Vitu vya Maana vya Historia Yetu
“Siweze Kuisahau”
“SIWEZE KUISAHAU!” Hayo ndiyo maneno ambayo wengi walisema kuhusu “Drama ya Uumbaji.” Ilikuja pa wakati na watu walioitazama hawangeweza kuisahau. Kwa kweli, “Drama ya Uumbaji” ilitoa ushahidi mukubwa kuhusu Yehova muda mufupi mbele ya Hitler kuanza kuwatesa vikali Mashahidi wa Yehova katika Ulaya. Lakini, “Drama ya Uumbaji” ilikuwa nini?
Drama mupya ilipewa jina la kitabu Schöpfung (Création)
Katika mwaka wa 1914, makao makubwa ya Mashahidi wa Yehova huko Brooklyn, New York, États-Unis, ilionyesha watu picha ao “Foto-Drama ya Uumbaji.” Foto-drama hiyo ilikuwa filme ya saa munane ya picha zenye rangi za watu wenye kutembea na kusema, na za wanyama wenye kutembea. Watu walitazama Drama hiyo ya uumbaji duniani pote. Drama iliyoitwa “Eureka,” iliyokuwa filme iliyofupishwa ya Foto-Drama hiyo, ilitolewa pia katika mwaka wa 1914. Lakini, mwishoni mwa miaka ya 1920, filme na mashine za kuonyesha picha hizo zilikuwa zimezeeka sana. Hata hivyo, bado watu wengi walitaka kutazama “Foto-Drama.” Kwa mufano, wakaaji wa muji wa Ludwigsburg, huko Alemanye, waliuliza hivi: “Ni wakati gani ‘Foto-Drama’ itaonyeshwa tena?” Ni jambo gani lililopaswa kufanywa?
Ili watu zaidi watazame Drama hiyo, wasimamizi wa familia ya Beteli ya Magdeburg, huko Alemanye, walinunua filme kwa shirika la kutangaza habari katika muji wa Paris, France na walinunua picha kwa kompanyi ya picha katika Leipzig na Dresden katika miaka ya 1920. Waliondoa mambo yasiyofaa kwenye filme na picha hizo na kuziunganisha na filme za zamani za “Foto-Drama” zilizokuwa zingali muzuri.
Ndugu Erich Frost, mwanamuziki mwenye ufundi, alitunga muziki uliotiwa katika filme hizo. Masimulizi yalitayarishwa ili yasomwe wakati Foto-Drama inaonyeshwa. Masimulizi hayo yalichukuliwa katika kitabu Création na katika vitabu vingine. Hiyo ndio sababu, aina hiyo mupya ya “Foto-Drama” iliitwa “Drama ya Uumbaji.”
Drama hiyo mupya ilichukua pia muda wa saa munane kama vile “Foto-Drama” na ilionyeshwa kila mangaribi sehemu kwa sehemu. Drama hiyo ilitoa habari nyingi zenye kupendeza kuhusu siku za uumbaji, ilizungumuzia historia ya Biblia na ya ulimwengu, na ilionyesha kwamba dini ya uongo imewadanganya wanadamu. “Drama ya Uumbaji” ilionyeshwa katika Alemanye, Autriche, Luxembourg, na Suisse, na mahali popote ambapo watu walizungumuza Kialemand.
Erich Frost pamoja na maandishi ya muziki yaliyotiwa katika “Drama ya Uumbaji”
Erich Frost anaeleza hivi: “Mahali ambapo Drama hiyo ilionyeshwa, niliwatia moyo wenzangu, zaidi sana waliokuwa katika kikundi cha wapiga-muziki, watumie wakati wa mapumuziko kwenda kwenye kila mustari wa viti ambapo watu wanakaa na kuwatolea vitabu na vijitabu vyetu vyenye kupendeza. Kwa njia hiyo, tulitolea watu vitabu vingi kuliko vile tulivyotolea watu katika mahubiri ya nyumba kwa nyumba.” Johannes Rauthe, aliyeonyesha watu drama katika inchi ya Polonye na katika inchi inayoitwa sasa République Tchèque, anakumbuka kwamba watu wengi waliacha adresi zao ili watembelewe. Adresi hizo zilisaidia kufanya ziara za kurudia zenye matokeo.
Katika miaka ya 1930, majumba ambamo “Drama ya Uumbaji” ilionyeshwa yalijaa watu, na katika miji ambamo drama hiyo ilionyeshwa, watu walizungumuza sana kuhusu Mashahidi wa Yehova. Mwishoni mwa mwaka wa 1933, karibu watu milioni moja walitazama drama hiyo iliyoonyeshwa na biro ya tawi ya Alemanye. Käthe Krauss anakumbuka kwamba “ili kutazama siku moja kati ya siku tano ambamo drama ilionyeshwa, kila mumoja wao alitembea kilometre 10 kuenda na kurudi, kupitia katika misitu na kupanda milima na kushuka mabonde.” Else Billharz anasema hivi: “‘Drama ya Uumbaji’ ilinisaidia kuipenda kweli.”
Alfred Almendinger anaeleza kwamba kisha kutazama drama hiyo, mama yake “alikuwa na furaha sana, kwa hiyo alinunua Biblia na kutafuta neno ‘moto wa mateso.’” Kwa kuwa alikosa neno hilo katika Biblia hiyo, aliacha kuenda kanisani na alibatizwa. Ndugu Erich Frost anakumbuka kwamba “‘Drama ya Uumbaji’ iliwasaidia watu wengi wajifunze kweli.’”—3 Yoh. 1-3.
Muda muchache tu mbele watu wengi zaidi watazame “Drama ya Uumbaji,” utawala wa Nazi ulishambulia Ulaya yote. Kuanzia mwaka 1933, kazi ya Mashahidi wa Yehova ilikatazwa katika Alemanye. Kuanzia wakati huo mupaka mwisho wa vita ya pili ya ulimwengu katika mwaka wa 1945, Mashahidi wa Yehova waliteswa vikali katika Ulaya. Ndugu Erich Frost alipitisha karibu miaka munane katika kifungo. Lakini alifunguliwa na baadaye alitumikia kwenye Beteli ya Alemanye, iliyopatikana huko Wiesbaden. Inafurahisha kwa sababu “Drama ya Uumbaji” ambayo watu hawangeweza kusahau ilifika pa wakati kabisa ili kutia nguvu imani ya Wakristo wengi waliokuwa karibu na kujaribiwa wakati wa Vita ya Pili ya Ulimwengu.—Kutoka katika vitu vya maana vya historia yetu vya Alemanye.