Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w13 1/3 uku. 14-15
  • Petro na Anania Walisema Uongo—Tunaweza Kujifunza Somo Gani?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Petro na Anania Walisema Uongo—Tunaweza Kujifunza Somo Gani?
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Bwana Wake Alimufundisha Kusamehe
    Tuige Imani Yao
  • “Watu Wenye Hawana Elimu na Watu wa Kawaida”
    “Kutoa Ushahidi Kamili” juu ya Ufalme wa Mungu
  • Alibaki Mushikamanifu Ijapokuwa Majaribu
    Tuige Imani Yao
  • Petro Anamukana Yesu Kwenye Nyumba ya Kayafa
    Yesu—Ni Njia, Kweli, na Uzima
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
w13 1/3 uku. 14-15

UWAFUNDISHE WATOTO WAKO

Petro na Anania Walisema Uongo​—Tunaweza Kujifunza Somo Gani?

Kama vile unavyojua, uongo ni kusema jambo fulani ambalo unajua kwamba si la kweli. Je, umekwisha kusema uongo wakati fulani?—a Hata watu fulani waliokomaa ambao wanamupenda Mungu wamesema uongo. Na labda unajua mutu fulani katika Biblia ambaye alisema uongo. Jina lake ni Petro, mumoja kati ya mitume 12 wa Yesu. Acheni tusikilize habari juu yake na tuone kile kilichomufanya aseme uongo.

[Picha katika ukurasa wa 14]

Kisha Yesu kukamatwa, anapelekwa nyumbani kwa kuhani mukubwa. Saa sita ya usiku imekwisha kupita. Petro anaingia katika uwanja wa nyumba ya kuhani huyo mukubwa bila kutambuliwa na watu. Kupitia mwangaza wa moto, kijakazi wa kuhani mukubwa aliyemufungulia Petro mulango anamutambua. Anamuambia Petro hivi: “Wewe, pia, ulikuwa pamoja na Yesu.” Kwa sababu ya woga, Petro anasema kwamba hakuwa pamoja na Yesu.

Biblia inasema kwamba baadaye ‘musichana mwingine alimuona’ Petro. Musichana ao mutoto mwanamuke huyo alisema hivi: ‘Mutu huyu alikuwa pamoja na Yesu.’ Kwa mara nyingine tena, Petro anakana kwamba hakuwa pamoja na Yesu. Baada ya muda mufupi, watu wengine wanamukaribia Petro na kumuambia: ‘Hakika wewe pia ni mumoja wao.’

Petro anaogopa kwa sababu ni mara ya tatu anasema: ‘Simujui mutu huyo!’ Jogoo anawika. Yesu anamutazama Petro, na Petro anakumbuka kwamba saa chache zilizopita, Yesu alimuambia hivi: “Kabla ya jogoo kuwika, utanikana mara tatu.” Petro anavurugika na anaanza kulia. Anahuzunika sana!

[Picha katika ukurasa wa 15]

Je, jambo kama hilo linaweza kukupata?— Unaweza kuwa kwenye masomo na unasikia wanafunzi wenzako wanaongea vibaya juu ya Mashahidi wa Yehova. Mwanafunzi mumoja anasema hivi: “Mashahidi wa Yehova hawasalimie bendera.” Kisha, mwengine anaongeza hivi: “Wao hawapigane vita kwa ajili ya inchi yao.” Hata hivyo, mwanafunzi mwengine anasema hivi: “Kwa kweli, Mashahidi wa Yehova si Wakristo, kwa sababu hawafanye sikukuu ya Noeli.” Kisha mumoja wao anageuka na kukuuliza hivi: “Wewe pia ni Shahidi wa Yehova, sivyo?” Utasema nini?—

Mbele ya jaribu kutokea, unahitaji kujitayarisha ili utoe jibu nzuri. Petro hakujitayarisha. Alipokazwa sana na watu, alisema uongo. Hata hivyo, alihuzunika sana kwa sababu ya jambo ambalo alikuwa amefanya, na Mungu alimusamehe.

Anania, mwanafunzi mwengine wa Yesu, alisema pia uongo. Lakini, Mungu hakumusamehe yeye wala bibi yake, Safira. Safira na bwana yake Anania walikubaliana ili kusema uongo. Acheni tuone sababu gani Mungu hakumusamehe Anania wala Safira.

Siku kumi baada ya Yesu kuachana na mitume na kurudia kwa Mungu mbinguni, watu 3 000 walibatizwa huko Yerusalemu. Wengi kati ya watu hao walitoka katika inchi za mbali ili kuja kufanya sikukuu ya Pentekoste, na baada ya kuwa wanafunzi wa Yesu, walitaka kubaki muda murefu Yerusalemu ili wajifunze mambo mengi kuhusu imani yao mupya. Kwa hiyo, wanafunzi fulani wa Yesu wanatumia feza zao ili kuwasaidia.

Anania na bibi yake wanauzisha shamba lao ili wapate feza ambazo watatumia ili kuwasaidia wanafunzi wapya ambao wametoka tu kubatizwa. Wakati Anania analeta feza hizo kwa mitume, anasema kwamba analeta kiasi chote cha feza ambazo alipata alipouzisha shamba lake. Lakini ni uongo! Anaficha kiasi fulani cha feza kwa ajili yake mwenyewe! Lakini Mungu anamuwezesha Petro kujua kwamba Anania anasema uongo, kwa hiyo Petro anamuambia Anania hivi: “Umedanganya, si wanadamu, bali Mungu.” Mara moja, Anania anaanguka chini na kufa! Karibu saa tatu baadaye, Safira, bibi ya Anania anaingia. Kwa kuwa hajue kile kimemupata bwana yake, yeye pia anasema uongo na anaanguka chini na kufa.

Tunajifunza somo hili lenye nguvu: Kusema ukweli ni jambo la maana! Ndiyo, sisi wote tunapaswa kujifunza somo hilo! Hata hivyo, sisi wote tunafanya makosa, zaidi sana ikiwa sisi ni vijana. Je, wewe haufurahi kuona kwamba Yehova anakupenda na atakusamehe kama vile alivyomusamehe Petro?— Lakini kumbuka kwamba ni lazima tuseme ukweli. Na hata ikiwa tunafikia kufanya kosa kubwa la kusema uongo fulani, ni lazima tumuombe Mungu atusamehe. Labda Petro aliomba musamaha, na Mungu akamusamehe. Ikiwa tutajikaza sana kuacha kusema uongo, Mungu atatusamehe pia!

Soma katika Biblia yako

  • Mathayo 26:69-75

  • Matendo 2:38-42; 4:32-37; 5:1-11

a Ikiwa unasoma sehemu hii pamoja na mutoto, unapoona alama hii (—), utue na umutie moyo aeleze mawazo yake.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine