Magumu Ambayo Wanawake Wanavumilia
Gazeti GEO, linataja maneno ya ZAHRA, BINTI MWENYE UMRI WA MIAKA 15 aliyesema hivi: “Ninapoona namna wanawake wanavyotendewa, kwa kweli ninasikitika sababu gani niko mwanamuke.”
MANENO ya binti huyo yaliyo hapa pembeni yanaonyesha jambo lenye kuhuzunisha—duniani pote, mabinti na wanawake wanatendewa vibaya na wanabaguliwa muda wa maisha yao yote. Acheni tuchunguze ripoti zinazofuata.
● Kubaguliwa kwa sababu ya kuwa mwanamuke. Huko Asia, wazazi wengi wanatamani wazae watoto wanaume kuliko kuzaa watoto wanawake. Ripoti ya UMOJA WA MATAIFA iliyofanywa katika mwaka wa 2011 inaonyesha kama huko Asia, wanawake karibu milioni 134 wanakosekana kwa sababu ya kutoa mimba, kuua watoto wadogo wanawake, na kwa sababu ya kupuuzwa ao kuonwa kuwa bure.
● Masomo. Duniani pote, kati ya watu ambao hawakusoma ao hawakumaliza masomo ya musingi, wengi ni wanawake na mabinti.
● Kusumbuliwa kingono. Zaidi ya wanawake bilioni 2 na nusu (2600 000000) wanaishi katika inchi ambamo hakuna sheria inayokataza wanaume kuwalala bibi zao kinguvu.
● Afya. Katika inchi masikini, karibu kila dakika 2, mwanamuke mumoja anakufa kwa sababu ya matatizo ya mimba ao matatizo wakati wa kuzaa, kwa sababu alikosa matunzo yenye kufaa.
● Haki za kuriti mali. Ijapokuwa wanawake ndio wanaolima zaidi ya nusu ya chakula cha dunia nzima, katika inchi nyingi, hawana haki ya kisheria ya kununua shamba fulani ao kuriti sehemu ya udongo.
Sababu gani wanawake hawapewe haki hizo ambazo watu wote wanapaswa kupewa? Watu wa desturi fulani wanafuata mafundisho na mazoea ya dini yanayochochea ao hata kuunga mukono wazo la kuwaonea wanawake na kuwatendea vibaya. Gazeti fulani (La croix et le croissant — Le christianisme face à l’islam) linataja maneno ya mwanasheria mumoja wa India anayeitwa Chandra Rami Chopra, ambaye alisema hivi: “Sheria za dini zote zinafanana katika jambo moja: Zote zinaunga mukono ubaguzi wa wanawake.”
Wewe unawaza nini juu ya jambo hilo? Unawaza kama Biblia inafundisha kwamba wanawake ni watu bure, kama vile vitabu vingine vingi vya dini vinavyofundisha? Watu fulani wanawaza kama maandiko fulani ya Biblia yanaunga mukono wazo la kusema wanawake ni watu bure. Lakini, Mungu aliyeandikisha Biblia anawaona wanawake namna gani? Hata kama watu wengi wanasadiki kwamba wanawake ni watu bure, kuchunguza vizuri mambo ambayo Biblia inasema kunaweza kutusaidia kupata majibu ya maulizo hayo.
[Maneno ili kueleza mahali picha ilitokea, ukurasa wa 3]
© G.M.B. Akash/Panos Pictures