Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w12 1/9 uku. 21
  • ‘Mataifa Yatalazimika Kujua Kwamba Mimi Ni Yehova’

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • ‘Mataifa Yatalazimika Kujua Kwamba Mimi Ni Yehova’
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Sababu Gani Tunapaswa Kulitumia Jina la Mungu?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Jina la Mungu
    Amuka!—2017
  • Tuliheshimu Jina Kubwa la Mungu
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Yehova Analitukuza Jina Lake
    Ufalme wa Mungu Unatawala!
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
w12 1/9 uku. 21

Umukaribie Mungu

‘Mataifa Yatalazimika Kujua Kwamba Mimi Ni Yehova’

UTAJISIKIA namna gani ikiwa unasingiziwa jambo fulani? Na utafanya nini, ikiwa jambo ambalo umesingiziwa linaletea watu wengi mateso, hata watu ambao hawana kosa? Kwa kweli, utapenda kujitetea ili kuhakikisha kama haukufanya jambo lolote mbaya, sivyo? Je, unajua kama Yehova amefikiwa na jambo kama hilo? Leo, watu wengi wanamusingizia Mungu; wanasema kama ukosefu wa haki na mateso ambayo watu wanapata duniani ni mapenzi yake. Je, unawaza Yehova atajitetea, ni kusema, kulikatasa jina lake? Ndiyo! Soma yale anasema katika kitabu cha Ezekieli.​—Soma Ezekieli 39:7.

Yehova anasema hivi: “Sitaliacha tena jina langu litiwe [uchafu].” Watu wanaposema kama ukosefu wa haki ni mapenzi ya Mungu, wanalichafua jina lake. Sababu gani tunasema hivyo? Katika Biblia, mara nyingi “jina” linamaanisha sifa. Kitabu kimoja kinasema kama jina la Mungu linatumiwa ili kumaanisha ‘namna anavyojulikana​—namna anavyotambuliwa; na pia sifa yake na utukufu wake.’ Kwa hiyo, jina la Yehova linamaanisha sifa yake. Basi, Yehova anajulikana kuwa na sifa gani kuhusiana na ukosefu wa haki? Yeye anachukia ukosefu wa haki! Na tena anawasikilia huruma watu wanaoteseka kwa sababu ya ukosefu wa haki.a (Kutoka 22:22-24) Ikiwa Mungu anachukia sana mambo hayo mabaya, na huku watu wanasema kama hayo ni mapenzi yake, hauone kama wanamuharibishia sifa? Kwa kufanya hivyo, ‘wanalizarau jina lake.’​—Zaburi 74:10.

Ona kama katika andiko hilo la Ezekieli 39:7 (La Sainte Bible en swahili de la R.D. Congo), Yehova anatumia mara mbili maneno “jina langu takatifu.” Katika Biblia, mara nyingi jina la Yehova na maneno “takatifu” na “utakatifu” vinatembea pamoja. Neno “takatifu” linatoa wazo la kitu kilichotengwa; linaonyesha pia kitu kilicho safi na kilichotakata. Jina la Yehova ni takatifu kwa sababu Mungu anayeitwa kwa jina hilo ni mutakatifu—anajitenga kabisa na kitu chochote kichafu na chenye zambi. Je, unaelewa sasa sababu gani wale wanaosema kama mambo mabaya yanayotupata ni mapenzi ya Mungu wanalichafua sana ‘jina lake takatifu’?

Wazo kubwa linalopatikana katika Biblia ni hili: Yehova anakusudia kulitakasa jina lake kupitia Ufalme wake. Wazo hilo linakaziwa katika kitabu cha Ezekieli, ambacho kinarudilia mara nyingi maneno ‘mataifa yatalazimika kujua kwamba mimi ni Yehova.’ (Ezekieli 36:23; 37:28; 38:23; 39:7) Maandiko hayo hayaseme kama mataifa ndiyo yatachagua ikiwa yatamujua Yehova ao hapana. Lakini, mataifa ‘yatalazimika kujua.’ Ao tunaweza kusema kama Yehova anakusudia kutenda jambo fulani litakalolazimisha mataifa ya duniani yajue kama Yeye ni Yehova, Bwana Mutawala Mukubwa ambaye jina lake linamaanisha mambo yote yaliyo takatifu, safi na yenye kutakata.

Ahadi ambayo Yehova anarudilia mara nyingi kwa kusema kama ‘mataifa yatalazimika kujua kwamba yeye ni Yehova’ ni habari njema kwa wale wote wanaotamani sana kuona mwisho wa ukosefu wa haki na mateso. Hivi karibuni, Yehova atatimiza ahadi hiyo na kulitakasa jina lake. Ataondoa mambo yote mabaya na wale wanaoyaleta, lakini atawalinda wale wanaolijua jina lake na maana ya jina hilo na wale wanaoliheshimu. (Methali 18:10) Basi, sababu gani usijifunze mengi juu ya namna unavyoweza kumukaribia Yehova, Mungu mutakatifu, aliye ‘mupenda-haki’?​—Zaburi 37:9-11, 28.

Tafazali, mwezi huu wa 9, soma maandiko haya katika Biblia:

◼ Ezekieli sura ya 39-48 mupaka Danieli sura ya 1-3

[Maelezo ya chini]

a Soma habari “Mkaribie Mungu—Mpenda-Haki,” katika Munara wa Mulinzi wa tarehe 1 Mwezi wa 11, 2008.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine