Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w12 1/12 uku. 30-31
  • Yothamu Alibakia Mwaminifu Ijapokuwa Kulikuwa Matatizo Nyumbani Kwao

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Yothamu Alibakia Mwaminifu Ijapokuwa Kulikuwa Matatizo Nyumbani Kwao
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Habari za Kufanana na Zile
  • ‘Aliendelea Kushikamana na Yehova’
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Daudi na Goliati
    Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
  • Mtu Anayekubalika kwa Moyo wa Yehova
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • “Unifundishe Kufanya Mapenzi Yako”
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
w12 1/12 uku. 30-31

Uwafundishe Watoto Wako

Yothamu Alibakia Mwaminifu Ijapokuwa Kulikuwa Matatizo Nyumbani Kwao

WAKATI muzazi anaacha kumutumikia Mungu wa kweli, Yehova, hilo linaweza kufanya maisha ya mutoto yawe magumu. Acheni tuzungumuze juu ya Yothamu. Tutajifunza juu ya matatizo aliyopambana nayo nyumbani alipokuwa akiendelea kukomaa.

Uzia, baba ya Yothamu, alikuwa mufalme wa Yuda. Alikuwa mutu mwenye nguvu zaidi katika inchi yote. Uzia alikuwa mufalme muzuri kwa miaka mingi, hata mbele ya Yothamu kuzaliwa. Lakini baadaye, Yothamu alipokuwa angali kijana, Uzia akawa mwenye kiburi na akavunja Sheria ya Mungu. Kwa hiyo, Mungu akamupiga kwa ukoma, ugonjwa mubaya sana. Je, unajua jambo ambalo Yothamu alifanya wakati huo?—a

Yothamu aliendelea kumutumikia Yehova. Labda mama yake, Yerusha, alimusaidia. Hata hivyo, inawezekana ilikuwa vigumu kwa Yothamu kubakia mwaminifu kwa Yehova kisha baba yake, Uzia, kufukuzwa katika nyumba ya Yehova.

Utafanya nini ikiwa baba yako ao mama yako anaacha kumuabudu Yehova? Hilo litafanya iwe vigumu kwako kumuabudu Yehova, sivyo?— Lakini si vibaya kufikiri juu ya kile unachoweza kufanya ikiwa jambo hilo linatokea. Kusoma yale ambayo Daudi aliandika katika Biblia kunatuonyesha hivyo.

Yese, baba ya Daudi alikuwa mutu muzuri. Alimutumikia Yehova, na tunaweza kuwa na uhakika kwamba Daudi alimupenda baba yake. Lakini Daudi alijifunza kumupenda Yehova hata zaidi kuliko alivyomupenda baba yake, Yese. Acheni tuone sababu gani tunasema hivyo.

Tafazali, ufungue Biblia yako kwenye Zaburi 27:10. Daudi aliandika hivi: “Hata ikiwa baba yangu na mama yangu wangeniacha, Yehova mwenyewe angenichukua.” Fikiria jambo hili: Kile ambacho Biblia inasema ni kwamba ikiwa Yese, baba ya Daudi, ao mama yake angeacha kumutumikia Yehova, Daudi yeye angeendelea kumutumikia.

Namna gani wewe? Je, unaweza kuendelea kumutumikia Yehova hata ikiwa baba yako ao mama yako anaacha kumutumikia?— Hilo ni ulizo nzuri ambalo unapaswa kujiuliza. Sababu ya ulizo hilo inahusiana na amri ya maana zaidi katika Biblia. Amri hiyo ni: ‘Lazima umupende Yehova Mungu wako kwa moyo wako wote na kwa nafsi yako yote na kwa akili yako yote.’

Amri hiyo inamaanisha kuwa mwaminifu kwa Yehova hata wakati ni vigumu kufanya hivyo. Unafikiri ni nani ambaye anataka tuache kumutumikia Yehova?— Ni Shetani, adui wa Mungu. Yesu alimuita ‘mutawala wa ulimwengu huu.’ Biblia inasema pia kama yeye ni ‘mungu wa mufumo huu wa mambo.’ Je, tunahitaji kumuogopa Shetani?—

Hapana. Kuliko kumuogopa, tunahitaji kukumbuka kwamba Yehova ni mwenye nguvu zaidi kuliko Shetani. Yehova atatulinda ikiwa tunamutegemea. Usome katika Biblia namna Yehova alivyomulinda Daudi ili asishindwe na Goliathi, yule mutu mukubwa mwenye kuogopesha. Yehova anaweza pia kukulinda ikiwa unabakia mwaminifu kwake.

USOME KATIKA BIBLIA YAKO

2 Mambo ya Nyakati 26:16-21; 27:1, 2

Mathayo 22:37

Yohana 12:31; 2 Wakorintho 4:4

Waebrania 13:5, 6

1 Samweli 17:41-54

[Maelezo ya chini]

a Ikiwa unasoma sehemu hii pamoja na mutoto, unapoona alama hii (—), utue na umutie moyo aeleze mawazo yake.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine