Habari Zenye Kuwa Ndani
JUMA LA TAREHE 27/02–5/03/2017
7 ‘Umutegemee Yehova na Ufanye Mema’
Habari hii inazungumuzia namna andiko letu la mwaka wa 2017 linatutia moyo kutegemea musaada wa Yehova wakati wa magumu. Mifano ya watumishi waaminifu wa Yehova wa wakati wa zamani, itatufundisha namna tunaweza kumutegemea Yehova ili atusaidie wakati tunajikaza kumaliza magumu yetu na kusaidia wengine.
JUMA LA TAREHE 6-12/03/2017
12 Upendezwe Sana na Zawadi Yako ya Uhuru wa Kuchagua
Katika habari hii, tutajifunza namna gani tunaweza kupendezwa sana na zawadi ya Mungu ya uhuru wa chagua kwa kuitumia katika njia yenye kumupendeza Mupaji wa zawadi hiyo. Itatusaidia pia kuona namna gani tunaweza kuheshimia namna wengine wanatumikisha zawadi yao ya uhuru wa kuchagua.
JUMA LA TAREHE 13-19/03/2017
17 Sababu Gani Sifa ya Kiasi Ingali ya Maana?
JUMA LA TAREHE 20-26/03/2017
22 Unaweza Kuendelea Kuwa Mwenye Kiasi Wakati wa Majaribu
Habari hizi zitatusaidia kuelewa muzuri sifa ya maana, ni kusema, sifa ya kiasi. Habari ya kwanza inaeleza sifa ya kiasi inamaanisha nini, na haimaanishe nini. Habari ya pili inatufundisha namna ya kuendelea kuwa na kiasi hata wakati ni vigumu kufanya hivyo.
JUMA LA TAREHE 27/03–2/04/2017
27 Mambo Hayo Uwapatie Wanaume Waaminifu
Kadiri wakati unapita, ndugu wenye kuzeeka wanazoeza vijana ili watimize madaraka zaidi katika tengenezo la Yehova. Habari hii inaonyesha namna vijana na ndugu wenye kuzeeka wanaweza kutegemezana.
32 ULIJUA?