Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w11 1/5 uku. 7
  • 4. Watu hawatapenda watu wa familia yao

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • 4. Watu hawatapenda watu wa familia yao
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Mwisho wa Jeuri Inayotokea Nyumbani
    Amuka!—2013
  • Inawezekana Kusikuwe Jeuri Katika Dunia?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2016
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
w11 1/5 uku. 7

4. Watu hawatapenda watu wa familia yao

“Watu watakuwa wenye . . . hawana upendo wa asili.”​—2 TIMOTEO 3:1-3.

● Chris anaishi kaskazini mwa Pays de Galles. Anatumikaka na kikundi ya kusaidia watu wenye kutendewa mubaya ku nyumba. Anasema hivi: “Ninakumbuka mwanamuke mwenye alikuwa amepigwa sana kiasi ya kwamba sikumutambua, hata kama nilikuwaka nilishamuona. Wanamuke wengine wameumia sana katika moyo mupaka wanashindwa hata kukuangalia.”

USHUHUDA UNAONYESHA NINI? Mu inchi moja ya Afrika karibu mutu 1 kati ya watu 3 alitendewa mubaya kingono wakati alikuwa mutoto. Uchunguzi wenye ulifanywa mu ile inchi ulionyesha kama zaidi ya mwanaume 1 kati ya wanaume 3 aliona kama haiko mubaya mutu kupiga bibi yake. Lakini haiko wanamuke tu njo wanatendewaka mubaya ku nyumba. Kwa mufano, mu inchi ya Kanada, karibu wanaume 3 kati ya wanaume 10 wamepigwa ao kutendewa mubaya na bibi zao.

WATU FULANI WANASEMA NINI? Tangu zamani watu wanatendewaka mubaya ku nyumba. Leo tu njo watu wanakazia akili ile jambo kuliko zamani.

ILE NI KWELI? Ni kweli kama leo njo watu wengi wanazungumuzia sana tatizo ya kutendewa mubaya ku nyumba. Lakini, ile imefanya hesabu ya watu wenye kutendewa mubaya ku nyumba ipunguke? Hapana. Leo, hesabu ya watu wenye hawaonyeshane upendo mu familia inaendelea kuongezeka.

UNAWAZA NINI? 2 Timoteo 3:1-3 iko inatimia? Watu wengi wanakosa kuonyesha watu wa familia yao upendo wenye kwa kawaida watu wa familia wanapaswa kuonyeshana?

Unabii wa tano wenye uko unatimia leo unahusu dunia. Ona jambo yenye Biblia inasema juu ya ule unabii.

[Wazo la fungu kwenye ukurasa wa 7]

“Watu hawazoee kujulisha polisi wakati wanatendewa mubaya ku nyumba. Kwa kukadiria, mwanamuke anaendaka kushitaki bwana yake kisha bwana yake kumutendea mubaya mara 35.”​—MUSEMAJI WA KIKUNDI YA KUTETEA WATU WENYE KUTENDEWA MUBAYA KU NYUMBA, MU PAYS DE GALLES.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine