo.

15 Ufahamu mwingi unafanya mutu akubaliwe,

Lakini njia ya wadanganyifu iko nguvu sana.

16 Mutu mwerevu anatenda kwa ujuzi,+

Lakini mupumbavu anafunua upumbavu wake mwenyewe.+

17 Mujumbe muovu anaanguka katika taabu,+

Lakini mujumbe muaminifu analeta maponyo.+

18 Mutu yeyote mwenye anapuuza nizamu anakuwa maskini na anapata haya,

Lakini mwenye anakubali kurekebishwa* atatukuzwa.+

19 Wakati tamaa inatimizwa ni tamu kwa mutu,*+

Lakini wajinga wanachukia kuacha ubaya.+

20 Mwenye anatembea na wenye hekima atakuwa na hekima,+

Lakini mwenye kufanya urafiki na wajinga ataumia.+

21 Musiba unafuatilia watenda-zambi,+

Lakini mafanikio yanapatia wenye haki zawabu.+

22 Mutu mwema anaachia wajukuu wake uriti,

Lakini mali ya mutenda-zambi itawekwa akiba kwa ajili ya mwenye haki.+

23 Shamba la maskini lenye kulimwa linazaa chakula kingi,

Lakini ukosefu wa haki unaweza kuliharibu.*

24 Mutu yeyote mwenye anazuia fimbo yake* anachukia mwana wake,+

Lakini ule mwenye anamupenda anamutia nizamu kwa bidii.*+

25 Mwenye haki anakula na kutosheleza hamu* yake ya kula,+

Lakini tumbo la waovu liko wazi.+

14 Mwanamuke mwenye hekima kabisa anajenga nyumba yake,+

Lakini mwanamuke mupumbavu anaibomoa kwa mikono yake mwenyewe.

 2 Mutu mwenye kutembea katika unyoofu wake anamuogopa Yehova,

Lakini ule mwenye njia zake ni za udanganyifu* anamuzarau Yeye.

 3 Fimbo ya kiburi iko katika kinywa cha mupumbavu,

Lakini midomo ya wenye hekima itawalinda.

 4 Kwenye hakuna ngombe, chombo cha kukulishia wanyama kiko safi,

Lakini nguvu za ngombe-dume zinaleta mavuno mengi.

 5 Shahidi muaminifu hatasema uongo,

Lakini shahidi wa uongo anasema uongo kila wakati anapumua.+

 6 Mutu mwenye kuchekelea wengine anatafuta hekima lakini haipate hata kidogo,

Lakini ujuzi unakuja kwa urahisi kwa mutu mwenye uelewaji.+

 7 Kaa mbali na mutu mupumbavu,

Kwa maana hautapata ujuzi kwenye midomo yake.+

 8 Kwa hekima, mutu mwerevu anaelewa njia yenye anafuata,

Lakini wajinga wanadanganywa* na upumbavu wao.+

 9 Wapumbavu wanachekelea hatia,*+

Lakini watu wanyoofu wako tayari kufanya mapatano.*

10 Moyo unajua uchungu wake mwenyewe,*

Na hakuna mutu wa inje mwenye anaweza kushiriki katika furaha yake.

11 Nyumba ya waovu itaharibiwa,+

Lakini hema ya watu wanyoofu itasitawi.

12 Kuko njia yenye inaonekana kuwa sawa mbele ya macho ya mutu,+

Lakini mwishowe inaongoza kwenye kifo.+

13 Hata katika kicheko moyo unaweza kusikia maumivu,

Na shangwe inaweza kuishia katika huzuni.

14 Mutu mwenye kupotoka katika moyo atavuna matokeo ya njia zake,+

Lakini mutu muzuri anavuna zawabu ya matendo yake.+

15 Mujinga* anaamini kila neno,

Lakini mwerevu anafikiria sana kila hatua.+

16 Mwenye hekima ni muangalifu na anaepuka uovu,

Lakini mujinga hahangaike,* na anajiaminia sana.

17 Mutu mwenye kukasirika haraka anatenda kwa ujinga,+

Lakini mutu mwenye kufikiri sana juu ya mambo* anachukiwa.

18 Mujinga* atariti upumbavu,

Lakini werevu wanavalishwa taji la ujuzi.+

19 Watu wabaya watalazimika kuinama mbele ya watu wema,

Na waovu watainama kwenye milango mikubwa ya wenye haki.

20 Maskini anachukiwa hata na majirani wake,+

Lakini tajiri iko* na marafiki wengi.+

21 Mwenye anazarau jirani yake anatenda zambi,

Lakini mutu yeyote mwenye anaonyesha huruma watu wa hali ya chini ni mwenye furaha.+

22 Je, wale wenye kufanya mipango mibaya hawatapotea njia?

Lakini wale wenye nia ya kutenda mema watapata upendo mushikamanifu na uaminifu.+

23 Kila namna ya kazi ya nguvu iko na faida,

Lakini maongezi bure yanaleta umaskini.+

24 Taji la wenye hekima ni mali yao;

Lakini upumbavu wa wajinga ni upumbavu tu.+

25 Shahidi wa kweli anaokoa uzima,*

Lakini shahidi mudanganyifu anasema uongo kila wakati anapumua.

26 Kuko tumaini lenye nguvu katika kumuogopa Yehova,+

Na woga huo utakuwa kimbilio la watoto wake.+

27 Kumuogopa Yehova ni chemchemi ya uzima,

Ili kuepusha mutu na mitego ya kifo.

28 Wingi wa watu ni utukufu wa mufalme,+

Lakini mutawala mwenye hana raia ameanguka.

29 Mutu mwenye hakasirike haraka iko* na utambuzi mwingi,+

Lakini mwenye hana uvumilivu anaonyesha upumbavu wake.+

30 Moyo mutulivu unapatia mwili uzima,*

Lakini wivu unaozesha mifupa.+

31 Mwenye anapunja mutu wa hali ya chini anatukana Mutengenezaji wake,+

Lakini mutu yeyote mwenye anasikilia maskini huruma anamutukuza Mungu.+

32 Uovu wa muovu utamushusha chini,

Lakini mwenye haki atapata kimbilio katika uaminifu-mushikamanifu wake.+

33 Hekima inakaa kimya katika moyo wa mutu mwenye uelewaji,+

Lakini inapaswa kujijulisha kati ya wajinga.

34 Haki inainua taifa,+

Lakini zambi ni haya kwa taifa.

35 Mufalme anafurahia mutumishi mwenye anatenda kwa ufahamu,+

Lakini kasirani yake inawaka juu ya ule mwenye kutenda kwa haya.+

15 Jibu la upole* linatuliza kasirani kali,+

Lakini neno la ukali* linachochea hasira.+

 2 Ulimi wa mwenye hekima unatumia muzuri ujuzi,+

Lakini kinywa cha mujinga kinasema-sema upumbavu.

 3 Macho ya Yehova yako kila mahali,

Yakiangalia wabaya na wema.+

 4 Ulimi mutulivu* ni muti wa uzima,+

Lakini maneno yenye kupotoka yanakatisha tumaini.*

 5 Mupumbavu anazarau nizamu ya baba yake,+

Lakini mutu mwerevu anakubali kurekebishwa.*+

 6 Katika nyumba ya mwenye haki muko hazina nyingi,

Lakini mazao* ya muovu yanamuletea taabu.+

 7 Midomo ya wenye hekima inaeneza ujuzi,+

Lakini moyo wa mujinga haufanye vile.+

 8 Zabihu ya waovu ni chukizo kwa Yehova,+

Lakini sala ya watu wanyoofu inamufurahisha Yeye.+

 9 Yehova anachukia njia ya muovu,+

Lakini anapenda mutu mwenye kufuatilia haki.+

10 Nizamu inaonekana kuwa mubaya* kwa mutu mwenye anaacha njia,+

Lakini mutu yeyote mwenye anachukia karipio atakufa.+

11 Kaburi* na mahali pa uharibifu* viko wazi kabisa mbele ya macho ya Yehova.+

Namna gani mioyo ya wanadamu!+

12 Mutu mwenye kuchekelea wengine hapendi mutu mwenye anamurekebisha.*+

Hatatafuta shauri kwa wenye hekima.+

13 Moyo wenye furaha unafanya sura ichangamuke,

Lakini maumivu ya moyo yanaponda roho.+

14 Moyo wenye uelewaji unatafuta ujuzi,+

Lakini kinywa cha wajinga kinakula* upumbavu.+

15 Siku zote za mutu mwenye kuteseka ziko mubaya,+

Lakini mutu mwenye moyo wa furaha* iko* na karamu sikuzote.+

16 Ni muzuri zaidi kuwa na vitu kidogo na unamuogopa Yehova+

Kuliko kuwa na mali nyingi pamoja na mahangaiko.*+

17 Ni muzuri zaidi kula mboga za majani mahali kwenye kuko upendo+

Kuliko kula ngombe-dume mwenye kunenepa* mahali kwenye kuko chuki.+

18 Mutu mwenye kukasirika-kasirika anachochea muzozo,+

Lakini mutu mwenye hakasirike haraka anatuliza ugomvi.+

19 Njia ya muvivu ni kama lupango ya miiba,+

Lakini njia ya watu wanyoofu ni kama barabara kubwa yenye kusawazika.+

20 Mwana mwenye hekima anamufurahisha baba yake,+

Lakini mutu mujinga anamuzarau mama yake.+

21 Mutu mwenye hana akili ya muzuri* anafurahia upumbavu,+

Lakini mutu mwenye utambuzi anaenda mbele bila kugeuka.+

22 Mipango inashindikana wakati hakuna mazungumuzo,*

Lakini mambo yanatimizwa kupitia washauri wengi.+

23 Mutu anafurahi sana wakati anatoa jibu lenye kufaa,*+

Na neno lenye kusemwa wakati wenye kufaa⁠—​ni la muzuri sana!+

24 Kwa mwenye ufahamu njia ya uzima inapeleka juu,+

Ili kumuepusha na Kaburi* lenye kuwa chini.+

25 Yehova atabomoa nyumba ya wenye majivuno,+

Lakini atalinda mupaka wa mujane.+

26 Yehova anachukia sana mipango ya mubaya ya mutu muovu,+

Lakini maneno yenye kupendeza ni safi Kwake.+

27 Mutu mwenye anapata faida yenye haiko ya haki analetea taabu* watu wa nyumba yake mwenyewe,+

Lakini mwenye anachukia rushwa* ataendelea kuishi.+

28 Moyo wa mwenye haki unafikiri sana mbele ya kujibu,*+

Lakini kinywa cha waovu kinasema-sema mambo ya mubaya.

29 Yehova iko* mbali sana na waovu,

Lakini anasikia sala ya wenye haki.+

30 Macho yenye kungaa* yanafurahisha moyo;

Habari ya muzuri inatia nguvu mifupa.*+

31 Mutu mwenye anasikiliza karipio lenye kutoa uzima

Anatulia kati ya wenye hekima.+

32 Mutu yeyote mwenye anakataa nizamu anazarau uzima wake,*+

Lakini kila mutu mwenye anasikiliza karipio anapata uelewaji.*+

33 Kumuogopa Yehova ni mazoezi ya kupata hekima,+

Na mbele ya utukufu kuko unyenyekevu.+

16 Mutu anatayarisha mawazo ya moyo wake,*

Lakini jibu lenye anatoa* linatoka kwa Yehova.+

 2 Njia zote za mwanadamu zinaonekana kuwa sawa* mbele ya macho yake,+

Lakini Yehova anachunguza nia.*+

 3 Tia kila jambo lenye unafanya katika mukono wa Yehova,*+

Na mipango yako itafanikiwa.

 4 Yehova amefanya kila kitu kitimize kusudi lake,

Hata waovu kwa ajili ya siku ya musiba.+

 5 Kila mutu mwenye kiburi katika moyo ni chukizo kwa Yehova.+

Ukuwe hakika kwamba* hatakosa kupewa azabu.

 6 Kwa upendo mushikamanifu na uaminifu, kosa linafunikwa,+

Na kwa kumuogopa Yehova mutu anajiepusha na ubaya.+

 7 Wakati Yehova anafurahia njia za mutu,

Anafanya hata maadui wake waishi kwa amani pamoja naye.+

 8 Ni muzuri zaidi kuwa na kidogo pamoja na uadilifu*+

Kuliko kuwa na mapato mengi pasipo haki.+

 9 Mutu anaweza kupanga njia yake katika moyo wake,

Lakini Yehova ndiye anaongoza hatua zake.+

10 Uamuzi wenye kuongozwa na roho* unapaswa kuwa kwenye midomo ya mufalme;+

Hapaswe hata kidogo kusaliti haki.+

11 Mizani* na vipimo vyenye kuwa sawa vinatoka kwa Yehova;

Majiwe yote ya kupimia yenye kuwa katika mufuko ni kazi yake.+

12 Matendo maovu yanachukiza wafalme,+

Kwa maana kiti cha ufalme kinafanywa kuwa imara kabisa kupitia haki.+

13 Maneno ya haki yanafurahisha wafalme.

Wanapenda mutu mwenye anasema kweli.+

14 Kasirani kali ya mufalme ni kama mujumbe wa kifo,+

Lakini mutu mwenye hekima anaituliza.*+

15 Katika mwangaza wa uso wa mufalme kuko uzima;

Kukubaliwa naye ni kama wingu la mvua wakati wa kipindi cha mvua ya mwisho.+

16 Ni muzuri sana kupata hekima kuliko zahabu!+

Inafaa kuchagua uelewaji kuliko kuchagua feza.+

17 Barabara kubwa ya watu wanyoofu inaepuka mambo ya mubaya.

Kila mutu mwenye analinda njia yake analinda uzima wake.*+

18 Kiburi kinatangulia kuanguka,

Na roho yenye majivuno inatangulia kujikwaa.+

19 Ni muzuri zaidi kuwa munyenyekevu* kati ya wapole+

Kuliko kupata sehemu ya vitu vyenye watu wenye majivuno walichukua katika vita.

20 Mutu mwenye anaonyesha ufahamu katika jambo atapata mafanikio,*

Na mwenye furaha ni ule mwenye anamutegemea Yehova.

21 Mutu mwenye hekima katika moyo ataitwa mutu mwenye uelewaji,+

Na mutu mwenye kuongea kwa upole anaongeza* usadikisho.+

22 Ufahamu ni chemchemi ya uzima kwa wenye kuwa nao,

Lakini wapumbavu wanapewa nizamu kwa upumbavu wao wenyewe.

23 Moyo wa mwenye hekima unapatia kinywa chake ufahamu+

Na unaongeza ushawishi kwenye maneno yake.

24 Maneno yenye kupendeza ni sega la asali,

Ni matamu kwa nafsi* na yanaponyesha mifupa.+

25 Kuko njia yenye inaonekana kuwa sawa mbele ya macho ya mutu,

Lakini mwishowe inaongoza kwenye kifo.+

26 Hamu ya kula* ya mufanyakazi inamufanya atumike kazi kwa bidii

Kwa sababu njaa yake inamuchochea* aendelee kufanya kazi.+

27 Mutu mwenye hana mafaa yoyote anachimbua mambo ya mubaya;+

Na maneno yake ni kama moto wenye kuunguza.+

28 Mufanya-fujo* anatokeza mugawanyiko,+

Na muchongezi anatenganisha marafiki wa karibu.+

29 Mutu mwenye jeuri anashawishi jirani yake

Na kumuongoza katika njia ya mubaya.

30 Anafinya jicho lake wakati anafanya mipango yenye kuumiza.

Anakaza midomo yake pamoja wakati anafanya jambo lenye kuumiza.

31 Imvi ni taji la uzuri*+

Wakati zinapatikana katika njia ya haki.+

32 Mutu mwenye hakasirike haraka+ ni muzuri zaidi kuliko mwanaume mwenye nguvu,

Na mutu mwenye kuzuia kasirani yake* ni muzuri zaidi kuliko mutu mwenye anashinda muji.+

33 Kura inapigwa katika sehemu ya nguo yenye kufunika mapaja,+

Lakini kila uamuzi wenye unafanywa kwa kura hiyo unatoka kwa Yehova.+

17 Afazali kipande chenye kukauka cha mukate mahali kwenye kuko amani*+

Kuliko nyumba yenye kujaa karamu* pamoja na ugomvi.+

 2 Mutumishi mwenye ufahamu atatawala juu ya mwana mwenye anatenda kwa haya;

Atapokea uriti kama mumoja wa ndugu za mwana huyo.

 3 Chungu cha kusafishia ni kwa ajili ya feza na tanuru ni kwa ajili ya zahabu,+

Lakini Yehova ndiye anachunguza mioyo.+

 4 Mutu muovu anasikiliza maneno yenye kuumiza,

Na mutu mudanganyifu anasikiliza ulimi wenye uovu.+

 5 Mutu yeyote mwenye kuchekelea maskini anatukana Mutengenezaji wake,+

Na kila mutu mwenye anafurahia musiba wa mwingine hatakosa kupewa azabu.+

 6 Wajukuu ni taji kwa wenye wamezeeka,

Na baba* ni utukufu wa wana* wao.

 7 Maneno manyoofu* hayamufae mupumbavu.+

Namna gani maneno ya uongo kwa mutawala!*+

 8 Zawadi ni kama jiwe lenye samani kwa mwenye kuwa nayo;*+

Kila mahali kwenye anageukia, linamuletea mafanikio.+

 9 Kila mutu mwenye anasamehe* kosa anatafuta upendo,+

Lakini ule mwenye anaendelea kuongea juu ya jambo anatenganisha marafiki wa karibu.+

10 Kemeo linamugusa moyo zaidi mutu mwenye uelewaji+

Kuliko kumupiga mujinga mara mia moja (100).+

11 Mutu mubaya anatafuta uasi tu,

Lakini mujumbe mwenye hana huruma atatumwa ili kumupatia azabu.+

12 Ni muzuri zaidi kukutana na dubu mwenye amepoteza vitoto vyake

Kuliko kukutana na mujinga katika upumbavu wake.+

13 Kama mutu analipa ubaya kwa wema,

Ubaya hautaondoka katika nyumba yake.+

14 Kuanzisha vita ni kama kufungua mulango mukubwa wa mafuriko;*

Mbele ugomvi uanze, ondoka.+

15 Mutu yeyote mwenye kumuhesabia muovu kuwa hana kosa na mutu yeyote mwenye kumuhukumu mwenye haki kuwa na kosa+

⁠—​Wote wawili ni chukizo kwa Yehova.

16 Kuko faida gani kwa mujinga kuwa na uwezo wa kupata hekima

Wakati hana moyo wa kuipata?*+

17 Rafiki wa kweli anapenda nyakati zote+

Naye ni ndugu mwenye amezaliwa kwa ajili ya nyakati za taabu.+

18 Mutu mwenye hana akili ya muzuri* anapana mukono na kukubali

Kulipia mwingine mukopo mbele ya jirani yake.+

19 Mutu mwenye anapenda ugomvi anapenda kosa.+

Kila mutu mwenye anainua mahali pake pa kuingilia anaalika taabu.+

20 Mutu mwenye kupotoka katika moyo hatapata mafanikio,*+

Na ule mwenye kusema maneno ya udanganyifu ataanguka katika uharibifu.

21 Baba mwenye anazaa mutoto mwenye hana akili atakuwa na huzuni;

Na baba ya mutoto mwenye hana akili hana furaha.+

22 Moyo wenye furaha ni dawa ya muzuri,*+

Lakini roho yenye kupondwa inamaliza mutu nguvu.*+

23 Mutu muovu atakamata rushwa* kwa uficho*

Ili apotoshe njia ya haki.+

24 Hekima iko kabisa mbele ya mutu mwenye utambuzi,

Lakini macho ya mujinga yanaenda huku na huku mupaka kwenye miisho ya dunia.+

25 Mwana mujinga analetea baba yake huzuni

Na kuletea ule mwenye alimuzaa maumivu ya moyo.*+

26 Haiko muzuri kumupatia mwenye haki azabu,*

Na kupiga viboko watu wenye kuheshimiwa ni kinyume na mambo yenye kuwa sawa.

27 Mutu mwenye ujuzi anazuia maneno yake,+

Na mutu mwenye utambuzi atabakia mutulivu.*+

28 Hata mupumbavu mwenye anabakia kimya ataonwa kuwa mwenye hekima,

Na ule mwenye anafunga midomo yake, ataonwa kuwa mwenye utambuzi.

18 Kila mutu mwenye anajitenga na wengine anafuatilia tamaa zake mwenyewe za uchoyo;

Anakataa* hekima yote yenye kutumika.

 2 Mutu mujinga hafurahie uelewaji;

Lakini anafurahia kufunua mambo yenye kuwa katika moyo wake.+

 3 Wakati mutu muovu anakuja, zarau inakuja pia,

Na kukosa heshima kunakuja pamoja na haya.+

 4 Maneno ya kinywa cha mutu ni maji yenye kuenda chini sana.+

Chemchemi ya hekima ni muto mudogo wenye kububujika.

 5 Haiko muzuri kuonyesha muovu upendeleo+

Wala kuima muadilifu haki.+

 6 Maneno ya mujinga yanatokeza mabishano,+

Na kinywa chake kinafanya apigwe.+

 7 Kinywa cha mujinga ndicho kinamuharibu,+

Na midomo yake ni mutego kwa uzima wake.*

 8 Maneno ya muchongezi ni kama matonge matamu;*+

Yanamezwa na kushuka mara moja katika tumbo.+

 9 Kila mutu mwenye kuwa muvivu katika kazi yake

Ni ndugu ya mutu mwenye kuleta uharibifu.+

10 Jina la Yehova ni munara wenye nguvu.+

Mwenye haki anakimbilia ndani na kupata ulinzi.*+

11 Mali ya tajiri ni muji wake wenye ngome;

Ni kama ukuta wa ulinzi katika mawazo yake.+

12 Mbele ya kuanguka kwa kishindo moyo wa mutu ni wenye kiburi,+

Na mbele ya utukufu kuko unyenyekevu.+

13 Wakati mutu anajibu mbele ya kusikia ukweli wa mambo,

Huo ni upumbavu na haya.+

14 Roho ya mutu inaweza kumutegemeza katika ugonjwa,+

Lakini ni nani anaweza kuvumilia roho yenye kupondwa?*+

15 Moyo wa mutu mwenye uelewaji unapata ujuzi,+

Na sikio la mwenye hekima linatafuta kupata ujuzi.

16 Zawadi ya mwanadamu inamufungulia njia;+

Inamuwezesha kufika mbele ya wakubwa.

17 Mutu wa kwanza kueleza kesi yake ya hukumu anaonekana kuwa anasema kweli,+

Mupaka wakati mwingine anafika na kumuuliza maulizo.*+

18 Kupiga kura kunakomesha mabishano+

Na kunakata maneno kati ya* wapinzani wenye nguvu.

19 Ndugu mwenye wamekosea ni mugumu kuliko muji wenye ngome,+

Na kuko mabishano yenye kuwa kama mapingo* ya ngome.+

20 Tumbo la mutu litajazwa kutokana na matunda ya maneno yake;*+

Atashiba mazao ya midomo yake.

21 Kifo na uzima viko katika nguvu za ulimi;+

Wale wenye wanapenda kuutumia watakula matunda yake.+

22 Mwenye anapata bibi muzuri anapata kitu kizuri,+

Na anapata wema wa* Yehova.+

23 Maskini anabembeleza wakati anaongea,

Lakini tajiri anajibu kwa ukali.

24 Kuko marafiki wenye kuwa tayari kuumizana,+

Lakini kuko rafiki mwenye anashikamana sana na mutu kuliko ndugu.+

19 Ni muzuri zaidi kuwa maskini na kutembea katika uaminifu-mushikamanifu+

Kuliko kuwa mujinga na kusema uongo.+

 2 Mutu mwenye hana ujuzi haiko mutu muzuri,*+

Na mutu mwenye kutenda bila kufikiri* anatenda zambi.

 3 Upumbavu wa mutu ndio unapotosha njia yake,

Na moyo wake unamukasirikia sana Yehova.

 4 Mali inavuta marafiki wengi,

Lakini hata rafiki ya maskini atamuacha.+

 5 Shahidi wa uongo hatakosa kupewa azabu,+

Na ule mwenye anasema uongo kila wakati anapumua hataponyoka.+

 6 Wengi wanatafuta kukubaliwa na mutu mwenye cheo,*

Na kila mutu ni rafiki ya mutu mwenye kutoa zawadi.

 7 Ndugu wote wa mutu maskini wanamuchukia;+

Marafiki wake wanamuepuka hata zaidi!+

Anawafuatilia ili awaombe mambo fulani, lakini hakuna mwenye anamusikiliza.

 8 Kila mutu mwenye anapata akili ya muzuri* anajipenda mwenyewe.*+

Kila mutu mwenye anapendezwa sana na utambuzi atapata mafanikio.*+

 9 Shahidi wa uongo hatakosa kupewa azabu,

Na ule mwenye anasema uongo kila wakati anapumua ataangamia.+

10 Mupumbavu hastahili kuishi maisha ya raha;

Namna gani mutumishi kutawala wakubwa!+

11 Ufahamu wa mutu hakika unatuliza kasirani yake,+

Na ni uzuri kwake kuachilia* kosa.+

12 Kasirani kali ya mufalme ni kama mungurumo wa simba,*+

Lakini kukubaliwa naye ni kama umande juu ya majani.

13 Mwana mujinga anamuletea baba yake shida,+

Na bibi mugomvi* ni kama sehemu ya juu ya nyumba yenye haiache kuvuya hata kidogo.+

14 Nyumba na mali vinaritiwa kutoka kwa baba,

Lakini bibi mwenye busara anatoka kwa Yehova.+

15 Uvivu unaleta usingizi muzito,

Na mutu muregevu atakuwa na njaa.+

16 Mwenye anashika amri analinda uzima wake;*+

Mwenye hahangaikie njia zake atakufa.+

17 Mwenye anaonyesha mutu wa hali ya chini wema anamukopesha Yehova,+

Na Yeye atamulipa* kwa sababu ya mambo yenye anatenda.+

18 Patia mwana wako nizamu wakati kungali tumaini,+

Na usimufanye* akufe.+

19 Mutu mwenye kukasirika-kasirika atalipia kosa lake;

Ukijaribu kumuokoa, utalazimika kufanya vile tena na tena.+

20 Sikiliza shauri na ukubali nizamu,+

Ili ukuwe na hekima katika wakati wako wenye kuja.+

21 Moyo wa mwanadamu uko na mipango mingi,

Lakini shauri* la Yehova ndilo litadumu.+

22 Kitu chenye kutamanika ndani ya mutu ni upendo wake mushikamanifu;+

Na ni muzuri zaidi kuwa maskini kuliko kuwa muongo.

23 Kumuogopa Yehova kunaongoza kwenye uzima;+

Ule mwenye kuwa na woga huo atapumuzika muzuri, hatapatwa na mambo yenye kuumiza.+

24 Muvivu anazika mukono wake katika bakuli la karamu,

Lakini hajikaze hata kuurudisha katika kinywa chake.+

25 Piga mwenye zihaka,+ ili mwenye hana uzoefu akuwe mwerevu,+

Karipia mwenye uelewaji, ili aongeze ujuzi wake.+

26 Mwenye anatendea baba yake mubaya na kufukuza mama yake

Ni mwana mwenye kuleta haya na aibu.+

27 Mwana wangu, ukiacha kusikiliza nizamu,

Utakengeuka na kuacha maneno ya ujuzi.

28 Shahidi mwenye hana mafaa yoyote anachekelea haki,+

Na kinywa cha waovu kinameza-meza uovu.+

29 Hukumu inangojea wenye zihaka,+

Na mugongo wa wajinga unangojea kupigwa.+

20 Divai ni muzihaki,+ pombe inamufanya mutu kuwa kichwa-nguvu;+

Kila mutu mwenye anapotoshwa navyo hana hekima.+

 2 Kuogopesha sana kwa mufalme ni kama mungurumo wa simba;*+

Kila mutu mwenye anaamusha kasirani yake anatia uzima wake mwenyewe katika hatari.+

 3 Ni heshima kwa mutu kujiepusha na mabishano,+

Lakini kila mupumbavu atajiingiza ndani.+

 4 Muvivu halime wakati wa kipindi cha baridi,

Kwa hiyo atakuwa anaomba-omba katika kipindi cha mavuno wakati hatakuwa na kitu.*+

 5 Mawazo* ya moyo wa mutu ni kama maji yenye kuenda chini sana,

Lakini mutu mwenye utambuzi anayashota.

 6 Watu wengi wanatangaza upendo wao mushikamanifu,

Lakini ni nani anaweza kupata mutu muaminifu?

 7 Mwenye haki anatembea katika uaminifu-mushikamanifu wake.+

Watoto* wake wenye kuja kisha yeye watakuwa na furaha.+

 8 Wakati mufalme anakaa kwenye kiti cha ufalme ili kuhukumu,+

Anayungulula uovu wote kwa macho yake.+

 9 Ni nani anaweza kusema: “Nimesafisha moyo wangu;+

Niko safi kutokana na zambi yangu”?+

10 Vipimo vya udanganyifu na mizani* za uongo*

⁠—​Vyote viwili ni chukizo kwa Yehova.+

11 Hata mutoto* anajulikana kwa matendo yake,

Kama tabia yake ni safi na yenye kufaa.+

12 Sikio lenye linasikia na jicho lenye linaona

⁠—​Yehova ameumba vyote viwili.+

13 Usipende usingizi, ukiupenda utakuwa maskini.+

Fungua macho yako, na utashiba mukate.+

14 “Haiko kizuri, haiko kizuri!” ni vile mwenye kununua anasema;

Kisha anaenda zake na kujisifu.+

15 Kuko zahabu, kuko pia marijani* kwa wingi,

Lakini midomo ya ujuzi ni kitu chenye samani.+

16 Kamata nguo ya mutu ikiwa ameahidi kulipia mugeni mukopo;+

Umunyanganye kitu chenye aliwekesha kwa ajili ya mukopo ikiwa alifanya vile kwa ajili ya mwanamuke mugeni.*+

17 Mukate wenye ulipatikana kwa udanganyifu ni mutamu kwa mutu,

Lakini kisha, kinywa chake kitajaa majiwe ya kidogo-kidogo.+

18 Mipango itafanikiwa* wakati kuko kupatiana mawazo,*+

Na upigane vita yako kwa ufundi wa kuongoza.*+

19 Muchongezi anaenda huku na huku akifunua mazungumuzo ya siri;+

Usishirikiane na mutu mwenye anapenda kupiga porojo.*

20 Kila mutu mwenye analaani baba yake na mama yake,

Taa yake itazimwa wakati giza litaingia.+

21 Uriti wenye unapatikana kwanza kwa pupa

Mwishowe hautakuwa baraka.+

22 Usiseme: “Nitalipiza uovu!”+

Tumainia Yehova,+ naye atakuokoa.+

23 Vipimo vya udanganyifu* ni chukizo kwa Yehova,

Na mizani* za uongo haziko muzuri.

24 Hatua za mutu zinaongozwa na Yehova;+

Namna gani mwanadamu anaweza kuelewa njia yake mwenyewe?*

25 Ni mutego kwa mutu kutangaza haraka-haraka, “Ni kitakatifu!”+

Na kisha tu wakati fulani anachunguza kile aliwekea naziri.+

26 Mufalme mwenye hekima anayungulula waovu+

Na kupitisha gurudumu* la kupiga-piga nafaka juu yao.+

27 Pumuzi ya mutu ni taa ya Yehova,

Inachunguza kabisa utu wake wa ndani sana.

28 Upendo mushikamanifu na uaminifu vinamulinda mufalme;+

Kwa upendo mushikamanifu anafanya kiti chake cha ufalme kikuwe imara.+

29 Utukufu wa vijana ni nguvu zao,+

Na uzuri wa wazee ni imvi zao.+

30 Michubuko na vidonda vinaondoa kabisa* uovu,+

Na mapigo yanasafisha utu wa ndani sana wa mutu.

21 Moyo wa mufalme ni kama mito midogo ya maji katika mukono wa Yehova.+

Anauongoza mahali popote kwenye anapenda.+

 2 Njia zote za mwanadamu zinaonekana kuwa sawa mbele ya macho yake,+

Lakini Yehova anachunguza mioyo.*+

 3 Kufanya mambo yenye kuwa sawa na ya haki

Kunamupendeza Yehova zaidi kuliko zabihu.+

 4 Macho yenye kiburi na moyo wenye majivuno

⁠—​Taa yenye inaongoza waovu ni zambi.+

 5 Mipango ya wenye bidii hakika inaleta mafanikio,*+

Lakini wale wote wenye kutenda haraka-haraka hakika watakuwa maskini.+

 6 Kupata hazina kupitia ulimi wenye kusema uongo

Ni kama kunguku yenye kuisha, mutego wenye kuleta kifo.*+

 7 Jeuri ya waovu itawaharibu,+

Kwa maana wanakataa kutenda haki.

 8 Njia ya mutu mwenye hatia ni yenye kujikunja-kunja,

Lakini matendo ya mutu safi ni yenye kunyooka.+

 9 Ni muzuri zaidi kuishi kwenye pembe ya sehemu ya juu ya nyumba

Kuliko kuishi katika nyumba moja na bibi mugomvi.*+

10 Mutu muovu anatamani mambo ya mubaya;+

Hamuonyeshe jirani yake wema.+

11 Wakati mwenye zihaka anapewa azabu, mwenye hana uzoefu anakuwa na hekima zaidi,

Na wakati mutu mwenye hekima anapata ufahamu, anapata ujuzi.*+

12 Mwenye Haki anachunguza nyumba ya muovu;

Anapindua waovu na kuwaharibu.+

13 Kila mutu mwenye anafunga sikio lake ili asisikie kilio cha mutu wa hali ya chini

Yeye mwenyewe ataita naye hatajibiwa.+

14 Zawadi yenye kutolewa kwa uficho inatuliza hasira,+

Na rushwa* yenye kufichwa* inatuliza kasirani kali.

15 Mwenye haki anafurahia kutenda kwa haki,+

Lakini ni jambo la mubaya sana kwa wale wenye kutenda uovu.

16 Mutu mwenye anakengeuka na kuacha njia ya ufahamu

Atapumuzika katika kikundi cha wale wenye hawana uwezo katika kifo.+

17 Mwenye anapenda kujifurahisha* atakuwa maskini;+

Mwenye anapenda divai na mafuta hatakuwa tajiri.

18 Muovu ni bei ya ukombozi kwa ajili ya mwenye haki,

Na mudanganyifu atakamatwa pa nafasi ya watu wanyoofu.+

19 Ni muzuri zaidi kuishi katika jangwa

Kuliko kuishi na bibi mugomvi* na mwenye kukasirika-kasirika.+

20 Hazina yenye samani na mafuta vinapatikana katika nyumba ya mwenye hekima,+

Lakini mutu mujinga atatumia mubaya* vitu vyenye iko* navyo.+

21 Kila mutu mwenye anafuatilia haki na upendo mushikamanifu

Atapata uzima, haki, na utukufu.+

22 Mutu mwenye hekima anaweza kupanda katika* muji wa watu wenye nguvu

Na kupunguza nguvu zenye wanategemea.+

23 Mwenye analinda kinywa chake na ulimi wake

Anajiepusha* na taabu.+

24 Mutu mwenye kimbelembele, mwenye kujisifu-sifu, ni vile unamuita

Mutu mwenye kutenda kwa kimbelembele bila kujali.+

25 Kile mutu muvivu anatamani sana kitamuua,

Kwa maana mikono yake inakataa kufanya kazi.+

26 Anatamani sana kwa pupa muchana wote,

Lakini mwenye haki anatoa, haime wengine kitu.+

27 Zabihu ya muovu inachukiza.+

Namna gani wakati anaitoa na nia yenye uovu!*

28 Shahidi mwenye kusema uongo ataangamia,+

Lakini mutu mwenye anasikiliza atatoa ushuhuda kwa mafanikio.*

29 Mutu muovu anavaa uso wenye hauna haya,+

Lakini njia ya mutu munyoofu ni hakika.*+

30 Hakuna hekima, wala utambuzi wowote, wala shauri katika kumupinga Yehova.+

31 Farasi anatayarishwa kwa ajili ya siku ya vita,+

Lakini wokovu ni wa Yehova.+

22 Inafaa kuchagua jina la muzuri* kuliko kuchagua mali nyingi;+

Kuheshimiwa* ni muzuri kuliko feza na zahabu.

 2 Matajiri na maskini wanafanana katika jambo hili:*

Yehova aliwaumba wote.+

 3 Mutu mwerevu anaona hatari na kujificha,

Lakini wenye hawana uzoefu wanaendelea mbele na kupata matokeo ya mubaya.*

 4 Matokeo ya unyenyekevu na kumuogopa Yehova

Ni utajiri na utukufu na uzima.+

 5 Miiba na mitego iko kwenye njia ya mutu mwenye kupotoka,

Lakini kila mutu mwenye anaona uzima wake kuwa wa* maana anakaa mbali nayo.+

 6 Zoeza mutoto mwanaume* katika njia yenye anapaswa kufuata;+

Hata wakati atazeeka hataiacha.+

 7 Tajiri anatawala maskini,

Na mukopaji ni mutumwa wa mukopeshaji.+

 8 Kila mutu mwenye anapanda ukosefu wa haki atavuna musiba,+

Na fimbo ya kasirani yake kali itafikia mwisho wake.+

 9 Mutu mukarimu* atabarikiwa,

Kwa maana anagawana chakula chake pamoja na maskini.+

10 Fukuza mutu mwenye zarau,

Na ugomvi utaisha;

Mabishano* na matusi yataisha.

11 Mutu mwenye anapenda moyo safi na mwenye anasema maneno yenye kupendeza

Atakuwa rafiki ya mufalme.+

12 Macho ya Yehova yanalinda ujuzi,

Lakini Yeye anapindua maneno ya wadanganyifu.+

13 Muvivu anasema: “Simba iko* inje!

Nitauawa katikati ya kiwanja cha watu wote!”+

14 Kinywa cha wanamuke wenye kupotoka* ni shimo la murefu.+

Mwenye anahukumiwa na Yehova ataangukia ndani yake.

15 Upumbavu umefungwa katika moyo wa mutoto mwanaume,*+

Lakini fimbo ya nizamu itauondolea mbali naye.+

16 Mwenye anamupunja maskini ili aongeze mali yake+

Na ule mwenye anapatia matajiri zawadi

Mwishowe watakuwa maskini.

17 Tega sikio lako na usikilize maneno ya wenye hekima,+

Ili ufanye moyo wako uzame katika ujuzi wangu,+

18 Kwa maana inapendeza kuchunga maneno hayo ndani yako kabisa,+

Ili yote yakuwe kwenye midomo yako kila wakati.+

19 Ili umutumainie Yehova,

Ninakupatia ujuzi leo.

20 Je, tayari sijakuandikia,

Ili kukupatia mashauri na ujuzi,

21 Ili nikufundishe maneno ya kweli yenye kutegemeka,

Kusudi uweze kumupelekea habari ya kweli ule mwenye alikutuma?

22 Usinyanganye vitu vya mutu maskini kwa sababu yeye ni maskini,+

Wala usiponde mutu wa hali ya chini katika mulango mukubwa wa muji,+

23 Kwa maana Yehova mwenyewe atatetea mashitaka yao+

Na ataondoa uzima wa* wale wenye kuwapunja.

24 Usishirikiane na mutu mwenye kukasirika-kasirika

Wala kujiunga na mutu mwenye muelekeo wa kukasirika sana,

25 Ili usijifunze hata kidogo njia zake

Na kujitia katika mutego.+

26 Usikuwe kati ya wale wenye kupana mikono wakati wanaahidi kulipia wengine mukopo,

Wenye wanaahidi kulipa mikopo.+

27 Kama hauna kitu cha kulipa,

Kitanda chako kitapelekwa moja kwa moja inje kutoka chini yako!

28 Usihamishe alama ya zamani ya mupaka

Yenye iliwekwa na mababu zako.+

29 Je, umemuona mutu mwenye ufundi katika kazi yake?

Atasimama mbele ya wafalme;+

Hatasimama mbele ya watu wa kawaida.

23 Wakati unakaa ili kula pamoja na mufalme,

Chunguza kwa uangalifu kile chenye kuwa mbele yako;

 2 Tia kisu kwenye koo lako*

Kama uko na hamu kubwa ya kula.*

 3 Usitamani vyakula vyake vitamu,

Kwa maana ni vyakula vya udanganyifu.

 4 Usijichokeshe ili kupata utajiri.+

Acha na uonyeshe uelewaji.*

 5 Wakati unautupia jicho, hauko pale,+

Kwa maana hakika utaota mabawa kama tai na kuruka mbali katika anga.+

 6 Usikule chakula cha mutu muchoyo;*

Usitamani vyakula vyake vitamu,

 7 Kwa maana yeye ni kama mutu mwenye kuweka hesabu.*

Anakuambia: “Kula na ukunywe,” lakini haiko vile anamaanisha.*

 8 Utatapika matonge yenye ulikula

Na utakuwa umepoteza maneno yako ya kumusifu.

 9 Usiongee katika masikio ya mujinga,+

Kwa maana atazarau hekima ya maneno yako.+

10 Usihamishe alama ya zamani ya mupaka+

Wala kuingia katika shamba la wenye hawana baba.

11 Kwa maana Muteteaji* wao iko* na nguvu;

Atawatetea juu yako.+

12 Fanya moyo wako uzame katika nizamu

Na sikio lako katika maneno ya ujuzi.

13 Usiime mutoto mwanaume* nizamu.+

Kama unamupiga kwa fimbo, hatakufa.

14 Unapaswa kumupiga kwa fimbo,

Ili umuokoe asiingie* katika Kaburi.*

15 Mwana wangu, kama moyo wako unakuwa na hekima,

Basi moyo wangu mwenyewe utafurahi sana.+

16 Utu wangu wa ndani sana utafurahi*

Wakati midomo yako itasema mambo yenye kuwa sawa.

17 Moyo wako usisikilie wivu watenda-zambi,+

Lakini umuogope Yehova muchana wote,+

18 Kwa maana ukifanya vile utakuwa na wakati muzuri wenye kuja+

Na tumaini lako halitaondolewa.

19 Mwana wangu, sikiliza na ukuwe na hekima,

Na uelekeze moyo wako katika njia yenye kufaa.

20 Usikuwe kati ya wale wenye kunywa divai nyingi sana,+

Kati ya wale wenye kula nyama nyingi sana,+

21 Kwa maana mulevi na mulafi watakuwa maskini,+

Na kusinzia kutavalisha mutu nguo zenye kupasuka-pasuka.

22 Sikiliza baba yako mwenye alikuzaa,

Na usizarau mama yako kwa sababu tu amezeeka.+

23 Ununue* kweli na usiiuzishe hata kidogo,+

Pia hekima na nizamu na uelewaji.+

24 Baba ya mwenye haki hakika atakuwa na furaha;

Kila baba mwenye anazaa mwana mwenye hekima atamufurahia sana.

25 Baba yako na mama yako watafurahi sana,

Na mama mwenye alikuzaa atakuwa na shangwe.

26 Mwana wangu, unipatie moyo wako,

Na macho yako yafurahie njia zangu.+

27 Kwa maana kahaba ni shimo la murefu,

Na mwanamuke mwasherati* ni kisima chembamba.+

28 Anavizia kama munyanganyi;+

Anaongeza hesabu ya wanaume wenye hawako waaminifu.

29 Ni nani mwenye ole? Ni nani mwenye wasiwasi?

Ni nani mwenye ugomvi? Ni nani mwenye malalamiko?

Ni nani mwenye vidonda bila sababu? Ni nani mwenye macho mekundu?*

30 Ni wale wenye kupitisha wakati mwingi kwenye divai;+

Wale wenye kutafuta* divai yenye kuchanganywa.

31 Usiangalie rangi nyekundu ya divai

Wakati inangaa katika kikombe na kushuka kwa urahisi,

32 Kwa maana mwishowe inauma kama nyoka,

Na inatoa sumu kama nyoka-kipiri.

33 Macho yako yataona mambo ya ajabu,

Na moyo wako utasema mambo yenye kupotoka.+

34 Na utakuwa kama mutu mwenye kulala katikati ya bahari,

Kama mutu mwenye kulala kwenye sehemu ya juu ya mulingoti wa mashua.*

35 Utasema: “Wamenipiga, lakini sikusikia kitu.*

Walinipiga, lakini sikujua.

Nitaamuka wakati gani?+

Ninahitaji kinywaji kingine.”*

24 Usisikilie waovu wivu,

Na usitamani kushirikiana nao,+

 2 Kwa maana moyo wao unafikiri sana juu ya jeuri,

Na midomo yao inaongea juu ya kuleta matata.

 3 Nyumba* inajengwa kwa hekima,+

Na kwa utambuzi inafanywa kuwa salama.

 4 Kwa ujuzi vyumba vyake vinajazwa

Kila namna ya hazina za samani na zenye kupendeza.+

 5 Mutu mwenye hekima iko* na nguvu,+

Na kwa ujuzi mutu anaongeza nguvu zake.

 6 Utapigana vita yako kwa ufundi wa kuongoza,*+

Na kupitia washauri wengi kuko ushindi.*+

 7 Mupumbavu hawezi kupata hekima ya kweli;+

Hana jambo la kusema katika mulango mukubwa wa muji.

 8 Kila mutu mwenye anapanga uovu

Ataitwa fundi wa kufanya mipango ya mubaya.+

 9 Mipango ya mubaya ya upumbavu* ni zambi,

Na watu wanachukia sana mwenye zihaka.+

10 Kama unavunjika moyo siku ya taabu,*

Nguvu zako zitakuwa kidogo.

11 Okoa wale wenye kupelekwa kwenye kifo,

Na uzuie wale wenye kuyumba-yumba wakienda kuchinjwa.+

12 Kama unasema: “Lakini hatukujua jambo hili,”

Je, Mwenye kuchunguza mioyo* hatatambua hilo?+

Ndiyo, Mwenye kukuangalia* atajua

Na atalipa kila mwanadamu kulingana na matendo yake.+

13 Mwana wangu, kula asali, kwa sababu ni ya muzuri;

Asali ya sega ni tamu kuonja.

14 Vilevile, jua kwamba hekima ni ya muzuri kwako.*+

Kama unaipata, utakuwa na wakati muzuri wenye kuja

Na tumaini lako halitaondolewa.+

15 Usivizie kwa uovu karibu na makao ya mwenye haki;

Usiharibu mahali pake pa kupumuzikia.

16 Kwa maana mwenye haki anaweza kuanguka mara saba (7), na atasimama tena,+

Lakini musiba utafanya waovu wajikwae.+

17 Wakati adui yako anaanguka, usishangilie,

Na wakati anajikwaa, usiache moyo wako ufurahi;+

18 Kama unafanya vile, Yehova ataona jambo hilo na hatafurahi,

Naye ataondoa kasirani yake juu yake.*+

19 Usikasirike* kwa sababu ya waovu;

Usisikilie watu waovu wivu,

20 Kwa maana hakuna wakati muzuri wenye kuja kwa ajili ya muovu hata mumoja;+

Taa ya waovu itazimwa.+

21 Mwana wangu, ogopa Yehova na mufalme.+

Na usishirikiane na waasi,*+

22 Kwa maana musiba wao utatokea kwa kushitukia.+

Ni nani anajua ni uharibifu gani wote wawili* wataleta juu ya waasi hao?+

23 Haya pia ni maneno ya wenye hekima:

Kuonyesha upendeleo katika hukumu haiko muzuri.+

24 Mutu yeyote mwenye anamuambia muovu, “Wewe ni mwenye haki,”+

Atalaaniwa na vikundi vya watu na kulaumiwa na mataifa.

25 Lakini mambo yataendea muzuri wale wenye kumukaripia;+

Watapata baraka ya vitu vya muzuri.+

26 Watu watabusu midomo ya mutu mwenye kujibu kwa unyoofu.*+

27 Tayarisha kazi yako ya inje, na utayarishe kila kitu katika shamba;

Kisha ujenge nyumba* yako.

28 Usitoe ushuhuda juu ya jirani yako bila kuwa na sababu za kweli.+

Usitumie midomo yako ili kudanganya wengine.+

29 Usiseme: “Nitamutendea kama vile alinitendea;

Nitamulipa kwa sababu ya mambo yenye alifanya.”*+

30 Nilipita karibu na shamba la muvivu,+

Karibu na shamba la mizabibu la mutu mwenye hana akili ya muzuri.*

31 Niliona limejaa magugu;

Udongo ulikuwa umefunikwa na mimea yenye kuwasha,

Na ukuta wake wa majiwe ulikuwa umebomoka.+

32 Niliangalia hilo na kulitia katika moyo;

Nililiona na kujifunza somo hili:*

33 Kulala kidogo, kusinzia kidogo,

Kukunja mikono kidogo ili kupumuzika,

34 Na umaskini wako utakuja kama munyanganyi,

Na uhitaji wako kama mwanaume mwenye silaha.+

25 Hizi pia ni mezali za Sulemani,+ zenye watu wa Hezekia+ mufalme wa Yuda waliandika:*

 2 Ni utukufu wa Mungu kuweka jambo likiwa siri,+

Na utukufu wa wafalme ni kuchunguza jambo kwa undani.

 3 Kama vile mbingu ziko juu na kama vile dunia iko na urefu kuenda chini,

Vilevile moyo wa wafalme hauchunguzike.

 4 Ondoa takataka kwenye feza,

Nayo itatoka ikiwa imesafishwa kabisa.+

 5 Ondoa muovu mbele ya mufalme,

Na kiti chake cha ufalme kitafanywa kuwa imara kabisa katika haki.+

 6 Usijipatie heshima mbele ya mufalme,+

Na usikae kati ya watu wa maana,+

 7 Kwa maana ni muzuri zaidi yeye akuambie, “Kuja hapa juu,”

Kuliko akupatishe haya mbele ya mutu mwenye cheo.+

 8 Usipeleke haraka-haraka mashitaka kwenye tribinali,

Kwa maana utafanya nini kisha kama jirani yako anakupatisha haya?+

 9 Utetee shida yako pamoja na jirani yako,+

Lakini usifunue mambo yenye uliambiwa kwa siri,*+

10 Ili mwenye kukusikiliza asikupatishe haya

Na ili usieneze habari ya mubaya* yenye haiwezi kukusanywa tena.

11 Kama matunda ya mutofaa ya zahabu kwenye vyombo vya feza vyenye kupambwa*

Ni vile pia neno lenye kusemwa wakati wenye kufaa.+

12 Kama hereni la sikio la zahabu na pambo la zahabu safi

Ni vile pia mukaripiaji mwenye hekima kwa sikio lenye kusikia.+

13 Kama baridi ya teluji* siku ya mavuno

Ni vile pia mujumbe muaminifu kwa wale wenye walimutuma

Kwa maana mujumbe huyo anaburudisha bwana wake.*+

14 Kama mawingu na upepo wenye haulete mvua

Ni vile pia mutu mwenye anajisifu kuhusu zawadi yenye haijatolewa hata kidogo.*+

15 Kwa uvumilivu kamanda anashawishiwa,

Na ulimi laini* unaweza kuvunja mufupa.+

16 Ukipata asali, kula tu yenye unahitaji,

Kwa maana ukikula nyingi sana, unaweza kuitapika.+

17 Muguu wako usifike mara nyingi katika nyumba ya jirani yako,

Ili asikuchoke na kukuchukia.

18 Kama gongo* ya vita na upanga na mushale wenye kuwa na makali

Ni vile pia mutu mwenye anatoa ushahidi wa uongo juu ya jirani yake.+

19 Kama jino lenye kuvunjika ao muguu wenye kuyumba-yumba

Ni vile pia kutumainia mutu mwenye hategemeke* nyakati za taabu.

20 Kama mutu mwenye anatosha nguo siku ya baridi

Na kama siki* yenye kumwangwa kwenye chumvi ya asili

Ni vile pia mutu mwenye kuimbia moyo wenye huzuni nyimbo.+

21 Kama adui yako* iko* na njaa, umupatie mukate akule;

Kama iko* na kiu, umupatie maji akunywe,+

22 Kwa maana utakuwa unakusanya makaa yenye kuwaka juu ya kichwa chake,*+

Na Yehova atakupatia zawabu.

23 Upepo wa kaskazini unaleta mvua kubwa,

Na ulimi wenye kupiga porojo unaleta uso wenye kasirani.+

24 Ni muzuri zaidi kuishi kwenye pembe ya sehemu ya juu ya nyumba

Kuliko kuishi katika nyumba moja na bibi mugomvi.*+

25 Kama maji ya baridi juu ya nafsi* yenye kuchoka

Ni vile pia habari ya muzuri yenye inatoka katika inchi ya mbali.+

26 Kama chemchemi yenye matope na kisima chenye kuharibika

Ni vile pia mwenye haki ambaye anakubali kufuata* muovu.

27 Haiko muzuri kula asali nyingi sana,+

Wala haiko utukufu kujitafutia utukufu wako mwenyewe.+

28 Kama muji wenye umebomolewa, wenye hauna ukuta

Ni vile pia mutu mwenye hawezi kuzuia kasirani yake.*+

26 Kama vile teluji* wakati wa kipindi cha joto na mvua wakati wa mavuno,

Vilevile heshima haistahili mujinga.+

 2 Kama vile ndege iko* na sababu ya kukimbia na mbaruwayu sababu ya kuruka,

Vilevile laana haiwezi kuja bila sababu fulani.*

 3 Mujeledi ni kwa ajili ya farasi, lijamu* ni kwa ajili ya punda,+

Na fimbo ni kwa ajili ya mugongo wa watu wajinga.+

 4 Usijibu mujinga kulingana na upumbavu wake,

Ili usikuwe kama yeye.*

 5 Jibu mujinga kulingana na upumbavu wake,

Ili asifikiri kwamba iko* na hekima.+

 6 Kama mutu mwenye anajivunja miguu yake mwenyewe na kujiumiza mwenyewe*

Ni vile pia mutu mwenye anatia mambo katika mikono ya mujinga.

 7 Kama miguu yenye kuyumba-yumba* ya kilema,

Ni vile pia mezali katika kinywa cha watu wajinga.+

 8 Kama kufunga jiwe kwenye kombeo,

Ni vile pia kumupatia mutu mujinga utukufu.+

 9 Kama mumea wa miiba katika mukono wa mulevi,

Ni vile pia mezali katika kinywa cha watu wajinga.

10 Kama mupiga-mishale mwenye anaumiza ovyo-ovyo,*

Ni vile pia mutu mwenye anapatia mujinga ao wapita-njia kazi.

11 Kama vile imbwa anarudilia matapiko yake,

Mujinga anarudilia upumbavu wake.+

12 Je, umemuona mutu mwenye anafikiri kama iko* na hekima?+

Kuko tumaini zaidi kwa mujinga kuliko kwa mutu huyo.

13 Muvivu anasema: “Mwana-simba iko* katika barabara,

Simba iko* katika kiwanja cha watu wote!”+

14 Mulango unaendelea kuzunguka kwenye bawaba zake,*

Na muvivu kwenye kitanda chake.+

15 Muvivu anazika mukono wake katika bakuli la karamu,

Lakini amechoka sana kuurudisha katika kinywa chake.+

16 Muvivu anafikiri kwamba iko* na hekima zaidi

Kuliko watu saba (7) wenye wanajibu kwa busara.

17 Kama mutu mwenye kukamata masikio ya imbwa

Ni vile pia mupita-njia mwenye anakasirishwa* na ugomvi wenye hauko wake.+

18 Kama mwenda-wazimu mwenye anatupa silaha zenye kuwaka moto, mishale, na kifo*

19 Ni vile pia mutu mwenye anamudanganya jirani yake na kusema, “Nilikuwa ninafanya muzaha tu!”+

20 Kwenye hakuna kuni, moto unazimika,

Na kwenye hakuna muchongezi, ugomvi unaisha.+

21 Kama vile makaa yanaongezwa kwenye makaa yenye kuwaka na kuni kwenye moto

Ni vile mutu wa ugomvi anachochea ugomvi.+

22 Maneno ya muchongezi ni kama matonge matamu;*

Yanamezwa na kushuka mara moja katika tumbo.+

23 Kama feza yenye kupakwa juu ya chombo cha udongo

Ni vile pia maneno ya upendo kutoka katika* moyo muovu.+

24 Mwenye anachukia wengine anaficha chuki hiyo kwa midomo yake,

Lakini ndani anaweka udanganyifu.

25 Hata kama anasema maneno yenye kupendeza, usimuamini,

Kwa maana kuko mambo saba (7) yenye kuchukiza katika moyo wake.*

26 Hata kama chuki yake imefichwa kwa udanganyifu,

Uovu wake utafunuliwa katika kutaniko.

27 Mwenye anachimba shimo ataangukia ndani,

Na kila mutu mwenye anaviringisha jiwe⁠—​litamurudilia.+

28 Ulimi wenye kusema uongo unachukia watu wenye uliponda,

Na kinywa chenye kusifu-sifu kinaleta uharibifu.+

27 Usijisifu juu ya kesho,

Kwa maana haujue siku italeta nini.*+

 2 Acha mutu mwingine* akusifu, hapana kinywa chako mwenyewe;

Wengine,* hapana midomo yako mwenyewe.+

 3 Jiwe ni nzito na muchanga ni muzito,

Lakini usumbufu wenye unaletwa na mupumbavu ni muzito zaidi kuliko vyote viwili.+

 4 Kuko ukali wa hasira na mafuriko ya kasirani kali,

Lakini ni nani anaweza kuvumilia wivu?+

 5 Karipio lenye kuwa wazi ni muzuri zaidi kuliko upendo wenye kufichwa.+

 6 Vidonda vyenye kutokezwa na rafiki ni vya uaminifu,+

Lakini busu za adui ni nyingi.*

 7 Mwenye hamu yake ya kula imetoshelezwa anazarau* asali ya sega,

Lakini kwa mwenye njaa, hata kitu kichungu ni kitamu.

 8 Kama ndege mwenye anaenda* mbali na chicha yake*

Ni vile pia mutu mwenye anaenda mbali na nyumba yake.

 9 Mafuta na uvumba vinafurahisha moyo;

Ni vile pia urafiki mutamu wenye unatokana na shauri la unyoofu.*+

10 Usimuache rafiki yako ao rafiki ya baba yako,

Na usiingie katika nyumba ya ndugu yako siku yenye uko na musiba;

Jirani wa karibu anashindia ndugu wa mbali.+

11 Ukuwe na hekima, mwana wangu, na ufurahishe moyo wangu,+

Ili niweze kumujibu ule mwenye ananichokoza.+

12 Mutu mwerevu anaona hatari na kujificha,+

Lakini wenye hawana uzoefu wanaendelea mbele na kupata matokeo ya mubaya.*

13 Kamata nguo ya mutu ikiwa ameahidi kulipia mugeni mukopo;

Umunyanganye kitu chenye aliwekesha kwa ajili ya mukopo ikiwa alifanya vile kwa ajili ya mwanamuke mugeni.*+

14 Wakati mutu anabariki jirani yake kwa sauti kubwa asubui sana,

Itaonwa kuwa laana kwake.

15 Bibi mugomvi* ni kama sehemu ya juu ya nyumba yenye inavuya bila kuacha katika siku ya mvua.+

16 Kila mutu mwenye anaweza kumuzuia anaweza kuzuia upepo

Na anaweza kukamata mafuta kwa mukono wake wa kuume.

17 Kama vile chuma kinanoa chuma,

Ni vile pia mutu ananoa rafiki* yake.+

18 Mwenye anatunza muti wa tini atakula matunda yake,+

Na mwenye anatunza bwana wake ataheshimiwa.+

19 Kama vile maji yanaonyesha uso wa mutu,

Ni vile pia moyo wa mutu unaonyesha moyo wa mwingine.

20 Kaburi na mahali pa uharibifu* havitosheke hata kidogo,+

Wala macho ya mwanadamu hayatosheke hata kidogo.

21 Chungu cha kusafishia ni kwa ajili ya feza na tanuru ni kwa ajili ya zahabu,+

Vilevile mutu anapimwa kupitia sifa yenye anapokea.*

22 Hata kama unatwanga mupumbavu kwa mutwangio

Kama vile nafaka yenye kupondwa katika kinu,

Upumbavu wake hautamutoka.

23 Unapaswa kujua muzuri hali ya kundi lako.

Tunza muzuri* kondoo wako,+

24 Kwa maana mali haidumu milele,+

Wala taji halidumu vizazi vyote.

25 Majani ya mubichi yanaisha, na majani ya mupya yanatokea,

Na majani ya milima yanakusanywa.

26 Wana-kondoo dume wanakupatia nguo zako,

Na mbuzi-dume wanakupatia bei ya shamba.

27 Na kutakuwa maziwa ya kutosha ya mbuzi ya kukulisha wewe,

Kukulisha familia yako, na kutegemeza watumishi wako wanamuke.

28 Waovu wanakimbia hata kama hakuna mwenye anawafuatilia,

Lakini wenye haki wako hodari kama simba.*+

 2 Wakati kuko kosa* katika inchi, inchi inakuwa na mukubwa mumoja kisha mwingine,+

Lakini kwa musaada wa mutu mwenye utambuzi na ujuzi, mukubwa* atadumu wakati murefu.+

 3 Mutu maskini mwenye anapunja mutu wa hali ya chini+

Ni kama mvua yenye inaharibu chakula chote.

 4 Wale wenye kuacha sheria wanasifu mutu muovu,

Lakini wale wenye kushika sheria wanawakasirikia.+

 5 Waovu hawawezi kuelewa haki,

Lakini wale wenye kumutafuta Yehova wanaweza kuelewa kila kitu.+

 6 Maskini mwenye kutembea kwa uaminifu-mushikamanifu wake ni muzuri zaidi

Kuliko tajiri mwenye njia zake zimepotoka.+

 7 Mwana mwenye uelewaji anashika sheria,

Lakini rafiki ya walafi analetea baba yake haya.+

 8 Mwenye anaongeza mali yake kwa faida+ na faida ya juu sana

Anaikusanyia ule mwenye anaonyesha maskini wema.+

 9 Mwenye anakataa kusikiliza sheria

⁠—​Hata sala yake inachukiza.+

10 Mwenye anapoteza watu wanyoofu ili wafuate njia ya uovu ataanguka katika shimo lake mwenyewe,+

Lakini wenye hawana lawama watariti mambo ya muzuri.+

11 Tajiri anajiona mwenyewe kuwa mwenye hekima,+

Lakini mutu maskini mwenye utambuzi anaweza kumuchunguza kwa undani.+

12 Wakati wenye haki wanashinda, kunakuwa utukufu mwingi,

Lakini wakati waovu wanapata mamlaka, watu wanajificha.+

13 Mwenye anafunika makosa yake hatafanikiwa,+

Lakini kila mutu mwenye anayaungama na kuyaacha ataonyeshwa rehema.+

14 Mwenye furaha ni mutu mwenye kuwa muangalifu sikuzote,*

Lakini kila mutu mwenye anafanya moyo wake kuwa mugumu ataanguka katika musiba.+

15 Kama simba mwenye kunguruma na dubu mwenye kushambulia

Ni vile pia mutawala muovu mwenye anatawala juu ya watu wenye hawana uwezo.+

16 Kiongozi mwenye hana utambuzi anatumia mubaya mamlaka yake,+

Lakini mutu mwenye anachukia faida yenye haiko ya haki atarefusha maisha yake.+

17 Mutu mwenye kulemewa na hatia ya damu kwa sababu ya kuondoa uzima wa mutu* ataendelea kukimbia mupaka katika kaburi.*+

Mutu yeyote asimusaidie.

18 Mwenye anatembea bila kosa ataokolewa,+

Lakini ule mwenye njia zake zimepotoka ataanguka bila kutazamia.+

19 Mwenye analima udongo wake atakuwa na mikate mingi,

Lakini mwenye anafuatilia vitu vyenye havina mafaa yoyote atakuwa maskini sana.+

20 Mutu muaminifu atapata baraka nyingi,+

Lakini mwenye anaharakisha kupata utajiri hatakosa kuwa na hatia.+

21 Haiko muzuri kuonyesha upendeleo;+

Lakini mutu anaweza kukosea kwa sababu ya kipande cha mukate.

22 Mutu mwenye wivu* anajikaza sana kupata mali,

Lakini hajue kwamba umaskini utamupata.

23 Kila mutu mwenye anakaripia mwingine+ atafikia kukubaliwa zaidi+

Kuliko mutu mwenye anasifu-sifu kwa ulimi wake.

24 Kila mutu mwenye anaiba vitu vya baba yake na vya mama yake na kusema, “Haiko kosa,”+

Ni rafiki ya mutu mwenye analeta uharibifu.+

25 Mutu mwenye pupa anachochea* mugawanyiko,

Lakini kila mutu mwenye anamutegemea Yehova atapata mafanikio.*+

26 Kila mutu mwenye anategemea moyo wake mwenyewe ni mujinga,+

Lakini ule mwenye anatembea kwa hekima ataponyoka.+

27 Kila mutu mwenye anapatia maskini hatakosa kitu,+

Lakini ule mwenye anawafungia macho atapata laana nyingi.

28 Wakati waovu wanapata mamlaka, mutu anajificha,

Lakini wakati wanaangamia, wenye haki wanaongezeka.+

29 Mutu mwenye anafanya shingo yake ikuwe nguvu* kisha kukaripiwa mara nyingi+

Atavunjwa bila kutazamia na hataweza kupona.+

 2 Wakati wenye haki ni wengi, watu wanafurahi sana,

Lakini wakati muovu anatawala, watu wanalia kwa maumivu.+

 3 Mutu mwenye anapenda hekima anamufurahisha baba yake,+

Lakini mwenye anashirikiana na makahaba anatumia mubaya mali yake.+

 4 Kwa haki mufalme anafanya inchi ikuwe imara,+

Lakini mutu mwenye kutafuta rushwa* anaiharibu.

 5 Mutu mwenye anasifu-sifu jirani yake

Anatandika wavu wa* kunasa miguu yake.+

 6 Kosa la mutu mubaya linamunasa yeye mwenyewe,+

Lakini mwenye haki anapiga vigelegele vya shangwe na kufurahi sana.+

 7 Mwenye haki anahangaikia haki za kisheria za maskini,+

Lakini muovu hana hangaiko kama hilo.+

 8 Watu wenye kujisifu wanawasha muji moto,+

Lakini wenye hekima wanatuliza kasirani.+

 9 Wakati mutu mwenye hekima anabishana na mupumbavu,

Kutakuwa makelele na zihaka, lakini hawatatosheka.+

10 Watu wenye kiu ya damu wanachukia kila mutu mwenye hana kosa,*+

Na wanatafuta kuondoa uzima wa* watu wanyoofu.*

11 Mutu mujinga anaonyesha hisia zake zote,*+

Lakini mwenye hekima anazizuia kwa utulivu.+

12 Wakati mutawala anasikiliza uongo,

Watumishi wake wote watakuwa waovu.+

13 Maskini na mukandamizaji wanafanana katika jambo hili:*

Yehova anapatia macho ya wote wawili mwangaza.*

14 Wakati mufalme anahukumu maskini kwa haki,+

Kiti chake cha ufalme kitakuwa salama sikuzote.+

15 Fimbo* na karipio vinaleta hekima,+

Lakini mutoto mwenye kuachiliwa analetea mama yake haya.

16 Wakati waovu wanaongezeka, makosa yanaongezeka,

Lakini wenye haki wataona kuanguka kwao.+

17 Tia mwana wako nizamu naye atakupumuzisha;

Na atakufurahisha sana.*+

18 Wakati hakuna maono,* watu wanafanya kile wanapenda,+

Lakini wenye furaha ni wale wenye wanashika sheria.+

19 Mutumishi hatajiacha arekebishwe na maneno,

Kwa maana hata kama anaelewa, hatii.+

20 Je, umemuona mutu mwenye kuwa haraka kusema?+

Kuko tumaini zaidi kwa mupumbavu kuliko yeye.+

21 Kama mutumishi anabembelezwa tangu ujana wake,

Kisha wakati fulani atakuwa mutu mwenye hana shukrani.

22 Mutu mwenye kukasirika haraka anachochea ugomvi;+

Kila mutu mwenye kukasirika-kasirika sana anafanya makosa mengi.+

23 Kiburi cha mutu kitamunyenyekeza,+

Lakini kila mutu mwenye roho ya unyenyekevu atapata utukufu.+

24 Mwenye kushirikiana na mwizi anajichukia mwenyewe.*

Anaweza kusikia mwito wa kutoa ushahidi,* lakini hatoe habari yoyote.+

25 Kutetemeka mbele ya* wanadamu ni* mutego,+

Lakini ule mwenye anamutegemea Yehova atalindwa.+

26 Watu wengi wanatafuta kukutana na* mutawala,

Lakini mutu anapata haki kutoka kwa Yehova.+

27 Mutu mwenye hatende haki anachukiza mwenye haki,+

Lakini ule mwenye njia yake imenyooka anachukiza muovu.+

30 Ujumbe muzito wenye kuwa katika maneno ya Aguri mwana wa Yake, wenye alimuambia Itieli, ndiyo, Itieli na Ukali.

 2 Mimi ni mujinga kuliko mutu mwingine yeyote,+

Na sina uelewaji wenye mwanadamu anapaswa kuwa nao.

 3 Sijajifunza hekima,

Na sina ujuzi kuhusu Mwenye Kuwa Mutakatifu Zaidi.

 4 Ni nani amepanda mbinguni na kisha akashuka?+

Ni nani amekusanya upepo katika viganja vya mikono mbili?

Ni nani amefunga maji katika nguo yake?+

Ni nani amefanya miisho yote ya dunia kuwa imara?*+

Jina lake ni nani na jina la mwana wake ni nani⁠—kama unajua?

 5 Kila neno la Mungu ni safi.+

Yeye ni ngao kwa wale wenye kumukimbilia.+

 6 Usiongeze kitu kwenye maneno yake,+

Ukifanya vile atakukaripia,

Na utaonekana kuwa muongo.

 7 Ninakuomba mambo mbili.

Usiniime mambo hayo mbele nikufe.

 8 Ondolea mbali na mimi mambo yenye hayako ya kweli na ya uongo.+

Usinipatie umaskini wala utajiri.

Acha tu nikule fungu langu la chakula,+

 9 Ili nisishibe na kukukana na kusema, “Yehova ni nani?”+

Wala usiruhusu nikuwe maskini, niibe na kuletea haya* jina la Mungu wangu.

10 Usimuchongee mutumishi kwa bwana wake,

Ukifanya vile anaweza kukulaani na utapatikana na hatia.+

11 Kuko kizazi cha watu wenye wanamulaani baba yao

Na hawamubariki mama yao.+

12 Kuko kizazi cha watu wenye wanajiona kuwa safi+

Lakini hawajasafishwa uchafu wao.*

13 Kuko kizazi cha watu wenye macho yenye kujaa kiburi

Na wenye macho yao yanaangalia kwa majivuno mengi!+

14 Kuko kizazi cha watu wenye meno yao ni panga

Na wenye mataya* yao ni visu vya kuchinjia;

Wanameza watu wa hali ya chini wa dunia

Na maskini kutoka kati ya wanadamu.+

15 Vidudu-ruba viko na mabinti wawili wenye kulia, “Nipatie! Nipatie!”

Kuko vitu tatu (3) vyenye havishibake,

Vitu ine (4) vyenye havisemake, “Inaenea!”

16 ⁠—​Kaburi*+ na tumbo lenye kuwa tasa,

Inchi yenye kuimwa maji,

Na moto wenye hausemake, “Inaenea!”

17 Jicho lenye linamuchekelea baba na kuzarau kumutii mama+

⁠—​Kunguru wa bonde* watalingoa,

Na tai wadogo watalikula.+

18 Kuko mambo tatu (3) yenye kunipita uelewaji,*

Na mambo ine (4) yenye sielewe:

19 Njia ya tai katika mbingu,

Njia ya nyoka juu ya mwamba,

Njia ya mashua* katika bahari kubwa,

Na njia ya mwanaume pamoja na kijana mwanamuke.

20 Hii ndiyo njia ya mwanamuke muzinifu:

Anakula, anapangusa kinywa chake;

Kisha anasema, “Sikufanya kosa lolote.”+

21 Kuko mambo tatu (3) yenye kutetemesha dunia

Na mambo ine (4) yenye dunia haiwezi kuvumilia:

22 Wakati mutumwa anatawala akiwa mufalme,+

Wakati mupumbavu anashiba sana,

23 Wakati mwanamuke mwenye kuchukiwa* anaolewa,

Na wakati mutumishi mwanamuke anachukua nafasi ya bimukubwa wake.+

24 Kuko vitu ine (4) katika dunia vyenye kuwa kati ya vitu vidogo zaidi,

Lakini viko na hekima ya kisilika:*+

25 Siafu hawako viumbe vyenye nguvu,*

Lakini wanatayarisha chakula chao wakati wa kipindi cha joto.+

26 Wibari*+ hawako viumbe vyenye nguvu,*

Lakini wanajenga nyumba zao kwenye miamba.+

27 Nzige+ hawana mufalme,

Lakini wote wanaenda mbele kwa mupangilio.*+

28 Mujusi+ anashikilia kwa miguu yake,

Na anaingia katika nyumba ya mufalme.

29 Kuko vitu tatu (3) vyenye mwendo wa kuvutia,

Vitu ine (4) vyenye kuvutia wakati vinatembea:

30 Simba, munyama mwenye nguvu zaidi kuliko wanyama wote,

Mwenye hamukimbie mutu yeyote;+

31 Imbwa-muwindaji; mbuzi-dume;

Na mufalme mwenye kuwa pamoja na jeshi lake.

32 Kama umejiinua kwa ujinga+

Ao kama umepanga kufanya vile,

Tia mukono wako juu ya kinywa chako.+

33 Kwa maana kama vile kupiga-piga maziwa kunatokeza siagi

Na kufinya pua kunafanya damu itoke,

Ni vile pia kuchochea kasirani kunatokeza magomvi.+

31 Maneno ya Mufalme Lemueli, ujumbe muzito wenye mama yake alimupatia ili kumufundisha:+

 2 Nikuambie nini, Ee mwana wangu,

Nikuambie nini, Ee mwana wa tumbo langu la uzazi,

Na nikuambie nini, Ee mwana wa naziri zangu?+

 3 Usipatie wanamuke nguvu zako,+

Wala kufuata njia zenye zinaharibu wafalme.+

 4 Haiko muzuri kwa wafalme, Ee Lemueli,

Haiko muzuri kwa wafalme kunywa divai

Wala watawala kusema, “Kinywaji changu kiko wapi?”+

 5 Ili wasikunywe na kusahau mambo yenye yameagizwa

Na kupotosha haki za watu wa hali ya chini.

 6 Patia pombe watu wenye kuangamia+

Na divai wale wenye kuwa katika mateso makubwa.*+

 7 Acha wakunywe na kusahau umaskini wao;

Na wasikumbuke tena taabu yao.

 8 Semea wale wenye hawana uwezo wa kusema;

Tetea haki za wote wenye kuangamia.+

 9 Sema waziwazi na uhukumu kwa haki;

Tetea haki za* watu wa hali ya chini na maskini.+

א [Aleph]

10 Ni nani anaweza kupata bibi mwenye uwezo?*+

Samani yake inapita sana samani ya marijani.*

ב [Beth]

11 Bwana yake anamutumainia katika moyo wake,

Na hakose kitu chochote chenye samani.

ג [Gimel]

12 Anamupatia bwana yake zawabu ya mema, hapana mabaya,

Siku zote za maisha yake.

ד [Daleth]

13 Anapata manyoya ya kondoo na kitani;

Anafurahia sana kufanya kazi kwa mikono yake.+

ה [He]

14 Yeye ni kama mashua* za mufanyabiashara,+

Analeta chakula chake kutoka mbali.

ו [Waw]

15 Tena, anaamuka wakati ingali usiku,

Na kupatia watu wa nyumba yake chakula

Na kupatia mafungu watumishi wake wanamuke.+

ז [Zayin]

16 Anafikiria shamba na kulinunua;

Anapanda shamba la mizabibu kwa kazi zake mwenyewe za jasho.*

ח [Heth]

17 Anajitayarisha kwa ajili ya kazi ya nguvu,*+

Na anatia nguvu mikono yake.

ט [Teth]

18 Anahakikisha kwamba biashara yake iko na faida;

Taa yake haizimike usiku.

י [Yod]

19 Mikono yake inashika kipande cha muti cha kufungia uzi,

Na mikono yake inashika kipande cha muti cha kusukia uzi.+

כ [Kaph]

20 Ananyooshea mukono mutu wa hali ya chini,

Anafungulia maskini mikono yake.+

ל [Lamed]

21 Hana wasiwasi kuhusu watu wa nyumba yake kwa sababu ya teluji,*

Kwa sababu watu wote wa nyumba yake wamevaa nguo za kuleta joto.*

מ [Mem]

22 Anajitengenezea matandiko ya kufunika kitanda.

Nguo zake ni za kitani na manyoya ya kondoo ya rangi ya zambarau.

נ [Nun]

23 Bwana yake anajulikana sana katika milango mikubwa ya muji,+

Kwenye anakaa kati ya wazee wa inchi.

ס [Samekh]

24 Anatengeneza nguo za kitani* na kuziuzisha

Na kuletea wafanyabiashara mikaba.*

ע [Ayin]

25 Amevaa nguvu na utukufu,

Na iko* hakika kuhusu wakati wenye kuja.*

פ [Pe]

26 Anafungua kinywa chake kwa hekima;+

Sheria ya fazili iko* kwenye ulimi wake.

צ [Tsade]

27 Anaangalia kazi za nyumba yake,

Na hakule mukate wa uvivu.+

ק [Qoph]

28 Watoto wake wanasimama na kumutangaza kuwa mwenye furaha;

Bwana yake anasimama na kumusifu.

ר [Resh]

29 Kuko bibi wengi wenye uwezo,*

Lakini wewe⁠—​wewe umewapita wote.

ש [Shin]

30 Uvutio unaweza kudanganya, na uzuri unaweza kupita haraka,*+

Lakini bibi mwenye anamuogopa Yehova atasifiwa.+

ת [Taw]

31 Mumupatie zawabu kwa sababu ya mambo yenye anafanya,*+

Na kazi zake zimusifu katika milango mikubwa ya muji.+

Tnn., “kujua.”

Ao “mambo ya haki.”

Ao “haki.”

Ao “muongozo wenye hekima.”

Ao “mufano.”

Ao “Kumuheshimia.”

Ao “sheria.”

Ao “Sheoli,” ni kusema, kaburi la wanadamu wote. Angalia Maana ya Maneno.

Ao “Tupa kura yako pamoja na sisi.”

Ao “tutakuwa na mufuko mumoja.”

Ao “makila.”

Ao “eko.”

Ao “nafsi za.”

Ao “nafsi ya.”

Tnn., “kichwa cha.”

Ao “Mugeuke wakati ninawakaripia.”

Tnn., “watakula matunda.”

Ao “mipango yao wenyewe ya mubaya.”

Angalia Maana ya Maneno.

Angalia Maana ya Maneno.

Tnn., “mugeni.” Inaonekana ni mutu mwenye amejitenga na Mungu kwa sababu ya mwenendo mupotovu.

Ao “maneno yenye ushawishi.”

Tnn., “mugeni.” Inaonekana ni mutu mwenye amemuacha Mungu kwa sababu ya mwenendo mupotovu.

Ao “bwana.”

Tnn., “mapito yake.”

Tnn., “wenye wanaingia kwake.”

Ao “wenye kushika uaminifu-mushikamanifu.”

Ao “sheria.”

Ao “kweli.”

Tnn., “usiegemee.”

Tnn., “kitofu chako.”

Ao “vitu vya muzuri sana vya.”

Ao “mapato.”

Ao “vikamulio vyako vya divai vitajaa sana.”

Angalia Maana ya Maneno.

Inaonekana mustari huu unazungumuzia sifa za Mungu zenye kutajwa katika mistari yenye kutangulia.

Ao “Zitapatia nafsi yako.”

Ao “hautagonga kitu chochote.”

Ao “wale wenye kustahili mema hayo.”

Ao “Kama mukono wako uko na nguvu za kusaidia.”

Ao “sheria.”

Ao “la kwanza.”

Tnn., “Tegea sikio.”

Ao “macho yako yenye kungaa.”

Ao pengine, “Chunguza kwa uangalifu.”

Tnn., “Tegea sikio lako.”

Tnn., “mugeni.” Angalia Mez 2:16.

Ao “Sheoli,” ni kusema, kaburi la wanadamu wote. Angalia Maana ya Maneno.

Ao “nguvu.”

Tnn., “Katikati ya mukusanyiko na kutaniko.”

Ao “safi.”

Ao “Chanzo chako cha maji kibarikiwe.”

Ao “mbuzi wa pori.”

Ao “yakuleweshe.”

Tnn., “mugeni.” Angalia Mez 2:16.

Tnn., “mugeni.” Angalia Mez 2:16.

Ni kusema, wakati unaahidi kumulipia mukopo.

Ao “vyenye nafsi yake inachukia.”

Ao “sheria.”

Ao “itakufundisha.”

Tnn., “mugeni.” Angalia Mez 2:16.

Ao “nafsi yenye.”

Ao “ajaze nafsi yake.”

Tnn., “iko katika ukosefu wa moyo.”

Ao “bei yoyote ya ukombozi.”

Ao “sheria.”

Tnn., “mugeni.” Angalia Mez 2:16.

Tnn., “mugeni.” Angalia Mez 2:16.

Ao “yenye kushawishi.”

Ao “wenye hawana uzoefu.”

Tnn., “iko katika ukosefu wa moyo.”

Ao “Alikuwa na nguo ya.”

Ao “eko.”

Tnn., “Miguu yake haibakiake.”

Ao “eko.”

Ao “eko.”

Kunyunyiza ni kumwanga kidogo-kidogo kitu cha majimaji ao ungaunga.

Ao “pingu.”

Ao “nafsi yake.”

Ao “Sheoli,” ni kusema, kaburi la wanadamu wote. Angalia Maana ya Maneno.

Tnn., “wana wa binadamu.”

Tnn., “muelewe moyo.”

Angalia Maana ya Maneno.

Ao “Kanuni zenye kuritiwa.”

Angalia Maana ya Maneno.

Ao “zamani za kale.”

Ao “nilizaliwa kama vile kwa maumivu ya kuzaa.”

Tnn., “muzunguko.”

Tnn., “alifanya nguvu.”

Ao “alitunga sheria kuhusu.”

Ao “wanadamu.”

Ao “Kwa kukesha.”

Ao “anaumiza nafsi yake.”

Tnn., “Amechinja machinjo yake.”

Tnn., “iko katika ukosefu wa moyo.”

Ao “watu wenye hawana uzoefu.”

Tnn., “wako katika ukosefu wa moyo.”

Ao “Sheoli,” ni kusema, kaburi la wanadamu wote. Angalia Maana ya Maneno.

Ao “nafsi ya mwenye haki ikae.”

Ao “Sifa ya.”

Tnn., “amri.”

Tnn., “iko katika ukosefu wa moyo.”

Ao “Kitu cha maana cha.”

Ao pengine, “iko kwenye njia yenye inapeleka kwenye uzima.”

Ao “habari zenye haziko hakika.”

Ao “inaongoza.”

Ao “huzuni; magumu.”

Ao “vinaigre.”

Ao “eko.”

Ao “bwana wake wa kazi.”

Ao “Tarajio.”

Ao “kinazaa tunda la.”

Ao “Kilo.”

Ao “udanganyifu.”

Ao “jiwe kamili la kupimia.”

Ao “Vitu vya maana havitakuwa.”

Ao “mutu mwenye hamuogope Mungu.”

Tnn., “iko katika ukosefu wa moyo.”

Tnn., “muaminifu katika roho.”

Tnn., “anafunika jambo.”

Ao “muongozo wa hekima.”

Ao “wokovu.”

Tnn., “anachukia.”

Ao “mwenye kuvutia.”

Ao “Mutu mwenye upendo mushikamanifu.”

Ao “anatendea mema nafsi yake.”

Ao “haya.”

Tnn., “Mukono kwa mukono.”

Tnn., “anasambaza.”

Ao “Nafsi yenye ukarimu.”

Tnn., “atanenepeshwa.”

Tnn., “mwenye kunywesha wengine kwa ukarimu.”

Ao “haya.”

Angalia Maana ya Maneno.

Ao “hana ufahamu.”

Tnn., “yanavizia ili kumwanga damu.”

Tnn., “mukate.”

Ao “nafsi ya munyama wake wa kufugwa.”

Tnn., “iko katika ukosefu wa moyo.”

Tnn., “kinywa chake.”

Ao “siku ileile.”

Tnn., “anafunika.”

Tnn., “mambo yenye haki.”

Tnn., “Lakini washauri wa.”

Ao “yanamufanya ashuke moyo.”

Ao “anarekebishwa.”

Tnn., “kinywa chake.”

Ao “Lakini nafsi kabisa.”

Ao “mambo yenye anasema.”

Ao “nafsi yake.”

Ao “nafsi yake haina.”

Ao “nafsi ya mwenye bidii.”

Tnn., “atanenepeshwa.”

Ao “eko.”

Ao “nafsi ya mutu.”

Tnn., “hawasikie kemeo lolote.”

Tnn., “unashangilia.”

Ao “wenye kupatiana mawazo.”

Ao “Mali yenye inatokana na ubatili.”

Tnn., “mwenye anaikusanya kwa mukono.”

Ao “Tumaini.”

Ao “neno.”

Ao “Sheria.”

Ao “karipio.”

Ao “nafsi.”

Ao “kumuharibu.”

Ao “hatoe nizamu; azabu.”

Ao pengine, “bila kukawia.”

Ao “nafsi.”

Ao “zenye kupotoka.”

Ao pengine, “wajinga wanadanganya wengine.”

Ao “wanafanya muzaha wakati wanaombwa kufanya marekebisho.”

Ao “Lakini kuko nia njema kati ya watu wanyoofu.”

Ao “uchungu wa nafsi yake.”

Ao “Mwenye hana uzoefu.”

Ao “iko na kasirani kali.”

Ao “mutu mwenye uwezo wa kufikiri.”

Ao “Mwenye hana uzoefu.”

Ao “eko.”

Ao “nafsi.”

Ao “eko.”

Ao “afya ya muzuri.”

Ao “lenye utulivu.”

Ao “lenye kuumiza.”

Ao “Ulimi wenye kuponyesha.”

Tnn., “ni kupondeka kwa roho.”

Ao “karipio.”

Ao “mapato.”

Ao “kali.”

Ao “Sheoli,” ni kusema, kaburi la wanadamu wote. Angalia Maana ya Maneno.

Ao “na Abadoni.”

Ao “mwenye anamukaripia.”

Ao “kinafuatia.”

Ao “muzuri.”

Ao “eko.”

Ao “muvurugo.”

Tnn., “mwenye alikulishwa katika chombo cha kukulishia wanyama.”

Tnn., “iko katika ukosefu wa moyo.”

Ao “mazungumuzo ya siri.”

Tnn., “anafurahia sana jibu la kinywa chake.”

Ao “Sheoli,” ni kusema, kaburi la wanadamu wote. Angalia Maana ya Maneno.

Ao “haya.”

Ao “kata-midomo.”

Ao “unafikiria kwa uangalifu namna ya kujibu; unawaza mbele ya kusema.”

Ao “eko.”

Ao “Kumutupia mutu jicho kwa furaha.”

Tnn., “inanenepesha mifupa.”

Ao “nafsi yake.”

Tnn., “moyo.”

Tnn., “Mipangilio ya moyo ni ya mutu.”

Ao “jibu lenye kufaa.” Tnn., “jibu la ulimi.”

Tnn., “safi.”

Tnn., “roho.”

Tnn., “Umuviringishie Yehova kazi zako.”

Tnn., “Mukono kwa mukono.”

Angalia Maana ya Maneno.

Ao “Uamuzi wenye kuongozwa na Mungu.”

Ao “Kilo.”

Ao “anaiepuka.”

Ao “nafsi yake.”

Tnn., “munyenyekevu wa roho.”

Tnn., “mema.”

Ao “Na maneno yenye kuvutia yanaongeza.” Tnn., “Na utamu wa midomo unaongeza.”

Ao “Yako na onjo tamu.” Angalia Maana ya Maneno.

Ao “Nafsi.”

Tnn., “kinywa chake kinamuchochea.”

Ao “Mwenye kufanya mipango ya mubaya.”

Ao “utukufu.”

Tnn., “anatawala juu ya roho yake.”

Ao “utulivu.”

Tnn., “zabihu.”

Ao “wazazi.”

Ao “watoto.”

Ao “ya muzuri.”

Ao “mutu mwenye cheo.”

Ao “ni jiwe lenye kufanya mwenye kuwa nalo akubaliwe.”

Tnn., “mwenye anafunika.”

Ao “kufungua ukuta wa maji.” Tnn., “kuachilia maji.”

Ao “Wakati hana akili ya muzuri?”

Tnn., “iko katika ukosefu wa moyo.”

Tnn., “mema.”

Ao “unasaidia mutu kupona.”

Ao “inakausha kabisa mifupa.”

Ao “kata-midomo.”

Tnn., “rushwa kutoka katika kifua.”

Tnn., “uchungu.”

Ao “kulipisha mwenye haki amande.”

Tnn., “atabakia na roho yenye kutulia.”

Ao “Anazarau.”

Ao “nafsi yake.”

Ao “ni kama vitu vya kumezwa kwa pupa.”

Tnn., “na kuinuliwa juu,” ni kusema, hawezi kufikiwa, iko salama.

Ao “hali ya kupoteza kabisa tumaini?”

Ao “kumuchunguza kwa undani.”

Tnn., “kunatenganisha.”

Pingu ni kipande cha muti ao cha chuma cha kufungia mulango kwa ndani.

Tnn., “kinywa chake.”

Ao “anapata nia njema ya.”

Ao “Nafsi yenye haina ujuzi haiko nafsi ya muzuri.”

Tnn., “mwenye anaenda haraka kwa miguu yake.”

Ao “mutu mukarimu.”

Tnn., “anapata moyo.”

Ao “anapenda nafsi yake.”

Tnn., “mema.”

Tnn., “kupita juu ya.”

Ao “mwana-simba mwenye manyoya ya murefu kwenye shingo.”

Ao “musumbufu.”

Ao “nafsi yake.”

Ao “atamupatia zawabu.”

Ao “usitamani.” Tnn., “usiinue nafsi yako ili.”

Ao “kusudi.”

Ao “mwana-simba mwenye manyoya ya murefu kwenye shingo.”

Ao pengine, “Ataangalia wakati wa mavuno lakini hatapata kitu.”

Ao “Nia.” Tnn., “Shauri.”

Tnn., “Wana.”

Ao “kilo.”

Ao “Majiwe mbili ya kupimia yenye kuwa tofauti na pia vyombo mbili vya kupimia vyenye kuwa tofauti.”

Ao “kijana mwanaume.”

Angalia Maana ya Maneno.

Ao “mugeni.”

Ao “itafanywa kuwa imara.”

Ao “shauri.”

Ao “muongozo wenye hekima.”

Ao “mwenye anashawishi kwa midomo yake.”

Ao “Majiwe mbili ya kupimia yenye kuwa tofauti.”

Ao “kilo.”

Ao “njia ya kufuata.”

Ao “mupeto; pneu.”

Ao “vinasugua na kuondoa.”

Ao “nia.”

Ao “faida.”

Ao pengine, “kwa wale wenye kutafuta kifo.”

Ao “musumbufu.”

Ao “anajua jambo la kufanya.”

Ao “kata-midomo.”

Tnn., “yenye kuwa katika kifua.”

Ao “mwenye anapenda raha.”

Ao “musumbufu.”

Tnn., “atameza.”

Ao “eko.”

Ao “kushinda.”

Ao “Anaepusha nafsi yake.”

Ao “pamoja na mwenendo wa haya!”

Tnn., “atazungumuza milele.”

Ao “mutu munyoofu anafanya njia yake kuwa hakika.”

Ao “sifa ya muzuri.” Tnn., “jina.”

Tnn., “Kukubaliwa.”

Tnn., “wanakutana pamoja.”

Ao “azabu.”

Ao “nafsi yake kuwa ya.”

Ao “mutoto; kijana.”

Tnn., “Mwenye kuwa na jicho la muzuri.”

Ao “Mashitaka ya kisheria.”

Ao “eko.”

Tnn., “wageni.” Angalia Mez 2:16.

Ao “mutoto; kijana.”

Ao “atanyanganya nafsi ya.”

Ao “Jizuie.”

Ao “nafsi yenye kujaa tamaa.”

Ao pengine, “Acha kufuata uelewaji wako mwenyewe.”

Ao “cha mutu yeyote mwenye jicho lenye uovu.”

Ao “mwenye kuhesabia katika nafsi yake.”

Tnn., “moyo wake hauko pamoja na wewe.”

Tnn., “Mukombozi.”

Ao “eko.”

Ao “mutoto; kijana.”

Ao “uokoe nafsi yake isiingie.”

Ao “Sheoli,” ni kusema, kaburi la wanadamu wote. Angalia Maana ya Maneno.

Tnn., “Figo zangu zitafurahi.”

Ao “Ujipatie.”

Tnn., “mugeni.” Angalia Mez 2:16.

Ao “macho mazito.”

Ao “wenye wanakusanyika ili kuonja-onja.”

Ao “mashua ya maji; bateau.”

Ao “sikusikia maumivu yoyote.”

Ao “Nitakitafuta tena.”

Ao “Familia.”

Ao “eko.”

Ao “muongozo wenye hekima.”

Ao “mafanikio; wokovu.”

Ao “Mipango ya mubaya ya mupumbavu.”

Ao “nyakati za taabu.”

Ao “nia.”

Ao “kuangalia nafsi yako.”

Ao “ni tamu kwa nafsi yako.”

Ni kusema, juu ya ule adui.

Ao “Usijionyeshe umewaka kasirani.”

Ao “wale wenye kutaka mabadiliko.”

Ni kusema, Yehova na mufalme.

Ao pengine, “Kujibu kwa njia yenye kuwa wazi ni kama kubusu mutu.”

Ao “familia.”

Ao “Nitamulipa sawasawa na matendo yake.”

Tnn., “iko katika ukosefu wa moyo.”

Tnn., “Nilipokea nizamu.”

Ao “walifanya kopi na kukusanya.”

Ao “siri za wengine.”

Ao “habari ya mubaya yenye haiko hakika.”

Ao “vikalio vya feza.”

Ao “neige.”

Ao “nafsi ya bwana wake.”

Tnn., “anajisifu kuhusu zawadi ya uongo.”

Ao “wenye upole.”

Gongo ni fimbo yenye kuvimba kwenye mwisho wake mumoja.

Ao pengine, “mudanganyifu.”

Ao “vinaigre.”

Tnn., “mwenye anakuchukia.”

Ao “eko.”

Ao “eko.”

Ni kusema, kupunguza uadui wake na kuyeyusha ugumu wake.

Ao “musumbufu.”

Angalia Maana ya Maneno.

Ao “mwenye anakubaliana na.” Tnn., “mwenye anayumba-yumba mbele ya.”

Ao “mwenye anashindwa kuzuia roho yake.”

Ao “neige.”

Ao “eko.”

Ao pengine, “Vilevile laana yenye mutu hastahili haimupatake.”

Lijamu ni kipande cha chuma chenye kinawekwa kwenye kinywa cha munyama ili kumuongoza na kumuzuia.

Ao “Ili usijifanye kuwa kama yeye.”

Ao “eko.”

Tnn., “kunywa jeuri.”

Ao “yenye kuninginia.”

Ao “mwenye anaumiza kila mutu.”

Ao “eko.”

Ao “eko.”

Ao “eko.”

Ao “maegemeo yake.”

Ao “eko.”

Ao pengine, “mwenye anajiingiza katika.”

Ao “mishale yenye kuua.”

Ao “ni kama vitu vya kumezwa kwa pupa.”

Tnn., “midomo yenye shauku pamoja na.”

Ao “Kwa maana moyo wake ni wenye kuchukiza kabisa.”

Tnn., “itazaa nini.”

Tnn., “mugeni.”

Tnn., “Mugeni.”

Ao pengine, “haziko za kweli; ni za kulazimishwa.”

Ao “Nafsi yenye kutosheka inazarau.” Tnn., “anakanyangia chini.”

Ao “mwenye anakimbia.”

Ao “nyumba yake; kiota chake.”

Ao “shauri la nafsi.”

Ao “azabu.”

Ao “mugeni.”

Ao “musumbufu.”

Tnn., “uso wa rafiki.”

Ao “Sheoli na Abadoni.”

Ao “Vilevile mutu ni kulingana na sifa yake.”

Ao “Weka moyo juu ya; Kazia uangalifu.”

Ao “mwana-simba.”

Ao “uasi.”

Tnn., “yeye.”

Ao “mwenye anaogopa kila wakati.”

Ao “mwenye kulemewa na damu ya nafsi.”

Ao “shimo.”

Ao “pupa.”

Ao pengine, “Nafsi yenye kiburi inachochea.”

Tnn., “atanenepeshwa.”

Ao “mwenye anaendelea kuwa kichwa-nguvu.”

Ao “kata-midomo.”

Ao “makila ya.”

Ao “mwenye hana lawama.”

Ao “nafsi ya.”

Ao pengine, “Lakini mutu munyoofu anatafuta kulinda uzima wake.”

Tnn., “roho yake yote.”

Tnn., “wanakutana pamoja.”

Ni kusema, Yeye anawapatia uzima.

Ao “Nizamu; Azabu.”

Ao “atafurahisha sana nafsi yako.”

Ao “maono ya unabii; ufunuo.”

Ao “anachukia nafsi yake mwenyewe.”

Ao “kiapo chenye laana.”

Ao “Kuogopa.”

Ao “kunatega.”

Ao pengine, “wanatafuta kukubaliwa na.” Tnn., “wanatafuta uso wa.”

Tnn., “ameinua miisho yote ya dunia.”

Ao “kushambulia.”

Tnn., “mavi yao.”

Mataya ni mifupa ya kinywa yenye kubeba meno.

Ao “Sheoli,” ni kusema, kaburi la wanadamu wote. Angalia Maana ya Maneno.

Ao “bonde la muto.”

Ao “yenye kuwa ya ajabu sana kwangu.”

Ao “mashua ya maji; bateau.”

Ao “mwenye hapendwe.”

Ao “viko na hekima nyingi sana.”

Tnn., “hawako kikundi cha watu wenye nguvu.”

Ao “Pelele.”

Tnn., “hawako kikundi cha watu wenye nguvu.”

Ao “wakiwa wamegawanywa vikundi-vikundi.”

Ao “wenye uchungu wa nafsi.”

Ao “Tetea mashitaka ya.”

Ao “bibi muzuri.”

Angalia Maana ya Maneno.

Ao “mashua za maji; bateaux.”

Ao “kwa mapato yake.” Tnn., “kutokana na matunda ya mikono yake.”

Tnn., “Anafunga nguvu kwenye viuno vyake.”

Ao “neige.”

Tnn., “nguo mbili.”

Ao “nguo za ndani.”

Ao “mishipi.”

Ao “eko.”

Ao “anacheka siku yenye kuja.”

Ao “Mafundisho ya upendo yako; Sheria ya upendo mushikamanifu iko.”

Ao “wazuri.”

Ao “unaweza kuwa kitu bure.”

Tnn., “Mumupatie kutokana na matunda ya mikono yake.”

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine