Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w11 1/10 uku. 9
  • Ukweli Unaweza Kubadili Maisha Yako

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Ukweli Unaweza Kubadili Maisha Yako
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Mashahidi wa Yehova Njo Wakristo wa Kweli?
    Furahia Maisha Milele!—Ujifunze Biblia kwa Njia ya Mazungumuzo
  • Ukuwe Hakika Kama Mambo Yenye Unaamini Ni ya Kweli
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2020
  • Kweli Inaweza Kukuweka Huru
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
w11 1/10 uku. 9

Ukweli Unaweza Kubadili Maisha Yako

HUENDA umesikia au umefundishwa mojawapo ya mafundisho ya uwongo kumhusu Mungu ambayo yamefunuliwa katika makala zilizotangulia. Hata hivyo, huenda ukasitasita kubadili imani yako kuhusu fundisho hilo, hasa ikiwa umeliamini kwa muda mrefu.

Hali hiyo ya kusitasita inaeleweka. Dini fulani hazipendi kulinganisha mafundisho yao na yale ambayo Biblia inasema. Nyingine hujaribu kutetea mafundisho yao ya uwongo kwa kusema kwamba si rahisi kuilewa Biblia, hivyo haikusudiwi kueleweka na kila mtu. Hata hivyo, wengi wa wanafunzi wa Yesu walikuwa watu wa kawaida tu, wasio na elimu ya juu, na walielewa kwa urahisi mambo aliyofundisha.—Matendo 4:13.

Huenda ukasitasita kuchunguza kama mafundisho unayoamini ni ya kweli ukiogopa kwamba kufanya hivyo kutaonyesha ukosefu wa imani. Lakini je, unafikiri ni jambo linalopatana na akili kwamba Mungu hatapendezwa nawe eti kwa sababu umeamua kuchunguza Biblia, ujumbe wake kwa wanadamu, ili kuelewa anachotaka ufanye? Kinyume cha hilo, Neno lake linakutia moyo uyachunguze Maandiko kibinafsi, linaposema: ‘Jihakikishieni wenyewe mapenzi ya Mungu yaliyo mema na yenye kukubalika na makamilifu.’—Waroma 12:2.

Kujifunza ukweli kumhusu Mungu kunamaanisha mengi zaidi ya kupata tu ujuzi—kunaweza kuboresha maisha yako. (Yohana 8:32) Sasa Deanne, aliyetajwa katika makala ya kwanza, amesitawisha imani inayotegemea Neno la Mungu. Anasema: “Sikujua kamwe kwamba kuelewa Maandiko si jambo gumu hadi nilipoanza kujifunza Biblia. Sasa ninamjua Yehova kama Baba yangu wa mbinguni mwenye upendo, bali si kama Mungu tu nisiyeweza kuwa na uhusiano wa karibu pamoja naye. Sasa nimepata kusudi halisi maishani.”

Labda umewahi kujifunza Biblia lakini hukuona kama unafaidika. Ikiwa ndivyo, usikate tamaa. Kujaribu kuilewa Biblia ukiwa umefundishwa mambo ya uwongo kumhusu Mungu ni kama kufunga safari ya kwenda mahali ambako hujui ukitumia ramani ambayo si sahihi. Huenda ukaanza safari yako vizuri, lakini ukakata tamaa baada ya kukosea njia mara kadhaa. Hivyo, ikiwa unataka kufika mahali hapo, anza safari kwa kufuata barabara inayofaa ukiwa na ramani yenye maelezo sahihi kuhusu mahali unakoenda.

Je, ungependa kujifunza ukweli wa mambo kumhusu Mungu? Ikiwa unataka kujifunza Biblia nyumbani kwako bila malipo, tunakualika uwasiliane na Mashahidi wa Yehova katika eneo lenu au uandike barua ukitumia anwani kwenye ukurasa wa 4 wa gazeti hili.

[Blabu katika ukurasa wa 9]

‘Jihakikishieni wenyewe mapenzi ya Mungu yaliyo mema na yenye kukubalika na makamilifu.’​—WAROMA 12:2

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine