Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w15 1/1 uku. 13
  • Je, Ulijua?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Je, Ulijua?
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Mufalme Yesu Kristo Anahukumu Kondoo na Mbuzi
    Yesu—Ni Njia, Kweli, na Uzima
  • Uendelee Kutegemeza Ndugu za Kristo kwa Uaminifu
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Maisha ya Watu Wakati wa Zamani—Muchungaji
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Mthawabishaji wa Wote Wanaomtumikia
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
w15 1/1 uku. 13

JE, ULIJUA?

Neno “towashi” linalotumiwa katika Biblia linamaanisha nini?

Muchoro wa Waasiria wa towashi

Sehemu ya Muchoro wa Waasiria wa Towashi

Wakati fulani, neno hilo linamaanisha mwanaume aliyevunjwa mapumbu. Wakati wa zamani, wanaume fulani walivunjwa mapumbu kwa sababu ya kukamatwa kwa nguvu ao kufanywa kuwa watumwa. Wanaume wenye kutumainika waliovunjwa mapumbu walisimamia makao ya wanawake, ao masuria, katika nyumba za kifalme. Kwa mufano, matowashi Hegai na Shaashgazi walikuwa walinzi wa bibi na masuria wa Mufalme wa Perse Ahasuero, anayewaziwa kuwa Shasta wa kwanza.—Esta 2:3, 14.

Lakini, haiko matowashi wote ambao Biblia inasema waliovunjwa mapumbu. Watu fulani wenye elimu wanasema kuwa neno hilo lilitumiwa pia katika maana kubwa ili kumaanisha ofisa aliyekuwa anafanya kazi katika makao ya mufalme. Inaonekana kuwa neno hilo linatumiwa katika maana hiyo juu ya Ebed-meleki, rafiki ya Yeremia, na juu ya Muetiopia mwenye hatajwe jina ambaye Filipo alihubiria. Inawezekana Ebed-meleki alikuwa ofisa wa cheo cha juu sana, kwa sababu alikuwa anazungumuza na Mufalme Sedekia moja kwa moja. (Yeremia 38:7, 8) Na Muetiopia ambaye “alikuwa ameenda Yerusalemu kuabudu” anaelezwa kuwa muweka-hazina katika nyumba ya mufalme.—Matendo 8:27.

Sababu gani wachungaji walitenganisha kondoo na mbuzi wakati wa zamani?

Muchungaji aliye na kundi la kondoo

Yesu alipozungumuzia wakati wa hukumu unaokuja, alisema hivi: ‘Wakati Mwana wa binadamu atakapofika katika utukufu wake, ... atawatenganisha watu, mumoja kutoka kwa mwenzake, kama vile muchungaji anavyotenganisha kondoo na mbuzi.’ (Mathayo 25: 31, 32) Sababu gani wachungaji wa kwelikweli walitenganisha wanyama hao?

Kwa kawaida, kondoo na mbuzi walichungwa pamoja na waliruhusiwa kula majani pamoja wakati wa muchana. Usiku walikusanywa katika zizi (enclos) ili kulindwa na wanyama wa pori, watu wenye kuiba, na baridi. (Mwanzo 30:32, 33; 31:38-40) Aina hizo mbili za wanyama zilitenganishwa katika zizi mbili tofauti ili kulinda kondoo wapole, zaidi sana kondoo wa kike na wana-kondoo, ili wasiumizwe na mbuzi wakali zaidi. Kulingana na kitabu kimoja, muchungaji alitenganisha pia kondoo na mbuzi wakati wa “kuwazalisha, kuwakamua maziwa, na kuwakata manyoya.” (All Things in the Bible) Kwa hiyo, mufano wa Yesu unatumia desturi na maelezo yanayoeleweka kwa wasikilizaji wanaoishi katika eneo watu wanafuga wanyama, kama eneo la Israeli ya zamani.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine