Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • g 1/15 uku. 6
  • Jibu Tunalopaswa Kufikiria

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Jibu Tunalopaswa Kufikiria
  • Amuka!—2015
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Mashahidi wa Yehova Wanaamini Kama Mungu Aliumba Mbingu na Dunia kwa Siku Sita Zenye Urefu wa Saa 24?
    Maulizo Yenye Watu Wanaulizaka Sana Juu ya Mashahidi wa Yehova
  • Uzima Ulianza Namna Gani?
    Amuka!—2015
  • Mambo Yenye Biblia Inatuambia
    Amuka!—2021
  • Uumbaji
    Amuka!—2014
Ona Habari Zaidi
Amuka!—2015
g 1/15 uku. 6
Biblia yenye kufunguliwa

KICWA | UZIMA ULIANZA NAMNA GANI?

Jibu Tunalopaswa Kufikiria

KISHA kuchunguza uhakikisho mbalimbali, watu wengi wamefikia kuona kuwa uzima uliumbwa na mutu mwenye akili ya hali ya juu. Fikiria mufano wa Antony Flew, profesa wa filozofia mwenye wakati fulani alikuwa muteteaji mukubwa wa imani ya kuwa hakuna Mungu. Wakati alijifunza juu ya mambo ya kushangaza na yaliyo magumu kueleweka kuhusu uzima na sheria za asili za ulimwengu, Flew alibadilisha mawazo yake. Alitaja namna ya kufikiri ya wanafilozofia wa zamani kwa kuandika hivi: “Tunapaswa kukubali mambo ya hakika yanayoonyeshwa wazi hata ikiwa hatukubaliane nayo.” Kulingana na Profesa Flew, mambo mbalimbali yanahakikisha kuwa kuna Muumbaji.

Gerard, aliyetajwa katika habari iliyotangulia, alifikia uamuzi kama huo. Hata ikiwa alisoma sana na kazi yake katika elimu ya wadudu, alisema hivi: “Sikuona jambo lolote linalohakikisha kuwa uzima ulijitokeza wenyewe tu kutokana na kitu kisichokuwa na uzima. Utaratibu na mambo yasiyoeleweka kuhusu vitu vyenye uzima vilinisadikisha kuwa kunapaswa kuwa Mupangaji na Muumbaji.”

Kama vile mutu anaweza kujifunza kutokana na muchoraji kwa kuchunguza mambo aliyochora, Gerard alifikia kutambua sifa za Muumbaji kwa kujifunza uumbaji. Tena, Gerard alichukua wakati wa kuchunguza Biblia, kitabu kilichotoka kwa Muumbaji. (2 Timotheo 3:16) Katika kitabu hicho, alipata majibu kwa maulizo juu ya wakati uliopita wa watu na njia mbalimbali za muzuri za kupambana na magumu yenye kutupata leo. Kwa kufanya hivyo, alifikia kusadiki kuwa Biblia ni kitabu kutoka kwa mutu mwenye akili ya juu sana.

Kama vile Gerard aliona, majibu ya Biblia yanapaswa kufikiriwa. Tunakutia moyo uyachunguze wewe mwenyewe.

Je, Ulijua?

BIBLIA HAIPINGE SAYANSI. Tofauti na hilo, inatia watu moyo wachunguze uumbaji. (Isaya 40:26) Hata ikiwa Biblia haiko kitabu cha sayansi, inapatana na mambo hakika ya sayansi. Kwa mufano, Biblia haiunge mukono mawazo ya wanauumbaji. Haiseme kama ulimwengu uliumbwa kwa kipindi cha siku sita zenye saa 24 kila moja. Neno “siku” linalotumiwa katika Mwanzo linamaanisha vipindi virefu vya wakati.a

a Ili kupata habari zaidi, soma broshua Uhai Ulitokana na Muumba? iliyochapishwa na Mashahidi wa Yehova. Unaweza pia kupata broshua hiyo kwenye adresi yetu ya Internete www.jw.org/sw.

Biblia Inafundisha Kama . . .

UZIMA UNATOKANA TU NA UZIMA. “Kwako wewe [Mungu] iko chemchemi ya uzima.”—Zaburi 36:9.

MUNGU ALIUMBA MIMEA NA WANYAMA “KULINGANA NA AINA ZAKE.” (Mwanzo 1:11, 12, 21, 24, 25) Biblia haiseme juu ya mipaka kuhusu “aina” hizo. Hilo linafanya kuwe mabadiliko kwa kiasi fulani katika kila aina.

MUNGU ALIUMBA WATU NA UWEZO WA KUONYESHA SIFA KAMA ZAKE. Sifa hizo zinatia ndani upendo, wema, na haki. ‘Mungu akaendelea kusema: Na tufanye mutu kwa mufano wetu, kwa sura yetu.’—Mwanzo 1:26.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine