Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w14 15/6 uku. 7
  • Maulizo ya Wasomaji Wetu

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Maulizo ya Wasomaji Wetu
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Habari za Kufanana na Zile
  • “Wafu Watafufuliwa Namna Gani?”
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2020
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
w14 15/6 uku. 7
Kuwakaribisha wafufuliwa katika Paradiso

Maulizo Ya Wasomaji Wetu

Je, Wakristo Wanaweza Kuchoma Maiti ya Mutu?

Biblia ina habari nyingi zinazoonyesha kwamba maiti ao mifupa ya watu fulani waliokufa ilichomwa. (Yos. 7:25; 2 Nya. 34:4, 5) Pengine hilo lilimaanisha kwamba hawakustahili kuzikwa kwa heshima. Lakini, sikuzote haikumaanisha hivyo.

Habari ya kifo cha Mufalme Sauli na watoto wake watatu, inaweza kutusaidia kuelewa jambo hilo. Wote waine walikufa kwenye vita, Waisraeli walipopigana na Wafilisti. Mumoja kati ya watoto hao waliokufa ni Yonathani, aliyekuwa rafiki muzuri na aliyemutegemeza Daudi kwa uaminifu. Wakati Waisraeli wenye bidii walioishi Yabesh-gileadi walisikia jambo lililotokea, walichukua maiti hizo ine wakazichoma, na kisha walizika mifupa. Baadaye, Daudi aliwasifu Waisraeli hao kwa kutenda hivyo.—1 Sam. 31:2, 8-13; 2 Sam. 2:4-6.

Maandiko yanatutolea tumaini la ufufuo, ni kusema, Mungu atarudishia tena mutu uzima wake. Iwe mutu aliyekufa alichomwa ao hapana, Yehova ana uwezo mukubwa wa kumupatia tena mutu huyo uzima akiwa na mwili mupya. Vijana Waebrania watatu waaminifu waliokuwa karibu kutupwa katika tanuri la moto, kulingana na agizo la Mufalme Nebukadneza, hawakuogopa kwamba wataharibiwa katika moto huo, na kwamba Mungu hataweza kuwafufua. (Dan. 3:16-18) Watumishi waaminifu wa Yehova waliouawa na kuchomwa baadaye katika kambi ya mateso ya Wanazi, waliamini kwamba Yehova atawafufua. Watumishi wengine waaminifu wa Mungu walikufa katika milipuko fulani ao walikufa bila hata sehemu fulani ya miili kubakia. Hata hivyo, watafufuliwa.—Ufu. 20:13.

Yehova hatahitaji kukusanya mwili wa zamani ambao mutu alikuwa nao ili aweze kumufufua. Jambo hilo linaonekana namna Mungu anavyowafufua Wakristo watiwa-mafuta ili waende mbinguni. Kama vile Yesu, ambaye ‘alifanywa kuwa hai katika roho,’ Wakristo watiwa-mafuta wanafufuliwa wakiwa watu walewale lakini na mwili wa kiroho. Hawaende mbinguni wakiwa sehemu fulani ya mwili wao wa wanadamu.—1 Pet. 3:18; 1 Kor. 15:42-53; 1 Yoh. 3:2.

Tumaini letu la ufufuo halitegemee namna mwili wetu unaweza kutendewa, lakini, linategemea imani ya kwamba Mungu ana uwezo na anatamani kuwafufua wafu. (Mdo. 24:15) Ni kweli kwamba hatuwezi kuelewa vizuri namna Mungu amewafufua wafu kwa njia ya muujiza hapo zamani ao namna atakavyofanya hivyo wakati ujao. Hata hivyo, tunamutegemea Yehova. Ametutolea “uhakikisho” kwa kumufufua Yesu.—Mdo. 17:31; Lu. 24:2, 3.

Ni vizuri Wakristo wafikirie tabia za kwao, zamiri za wengine na sheria zinazohusu namna ya kutendea maiti za watu. (2 Kor. 6:3, 4) Kwa hiyo, kuchoma maiti ya mutu ao hapana ni uamuzi wa mutu mwenyewe ao familia yake.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine